Hoteli ya Sugu: Wafanyakazi wa Serikali wanavyoisaliti Serikali ya Magufuli

Sugu aliwadharau sana watendaji sasa ajipande kwenye kodi maana hawatamuacha salama ajaiita rais huku analialia kushukuru rais og.

Aliifanya mbeya yake upepo umegeuka atulie sindano iingie
Ukifuata sheria ya kodi hutababaishwa na TRA. Ninavyoamini lakini.
 
Fafa
Miswahili ni mijitu yenye roho mbaya sana. Yaani haitaki yenyewe ifanikiwe, inataka mkose wote, Basi tu wanafurahi sana wote mkiwa mafukara
Fafanua hili la Miswahili...ni watu wa Aina gani Hawa..wanapatikana wapi hapa Tanzania? Wanawakilisha Watanzania wote?!
 
Unaweza kuwa na ukweli fulani , lakini mara kadhaa Magufuli ameshangilia wapinzani kukomolewa .

Kwa Mfano , DC aliyeharibu shamba la kisasa la mboga la Mbowe kule Hai aliyeitwa Byakanwa alipewa bakhshishi ya kupandishwa Cheo na kuwa RC wa Mtwara , Magufuli mwenyewe alimsifia na kumpongeza aliyekuwa Mkurugenzi wa NHC Bilionea Mchechu kwa kuvunjilia mbali Club Billicanas iliyomilikiwa na Mbowe , hili alilifanya wakati akizindua ujenzi wa ghorofa za Magomeni .

Ninazo taarifa kwamba Serikali yenyewe ndio ilipanga njama za kubomoa hotel ya Sugu Mbeya ili kummaliza kiuchumi , maana inafahamika kwamba siku yoyote utakapofanyika uchaguzi huru Sugu anarudi bungeni , sasa baada ya kubaini kwamba hotel ile imejengwa kihalali kwa nyaraka zilizonyooka ndio wakaona kuivunja kutaharibu taswira ya nchi kwa wawekezaji wengine , ndio maana unaona Chalamila kaja na kinachoitwa maagizo ya Rais .

Ninayo mengi sana kuhusiana na njama hii ya Hotel ya Sugu na njama zingine kuwahusu wapinzani na hasa Chadema , ila kwa leo naishia hapa
 
Hili sakata la kutaka kufunga Hoteli ya Sugu huko Mbeya limeleta hisia nyingi.

Lakini baya zaidi ni lile la the dark side ya watu fulani ndani ya Serikali...
Serikali ya Tanzania haitaki wazawa wawe matajiri, hii ni moja ya Sera ya chama tawala tokea enzi za Nyerere.

Ndio maana unaona kila mzawa anayechipukia kuwa tajiri serikali lazima impige figisu kumdhoofisha.

Ila ikiwa mhindi fresh Tu hamna Noma!

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Mwezako sugu alikuwa nashukuru rais kuwa yeye amefuata sheria
Magufuli ndiye aliyetaka kuvunja hiyo hotel lakini alipoona anazomewa kila kona akabadilisha nia yake na kumtuma Chalamila apooze hasira za wananchi!
 
Wanaiga tabia yake
 
Hao ndio wanaowaabudu weupe na kukandamiza weusi wenzake.Nakumbuka marehemu Mengi aliandamwa sana weusi wenzake hawakupenda awe tajiri!
 
Hii mechi iko halftime tu, huko mbele yatakuwa makubwa zaidi, tabia ya panya huuma na kupuliza.

Sugu angekuwa na akili kubwa apauze tu, akawekeze kwingine.
Kweli nyoka anauguza kidonda akipona atakuja na hasira,naunga mkono auze huu utawala sio.
 
Hao ndio wanaowaabudu weupe na kukandamiza weusi wenzake.Nakumbuka marehemu Mengi aliandamwa sana weusi wenzake hawakupenda awe tajiri!
Tuwataje kwa majina waliomuandama Mengi.
Na je wao wametajirika?
 
Roho mbaya inaanzia kwake . kumbuka aliwahi kuapa kuwa atahakikisha matajiri watageuka kuwa mashetani.
Huu nao ni ujinga mwingine unaoishushia JF heshima yake. Kauli ya rais ilikuwa very specific ni watu gani aliwalenga. Ingekuwa general kihivyo asingefanya vitendo kama vipe kumpa Bakhresa shamba la ekari elf 10 bure. Hizi ID za kificho zinatoa uhuru watu kupost ujinga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…