Hotuba ya Jenista Mhagama wakati wa mkutano wa WHO Africa huko Brazaville

Teuzi za Tanzania zinategemea unasmile vipi kwa wakubwa, nashangaa yule jamaa wa "Samia awabubujisha machozi wamasai" hawamuoni kabisa
Dogo aelewi somo binafsi nishamwambia mara kadhaa hao watu wana pita pita humu na hawawezi kuchukulia serious kwa mambo yako ya chit-chat na uwezi waongopea kama una ID’s kutwa zinachangia ujinga.

Kwa tabia zake za JF nilishamwambia sehemu pekee wanaweza muonea huruma na kumpachika ni ndani ya chama maana ata hoja za msingi nje ya uchawa hana. Sasa nimeona uzi kapewa shavu kwenye chama kama kuna ukweli au la hatajua mwenyewe na mungu wake.
 
Hapana mbaya.... ni sawa na Amb. Chen Mingjian Balozi wa China hapa nchini, au Amb. Yasushi Misawa Balozi wa Japani hapa nchini; wanavyojikakamua kuongea kiswahili. Tofauti huku kwetu huwa tunacheka, lakini hapo naona anapigiwa makofi maana wanasilikiza maudhui ya hotuba na siyo lafudhi ya mtoa hotuba.
 
Hao watu wakiongea wanakuwa wanajua kasoro lafudhi. Huyu wetu angetumia tu Kiswahili kama kile anachotumia kuombea miongozo bungeni, ingefaa sana.
 
Huyu ni wa ...Utamaduni na Michezo huko.

Aliyekwambia wanaojua Kiingereza hawalambi asali nani!?
Nadhani sisi kasumba ya kutawaliwa na wakoloni bado inatusumbua sana. Wenzetu China, Urusi, na nchi zingine za Asia zilizopiga hatua kimaendeleo hawasumbuki kabisa na suala la kiingereza. Viongozi wao kwenye mikutano yote mikubwa wanatumia lugha zao na wakalimani na wakati kiingereza nacho wanakijua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…