Hotuba ya Mbowe: Huwezi ukaiandika historia ya Lowassa ukaacha kuitaja CHADEMA. Ni kujidanganya kuua historia ambayo huwezi kuiua

Hotuba ya Mbowe: Huwezi ukaiandika historia ya Lowassa ukaacha kuitaja CHADEMA. Ni kujidanganya kuua historia ambayo huwezi kuiua

WASIFU WA LOWASSA UNAMUELEZEA ALIWAHI KUTIA NIA YA KUGOMBEA URAIS CCM LAKINI HAIMUELEWEZEI ALIWAHI KUGOMBEA URAIS CHADEMA

MBOWE ANAWACHANA LIVE NA KUWAAMBIA HAWAWEZI KUIFUTA HISTORIA YA LOWASSA KWAMBA ALIWAHI KUWA MJUMBE WA CC-CDM NA KUGOMBEA URAIS CHADEMA
 
Kuna haja gani ya kuficha kitu ambacho kinajulikana?
Huwezi ficha kitu kinachojulikana ila unaweza usikizungumze na kutokizungumza hakutakifuta.
Kwani mkisema aligombea kupitia chadema mtapungukiwa nini?
Kwani wakisema wataongezewa nini? Hakuna logic yoyote kwenye kuumizwa na kutokutajwa chadema katika wasifu wa EL.
Ona sasa dk 5 tu mtu kaharibu sifa zote mlizozitaka.
Binafsi sioni kilichoharibika sababu hakuna kilichosemwa katika hizo dk 5 ambacho hakikujulikana kabla.
 
Historia ya Marehemu huidhimishwa na familia kipi wanataka kiwepo kwenye Risala na kipi kisiwepo

Mbowe kasimama na mihasira na CCM na Serikali na Familia kuwa Mbona kwenye Historia hawajaweka kuwa alikuwa Chadema

Wwenyewe Familia wameamua hivyo

Huu unaitwa ujinga wa kipaji, kama baba Yao angekuwa rais kupitia cdm wangeacha kuandika kwasababu sio Kila kitu kinawekwa kwenye historia?
 
Kuna haja gani ya kuficha kitu ambacho kinajulikana? Kwani mkisema aligombea kupitia chadema mtapungukiwa nini?

Ona sasa dk 5 tu mtu kaharibu sifa zote mlizozitaka.
Kama kinajulikana na Kila mtu Kuna haja Gani ya kukisema na kulazimisha kusema? Si kinajulikana.

Siku zingine jifunzeni protocol wasifu wa marehemu familia hushirikishwa Kuna vipengele waweza taka visiwepo mfano Mbowe akifariki wasifu hautamuka kuwa ana mke mwingine nje Joyce Mukya na kazaa naye.Familia itagoma pamoja na kuwa ni kitu Kiko wazi
 
Na kwenye shukrani familia inawatambuwa wengi na Kwa kipekee mama Samia, ila jina la Kikwete halijatajwa popote, Huyu Mzee ajitafakari atubu mapema kabla hajafa.
JK bora angekufa kabla ya Lowasa, maana msiba huu utampa sonona mpk atakufa.

Naona mpk amedhoofika ndani ya siku 5 hizi. Watu wamemnanga mno.
 
Kama kinajulikana na Kila mtu Kuna haja Gani ya kukisema na kulazimisha kusema? Si kinajulikana.

Siku zingine jifunzeni protocol wasifu wa marehemu familia hushirikishwa Kuna vipengele waweza taka visiwepo mfano Mbowe akifariki wasifu haitatamuka kuwa ana mke mwingine nje Joyce Mukya na kazaa naye.Familia itagoma pamoja na kuwa ni kitu Kiko wazi
Kuwa mgombea urais aliyeweka record ni kitu cha kuficha? Unatumia kitu gani kufikiria mkuu?
 
Historia ya Marehemu huidhimishwa na familia kipi wanataka kiwepo kwenye Risala na kipi kisiwepo

Mbowe kasimama na mihasira na CCM na Serikali na Familia kuwa Mbona kwenye Historia hawajaweka kuwa alikuwa Chadema

Wwenyewe Familia wameamua hivyo
Ambacho huelewi ni nini? Tunakosoa risala haijalishi nani kaandaa. Kusema aliwahi kutia nia CCM halafu ukaacha kusema aligombea urais na kupata 30%+ unaona ni matumizi ya akili?
 
Monduli sio Longido tafadhali!

Kati ya hotuba nzuri zilizojaa busara, ujasiri, ukweli na weledi wa kisiasa basi ni hii ya leo kule Monduli ambapo Mheshimiwa Freeman Mbowe amezungumza juu ya ukweli wa maisha ya kisiasa ya hayati Lowassa.

Hotuba hii iliyojaa ujasiri na umahiri mkubwa imegusa watu wengi na kujikuta wakipiga makofi mengi kwa Mh Mbowe. Mbowe amemtaja Lowassa kama mgombea urais wa CHADEMA aliyeipaisha demokrasia ya nchi na kuwaweka wapinzani katika ramani mpya ya siasa, kuwezesha wabunge zaidi ya 120 wa upinzani na madiwani zaidi ya 2,000 kutoka upinzani ikiwa ni karibu nusu ya madiwani wote nchini.

Mbele ya rais Samia na viongozi wakubwa kote nchini, Mbowe amehoji kwanini ukweli huu unafichwa? Huu ni unafiki wa kisiasa na Mbowe ameonekana kusikitishwa na kukasirishwa na unafiq huu mkubwa. Mbowe amemtaja Lowassa kama mhanga wa mifumo hovyo ya kidemokrasia nchini.

Hongera sana Freeman Mbowe kwa ujasiri huu!

Hotuba nzuri mno
 
Huwezi ficha kitu kinachojulikana ila unaweza usikizungumze na kutokizungumza hakutakifuta.

Kwani wakisema wataongezewa nini? Hakuna logic yoyote kwenye kuumizwa na kutokutajwa chadema katika historia ya EL

Binafsi sioni kilichoharibika sababu hakuna kilichosemwa katika hizo dk 5 ambacho hakikujulikana kabla.
kilichoongezeka ni kuwavua nguo wajinga wachache walioacha kutaja historia muhimu ya marehemu. What a shame? Yaani alikuwa waziri mkuu wa nchi then mtu analeta mambo ya uCCM na uCDM? Ni ujinga spana kama hizi zinasaidia machawa kukaa sawa.
 
Usikute hayo ndio mabwege yaliyoandaa risala
Hawa maboya huwa nawashangaa sana, yaani anataka kunambia mafanikio ya kuwa sijui mwenyekiti wa maasai sijui ya wapi ni kubwa kuliko kuongeza viti vya ubunge bungeni?

mbaya zaidi difference ndogo ya kura iliyotaka kubadili mfumo wa siasa anasema isitajwe, these guys kuna kitu hakipo sawa.
 
Kama kinajulikana na Kila mtu Kuna haja Gani ya kukisema na kulazimisha kusema? Si kinajulikana.

Siku zingine jifunzeni protocol wasifu wa marehemu familia hushirikishwa Kuna vipengele waweza taka visiwepo mfano Mbowe akifariki wasifu hautamuka kuwa ana mke mwingine nje Joyce Mukya na kazaa naye.Familia itagoma pamoja na kuwa ni kitu Kiko wazi
Sote tunajua kwamba alikuwa waziri mkuu mbona imesemwa? Sema ukweli japo unauma
 
Back
Top Bottom