Mkuu,
Hilo swala lipo sana Mbeya. Kwa Mwandosya barabara na umeme huwa zinaishia kwenye mpaka wa JIMBO lake la uchaguzi. Haizidi hata cm 1.
Labda hii inabidi iwe fundisho kwa WANANCHI WAPIGA KURA kuwa mambo ya kuchagua wabunge wa kupitisha bajeti yamepitwa na wakati. Mtu kama Komba kakata viuno wee basi MNAMPA ubunge. Sasa huko aje atetee nini? Kutetea kukata viuno? Kwake yeye kuwa na Nyumba pale alipo sasa ni the dream becomes true. Sasa ukianza kumwambia maji taka yasiwepo, barabara nzuri, maji masafi, umeme, ........ kwake ya nini??
Kama Kigoma walimchagua Zitto na kutoka kwake Upinzani ame-lobb hadi barabara itajengwa, hayo ndiyo mambo sasa. Sisi hapa Sikonge tulimchagua kunguru Saidi Nkumba wa CCM, tumepata nini? Hawa ndiyo wanaitwa wasindikizaji na wagawa KURA tu. Yeye kila siku ni KUULIZA ili asikike radioni au kuuza sura kwenye TV. Jibu lolote akipewa hata la kitoto basi huwa anaridhika. Kwanza ninawasiwasi hata kama huwa anasubiri jibu zaidi ya kufurahi kuwa kafanikiwa kuuliza swali.
YES, tuchague wabunge Wazuri wa kutufanyia Lobbying BUNGENI na kutupigania haki zetu kimajimbo na kitaifa. Hebu fikiri wangelitokea akina Zitto kama 30 hivi wakaanza kugombania hilo milions za ujenzi wa lami. Hapo ndiyo ungeliona kile kinafanyika nchi kama za Korea. Zingelitandikwa humo ndani ya bunge na waziri wa Miundombini angelikuwa milele ana hali mbaya. Nisingelishangaa wengine wangekuwa wanakataa. Lakini ndiyo unakuta kwa TANZANIA hata wanalilia wapewe ..........