Nyaluhusa87
JF-Expert Member
- Oct 14, 2011
- 1,303
- 262
*****SORY MADAM*****(65)
AGE....................................................................18+
WRITER.............................................................EDDAZARIA G.MSULWA
ILIOISHIA
Nilimuuliza Dorecy na kumfanya Phidaya kunitazama kwa jicho kali lililo jaa hasira
"Ndio, ila kuna ishu Khalid alitaka kukufanyia wewe na Phidaya akaiingilia kati na kuwa adui mwengine wa Khalid"
"Jambo gani hilo?"
Hata kabla Dorecy hajanijibu tukasikia milio mingi ya risasi kwenye kordo yetu huku kelele za watu wagonjwa na manesi wakike zikisikia jambo lililo tushtua sote ndani ya chumba
ENDELEA
Milio ya risasi ikaendelea kurindima nje ya chumba tulichopo na kuzidi kutupagawisha sote tuliopo ndani ya chumb hichi, wasiwasi mwingi ukawa kwa Dorecy ambaye fika anaoenekana kuchanganyikiwa
"Eddy hao ni watu wa mume wangu"
Dorecy alizungumza huku mwili mzima ukimtetemeka, nikapiga hatua za haraka hadi dirishani na kuchungulia chini ambapo kuna umbali wa ghorofa mbili kwenda chini.
"Hatuwezi kutoka humu ndani"
Nilizungumza huku nikiwatazama Dorery na Phidaya
"Itakuwaje sasa?"
Phidaya alizungumza huku machozi yakimwagika kwa wingi.Nikapiga hatua hadi mlangoni, nikachungulia kwenye sehemu ya kuingizia funguo, nikamshuhudia jamaa mmoja akitandika risasi ya kichwa mzee mmoja aliye ambiwa alale chini ila akaleta kiherehe cha kujinyanyua, ndipo akakutana na maafa hayo ambayo ni yakinyama sana.
Gafla simu ya Phidaya ikaita na kutufanya sote kumgeukia na kumtazama kwa macho ya mshangao, kwa kiwewe alicho nacho akashindwa hata kuikata na kujikuta akiiachia na kuanguka chini, nikachungulia tena kwenye tobo la kuingizia funguo na kumuona jamaa aliye muua mzee, akiutazama mlango wetu kwa umakini.
"Ingieni bafuni"
Nilizungumza kwa sauti ya chinichini, Dorecy akamshika mkono Phidaya na kukimbilia kwenye bafu liilopo humu ndani ya chumba changu.Jamaa akapiga hatua hadi ulipo mlango uku bunduki yake aina ya ‘short gun' ikiwa mkononi mwake.Nikajibanza nyuma ya mlango, huku mapigo ya moyo yakinienda mbio kiasi kwani bado sijaiamini afya yangu kwa kiasi kikubwa kutokana na majeraha ya risasi yaliyopo mwilini mwangu.Mlango taratibu ukafunguliwa, nikaanza kuona kiatu cheusi kikitangulia mbele, jamaa akasimama kwa muda, gafla simu ya Phidaya iliyo anguka chini ikaanza kuita tena na kumfanya jamaa kupiga hatua za taratibu hadi sehemu ilipo anguka simu na kuiokota.Mapigo ya moyo yakazidi kunienda mbio, kwani endapo jamaa atageuka nyuma nilazima ataniona.Akaitazama simu ya Phidaya kwa muda na kuitupa chini na kuchanguka, akatazama mlango wa kuingilia bafuni ambapo ndani yake yupo Phidaya na Dorecy
Simu ya jamaa ikaita, akaitoa kwenye koti lake, akaipokea nakuiweka sikioni mwake, akazungumza kwa lugha ya kiarabu, nikastukia kumuona jamaa akichomoka kwa kasi, ndani ya chumba pasipo kuniona nyuma ya mlango, ving'ora vya gari za polisi, nikaanza kuvisikia na kunifanya nishushe pumzi nyingi, na kujikalia chini, huku jasho jingi likimwagika.Ndani ya dakika kadaa askari kadhaa wakawa wameingia katika sehemu tulipo, Dorecy na Phidaya wakatoka bafuni, askari na madaktari walio salimika katika vamizi la majambazi hawa
***
Wagonjwa tulio salimika tukahamishwa kwenye hospitali moja, inayo milikiwa na jeshi la nchi ya Philipines, matiibabu yangu hayakuchukua muda mrefu sana, nikaruhusiwa kutoka hospitalini na kuhamia kwenye hoteli ambayo Phidaya anaishi kwa siri sana, na amelipiwa gharama zote na Dorecy ambaye tayari amerudi kwa mume wake.
"Phidaya,itatubidi turudi Tanzania"
Nilizungumza huku macho yangu yakimtazama Phidaya aliye jilalia kiuvivu kwenye kitanda, huku akiwa tumbo wazi akilichezea chezea kwa kiganja chake tumbo lake lenye kiumbe ndani
"Si usubiri niweze kujifungua kwanza"
"Hatuwezi kuishi hapa, pasipo sisi kuwa na kazi, unadhani tutayamudu vipi haya maisha?"
"Sawa mume wangu, je tukirudi huko Tanzania, tutafikia wapi wakati umesha sema kwamba mama yako alitekwa na baba yako mkubwa"
Nikamtazama Phidaya kwa muda, kwani kitu alicho kizungumza kinamaana kubwa sana kwangu, isitoshe sijajua ni hali gani inayo endela kati ya mzee Godwin na mama yangu.Nikanyanyuka taratibu na kuisogelea computer iliyopo kwenye meza humu chumbani kwetu, ambayo imeunganishwa na huduma ya Internet.Nikaiwasha taratibu, baada ya muda nikafungua mtandao wa Google
"Unataka kufanya nini?" Phidaya alizungumza huku akipiga hatua na kuja kukaa kwenye kiti nilicho kikalia mimi
"Kuna mtu nataka kumtafuta"
"Nani?"
"Baba yangu mzazi, anaishi Afrika kusini"
"Mmmm sawa"
Nikaliingiza jina la baba yangu mzazi kwenye sehemu ya kutafutia, kwenye mtandao huu ambao unasadikika ndio mtandao mkubwa duniani kote, ulio kusanya mambo mengi sana, ndani ya sekunde kadhaa nikawa nimefanikiwa kulipata jina la baba yangu mzazi pamoja na historia yake, cha kumshukuru Mungu nikakutana na taarifa nyingine iliyo nipendezesha moyoni mwangu, kwani ameingia kwenye orodha ya matajiri kumi nchini Afrika kusini huku yeye akiwa nafasi ya nne kutoka juu.
"Inabidi twende nyumba ni kwa baba"
"Sawa mume wangu"
Phidaya hakuwa na pingamizi na maamuzi yangu niliyo yachukua, nikaanza kufwatilia hati za kusafiria kuelekea Afrika kusini, kutuokana na pesa ambazo Dorecy anatusaidia, sikupata tabu sana katika kukamilisha maswala usafiri wa ndege.Siku ya pili tukakusanya kila kitu kilicho chetu kwenye hoteli ambayo tunaishi, tukakodi Tanksi hadi uwanja wa ndege, muda wa kupanda ndege ulipo wadia, tukaungana na wasafiri wengine na kuingia ndani ya ndege, na taratibu safari ikaanza, huku moyoni mwangu nikimuomba Mungu atufikieshe salama, kwani kumbukumbu za ajali iliyo tokea nchini Kenya kipindi nikitokea Afrika Kusini, inaendelea kuzunguka ndani ya kichwa changu kama mkanda wa filamu.Phidaya kwa kudeka muda wote kichwa cheka amekilaza kifuani mwangu, huku akiimba nyimbo za kunibembeleza kwa sauti ya chini
"Baby" Nilimuita kwa sauti ya upole
"Mmmmm"
"Naomba niende msalani"
"Sawa, ila usichelewe mume wangu"
Phidaya alinijibu taratibu huku akijinyanyua, kifuani kwangu taratibu, nikasimama, na kuanza kupiga hatua za kuelekea chooni, nikaingia ndani ya choo na kumaliza haja zangu zote, nikanawa uso wangu ili kuutoa uchovu na usingizi unao ninyemelea usoni mwangu.Nikafungua mlango, gafla nikastulia kitu chenye ncha kali kikinikita mgongoni mwangu, na sauti ikasikika kutoka nyuma yangu
"Tulia kama ulivyo upo chini ya ulinzi, Mr Eddy"
****Je ninani aliye aliye muwekea Eddy kitu chenye ncha kali, mgongoni mwake, wakiwa ndani ya ndege.Ungana nami kwenye toleo lijalo*****
ITAENDELEA
AGE....................................................................18+
WRITER.............................................................EDDAZARIA G.MSULWA
ILIOISHIA
Nilimuuliza Dorecy na kumfanya Phidaya kunitazama kwa jicho kali lililo jaa hasira
"Ndio, ila kuna ishu Khalid alitaka kukufanyia wewe na Phidaya akaiingilia kati na kuwa adui mwengine wa Khalid"
"Jambo gani hilo?"
Hata kabla Dorecy hajanijibu tukasikia milio mingi ya risasi kwenye kordo yetu huku kelele za watu wagonjwa na manesi wakike zikisikia jambo lililo tushtua sote ndani ya chumba
ENDELEA
Milio ya risasi ikaendelea kurindima nje ya chumba tulichopo na kuzidi kutupagawisha sote tuliopo ndani ya chumb hichi, wasiwasi mwingi ukawa kwa Dorecy ambaye fika anaoenekana kuchanganyikiwa
"Eddy hao ni watu wa mume wangu"
Dorecy alizungumza huku mwili mzima ukimtetemeka, nikapiga hatua za haraka hadi dirishani na kuchungulia chini ambapo kuna umbali wa ghorofa mbili kwenda chini.
"Hatuwezi kutoka humu ndani"
Nilizungumza huku nikiwatazama Dorery na Phidaya
"Itakuwaje sasa?"
Phidaya alizungumza huku machozi yakimwagika kwa wingi.Nikapiga hatua hadi mlangoni, nikachungulia kwenye sehemu ya kuingizia funguo, nikamshuhudia jamaa mmoja akitandika risasi ya kichwa mzee mmoja aliye ambiwa alale chini ila akaleta kiherehe cha kujinyanyua, ndipo akakutana na maafa hayo ambayo ni yakinyama sana.
Gafla simu ya Phidaya ikaita na kutufanya sote kumgeukia na kumtazama kwa macho ya mshangao, kwa kiwewe alicho nacho akashindwa hata kuikata na kujikuta akiiachia na kuanguka chini, nikachungulia tena kwenye tobo la kuingizia funguo na kumuona jamaa aliye muua mzee, akiutazama mlango wetu kwa umakini.
"Ingieni bafuni"
Nilizungumza kwa sauti ya chinichini, Dorecy akamshika mkono Phidaya na kukimbilia kwenye bafu liilopo humu ndani ya chumba changu.Jamaa akapiga hatua hadi ulipo mlango uku bunduki yake aina ya ‘short gun' ikiwa mkononi mwake.Nikajibanza nyuma ya mlango, huku mapigo ya moyo yakinienda mbio kiasi kwani bado sijaiamini afya yangu kwa kiasi kikubwa kutokana na majeraha ya risasi yaliyopo mwilini mwangu.Mlango taratibu ukafunguliwa, nikaanza kuona kiatu cheusi kikitangulia mbele, jamaa akasimama kwa muda, gafla simu ya Phidaya iliyo anguka chini ikaanza kuita tena na kumfanya jamaa kupiga hatua za taratibu hadi sehemu ilipo anguka simu na kuiokota.Mapigo ya moyo yakazidi kunienda mbio, kwani endapo jamaa atageuka nyuma nilazima ataniona.Akaitazama simu ya Phidaya kwa muda na kuitupa chini na kuchanguka, akatazama mlango wa kuingilia bafuni ambapo ndani yake yupo Phidaya na Dorecy
Simu ya jamaa ikaita, akaitoa kwenye koti lake, akaipokea nakuiweka sikioni mwake, akazungumza kwa lugha ya kiarabu, nikastukia kumuona jamaa akichomoka kwa kasi, ndani ya chumba pasipo kuniona nyuma ya mlango, ving'ora vya gari za polisi, nikaanza kuvisikia na kunifanya nishushe pumzi nyingi, na kujikalia chini, huku jasho jingi likimwagika.Ndani ya dakika kadaa askari kadhaa wakawa wameingia katika sehemu tulipo, Dorecy na Phidaya wakatoka bafuni, askari na madaktari walio salimika katika vamizi la majambazi hawa
***
Wagonjwa tulio salimika tukahamishwa kwenye hospitali moja, inayo milikiwa na jeshi la nchi ya Philipines, matiibabu yangu hayakuchukua muda mrefu sana, nikaruhusiwa kutoka hospitalini na kuhamia kwenye hoteli ambayo Phidaya anaishi kwa siri sana, na amelipiwa gharama zote na Dorecy ambaye tayari amerudi kwa mume wake.
"Phidaya,itatubidi turudi Tanzania"
Nilizungumza huku macho yangu yakimtazama Phidaya aliye jilalia kiuvivu kwenye kitanda, huku akiwa tumbo wazi akilichezea chezea kwa kiganja chake tumbo lake lenye kiumbe ndani
"Si usubiri niweze kujifungua kwanza"
"Hatuwezi kuishi hapa, pasipo sisi kuwa na kazi, unadhani tutayamudu vipi haya maisha?"
"Sawa mume wangu, je tukirudi huko Tanzania, tutafikia wapi wakati umesha sema kwamba mama yako alitekwa na baba yako mkubwa"
Nikamtazama Phidaya kwa muda, kwani kitu alicho kizungumza kinamaana kubwa sana kwangu, isitoshe sijajua ni hali gani inayo endela kati ya mzee Godwin na mama yangu.Nikanyanyuka taratibu na kuisogelea computer iliyopo kwenye meza humu chumbani kwetu, ambayo imeunganishwa na huduma ya Internet.Nikaiwasha taratibu, baada ya muda nikafungua mtandao wa Google
"Unataka kufanya nini?" Phidaya alizungumza huku akipiga hatua na kuja kukaa kwenye kiti nilicho kikalia mimi
"Kuna mtu nataka kumtafuta"
"Nani?"
"Baba yangu mzazi, anaishi Afrika kusini"
"Mmmm sawa"
Nikaliingiza jina la baba yangu mzazi kwenye sehemu ya kutafutia, kwenye mtandao huu ambao unasadikika ndio mtandao mkubwa duniani kote, ulio kusanya mambo mengi sana, ndani ya sekunde kadhaa nikawa nimefanikiwa kulipata jina la baba yangu mzazi pamoja na historia yake, cha kumshukuru Mungu nikakutana na taarifa nyingine iliyo nipendezesha moyoni mwangu, kwani ameingia kwenye orodha ya matajiri kumi nchini Afrika kusini huku yeye akiwa nafasi ya nne kutoka juu.
"Inabidi twende nyumba ni kwa baba"
"Sawa mume wangu"
Phidaya hakuwa na pingamizi na maamuzi yangu niliyo yachukua, nikaanza kufwatilia hati za kusafiria kuelekea Afrika kusini, kutuokana na pesa ambazo Dorecy anatusaidia, sikupata tabu sana katika kukamilisha maswala usafiri wa ndege.Siku ya pili tukakusanya kila kitu kilicho chetu kwenye hoteli ambayo tunaishi, tukakodi Tanksi hadi uwanja wa ndege, muda wa kupanda ndege ulipo wadia, tukaungana na wasafiri wengine na kuingia ndani ya ndege, na taratibu safari ikaanza, huku moyoni mwangu nikimuomba Mungu atufikieshe salama, kwani kumbukumbu za ajali iliyo tokea nchini Kenya kipindi nikitokea Afrika Kusini, inaendelea kuzunguka ndani ya kichwa changu kama mkanda wa filamu.Phidaya kwa kudeka muda wote kichwa cheka amekilaza kifuani mwangu, huku akiimba nyimbo za kunibembeleza kwa sauti ya chini
"Baby" Nilimuita kwa sauti ya upole
"Mmmmm"
"Naomba niende msalani"
"Sawa, ila usichelewe mume wangu"
Phidaya alinijibu taratibu huku akijinyanyua, kifuani kwangu taratibu, nikasimama, na kuanza kupiga hatua za kuelekea chooni, nikaingia ndani ya choo na kumaliza haja zangu zote, nikanawa uso wangu ili kuutoa uchovu na usingizi unao ninyemelea usoni mwangu.Nikafungua mlango, gafla nikastulia kitu chenye ncha kali kikinikita mgongoni mwangu, na sauti ikasikika kutoka nyuma yangu
"Tulia kama ulivyo upo chini ya ulinzi, Mr Eddy"
****Je ninani aliye aliye muwekea Eddy kitu chenye ncha kali, mgongoni mwake, wakiwa ndani ya ndege.Ungana nami kwenye toleo lijalo*****
ITAENDELEA