Ahsante Kichuguu kwa kuliona hilo, aksante.
Zaidi ya Mkapa na Vithlani, hakuna kichwa kinachotafutwa Tanzania kikajibu shutuma za ubadhilifu kama kichwa cha Andrew Chenge.
Zitto Kabwe, mbunge kiongozi wa upinzani, ameenda kuwaambia wananchi kwamba kwa kushirikiana na Ephraem Mrema aliyeilipisha TANROADS Sh bilioni 3.3 kwa kampuni illegal ya Norconsult na Zhakia Meghji aliyesaini makaratasi ya Billal wa EPA, Andrew Chenge amewajengea mabarabara!
Kana kwamba kina Zhakia Meghji na Chenge walifanya hisani kutoa hela, hela zinazopita kwa idhini ya Bunge.
Unalalamika Buzwagi, Buzwagi, Buzwagi halafu wakina Chenge waliosaini mikabata unaenda kuwauza kwa watu? Unasimama mbele za wananchi wenye disapointment na frustration unataja ``Chenge`` kwa ufahari kabisa?
Labda ni Waganda walikasirika mwaka '79 wakatutafutia dawa, au Wakenya walinyunyiza kimiminika na helikopta ili tupwelee tuwaachie ardhi, lakini kuna mkono wa mtu, hatuwezi kuwa wazima. Anamsifu Chenge hadharani?