Hotuba yangu jimboni Kigoma

Hotuba yangu jimboni Kigoma

Hapo kusifia mimi binafsi sio tatizo lakini mbona wale wa upande ule wakisifia wanaitwa majina mengi sana?

Mfano Lowasa kafanya mambo kushughurikia maji ya ziwa victoria,hapa kosa aje mtu wa ccm amsifie kwa hilo.

Na hata hivyo mimi siamini na wala sitaki kuingia kwenye mkumbo wa kusifia watu wanaapotekeleza 1/1000 ya majukumu yao.

Nahisi itafikia kumshukuru mwalimu kwa kuingia darasani kufundisha kipindi chake

Mie huwa nashukuru wazazi wangu kwa kunizaa......

MkamaP, hizo shukurani maana yake ni kuwa wale wasio nazo basi na wao wafahamu kuwa mambo yako hivi na nyie mkichachamaa, basi mtajengewa. Kama Mwakyembe alijengewa na daraja na wanajeshi akajisifu kuwa ni yeye kajenga na hata hakusema Asante kwa Mwamunyange mkuu wa JWTZ. Mhhh, sasa hivi nasikia JWTZ wanasema kuwa hilo daraja mwakani kabla ya uchaguzi litahitajika sehemu nyingine muhimu saana zaidi ya Kyela. Sasa wewe prove kuwa ni KYELA linahitajika zaidi.
Katika nchi yenye matatizo mengi, ni wanasiasa wanaamua kipi kiwe wapi. Wakikupa si vibaya ukasema asante. Kama wameweza kuchota pesa BoT pale walipohitaji, wanaweza kufanya lolote lile walipendalo. Hapa Zitto alitumia UBAVU wake wa Mkono kwa mkono. Chenge kapata hela nyingi na yeye akatiwe 10% kwa ajili ya wananchi wake.
 
Sina wasiwawasi kwamba Mh. Zitto ni mchapakazi! Tena sana.

Ila Du! nimehudhunishwa na ugongwa ule unaosema Mbunge anafanya mambo fulani fulani kama Mbunge. Eti wabunge wanajenga zahanati, wanajenga shule, wanajenga barabara... etc. etc. na waliopongezwa mawaziri kupeleka barabara
Yaani kwa nchi yetu hakuna appreciation yoyote ya wataalamu wa mawizara na halmashauri... ati wabunge/mawaziri ndio wanaofanya.

oooo pu!!!!

Kasheshe,

Ukiangalia kisheria SI KWELI kuwa Wabunge/Mawaziri/TANROADS wanaojenga. Hii ni kama Dodoma ni mji mkuu ila mambo yote kasoro Bunge yako Dar. Sasa wapi ni MAKAO MAKUU?

Viongozi wanakuwa na hela mkononi. Wao ndiyo wanaamua zijengwe wapi. Sehemu za kujenga zipo kibao. Kama ningelikuwa mie ndiyo waziri wa ujenzi, ningeliweka LAMI kiwanja cha ndege Tabora, kujenga barabara ya LAMI kutoka Nzega hadi Tabora na kuja Sikonge na ipitilize hadi Mbeya. Nikaweka barabara zote za Tabora Lami, maji, umeme, nk na kwengine huko kwa akina Zitto nikakusau na acha wafe na njaa au giza. Sasa mtu atakepigania kwa udi na uvumba hadi zile pesa ziende kwake, huyo ndiyo KAJENGA. Pesa kwenye majimbo haziji tu. Zahanati haziji tu. Umeme, maji na takataka nyingine haziji tu. Ni lazima UPIGANE ili zije. Mtu akipigana hadi zikaja, ukitaka unaweza kusema KAZIPIGANIA ila kisiasa twasema "KAJENGA".
 
Mnyonge Mnyongeni, Haki yake Mpeni!.
Hongera sana Mh.Zitto kwa changamoto zako Bungeni na uliyoyafanya jimboni mwako.
Pia nakuunga mkono ulichofanya kushukuru ni muhimu, huo ni uthibitisho kuwa wewe ni mtu unaekumbuka fadhila.
Shukrani ni jambo jema, haijalishi anayeshukuriwa amefanya mabaya mangapi, hata kama ana mabaya mia moja na jema moja, anastahili shukrani kwa hilo jema moja na shutuma kwa mabaya mia.
Angalizo, wote aliowashukuru, hakuna hata mmoja mwenye tuhuma zozote, labda ni shutuma tuu, kama ni suala la shutuma, hata hao wapiganaji wa ufisadi nao wanazo shutuma lukuki na wengine ni mafisadi walifisidi wakapata pesa, sasa wanapinga ufisadi.
Tusihukumu tusije tukahukumiwa.
Hongera tena Zitto, ila kwa hili la Uenyekiti, mimi Mh....
 
..hii hotuba ina mambo mengi sana positive ya kuangalia.

..kuna suala la soko la kahawa ambalo Zitto anadai amefanikisha.

..kuna msaada kwa vijana wasiokuwa na uwezo ambao anawasaidia kupata masomo.

..vijiji vimepimwa na kupewa hati ya ardhi.

..binafsi naelewa msimamo wa Zitto ktk masuala ya kitaifa, na nilikuwa namsubiri kwa hamu atueleze jinsi anavyoshughulikia masuala ya wananchi wa Kigoma-Kaskazini.

..sote tunapaswa kukumbuka kwamba bila wananchi wa Kigoma-Kaskazini kumchagua Zitto kuwa mbunge huenda wengi wetu tusingemjua ktk harakati za kupigana na mafisadi.
 
kitendo tu cha kukaa na kujadili hotuba ya Zitto tu; kunaonyesha jinsi gani alivyo mbali sana ya wengi wetu humu.Kama kuna kosa kwa mawazo ya mtu fulani basi si kosa kwa Zito na kwa watu wengine.

Inabidi na nyie muandae zenu tuzisome, after all huyu ni Kijana tu!

acheni LOW MIND!

Kama mna hasira hivyo hata nyumba zenu za kupamga za mafisadi hameni!
 
Mnyonge Mnyongeni, Haki yake Mpeni!.
Hongera sana Mh.Zitto kwa changamoto zako Bungeni na uliyoyafanya jimboni mwako.
Pia nakuunga mkono ulichofanya kushukuru ni muhimu, huo ni uthibitisho kuwa wewe ni mtu unaekumbuka fadhila.
Shukrani ni jambo jema, haijalishi anayeshukuriwa amefanya mabaya mangapi, hata kama ana mabaya mia moja na jema moja, anastahili shukrani kwa hilo jema moja na shutuma kwa mabaya mia.
Angalizo, wote aliowashukuru, hakuna hata mmoja mwenye tuhuma zozote, labda ni shutuma tuu, kama ni suala la shutuma, hata hao wapiganaji wa ufisadi nao wanazo shutuma lukuki na wengine ni mafisadi walifisidi wakapata pesa, sasa wanapinga ufisadi.
Tusihukumu tusije tukahukumiwa.
Hongera tena Zitto, ila kwa hili la Uenyekiti, mimi Mh....

Bado napinga suala la Zitto kutoa shukrani. Hivi mnataka tuwashukuru hata wakoloni kwa kuwa waliweza kujenga vishule, vijizahanati, reli na vijibarabara wakati wanatutawala? Hivi kweli ni halali kumshukuru mtu ambaye amelihujumu taifa au hata kama anashutumiwa tu - lisemwalo lipo la sivyo kwa nini ashutumiwe Chenge na wengine katika kundi la Watanzania lukuki?
 
Hongera Zitto .Mie naishia hapa kwa ufupi tu .Hongera sana na kazana urudi mjengoni Kaka .Unapigana vita kubwa ambayo wengi hapa ni maneno tu hata mtaani kujitokeza kuelezea umuhimuwa Waraka wana ogopa ila nguvu yao kuandika hapa .Nakubaliana na MkamaP kukubali kuto kubaliana na yote ni maoni jamani .
 
Watanzania ...hatuwezi kujieleza, halafu tuna a very complex communication system.

Kuelewa hiyo kauli ya Zitto inabidi uelewe culture yetu, hii culture inayomfanya mtu anayekufa na cancer kitandani akiulizwa unajisikiaje ajibu "najisikia vizuri".Kuna mambo fulani ambayo ni crucial sana -kama kum acknowledge mtu kama Chenge, regardless ya alichofanya- kwa sababu za ku play Mr. Nice Guy.This has more to do with our culture than Zitto personally.

Mimi nilifikiri watu tulivyoisema hotuba ya Zitto iliyomshukuru profusely Waziri Mkuu Pinda bila ya kuwa na sababu ya msingi, Zitto alielewa hii concept.

Lakini Bluray, unajua ubovu ya hiyo nadharia kwamba ni utamaduni wetu, kwamba ni aina yetu ya mawasiliano, ni kuwa kuelewa maana halisi ya kinachosemwa kinakuwa ni kubahatisha. Zamani nilifikiri mimi ndio sielewi walengwa - wananchi - wanaelewa, kumbe si peke yangu. Ingekuwa ni culture tungekuwa tunaelewana.

Sasa cheki, wewe hapo umesema ulivyoelewa alichotaka kusema. Lakini angalia huyu mchangiaji mwingine makini sana alivyoelewa yeye, au anavyomwombea Zitto msahama:


MkamaP, hizo shukurani maana yake ni kuwa wale wasio nazo basi na wao wafahamu kuwa mambo yako hivi na nyie mkichachamaa, basi mtajengewa.

Ushaona tafsiri ya huyu Mkuu hapo? Anasema Zitto alikuwa anaongea na watu wa majimbo mengine, sio audience iliyoko mbele yake! Upo?

Kwa hiyo, kila mtu anatafsiri kivyake, wengi tuna struggle kujaribu ku make sense of it, what was he trying to do lavishing praise on Andrew Chenge, tena akiwa katikati ya ngome ya upinzani, Kalinzi, ndani mwisho wa reli huko kwenye grassroots za CHADEMA ambako wanajaribu kujenga chama, vijijini. Unaenda kumhimidi Chenge!

Halafu angalia Zitto anavyowasiliana. Anasema CCM hawana mpango wa kujenga mabarabara ya lami, lakini anasema Chenge na Meghji na Mrema na Bukuku "walielewa tatizo letu... walitenga fedha...wamehakikisha tunajenga mabarabara ya lami"!

Mimi nawaambia viongozi wenzangu, mnapaswa kuwauliza ni wapi ndani ya Ilani ya CCM wameahidi kujenga barabara ya Mwandiga - Manyovu kwa kiwango cha lami?. Hakuna!
__________________________________

Napenda nimshukuru kwa dhati kabisa aliyekuwa Waziri wa Miundombinu ndugu Andrew Chenge na Katibu Mkuu ndugu Enos Bukuku kwa msaada mkubwa walionipa kuhakikisha tunajenga barabara hii kwa Lami. Napenda kumshukuru aliyekuwa Waziri wa Fedha ndugu Zakia Meghji kwa kuelewa tatizo letu na kutenga fedha

Kha!

Kumbe Chenge na Meghji ni chama gani, CUF?

Zitto aliwahi kuleta hapa draft ya speech anayokwenda kuitoa Bungeni, alikuwa kamwagia sifa Pinda, akaulizwa Pinda kafanya nini huyo, baada ya muda akaelewa somo, akaki edit out kile kipande, hakikufika Bungeni. Leo anaenda kumwinua Andrew Chenge mbele ya watu wa CHADEMA. Yeye anadhani ni political decency and maturity, wakati Chenge hakuna anaetaka kumsikia. Kama anampenda Chenge akanywe nae chai huko, pembeni huko, na akiona tunapita afunike kombe, na akimalizana nae asije kumsujudia sujudia Chenge mbele yetu.
 
..binafsi nadhani wa-Tanzania tuko too negative.

..kila kitu tunaona hakiwezekani, everybody is not good enough na lazima tumtoe kasoro na kumkatisha tamaa.
 
MkamaP,
Mkuu wangu Zitto hakuwasifia Chenge na Meghji, ila kawashukuru kwa msaada wao. Tatizo la watu wengi wa CCM wanataka wananchi tuamini kwamba Mkapa alikuwa kiongozi mzuri, Lowassa, Chenge na mafisadi wengine wote ni viongozi wazuri hapa ndipo tunapogongana..kwani yapo matukio ambao tunaweza kuwasifia kina Lowassa ila tusiwapambe kuwa wao ni wasafi, viongozi wazuri kwa kutumia mifano hiyo. hapa wasomaji tutakuwa tunaitazama picha kubwa zaidi ya fadhila ndogo waliyoifanya.
Na mwisho mkuu wangu tanzania itabidi Umsifie mwalimu aliyehudhulia darasani kwa sababu nchi nzima ni kama vile ina Union iliyogoma..wee fikiria kuna Union ya walimu walogoma toka Nyerere alipoachia ngazi na contract haijaainiwa tena..Mkuu wangu elimu Tanzania sasa hivi ni deal ambalo hata nchi tajiri duniani haziwezi kuishi kama sisi. Nadhani Tanzania tuna lead duniani kwa kuwa na elimu ghali kuliko US, UK Canada aui nchi zote kubwa za Kibepari!..Sasa nambie utaachaje kumsifia mwalimu wa bure anapoingia darasani sii kama vile umeona Malaika wa Mungu akiingia..
Elimu ya Tanzania siku hizi wanasema ni negotiable! utaipata kwa uwezo wa mfuko wako yaani mind concept ya watu ni kwamba fedha inaweza kununua Elimu!

Mkandara
Wenda mie ndio sielewi kwa hiyo usichoke kunielewesha si unajuwa elimu hakukwishi.

sasa mkuu nataka uniwekee haya mambo mawili bayana la kwanza ni wakati gani na mazingira yepi kitu unachopewa kinaitwa msaada.?

La pili ni wakati gani na mazingira gani mtu hustahili pongezi kwa zao alilotenda?
 
Ogah,
Mkuu wangu tafadhali!...Swala la kuwapongeza Chenge na mama Meghji ni ustaarabu mkubwa hata kama watu hawa ni mafiisadi kwani Zitto hakupokea fedha toka mfuko wa mafisadi hao ila shukran anazitoa ni Upande wa pili wa wahusika hao hao kiutendaji kazi.

unajua fika kwamba ktk lugha ya ustraabu ya kisiasa ni lazima Zitto atoe shukran zake kwa viongozi waliokuwa madarakani na walimsaidia kuwezesha yaliyopatikana.
Ubunge Tanzania mkuu wangu ni Utumwa wa kimawazo, utalazimika kumwomba shetani kwa ajili ya watu wako kwani ukikaa mbali na mawaziri au taasisi zinazohusika na ahadi ulowapa wananchi wako mkuu wangu utakesha.

Kwa maana kwamba Ukienda Zimbabwe na ukapokelewa na Mugabe itabidi umshukuru Mugabe ktk hotuba zako mahala popote kwa fadhila zake..Kuna watu nawafahamu sana waliwahi kuishi kwa Idd Amin na wanamsifia ajabu kwa yale alowawezesha wao na sehemu zao siwezi kuwaita wajinga kwa sababu ya historia kubwa ya Idd Amin..kwani mkosefu hapa ni Idd Amin kwa madhambi aloyafanya na sii ukisha kuwa fisadi basi imekuwa laana kwa wote..

Ni wajibu wa CCM kupanga mikakati ya maendeleo ya Tanzania nzima, lakini ni watu wanaofikisha maendeleo hayo kwa wananchi hivyo haijalishi kuwa ni Chenge au Mwandosya aliyeshika mpini.. kumbuka tu ni yule aloyeshika mpini ndiye mwamuzi wa jembe litakita wapi ili upate kupandikiza mbegu..na wakati huo Chenge na Meghji ndio walioshika mpini, amsifie nani zaidi ya ukweli?..

Kisha Kisiasa ni lazima Zitto atambue WATU ktk MAZINGIRA.. wananchi wote (watu) ni ktk NDIVYO TULIVYO, ambao ni Reflection ya Viongozi wao..hapa ni lazima utumie lugha wanayoielewa wao..kuwa hata mwizi kama anajenga kwao huyo ni shujaa.
Kisha mazingira ya Kigoma na kutambua Ni majuuzi tu Pinda aliondoka jimboni hapo akijisifia kuwa ni serikali yake iliyowawezesha..Ni chama CCM kilichowawezesha kupata barabara hiyo, hivyo Zitto ni lazima awaambie wanannchi hatua alizochukua yeye hadi kufikia mafanikio ya barabara hiyo hata kama kuna mkono wa shetani. Ndio Ukweli na siku zote msema ukweli ndiye kipenzi cha Mungu kuliko Pinda anayeweza kupindisha Ukweli kwa wananchi ili mradi tu kumchafua Zitto.

Ndio hiyo Tanzania yetu babu, sasa hivi ni mateso matupu, na ukibahatika kupata afueni ya kusikilizwa ama kaupendeleo kama hako shukuru Mungu. Binafsi nampongeza sana Mh. Zitto kwa kuwa mfano bora kwa wananchi, Kwa sababu tumeipata hotuba hii hata kabla yeye mwenyewe hajaiweka hapa..na wala sii mara ya kwanza kupata hotuba za Zitto akiwa Kigoma.

Ni Ashirio moja kubwa sana kwetu kuwa Zitto anajali sana maslahi ya wananchi wake na hakika naweza sema sijaona Hotuba ya mbunge wala kiongozi mwingine yeyote ktk jimbo lake. Kwa hiyo tumpeni sifa zake...hakuna mbunge mwingine aliyefanya hivi na kwa Zitto sii mara ya kwanza kiasi kwamba tumeweza kufuatilia safari zake jimboni kwake na Tanzania nzima kuliko hata viongozi wa serikali tawala.
Mkandara, Bob, Swahiba,
Hakuna siku ambayo umeni-bore kama hii!
Sorry, we are friends, but what zitto said is really cheap diplomacy seeking reverage (levelage check spellings) among the people in power, his cronies in his party (we might know what they think), mafisadi etc. It never cookes, this guy spoke the best about corruption, he made us into it, we are discussing it. We already onto it!

One thing, does he know politics, opportunities and loopholes? What do you want to buy by praising the corrupts? This enterprets we still have loopholes in opposition who cannot seize the opportunities, but can act as stoog(ies) for SisiM. I don't trust this boy satements, and I am par with Dilunga!!

We have long way to go achieving democracy!!
 
..binafsi nadhani wa-Tanzania tuko too negative.

..kila kitu tunaona hakiwezekani, everybody is not good enough na lazima tumtoe kasoro na kumkatisha tamaa.

Si hivyo, hii inaitwa analysis.Saa kwa sababu hatujazoea critical analysis hiki ni kitu kigeni kwetu.

Tunahitaji hi zaidi, zero tolerance.
 
Mie huwa nashukuru wazazi wangu kwa kunizaa......

MkamaP, hizo shukurani maana yake ni kuwa wale wasio nazo basi na wao wafahamu kuwa mambo yako hivi na nyie mkichachamaa, basi mtajengewa. Kama Mwakyembe alijengewa na daraja na wanajeshi akajisifu kuwa ni yeye kajenga na hata hakusema Asante kwa Mwamunyange mkuu wa JWTZ. Mhhh, sasa hivi nasikia JWTZ wanasema kuwa hilo daraja mwakani kabla ya uchaguzi litahitajika sehemu nyingine muhimu saana zaidi ya Kyela. Sasa wewe prove kuwa ni KYELA linahitajika zaidi.
Katika nchi yenye matatizo mengi, ni wanasiasa wanaamua kipi kiwe wapi. Wakikupa si vibaya ukasema asante. Kama wameweza kuchota pesa BoT pale walipohitaji, wanaweza kufanya lolote lile walipendalo. Hapa Zitto alitumia UBAVU wake wa Mkono kwa mkono. Chenge kapata hela nyingi na yeye akatiwe 10% kwa ajili ya wananchi wake.

Kuna mcameroon hapa aliniuliza plan yangu ipo je ? nikamwambia niko mbioni kurudi nyumbani ,akazidi kuniambia are u mad? nikamwambia kwanini akasema me better to suicide than going back .Nikamuuliza kulikoni??
Kasema cameroon kusainiwa karatasi lako inabidi utowe bribe and top of that itakubidi kushukuru kwa jamaa kuipokea bribe yako.
 
Niliandika:{MkamaP, hizo shukurani maana yake ni kuwa wale wasio nazo basi na wao wafahamu kuwa mambo yako hivi na nyie mkichachamaa, basi mtajengewa. Kama Mwakyembe alijengewa daraja na wanajeshi akajisifu kuwa ni yeye kajenga na hata hakusema Asante kwa Mwamunyange mkuu wa JWTZ. Mhhh, sasa hivi nasikia JWTZ wanasema kuwa hilo daraja mwakani kabla ya uchaguzi litahitajika sehemu nyingine muhimu saana zaidi ya Kyela. Sasa wewe prove kuwa ni KYELA linahitajika zaidi}


Ushaona tafsiri ya huyu Mkuu hapo? Anasema Zitto alikuwa anaongea na watu wa majimbo mengine, sio audience iliyoko mbele yake! Upo?

Dilunga,
kuna kitu kinaitwa REFERENCE. Unaweza kufanya kitu kwa kutumia mfano wa mtu mwingine ambaye alifanya kitu kama hicho au kinachofanana tu. Sasa ukishatumia REFERENCE ya mtu fulani, ina maana huyo mtu alipokuwa akifanya au akiandika au akivumbua basi alivumbua kwa ajili ya watu wengine?
Zitto kaonyesha jinsi alivyo-LOBBY. Nilitegemea kila mtu mwenye akili yake atakuwa ameliona hilo kuwa "mwenzetu Zitto kafanya hivi, basi na sisi akili kichwani". Wewe unakuja unasema kwa sababu mie nimeliona hilo na kuandika basi nimebadili maana kwa kuonyesha kuwa alikuwa anaongea na wabunge wengine.

Kuna wakati huwa kweli unaamsha hoja kwenye NEGATIVEs zako. Ila hili naona leo limekukalia kushoto. Au tafute makala nyingine au kajipange upya maana naona umeDANDIA KWA MBELE na limekutupa pwaaaaa!!!!

Dillunga, sasa naamini kuwa wewe ni mtu yule asemwaye:
1. Nilisikia wakiambiwa usinywe Pombe na kuendesha gari, ila kwa kuwa sikuwepo kwenye mkutano nikajua hilo mie halinisihusu.
2. Nilisikia akiwaambia kuwa kuna gonjwa na tujilinde, mie kwa kuwa sikuwepo kwenye mkutano, nilijua mimi hilo halinihusu.
3. Nilisikia wakiambiwa kuna Tsunami inakuja, ila kwa kuwa sikuwepo kwenye mkutano, nilijua mimi hilo halinihusu.

4. Nilisikia Zitto akiwaambia jinsi alivyo-Lobby. Kwa kuwa Dilunga(mbunge) mie sikuwepo kwenye mkutano , nilijua mimi hilo halinihusu.
 
Mh Zitto

Unaonaje hotuba zako ukazikusanya na kuweka kwenye kitabu kimoja ili iwe kumbu kumbu hata kwa vizazi vijavyo?
 
Kuna mcameroon hapa aliniuliza plan yangu ipo je ? nikamwambia niko mbioni kurudi nyumbani ,akazidi kuniambia are u mad? nikamwambia kwanini akasema me better to suicide than going back .Nikamuuliza kulikoni??
Kasema cameroon kusainiwa karatasi lako inabidi utowe bribe and top of that itakubidi kushukuru kwa jamaa kuipokea bribe yako.

MkamaP,

Kwenye SIASA mambo yako hivyo mkuu. Ukisikia mtu anasema mie sintampigia magoti fulani kwa kuwa yeye ni BIG MAN basi ujuwe magoti yake hadi yameota SIJIDA kwa kuyapiga. Heri ya Zitto kakiri waziwazi waliomsadia. Ila ya Cameroon ni kali maana hata kutoa Hongo inabidi uandike OMBI? Likikubaliwa ndiyo unatoa na hapo unapotoa unapiga magoti kuomba Mungu jamaa asibadili mawazo. Akipokea asante nyingi sanaa.

MkamaP, field ya Civil Engineering ukubali au ukatae, ni field moja ambayo MAFISADI wanaipenda sana. Kule kuna PESA na utafiti wake ni mgumu sana hasa kama wala 10%. Inapofika sehemu kwamba zipo pesa kidogo na mahitaji mengi, wakikupa wewe na kuendelea kumsahau Mkandara na Sikonge, basi inabidi uwape ASANTE. Kumbuka wengine tulipiga pia magoti na kuomba tutowe Hongo ila tukakataliwa vilevile. Matokeo yake Ukerewe na Sikonge ni Ndugu mmoja. Vipi kule kwenu, ile lami aliacha Nyerere bado ipo au ndiyo kuna mashimo kama vile mwajiandaa kujenga mahandaki?
 
Mh Zitto

Unaonaje hotuba zako ukazikusanya na kuweka kwenye kitabu kimoja ili iwe kumbu kumbu hata kwa vizazi vijavyo?

Duuu,

Yaani una maana kuwa hata vizazi vijavyo watakuwa kama sisi? Kumbe hii historia ni kweli:
Mao Zedong, JKN na Borris Yeltsin wameenda kwa Mungu ili kuuliza kule kwao hali itakuwaje in future:

1. Mao Zedong akaambiwa kuwa China inakwenda safi sana baada ya miaka 100, inakuwa super power duniani kwa kila kitu.

2. Borris Yeltsin akaambiwa Russia mambo yatakuwa bomba baada ya miaka kama 150 hivi.

3. Alipokuja Nyerere na swali hilohilo, Mungu akamwangalia na bila kusema neno akaanza kulia.
 
Back
Top Bottom