Hotuba ya Warioba Bungeni Dodoma: Jumanne, Tarehe 18 Machi 2014 na Hoja ya Muungano wa Serikali Tatu

Hotuba ya Warioba Bungeni Dodoma: Jumanne, Tarehe 18 Machi 2014 na Hoja ya Muungano wa Serikali Tatu

Natamani ile ndege ya Malaysia ingekua imewachukua na hawa wabunge wa bunge la katiba and Nape & the company.
 
Mwenyezi Mungu azidi kumsimamia na kumlinda katika yote kwa kuendelea kwake kusimama na kunena ukweli.
Ahsante sana mkuu kwa kuiweka humu jamvini hotuba hiyo. Hakika wengi walikuwa wanaiulizia sana
 
Cheki Pinda anavyowalambisha wenzake magarasa, kumbe ofisi yake imeshapendekeza serikali Tatu, lakini kwenye media anajifanya eti msimamo ni serikali mbili.
 
Ni sawa mkuu, makosa ya rais nimeyaeleza katika mchango wangu awali. Nakubaliana na wewe kwa sehemu kubwa. Kabla ya kujadili Katiba mpya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sharti tueleze wazi kuwa Zanzibar wamevunja Katiba. Wakubali kuwa wamevunja Katiba. Pili waelezwe athari za kuvunja Katiba ni kuvunja Muungano. Sasa kama wana nia ya dhati ya kudumisha Muungano wafute vipengere vinavyovunja Muungano. Kama hawakubaliani na hilo, basi waondoke kwenye Bunge Maalum ya Katiba kwa kuwa wao tayari wana Katiba yao. Maadamu wanasema Serikali ya Tanganyika imejificha ndani ya Serikali ya Muungano na wakaona suluhu ni kujitungia Katiba yao in maana moja tu! Katiba inayojadiliwa sio yaona haiwahusu. Wakiri kosa kiisha warudi kwenye mstari. Sielewi kwa nini CCM wanajifanya wazalendo huku wanachukia vitendo vya wenzao wa Zanzibar.
Kama ni viongozi wamekosea waambiwe ukweli pasipo Kificho. Unaposema Warioba ni Genius, kwa sababu amewapa mtego viongozi waliotufikisha hapaili watatue wenyewe tatizo hili. Sio kweli. Viongozi walioshindwa kuliona tatizo wakati wa kutunga Katiba ya Zanzibar watawezaje kutata tatizo gumu hili pasipo kuuvunja Muungano? Utampaje swali lenye mtego mwanafunzi wako wakati wa mtihani wa mwisho? Utamfundisha lini kutegua mtego asio uweza na hajafundishwa?Warioba ni kama mchezaji hodari wa kupiga chenga, lakini hana uwezo wa kufunga gori.
Unajua timu ya Warioba haikutakiwa kukosoa katiba yetu ya muungano au ile ya Z'bar. Kazi yake ilikuwa ni kuleta rasimu ya katiba mpya. Mazingira aliyoyaeleza au uliyoyataja ni sawa na yale ambayo pia hata yeye aliyatoa kwa wananchi. Hayo ni msingi wa rasimu yake.

Waliozembea ni viongozi wa CCM, ni Rais. Wakati Z'bar wanafanya hayo Rais alikuwa wapi? just laughing! Warioba hana kosa lolote! anajuwa kilichotokea lakini vyombo vya kuhangaika na hayo vipo. Yaani una Rais ambaye aliona kabisa sehemu moja ya nchi ikijitangazia kuwa ni nchi na serikali yake, yeye akanyamaza kimya!

Nami namsifu Warioba ni genius! Ameweza kuwaacha waliotengeneza maovu watatuwe wenyewe na yeye ameleta rasimu ili tupate katiba mpya. Sasa hao wapuuzi waliko Bungeni kukataa eyi kwa sababu Nape kasema, hao ndo wanaotugawia ujinga, ili nchi nzima iwe ya wajinga.
 
Inaoenaka CCM tukiwa peke yetu na tukiwa sehemu siri tunataka serekali 3 tukiwa mbele ya vyombo vya habari na watu tunataka srekali 2.
hapa ni wazi ndani ya CCM kuna tatizo.

KWANINI NIMESEMA HIVI


Kama tulivyomsikia Jaji warioba. Sehemu muhimu ndani ya serekali wamependekeza serekali 3.
Kwa mfano afisi ya waziri mkuu, afisi ya makamo wa rais. hizi kama sitakosea zimependekeza muundo wa serekali 3. Hizi ni Ofisi nyeti ambazo kazi yake ni kutatua kero za Muungano.kama zimependekeza muundo wa serekali 3 ni wazi kwamba kuna tatizo.
Hapa CCM tumeshika hatamu. Hapa kuna makatibu wakuu licha ya kutokwa watendaji wa Chama lkn wengi wao ni wakereketwa wa Chama. wakurugenzi na hata mawaziri wote hawa ni Chama chetu.
Kama haya ndio mapendekezo ya ofisi hizi mbele ya jaji Warioba ni wazi CCM pia inataka serekali 3 nyuma ya pazia lkn mbele ya vyombo vya habari inataka serekali 2.
Ofisi ya Bunge na ofisi ya baraza la wawakilishi. Hili kwa kiasi kiikubwa ndio wawakilishi wa wananchi. Kwa mujibu wa warioba hawa pia wamepndekeza serekali 3. hapa CCM imejaa.hapa ndipo alipo spika wa CCM , hapa ndipo penye wenyeviti wa CCM wa kamati za Bunge.Mapendekekezo haya yanaushawishi mkubwa kutoka ccm.




HII NI SEHEMEU YA MAPENEDEKEZO YA TAASISI ZA SEREKALI


103 .Baadhi ya taasisi za kiserikali, ama moja kwa moja au kwa tafsiri ya
mapendekezo yao, pia zilipendekeza au kukubali muundo wa Serikali Tatu. Kwa
mfano, Baraza la Wawakilishi Zanzibar lilipendekeza kuwepo kwa mamlaka huru ya
Zanzibar, mamlaka huru ya Tanganyika na mamlaka ya Muungano na iwekwe wazi maeneo, uwezo, nguvu, utendaji na mipaka ya kila mamlaka. Baraza la Ofisi ya Makamu wa Rais lilipendekeza, kuhusu Muundo wa Serikali kwamba, nanukuu
"kuwe na Rais mmoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wakuu wa Serikali za Washirika wa Muungano wapewe vyeo vingine 32 vinavyoendana na hadhi na mamlaka zao. Pia katika kutaja hizo serikali tatu inabidi zitenganishwe ili Serikali ya Muungano ionekane ndio ya juu"

104. Baraza la Ofisi ya Waziri Mkuu lilipendekeza, kuhusu uongozi wa taifa kwamba kuwe, na "Rais wa Jamhuri ya Muungano, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, Waziri Mkuu wa Serikali ya Tanganyika na Waziri Mkuu wa Serikali ya Zanzibar. Mapendekezo hayo ni kwa sababu hakuna umuhimu wa kuwa na marais watatu (3) katika nchi moja na wala neno Rais halimuongezei hadhi kiongozi yeyote. Pia kutoa nafasi kwa Mawaziri Wakuu kuwa watendaji zaidi na hivyo kusimamia Serikali za Washirika." Aidha, Bunge la Jamhuri ya Muungano katika maoni yake
lilipendekeza kuwepo kwa Tume ya Utumishi wa Bunge ambayo o inajumuisha, katika Wajumbe, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano (Mwenyekiti), Spika wa
Bunge la Tanzania Bara na Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar.



nA NDO MAANA WANAOOMBA KURA YA SIRI WANATAKA KUWATISHA WALE WENYE MLENGO WA KUTAKA SERIKALI TATU NDANI YA CCM
 
Warioba alizidi nifurahisha alipowaambia maCCM kuwa ..sheria iliiwekea mipango TUME ILA HAKUNA ILIPOWAWEKEA WANANCHI MIPAKA NA HIVYO wakatafsiri kuwa wananchi walitakiwa waseme kila kitu kwa uhuru na hawakuwa na mamlaka ya kuwazuia. Hii ilikuwa mwima kwa maCCM waliopiga debe ktk vipindi vya dkk 45 na vingine kuwa tume iliweka maawzo yao wenyewe...JK atajilaumu sana kuwa hakuona hilo...tunaojua fikra za CCM n akukumbuka walichosema kwa fahari hata waliposhtuliwa kuwa wamepotoka..tulikuwa tunayaona maumivu makali sana kwa werema, na maccm yote.

Mkuu kwa maelezo haya yaliyoshiba ya baba yetu jaji WARIOBA sitashangaa kama ijumaa tutapewa udhuru......
 
Inaoenaka CCM tukiwa peke yetu na tukiwa sehemu siri tunataka serekali 3 tukiwa mbele ya vyombo vya habari na watu tunataka srekali 2.
hapa ni wazi ndani ya CCM kuna tatizo.

KWANINI NIMESEMA HIVI


.............................................[snip] Kwa mfano afisi ya waziri mkuu, afisi ya makamo wa rais. hizi kama sitakosea zimependekeza muundo wa serekali 3. Hizi ni Ofisi nyeti ambazo kazi yake ni kutatua kero za Muungano.kama zimependekeza muundo wa serekali 3 ni wazi kwamba kuna tatizo.[snip] ......................


Kwa nini unasema kuna tatizo? Mtu asiyeamini hayo ndo ana tatizo. Ofisi inayotakiwa kuangalia na kutatua kero za muungano ikisema serikali 3 ujue ndo mbinu ya kutatua kero za muungano! tatizo liko kwa mtu kama Nape anayeambiwa mbinu za kuondoa kero yeye anakataa na kusema msimamo wa chama ni huu. Who or what is chama?

Chama kinafanywa kuwa ni kitu cha kipuuzi, kinachosema mampo ya hovyo hovyo tu! Hiyo haikubaliki kabisa!
 
nimeangalia tv na kumsikiliza jaji warioba vizuri sana. Tume yake imefanya kazi nzuri sana na mwiba kwa wanasiasa si wa ccm tu hata wa upinzani. Wanasiasa hawaipendi hii rasimu ya kuelekea katiba kamili,kisa ni wengi waliwekeza huko ili baadaye wapate marejesho manono.nimeziangalia sura za wenye vyama vya siasa ingawaje vinaitwa vyama vya wananchi,walikuwa wamekunja nyuso zao mithili ya mtu anayemeza sumu. Wanasiasa hawa wamemwaga mamillioni kwenye vyama na kujaribu kutumia nguvu kubwa ya kupata madaraka, katiba inayotakiwa na wananchi ndio warioba kaitilia mkazo kuliko yanayotakiwa na wanasiasa. Na sina hakika kama bunge hili litakwisha salama,maana hii rasimu inafanyiwa kila aina ya vioja,vitimbi na hujuma ili isifanikiwe.

sijui nikupe zawadi gani, umehit point mkuu!!!
Asante sana
 
Sasa wabunge wa bunge la katiba baada ya kusoma haya yote muache unafiki wa kichama, mfanye maamuzi magumu kwa maslahi yetu sote. Nitawashangaa Wazanzibar kufanya unafiki kwenye jambo hili. Kila kitu kiko wazi na Warioba hakumumunya maneno!
 
Inaoenaka CCM tukiwa peke yetu na tukiwa sehemu siri tunataka serekali 3 tukiwa mbele ya vyombo vya habari na watu tunataka srekali 2.
hapa ni wazi ndani ya CCM kuna tatizo.

KWANINI NIMESEMA HIVI


Kama tulivyomsikia Jaji warioba. Sehemu muhimu ndani ya serekali wamependekeza serekali 3.
Kwa mfano afisi ya waziri mkuu, afisi ya makamo wa rais. hizi kama sitakosea zimependekeza muundo wa serekali 3. Hizi ni Ofisi nyeti ambazo kazi yake ni kutatua kero za Muungano.kama zimependekeza muundo wa serekali 3 ni wazi kwamba kuna tatizo.
Hapa CCM tumeshika hatamu. Hapa kuna makatibu wakuu licha ya kutokwa watendaji wa Chama lkn wengi wao ni wakereketwa wa Chama. wakurugenzi na hata mawaziri wote hawa ni Chama chetu.
Kama haya ndio mapendekezo ya ofisi hizi mbele ya jaji Warioba ni wazi CCM pia inataka serekali 3 nyuma ya pazia lkn mbele ya vyombo vya habari inataka serekali 2.
Ofisi ya Bunge na ofisi ya baraza la wawakilishi. Hili kwa kiasi kiikubwa ndio wawakilishi wa wananchi. Kwa mujibu wa warioba hawa pia wamepndekeza serekali 3. hapa CCM imejaa.hapa ndipo alipo spika wa CCM , hapa ndipo penye wenyeviti wa CCM wa kamati za Bunge.Mapendekekezo haya yanaushawishi mkubwa kutoka ccm.




HII NI SEHEMEU YA MAPENEDEKEZO YA TAASISI ZA SEREKALI


103 .Baadhi ya taasisi za kiserikali, ama moja kwa moja au kwa tafsiri ya
mapendekezo yao, pia zilipendekeza au kukubali muundo wa Serikali Tatu. Kwa
mfano, Baraza la Wawakilishi Zanzibar lilipendekeza kuwepo kwa mamlaka huru ya
Zanzibar, mamlaka huru ya Tanganyika na mamlaka ya Muungano na iwekwe wazi maeneo, uwezo, nguvu, utendaji na mipaka ya kila mamlaka. Baraza la Ofisi ya Makamu wa Rais lilipendekeza, kuhusu Muundo wa Serikali kwamba, nanukuu
"kuwe na Rais mmoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wakuu wa Serikali za Washirika wa Muungano wapewe vyeo vingine 32 vinavyoendana na hadhi na mamlaka zao. Pia katika kutaja hizo serikali tatu inabidi zitenganishwe ili Serikali ya Muungano ionekane ndio ya juu"

104. Baraza la Ofisi ya Waziri Mkuu lilipendekeza, kuhusu uongozi wa taifa kwamba kuwe, na "Rais wa Jamhuri ya Muungano, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, Waziri Mkuu wa Serikali ya Tanganyika na Waziri Mkuu wa Serikali ya Zanzibar. Mapendekezo hayo ni kwa sababu hakuna umuhimu wa kuwa na marais watatu (3) katika nchi moja na wala neno Rais halimuongezei hadhi kiongozi yeyote. Pia kutoa nafasi kwa Mawaziri Wakuu kuwa watendaji zaidi na hivyo kusimamia Serikali za Washirika." Aidha, Bunge la Jamhuri ya Muungano katika maoni yake
lilipendekeza kuwepo kwa Tume ya Utumishi wa Bunge ambayo o inajumuisha, katika Wajumbe, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano (Mwenyekiti), Spika wa
Bunge la Tanzania Bara na Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar.

asante, mtajua tu muda si mrefu kikwete ni nani
 
Cheki Pinda anavyowalambisha wenzake magarasa, kumbe ofisi yake imeshapendekeza serikali Tatu, lakini kwenye media anajifanya eti msimamo ni serikali mbili.

huo utakuwa ni wa kwake binafsi, sio wa ofisi yake!
 
Back
Top Bottom