Hotuba yangu jimboni Kigoma

Nashindwa kabisa ku post topic mpya?how?

Chagua jukwaa unalotaka kuanzishia post mpya. Kisha ukiangalia juu kabisa (kuelekea upande wa kushoto wa page yako), kuna sehemu ya kuanzisha new thread.

Bonyeza hiyo kisha utapata page ya kuandikia new thread yako.
 
Mkuu umeeleweka.

Nilikuwa na mkuu mmoja wa sisi M hapa wakati nasoma hii thread ansema wewe ni tishio kwao.
😀
Mimi nakukubali mkuu. wewe uko juu. Hawa ndugu zako wasipokuelewa watakufa maskini vinywa wazi.

Wakupe tu ubunge tena bila kupingwa! Vyama mapinduzi sijui havitawatoa.
 
Sometimes tunahitaji kuweka mukhtasari wa habari au hotuba yenyewe ,na ingekuwa vizuri kama hotuba nzima ingekuwemo kwenye pdf file attached ,wengine tukisoma msusuru wa habari basi tukifika katikati yale ya mwanzo huwa hayapo tena ,inatokana na kasi ya kusoma,ila hongera Mheshimiwa Zitto kwa kuwaweka sawa wananchama na zaidi wambie ikiwa utanafasika kuwahutubia tena kuwa ,Chama ni wananchi na si viongozi,kwani viongozi wanaweza kuhama hama au kurejea CCM au kukisaliti Chama kama tulivyoona kwa baadhi ya viongozi wa kutegemewa katika kambi ya upinzani ,hivyo wao wananchi ndio wadau wakuu wa vyama vya upinzani.

Mwenyezi Mungu akipenda muumalize mkutano wenu kwa salama usalimini na mpate baraka za mwezi Huu mtukufu wa Ramadhani kwani nia zenu ni kuwakomboa na kuwatetea wanyonge popote pale walipo hapa Tz na Pemba.
 
siasa ni mchezo mchafu, lakini Zitto anapoelekea sio, naona yupo bize sana kuwasafisha hao jamaa wenye network ya DOWANS, kwa "kuwasifia" hao jamaa sisi unatuachia maswali mengi mno maana sasa hivi hali ya kisiasa ipo kwenye transition ya kugawanyika mafungu mawili Mafisadi na wasio.

Kwa hiyo hata wa upinzani nao pia wapo kwenye huo mchakato wa upepo wa kisiasa, unaweza ukawa unawasafisha wenzio huku wanakuachia matope na maji yameisha,
kwa hao jamaa (Chenge at el) kutoa na kusimamia huo mradi ilikuwa ni wajibu wao na wala hawakustaili kushukuriwa wala kusifiwa hao walikuwa wametimiza wajibu wao.

Lakini kama kulikuwa hakuna fungu la huo mradi na wewe ukaforce mpaka ukapata hilo fungu kwa mlango usio sahihi nadhanin sasa huko bize kulipa fadhila, na kwa mwelekeo munaoenda itakucost sana kulipa hizo fadhira, reputatuion yako itakuja kuondoka kabisa, maana ulitupa wasiwasi sana kwenye issue ya DOWANS, kwa ule msimamo wako wa kifisadi, nadhani pia ilikuwa ni kulipa fadhira sasa sijuhi ni hizi za hii barabara au ni nyingine.

Time will tell, muda wa shinikizo ukifika nadhani utakuwa wazi zaidi ya sasa ambapo unaingia na kutoka
 


Hongera Zitto na Wana Kigoma Kaskazimi chini ya CHADEMA
 
Mheshimiwa Zitto,
Hii hotuba ni ya lini? maanake naona tarehe hapo chini kidogo imenishtua... au ndio makosa ya uchapishaji.
 
Ahsante kwa yote mpambani wetu, hakika Jamii tunajivunia kuwa na kichwa kama wewe pale mjengoni. Mungu akuzidishie uhai ili tuendeleze mapambano ya kumkomboa mtanzania
 
Mheshimiwa Zitto,
Hii hotuba ni ya lini? maanake naona tarehe hapo chini kidogo imenishtua... au ndio makosa ya uchapishaji.

nafikiri ni tarehe ya kuandaliwa na sio ya kuwasilishwa...!!! Hotuba ndefu namna hio inahitaji muda kuiandaa...otherwise utakuwa mbabaishaji tu mbele za wananchi...!!!
 
Zitto unajitahidi sana. Nimeangalia CV kumbe ulisoma Galanos, hata mimi nilisoma Galanos Form 5 (1994-1995) kabla ya kuhamia Tambaza 1995. Mimi zitto naona kitu kimoja ambacho ningekuomba ufanye zaidi ni kuangalia mbali na haya ni mambo ambayo naomba ufanye

1) Pigania elimu ya watoto, cable imeshakuja ya internet lakini bila elimu kazi haziwezi kuja Tanzania mfano. Rafiki yangu alinieleza alipata tender ya kuweka software PPF sijui inaitwaje siku hizi lakini alikuwa hana wataalamu wa kutosha.
2)Usisahau Vijana wa nje sio kwenye mijadala tu. Tunaomba ututangaze tunavyosaidia nchi kwa kutuma pesa. Vilevile tupigie debe la uwekezaji na hata kazi kwa vijana waliosoma na wanataka kurudi. Sio lazima kila kitu kiwe siasa.Mfano vijana tunasumbuliwa bandarini hata kama tumeleta vifaa na mashine za maendeleo tungetakiwa tupongezwe hata kidogo basi.
3) Maendeleo mengi ya Watanzania ni bila msaada wa serikali. Watu wemejenga lakini hakuna barabara, mikoani hata kigoma kwa mfano hakuna barabara za uhakika. Watanzania wakiwekewa barabara wataendelea wenyewe. Mfano vijana kuja nje serikali haijasaidia chochote no mwamko wa Watanzania wenyewe hivyo barabara ikiwekwa watanzania wataweka mwamko wa maendeleo.
4)Productivity Tanzania inatatizo moja la kufanya kazi bila statistics. Kama tanzania ikiweka statistics za maendeleo kama shule, kilimo, afya itakuwa rahisi kwa serikali kufanya maamuzi. Mfano kama kilimo cha umwagiliaji kinafanikiwa Arusha ni kwanini kisifanikiwe sehemu nyingine kama kuna data ya vitu wanavyofanya Arusha ni kwa nini zilipelekwe mikoa mingine. Kwanini msichukue data za shule zinazofanya vizuri mfano watoto wa shule record zao, walimu, mazingira ya kusoma n.k na kuzipeleka sehemu ambazo shule zinafanya vibaya na kuzibadilisha. Nilishafanya project ya shule za Texas ili kujua ni kwanini shule zinafeli kwa kutumia Benchmark methodology data kama hizo tulipewa grant ya $3million. google APQC (America Productivity and Quality Cnt).
Sitachukuwa muda wako mwingi lakini usisahau vijana wa nje na jibu email.
 
nafikiri ni tarehe ya kuandaliwa na sio ya kuwasilishwa...!!! Hotuba ndefu namna hio inahitaji muda kuiandaa...otherwise utakuwa mbabaishaji tu mbele za wananchi...!!!
Sidhani kwa sababu kuna mengi yaliyotokea baada ya tarehe hiyo yamo ktk hotuba hii..Bila shaka ilitakiwa isomeke mwaka 2009 badala ya 2008, Mh. Zitto sii mchovu kiasi cha kutayarisha Hotuba mwaka mzima.
 

Bwana Sikonge naona unajichanganya,

Hapo juu kabisa umeonesha ubaya wa lobbying, kwa kuonesha miundombinu ikiwekwa kwa kufuata mipaka ya kisiasa. Na bahati nzuri au mbaya mwaka 2006 nilipita kule Mbeya, sikufanya utafiti wa kina lakini ktk mazungumzo ya kawaida na wenyeji wangu waligusia hili la umeme kuwekwa kisiasa na matokeo yake TANESCO kuingia hasara baada ya kutandaza mtandao lakini wateja hakuna!

Nadhani ktk larger picture huwezi ukakubalina na lobbying halafu then ulalamike jimboni kwako Sikonge hakuna maendeleo. Kumbuka hali hiyo imejitokeza kutokana na watu wenye influence ku-lobby na ku-pertubate funds zilizotakiwa zigawanywe kwa kutumia formula inayokubalika na kusababisha maeneo kama Sikonge et al kukosa funds.

Sijui kama umenipata.
 
Ahhhhh. Nimechoka kabisa.

Kwa maandiko yaliyoko huku ndani, hawa watu wanaoitwa mafisadi wameshasikilizwa na kukutwa na hatia na tayari wamehukumiwa. HII SI SAWA hasa ukizingatia kuwa hapa ni mahali pa watu wanaofikiri kwa kina.

Kuna mambo mengi na pengine karibu yote katika hotuba ya Mheshimiwa yanatakiwa kuthibitishwa hasa na wale wanaotoka kule kigoma. Hapa ndipo nilipotegemea hoja nyingi zaidi kutika kwa wana jf. kuliko kuwashukuru waliochangia kwenye safari ya yeye kufanikisha malengo yake.

Sidhani kama kuna ubaya wowote katika kushukuru kwake, tatizo liko mahali hapa, wana jf wengine wanataka mafisadi wote wasipewe tena nafasi ya kutajwa popote lakini naamini mafisadi hawa hawajsikilizwa? labda kwa sababu za kimfumo au kwa makosa ya watanzania wenyewe.

Ushauri
Kuna haja ya kuiambia sarikali ya CCM na Hasa JK, kama mafisadi watuhumiwa hawatafikishwa mahakamani na wao KURA HAWATAPATA. Dilunga ukija na hoja hii nitakuunga mkono.
 

Mkuu Abdulhalim,

Naona hukunielewa nilitaka kusema nini. Ukweli siku zote wanasema uko katikati. Ndiyo maana nikakuonyesha sura zote mbili. Lobbying inaweza kufanyika kwa manufaa au ikaleta hasara. Wakati wa Nyerere sijui kuna mtu ali-lobby basi na sisi tukapata kiwanda cha nyuzi pale Tabora mjini. Kile kiwanda kilikuwa kikitegemea mali ghafi kutoka Shinyanga na Mwanza. Kilikuwa kwa kutegemea malighafi zitoke mbali namna hiyo. Hapohapo karibu na kiwanda kulikuwa na kambi ya JKT ndogo ikiitwa Miyemba ambayo ilikuwa chini ya Msange JKT. Palikuwa na mashine kubwa la kupasua mawe. Ila mlima ulikuwa mbaaali na hamna roli la kuleta mawe na matokeo yake eti kuruta kama 20 ndiyo wanaenda kutafuta mawe na kuyaleta pale. Alipokuja Makame akaamuru ule mtambo upelekwe Mwanza sehemu ilipo milima/mawe mengi na demand kubwa.
Kama mie nakuwa Rais, nina Lobby na kupata kiwanda cha kuzalisha umeme na wakati huo makaa ya mawe au Gas inatoka Kyela/Songa si itakuwa wendawazimu? Huku ndiyo ku-lobby kwa kuleta umeme na wakati huo watumiaji hamna.
Kwa Sikonge kama nikijenga mtambo wa kutengeneza funiture kama za Ikea na watu wanaenda kuziunga wenyewe majumbani, itakuwa jambo la muhimu sana hasa ukichukulia tuna mbao nyingi pale na tunaexport nje ya mkoa/nje ya nchi MAGOGO. Ningelijenga kiwanda cha kusindika Asali. Ningelijenga kiwanda cha kuzalisha mafuta nk . Hivi ndiyo vitu kwa sasa Sikonge wanaweza kusema wanahitaji kwa nguvu. Kiwanda cha Sigara kama kingelikuwepo hapo basi ile Tumbaku yote ya Sikonge/Tabora ingelikuwa inatengenezwa hapo Sigara na hapo tunauza product na si mali ghafi. Watu wangu wanapata kazi na si kwenda kuwapa wengine kazi.

Mwisho kama nilivysema. Lobby ipo, upende usipende. Ila inategemea una lobby nini. Nenda Iraq na Afghanistan uone wauza silaha na vifaa vya usalama duniani wakiwa kazini. Wanahaha kuwezesha bidhaa zao zinunuliwe. Hii ndiyo sheria ya uchumi. Kama wanunuzi ni wachache na bidhaa ni nyingi, wenye bidhaa AKILI KICHWANI. Hapo ndipo nasema, Zitto katufungua macho kuwa ukichagua MBUNGE "kiwete" basi kazi mnayo.
 


I couldnt say it more!

Jamani hivi kweli dunia ya leo kuna politics bila lobbying? ulizia Marekani..Senator akiwa Chairman wa Committee..ndo jimbo lake limeula. Wazee mpaka wanatoana machozi kwa kugombania uenyekiti wa kamati...Kifupi ni kwamba politics na lobbying ni vitu ninaendana. Sema tu kama alivyoeleza muungwana Sikonge. LAZIMA U-lobby kwa kufuata priority. Na ndo tatizo letu sisi Tanzania. Unakuta Mtu ana lobby kujenga international Airport Arusha..wakati in less than 40 KMs kuna nyingine Moshi. Anashindwa kuwa creative. Una lobby kulingana na strength uliyo nayo. Hapo ndo wananchi wako watafaidika.

Leo Sikonge akiwa mbunge..ni kwamba kilimo cha Tumbaku Sikonge ndo kitakuwa kimeinuka. Unaweza lobby kujengewa kiwanda cha Sigara.

Harafu hapa mnasahau kitu kimoja. Zitto kaeleza kabisa. Wabunge wa CCM wa Mkoa wa Kigoma waliandamana kwenda kwa waziri kuzuia hiyo barabara isijengwe..kwa sababu iko kwenye jimbo la upinzani!!! Sasa jamani hiyo ni akili au ni tope??? sasa mbunge kama huyo kweli anaweza kupata hata akili ya ku-lobby kwa waziri apewe barabara? Na waziri atamuona ni buricheka.

Wanaomlaumu Zitto, nadhani wanaongea politics za kufikirika. In otherwords...wanachokiongea katika uhalisia wa siasa hakipo. Though in theory ndo tunafundishwa darasani...After all ndo maana tuna wabunge. Otherwise tungekaa bila wabunge-after all serikali ina jukumu la kuendeleza Tanzania bila wala upendeleo.

Siku hizi hata serikali za kiafrica zina-commission lobbying firms (paying them millions) huko Washington, Berlin, London nk..kuwasaidia kupata misaada kuliko nchi nyingine..au na hili hamlijui jamani?
 

Waambie, nikisema mimi itakuwa "it's just that godless Bluray"
 
Ukizungumza tena na wapiga kura wako epuka kuwafagilia mafisadi kwa namna yoyote ile. Ungeishukuru serikali kwa ujumla na sio kutaja majina kama Chenge ambayo yanatia kichefuchefu!
 
Big up Zitto, tunataka viongozi wenye hoja kama wewe, nimeisoma hotoba yako kwa umakini wa hali ya juu, umeanisha ahadi ulizotoa na jinsi ambavyo zimetekelezeka, safi sana.2015 nadhani utafaa kuchukua uraisi wa hii nchi kama ukizidi kuwa makini kama ulivyo sasa maana tumechoka na propaganda za CCM
 

Sikonge, Masanja, Bluray, Kitila, Phillemon M,Abdulhalim,

..kuna somo ambalo watu hawakulizangatia ktk hotuba ya Zitto.

..somo lenyewe ni kwamba Mbunge anapaswa ku-fight kwenye kamati za kisekta za bunge kabla bajeti ya wizara haijasomwa bungeni.

..bajeti ikishafika bungeni ni kwamba mchezo umekwisha, na ni lazima upite. kama mbunge alikuwa na masuala yake na yamesahauliwa itabidi asubiri bajeti ya mwaka unaofuatia.

..somo hilo ndilo linalonikumbusha wabunge wanaopiga makelele kila bunge la bajeti. malalamiko yao ni hayo hayo kila bunge la bajeti. hivi kwa mwaka mzima wanakuwa wameshindwa kuzungumza na ku-lobby wizarani na kwenye kamati matatizo yao yakashughulikiwa?

..halafu wabunge wa aina hiyo ndiyo wenye rekodi ya kuchaguliwa kwa vipindi vingi.
 
Nilichoambulia katika hotuba ya Mh Zitto:

(a) Anahofia upinzani kwenye jimbo lake hasa kutoka ccm na hivyo akaenda kwenye diffensive mode

(b) Akiwa anajaribu utetezi wake hotuba yake ikawa 100% reduced to Zitto vs CMM na sio Chadema vs CCM

(c) Hajakomaa kisiasa, mkomavu kisiasa kamwe hawasifii mafisadi kwa lolote. Fedha walizoiba mafisadi ni zaidi ya mazuri waliyofanya

Hitimisho: Hotuba hii ni chini ya kiwango na inanufaisha CCM kuliko Chadema. Inaonyesha woga wa Zitto dhidi ya CCM, imeshindwa kuonyesha malengo na mikakati ya Chadema kujipanua katika majimbo mengine, na kibaya zaidi inawashukuru mafisadi ambao hata CCM yenyewe haijawashukuru. Wapinzani tuna safari ndeeeeeeeeeefu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…