Hotuba ya Warioba Bungeni Dodoma: Jumanne, Tarehe 18 Machi 2014 na Hoja ya Muungano wa Serikali Tatu

Hotuba ya Warioba Bungeni Dodoma: Jumanne, Tarehe 18 Machi 2014 na Hoja ya Muungano wa Serikali Tatu

Rai wa nchi nyingine aruhusiwe kwenda kupiga kura na kugombea uongozi popote hii nayo imekaaje kisheria.

Muhimu hapa sio kupiga kura au kugombea tu,swala hapa ni kuwa muungano uwe na wa wananchi wa pande mbili,wananchi wa Tanzania.Na kwa muungano huo Mtanzania(Mzanzibar au Mtanganyika) bila kujali asili yake ni wapi ndani ya Tanzania ataruhusiwa kuishi popote atakapopapenda,na kwa kuwa mkazi wa huko ataruhusiwa kupiga kura au kupigiwa kura kwenye nafasi yoyote atakayohitaji.Ndio maana kwa nchi kama Marekani watoto wa Baba mmoja George Bush Sr mmoja alikuwa Gavana wa Texas (George W Bush ) na mwenzake akawa Gavana wa Florida (Jeb Bush) au George Romney kuwa Gavana wa Michigan na mtoto wake Mitt Romney kuhama huko na baadae kuwa Gavana wa Massachusetts. Kama kweli tumeungana basi asili yako ni wapi sio muhimu bali muhimu ni ukazi wako tu.Ni kama vile tusivyoshangaa leo mmasai kugombea ubunge Chalinze vivyovivyo isiwe ajabu kwa Mgogo kuwa mbunge wa Chakechake au Muunguja kuwa Mbunge Kagera,ni Mtanzania.
 
warioba ni jembe, huyo sendeka hana lolote kazi kupayukapayuka tuu, anafikiri yuko simanjiro na wamasai wenzake,nimeangalia sana hili bunge kuanzia mwanzo kupitisha kanuni sendeka alikuwa msumbufu sana ,tungekuwa na kiranja angemwandika kwenye orodha ya wasumbufu akapewa adhabu.yeye yuko kichama zaidi na siyo ki utaifa.

STOP TRIBALISM!...Usimhukumu kama Masai, mhukumu Kama OLESENDEKA..
 
Warioba the greatest , float like a
butterfly and sting like a bee.
 
Hiv maccm kwa ujumla wake mbona yalikuwa yamununa sana?

Je hayakujiandaa kuusikiliza ukweri japo mchungu kwao? Nilimuona msaliti zito muda mwing alikuwa anatingisha kichwa kutokukubaliana na nondo za jaji walioba.

Tumsubili ole sendeka sijui atakuja na ngonjeta gani na kujifanya yy mzalendo kuliko jaji walioba na wajumbe wote wa tume. Ila leo maccm yameumbuliwa yamechwa meupe.
 
Mowapo ya hoja za gwiji .
.. Zanzibar ni nchi, ina mipaka yake, bendera na wimbo.' Kwa maneno rahisi anasema ' Zanzibar imevunja Katiba ....
Mimi binafsi ningemwita Warioba mtu mwoga wa kuwambia ukweli Wazanzibar kuwa wametunga katiba inayokiuka Katiba mama. ...
Warioba ni mwoga kumwambia JK KUWA NI RAIS DHAIFU kwa kufumbia macho Zanzibar ilipokuwa inatunga Katiba inayokinzana na Katiba kuu. ... Uwoga unaubatizaje kwa jina UGWIJI?

Umeandika maneno mengi sana kuelezea uoga wa Jaji Warioba. Sote tuliomsikiluza Jaji Warioba tunajua kuwa hajamung'unya maneno. Amesema wazi kabisa kuea Katiba ya znz imevunja katiba ya JMT. Kwa kuzingatia umoja, amani na mshikamano ndio maana tume ikaona busara iliyopo ni kuwa na serikali tatu. Sasa kwa nini hilo linamtoa Jaji Warioba kuwa GWIJI?
 
VIVA Warioba...ndio nakubali degree za sheria za zamani zilikuwa nzuri..ila huyu mzee sijui hata km anajua kupiga cross na mwenzie Ramadhani ndio balaa kabisa walikuwa wakimwaga kila kitu bila kujua kuwa CCM ni mashetani walikuwa wakiungua sana na ho moto,na wanaogopa mwanga km kunguni na chawa.
 
Warioba na tume yake wanastahili pongezi hasa kwenye serekali 3.Simuelewi kwenye uraia mmoja wakati nchi ni 2.pia raia wa kila upande waweze kutumia huduma sawa wakati uchangiaji si sawa?unyonyaji wa Tanganyika!
.. Observation nzuri sana Mkuu.
 
WARIOBA ALIPOOMBA KWENDA KUPUMZIKA NIKAJUA ANAKUJA MALIZIA GAME.Aliwaacha maCCM wazidi kuwa confused kwa fikra zao wenyewe, na kudigest alichotangulia kisema.Halafu akaja piga score za mwisho...
 
Jamani naomba umnipe updates za asubuh kuhusu uwasilishwaj wa rasimu ya katibu. Vipi warioba ametiliamkazo kweye yap? Plz help me friends.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Warioba bhana, Pinda ni waziri mkuu wa muungano but hajawahi kwenda zanzibar kukagua mambo ya kimaendeleo vile vile kwa Jakaya, Pinda anachomoa macho tu.. warioba noma sana
 
attachment.php
 
MKUU SISI TUNAO SOMA mnachoandika mnatuchanganya. Mkuu Setuba Noel ameandika hivi......Kasema muungano wa serikali mbili waliotuachia waasisi sio huu wa sasa. waasisi walituachia nchi moja yenye serikali mbili, siyo nchi mbili zenye serikali mbili. Babu anaua kinoma.

SASA wewe umesema kinyume, so who is saying what na nani amemnukuu Warioba vizuri....Nchi moja serikali mbili ama nchi mbili serikali moja?

Watu wako so excited kwa nondo za warioba mpaka wanajichanganya. Ulichoandika wewe ndicho alichikisema warioba. Tuliachiwa nchi moja serikali mbili; sasa tuna nchi mbili serikali mbili, na hili limevunja katiba ya JMT.
 
Warioba ni mtu makini nakubaliana nae kwenye huu mchakato wa Katiba yetu.

Nashukuru kaka Ritz, tuko pamoja, tumeelewa nini Rasimu imetoa, na kuwa muundo ule uliopendekezwa ni maoni ya wananchi na mfumo wake ukawekwa sawa na tume, na lengo ni kulinda pia Muungano, serikali2 kwa sasa haiko kama zilivyoachwa na waasisi!
 
WARIOBA ALIPOOMBA KWENDA KUPUMZIKA NIKAJUA ANAKUJA MALIZIA GAME.Aliwaacha maCCM wazidi kuwa confused kwa fikra zao wenyewe, na kudigest alichotangulia kisema.Halafu akaja piga score za mwisho...

Alienda kupiga kiki dah
 
Back
Top Bottom