Hoyce Temu na Wabaguzi Mamboleo!

Hoyce Temu na Wabaguzi Mamboleo!

Mheshimiwa mwanakijiji,

Mimi nafahamu unaelewa tofauti ya mtanzania asilia na yule mzawa.

No i don't! na maneno hayo hayamo kwenye misamiati yangu. Raia wa Tanzania wanaitwa "Watanzania" hawa raia wengine wanaoitwa "Asilia na Wazawa" mimi sijui uwepo wao ndio maana nimeuliza maana.

Richa ni mtanzania mwenye asili ya Asia (Mtanzania Nusu??? M.M.) lakini kazaliwa Tanzania(uki-trace babu zake wako Asia) na mwingine anajulikana bila ubishi ni mtanzania wa kuzaliwa na kwa asili (uki-trace babu zake asili ni Tanzania).

Hawa mababu tunaenda nyuma kiasi gani? Babu wa Babu? Babu babu yake na Babu? Wairaqw wa Mbulu mababu zao wanatoka mashariki ya kati au pembezoni mwa Pembe ya Afrika, hawa ni Watanzania? Wanyakyusa asili yao ni Kusini mwa Sudan toka ufalme wa Malkia wa Kinubi hawa ni Watanzania licha ya kuwa mababu zao wanatoka Nubia? Wasukuma asili yao ni sehemu za Magharibi ya Uganda, na walihamia eneo la sasa la Tanzania miaka kama 700 hivi iliyopita, je hawa ni Watanzania nao? Wacchaga asili yao ni Niger-Congo, Wahaya nao ni hivyo hivyo! Wadigo nao ni hivyo hivyo, wahamiaji wa Tanzania, Wangoni kila mtu anajua hilo (tena Wangoni hawana hata miaka mia tatu Tanzania!), ! Na makabila mengi yote ni wahamiaji na wa eneo hilo!

Sasa mnaposema "Mzawa" ina maana ya aliyezaliwa Tanzania kitu ambacho Richa anacho, na mkisema "Asilia" ina maana ambaye wazazi wake na babu zake wamezaliwa Tanzania, Richa hata hicho anacho! Sasa, kama Richa ni Mzawa na Asilia, kwanini bado anapingwa?

Ukweli ni kuwa hamjawa na ujasiri wa kusema kile mnachotaka kusema na mnatuzungusha tu kwa euphemisms za "Mzawa na Asilia". Mnapotumia maneno hayo mna maana ya "mweusi". Kama ni hiyo maana yenu kwanini msiseme tu kuwa ushindi ungemuendea Mtanzania Mweusi, Mwafrika Mweusi? Mkisema hivyo hoja yenu inaweza kuwa na nguvu na itathibitisha tunachokisema sisi wengine kuwa tatizo lenu siyo uzawa wala asilia, tatizo lenu ni rangi!
 
Ha ha ha Wabaguzi sisi kwa kusema jamo kama tunavyoliona. Kwamba pamoja na wahindi kuzaliwa Tanzania na kuishi miaka mingi wengi wao hawaoni umuhimu wa kukijua kiswahili maana kwao wao ni lugha ya washenzi. Pamoja na kuishi Tanzania miaka chungu nzima bado wanajitenga katika maeneo maalum 'uhindini' na kamwe hawataki kujichanganya na sisi washenzi, pamoja na kuishi Tanzania miaka chungu nzima bado wanajiona wao ni bora kuliko sisi na hawako tayari kwa intermarriages kati yao na wamatumbi washenzi! lakini hili la huyo mhindi kutokuwa na sifa zozote za kupewa Umiss India...Ooops! Miss Tanzania na watu kusema ukweli wanavyoona wewe unaona ni ubaguzi! Mwe! Kazi kweli kweli na safari bado ni ndefu sana!

Pia unataka walioshiriki wamsupport huyo mhindi, kwa nini hasa alichokifanya hata wamsupport? kwa kupewa ushindi ambao washiriki wote wanajua hakustahili!? Hao wahindi lini walisimama na kuwasupport Miss Tanzania wa miaka ya nyuma? au kwa kuwa wao ni bora kuliko sisi hivyo hawana haja ya kufanya hivyo!? Acha hizo!

Kuna wengi Tanzania wasiojua Kiswahili. Bibi yangu amekufa akiwa na miaka 90+ na neno la Kiswahili alilokuwa analijua ni 'jambo' na 'habari gani' kwa lafudhi nzito ya Kisukuma!!!

Kuhusu intermarriages kati ya sisi weusi na wao; yaani wewe hili unaliona ni muhimu sana eeh? Wewe uko tayari kumuoa Mhindi?

Halafu hili la wewe kusema wao wanajiona kuwa ni bora kuliko sisi linaonyesha inferiority complex yako. Unaka-complex kakujisikia uko duni dhidi ya watu wa rangi nyeupe nyeupe (for lack of a better term)
 
Sen. Barack Obama (D Illinois)ana baguliwa na wazungu kwasababu ni mweusi na kwamba middle name yake Hussein ina connection na ugaidi. African Amercans (blacks) nao pia wanambagua ati kwa maelezo kwamba sio black enuff kwa sababu mama yake ni mzungu na msure wake alikuwa katokea kenya tena ni jaluo toka kisumu. Pia kwamba anaongea straight bila kuwa na ile accent ya ghetto........na mambo mengine kemkem ambayo hapa si ya lazima.
Kisa cha kuandika hayo hapo juu, ni katika juhudu za kuonyesha kwamba watu wakitaka kukubagua basi hawatakosa la kusema na kaupenyo ka kufanya hivyo. Issue ya wahindi Tanzania ni kubwa kushinda haka kalembo ambako pia inawezekana ni ka-victim kwa jinsi moja au nyingine ila sisi hatujui tu.
 
Ha ha ha Wabaguzi sisi kwa kusema jamo kama tunavyoliona. Kwamba pamoja na wahindi kuzaliwa Tanzania na kuishi miaka mingi wengi wao hawaoni umuhimu wa kukijua kiswahili maana kwao wao ni lugha ya washenzi. Pamoja na kuishi Tanzania miaka chungu nzima bado wanajitenga katika maeneo maalum 'uhindini' na kamwe hawataki kujichanganya na sisi washenzi, pamoja na kuishi Tanzania miaka chungu nzima bado wanajiona wao ni bora kuliko sisi na hawako tayari kwa intermarriages kati yao na wamatumbi washenzi!

Bado unazungumzia maelfu wakati mamoja yanakusumbua! Richa anaishi Uhindini? Richa hajawahi kutokea kwenye misiba ya jirani zake, Richa amewahi kusema Kiswahili ni lugha ya washenzi? Richa ajichanganye vipi zaidi na Watanzania? Kwenye mashindano ya urembo alikuwa anakula tofauti na wengine, alikuwa analala tofauti na wengine? Alikuwa akienda kwenye masuala mbalimbali na gari tofauti na wengine? We unazungumzia Wahindi miye namzungumai mhindi mmoja tu, Richa Adhia!!

lakini hili la huyo mhindi kutokuwa na sifa zozote za kupewa Umiss India...Ooops! Miss Tanzania na watu kusema ukweli wanavyoona wewe unaona ni ubaguzi! Mwe! Kazi kweli kweli na safari bado ni ndefu sana!

Kazi ipo, kwa sababu wabaguzi wamejitokeza tena kwa kisingizio cha "uzawa" na "asilia". Wabaguzi ndio wanaturudisha nyuma, na hawa ni lazima tuwaoneshe kwa rangi yao kamili, si watetezi wa Tanzania, si watetezi wa kanuni zilizojenga Taifa letu, ni wabaguzi wa rangi kama kina Botha, ni wabaguzi wa rangi kama watu KKK ni wabaguzi kama Skin Heads, ni WABAGUZI ambao sumu yao lazima ipingwe na Mtanzania yoyote yule! Na tutaendelea kuwapinga!


Pia unataka walioshiriki wamsupport huyo mhindi, kwa nini hasa alichokifanya hata wamsupport? kwa kupewa ushindi ambao washiriki wote wanajua hakustahili!? Hao wahindi lini walisimama na kuwasupport Miss Tanzania wa miaka ya nyuma? au kwa kuwa wao ni bora kuliko sisi hivyo hawana haja ya kufanya hivyo!? Acha hizo!

WAliyofanya wahindi au wasiofanya miye sijui! Nazungumzia Richa, ameshiriki mashindano mbalimbali na kushinda leo ati hastahili kuwa Miss Tanzania. Huu ni siyo tu ni ubaguzi bali ni unazi wa waziwazi! Unazi wenye kutukuza ukuu wa nasaba ya watu weusi! Ninyi wabaguzi wa rangi tutaendelea kuwapinga na kuwaumbua kuwa mnalidharirisha Taifa letu, hamna kanuni inayowaongoza, na mkipewa nafasi ya kushikiria nafasi yoyote yenye kufanya maamuzi mtaendelea kumwaga sumu yenu ya ubaguzi! Tutawapinga, na tutaendelea kuwapinga!
 
Sen. Barack Obama (D Illinois)ana baguliwa na wazungu kwasababu ni mweusi na kwamba middle name yake Hussein ina connection na ugaidi. African Amercans (blacks) nao pia wanambagua ati kwa maelezo kwamba sio black enuff kwa sababu mama yake ni mzungu na msure wake alikuwa katokea kenya tena ni jaluo toka kisumu. Pia kwamba anaongea straight bila kuwa na ile accent ya ghetto........na mambo mengine kemkem ambayo hapa si ya lazima.
Kisa cha kuandika hayo hapo juu, ni katika juhudu za kuonyesha kwamba watu wakitaka kukubagua basi hawatakosa la kusema na kaupenyo ka kufanya hivyo. Issue ya wahindi Tanzania ni kubwa kushinda haka kalembo ambako pia inawezekana ni ka-victim kwa jinsi moja au nyingine ila sisi hatujui tu.

guess what? Obama ni Seneta wa Marekani, na anagombea nafasi ya Urais na akishinda hata kama watu hawataki hawawezi kumzuia asiingie Ikulu au kumsikia Hillary analia "ohhh yaani wamarekani wameona hakuna mtu mweupe yoyote kuwa Rais wamemchagua mtu mwenye asili ya Afrika, tena siyo mzawa!"

Kwenye taifa lililokuwa na sera za kibaguzi, Obama kusimama na kugombea nafasi ya juu kabisa akizungukwa na walinzi weupe believe me.. it is something to desire!.. Leo sisi kugombea Umiss Tanzania tu imekuwa kasheshe!
 
Samahani mzee mwanakajiji kama unanielewa kwa maana hio, mimi sio mbaguzi lakini napinga kwa nguvu zote tabia zinazoshabihiana na ubaguzi siku zote ikiwemo ya ku- undermine jitihada za mtu mwingine kutokana na upungufu wa namna yoyote ile ili kujinufaisha.

Niko kwenye kukosoa ujanja na mbinu zilizotumika kufanikisha ushindi wa Richa na si vinginevyo na nimejaribu kuelezea ni jinsi gani mratibu amekuwa si Hashim Lundenga.
 
napinga ushindi wa huyo mhindi vikali sana ! hivi hivi watz asilia tutaanza kusema ooh wahindi tz hawatendewi haki ukiangalia hata sisi wenyewe asilia hatujitendei haki leo hii uniambie nimtendee mhindi haki, for what ? kama wazawa wenyewe tungekuwa mbali zaidi kimaendeleo basi hapo sawa kuanza kuwashirikisha hao wahindi katika mambo ya taifa, lakini hata wazawa wenyewe hatujajikomboa halafu uweke wahindi sahani moja na wazawa, ujinga gani huo ? sitaki kusikia kabisaaaaa kuhusu hawa wahindi, idd amini angekuwa mzima kwa miezi miwili ningemuomba aje tz kuwa rais kwa hiyo miezi 2 halafu wangeone shughuli yao !

wazawa kwanza, the rest wafuate behind !

Myopic views...
 
Sawa nimekusikia, je kama majaji wote wangekuwa Watanzania weusi na wangemchagua Richa ingekuwa na nguvu kidogo?
 
Kuna wengi Tanzania wasiojua Kiswahili. Bibi yangu amekufa akiwa na miaka 90+ na neno la Kiswahili alilokuwa analijua ni 'jambo' na 'habari gani' kwa lafudhi nzito ya Kisukuma!!!

Kuhusu intermarriages kati ya sisi weusi na wao; yaani wewe hili unaliona ni muhimu sana eeh? Wewe uko tayari kumuoa Mhindi?

Halafu hili la wewe kusema wao wanajiona kuwa ni bora kuliko sisi linaonyesha inferiority complex yako. Unaka-complex kakujisikia uko duni dhidi ya watu wa rangi nyeupe nyeupe (for lack of a better term)

LOL! Talking about inferiority complex! So to call a SPADE by its real name shows my inferiority complex....LOL! I am done with this discussion. You seem not to have the ability and depth to discuss about this issue, instead you are jumping to personal attack. I don't have time for that BS. SAYONARA!
 
Bubu usiondoke hivi hivi, tueleze kwanza Richa amefanya nini au hakufanya nini ambacho hakimstahilishi Umiss Tanzania zaidi ya nini yeye alivyo?
 
Nadhani Mwkjj unashindwa kuelewa hoja za watu wengi kuhusu jamii ya kihindi na suala zima la Richa.Inawezekana kabisa kuwa Richa ni binti tu,tena pengine asiye na matatizo na watu wengine, ila ni lazima uangalie suala zima in broad view.Kuna kundi kubwa tu la watanzania ambao wamelalamika kuwa wafanyabiashara wa kihindi kwa kutumia pesa zao na umaarufu wao wameingilia kati mchakato mzima wa uchaguzi wa miss Tanzania! kwa maneno mengine wamewanunua majaji ili kumchagua mhindi mwenzao awe miss TZ na kuwa watamtumia kwenye biashara zao! na ndiyo maana wanalalamika kuchaguliwa kwa huyo binti! sasa hiyo haimaanishi kuwa kwakuwa eti Richa anasema kisukuma au kiswahili watu wakae kimya ili wasionekane wabaguzi no!! au hata kama majaji watakuwa ni weusi tii kama mkaaa haimaanishi kuwa watu wasilalamike juu ya huo ushindi wa kutatanisha wa huyo binti mpole kama unavyosema wewe!
La pili lazima uelewe kuwa ushindi wa Richa si tu kwamba ni ushindi wa umiss kama watu wengi wanavyofikiri,bali unabeba message nzito katika taifa letu nalo ni kuwa jamii ya kihindi ikiongozwa na wafanyabiashara wao wakubwa wanaweza kufanya lolote nchini mwetu hata kama sheria zinapindishwa au jamii nzima ya kitanzania hakiubaliani nalo.Kwa meneno mengine ule ushindani haukuwa wa umiss tu bali ulikuwa unabeba message ya power juu ya jamii ya kihindi na ile ya watu wengine.

Nasubiri hoja yako....

Wembe
 
LOL! Talking about inferiority complex! So to call a SPADE by its real name shows my inferiority complex....LOL! I am done with this discussion. You seem not to have the ability and depth to discuss about this issue, instead you are jumping to personal attack. I don't have time for that BS. SAYONARA!

Hujajibu hoja hapa!! And you're bowing out using the easiest way by dismissing me of not having the "ability and depth to discuss about this issue, instead you are jumping to personal attack"...My friend, if you are saying I personally attacked you by saying you have an inferiority complex based on what you said, then all of "us" who are calling "you " who are unhappy and are against Richa winning the title because of her ancestral origin "wabaguzi", are also personally attacking you, correct? I just used your logic here.....
 
Nadhani Mwkjj unashindwa kuelewa hoja za watu wengi kuhusu jamii ya kihindi na suala zima la Richa.Inawezekana kabisa kuwa Richa ni binti tu,tena pengine asiye na matatizo na watu wengine, ila ni lazima uangalie suala zima in broad view.Kuna kundi kubwa tu la watanzania ambao wamelalamika kuwa wafanyabiashara wa kihindi kwa kutumia pesa zao na umaarufu wao wameingilia kati mchakato mzima wa uchaguzi wa miss Tanzania! kwa maneno mengine wamewanunua majaji ili kumchagua mhindi mwenzao awe miss TZ na kuwa watamtumia kwenye biashara zao! na ndiyo maana wanalalamika kuchaguliwa kwa huyo binti! sasa hiyo haimaanishi kuwa kwakuwa eti Richa anasema kisukuma au kiswahili watu wakae kimya ili wasionekane wabaguzi no!! au hata kama majaji watakuwa ni weusi tii kama mkaaa haimaanishi kuwa watu wasilalamike juu ya huo ushindi wa kutatanisha wa huyo binti mpole kama unavyosema wewe!
La pili lazima uelewe kuwa ushindi wa Richa si tu kwamba ni ushindi wa umiss kama watu wengi wanavyofikiri,bali unabeba message nzito katika taifa letu nalo ni kuwa jamii ya kihindi ikiongozwa na wafanyabiashara wao wakubwa wanaweza kufanya lolote nchini mwetu hata kama sheria zinapindishwa au jamii nzima ya kitanzania hakiubaliani nalo.Kwa meneno mengine ule ushindani haukuwa wa umiss tu bali ulikuwa unabeba message ya power juu ya jamii ya kihindi na ile ya watu wengine.

Nasubiri hoja yako....

Wembe

Yaani, tangu Miss Kitongoji, Miss Kinondoni, Miss Earth.. na sasa Miss Tanzania wahindi wamefanya njama hii yote. Aidha sisi unataka kusema hawa jamaa wana control kubwa sana kwa mawazo ya Watanzania, au sisi ni watu punguani sana kuweza kuendeshwa hivi! Hivi kweli una kigezo cha kusema wafanyabiashara waliwanunua majaji? Maana hiyo kwa kweli inaweza kuwa hoja, na kwa mara ya kwanza naisikia hapa. Kama kuna mtu ana ushahidi kuwa kuna ufisadi au rushwa hilo ni la kupelekekwa TAKUKURU (maana sasa hivi wana moto kweli). Je angeshinda Miss Tanzania Mchagga mwingine, na tunafahamu wachagga wengi ni wafanyabiashara, je yawezekana kwenye ushindi wa TEMU walinunua majaji pia?

Kwa kifupi, hauna hoja za kusema kwanini Richa asiwe Miss Tanzania, isipokuwa sijui wahindi walifanya hivi au wanafanya vile! Kwanini makosa ya watu wengine aadhibiwe Richa?
 
Hoja waliyonayo ni ya kibaguzi ndio maana wanazungukazunguka tu bila kuweka bayana kile kilicho moyoni. Mimi namuheshimu sana mtu ambaye hafichi chuki zake. It is okay kuchukia so long as humdhuru mtu yoyote.
 
Hoja waliyonayo ni ya kibaguzi ndio maana wanazungukazunguka tu bila kuweka bayana kile kilicho moyoni. Mimi namuheshimu sana mtu ambaye hafichi chuki zake. It is okay kuchukia so long as humdhuru mtu yoyote.
Mkuu, hata mimi naona wanashindwa kujieleza, maana kila engo wanayokuja yaani its not justifiable kumshambulia Richa.
Nyani Ngabu kumbe mtu wa Ntuzu hahaa. Eee mimi nimefurahi mwaka huu msukuma amekuwa Miss Tanzania, maana wachagga wamenitesa sana miaka iliyopita, sasa sijui wachagga walikuwa wanahonga kamati ya Miss Tanzania?
Nadhani waanzishe tu thread ya ubaguzi halafu ijadiliwe ishu. Ubaguzi upo ndio, lakini mimi naona zaidi ni 'class' ishu. Ubaguzi huo huo mnaoutaja kati ya mtanzania mhindi na mtanzania mweusi, mifano ipo pia ya namna hiyo hiyo ya ubaguzi wa mweusi kwa mweusi hapo Tanzania.

Wembemkali, wahindi wanafanya biashara zao Tanzania. Hao wanaotaka kumtumia Richa atangazie biashara zao (if we are to believe you), soko lao ni waTanzania, kama kweli mipango yao ni hivyo, at the end of the day the consumer can choose what to buy into.
 
Kuibuka kwa hisia na malalamishi baada ya Richa mwenye asili ya Kihindi kuibuka mlimbwende wa Taifa si jambo la kuachwa kupita juujuu tu. Binti wa watu kaibua dukuduku la jamii bila hata yeye kutarajia. Ubaguzi upo, hali ya kutoaminiana ipo, watanzania weusi na watanzania weupe hasa wenye asili ya Asia wana mvutano kitabaka na ubaguzi.

Tusifumbie macho historia, na kujidanganya kwamba tuko zama za usawa na haki. Watu wengi huamua kuchukua mkondo wa kuandika na kujifanya wazuri kumbe nao ni wabaguzi aidha wa chinichini na wakati mwingine wa wazi kabisa.

Tusipakane mafuta kwa mgongo wa chupa, mijadala hii inaonyesha tunaishi kwa kuegesha tu, na tunaunganishwa kwa pasipoti tuu, hakuna utaifa wa dhati kwa matabaka ya weusi na weupe hasa wa asili ya Kiasia.

Watu wangesema, lakini ushindi wa mndengereko mweusi au myao mweusi ungechukuliwa tofauti na jinsi Richa, japo aweza kuwa hata chotara mnyamwezi, alivyoshindwa.
Hadi hapo tutakapochukua hatua za dhati, hisia na au hali ya kubaguana vitaendelea
 
Umeyasema vilivyo "najivunia".. Ndiyo maana hisia za namna hizo lazima zimulikwe na kukemewa pasipo kuoneana haya. Uwepo wa hisia hizo siyo sababu ya kuzihalalisha, kama vile watu wenye kubaka watoto wapo na wataendelea kuwapo, hatuwezi kuhalalisha kwa vile hawawezi kujizuia!
 
..mabaguzi sio majitu ya kudeal nayo mezani kupata suluhu ni sheria tuu ndio zitaondoa ubaguzi,hapa states bila sheria za kupinga ubaguzi hapa leo pasingekalika na bongo ni hivyo hivyo na ndio maana mwanakijiji niliwahi kukushangaa kumsifu yule mbaguzi mtikila aliyeanzisha sera ya magabachori...to me ubaguzi ni kama crime nyingine tuu na unatakiwa uwe dealt kisheria kama crime nyingine tuu
 
Sijui kama unakumbuka nilimuuliza kuhusu "magabachori" alikuwa na maana gani?
 
Back
Top Bottom