Hoyce Temu na Wabaguzi Mamboleo!

Hoyce Temu na Wabaguzi Mamboleo!

atuambie! wote wanatumia kiingereza wakati wa kujibu maswali? si kweli! kama sikosei mashindano ya 2005 au 2006 kuna mrembo alikuwa na mfasiri wake na nadhani alikuwa kwenye top 5, mnaokumbuka vizuri naomba mnisaidie. Kuhusu wahindi kuwa wabaguzi mi nina experience yangu mwenyewe, mdosi yule sintomsahau and i really hate indians kwa jinsi a(wa)livyonitendea, tena nikiwa ndani ya nchi yangu!ieleweke kuwa wahindi ni wabaguzi na kinachompata Richa sasa ni payback time, anadeserve - wahindi wote wanadeserve! kama wana akili safi waanze kujisahihisha/kujisafisha or else ..... i dont care about legacy ya Nyerere! its too much and we wont mouth it anymore ..... Hoyce kawasha moto! hata kama kakanusha kuwa hakuwa akipinga rangi(more precisely tabia chafu iliyojificha ndani ya rangi ya kihindi), nahisi alikuwa akifanya hivyo, mimi na jamii nyingine yenye mtazamo huo au inayoonja ubaguzi na maudhi ya wahindi tunamtaka asikanushe wala kuomba radhi ... yupo sahihi! tena mumwacheni!
 
Nimesikia kwamba hoyce temu alilia kwa sababu ya kulewa pombe siku ile sio kwamba alilia richa kupewa ushindi ule

- mbona wana kazi, toka kulia sababu ya "uchungu wa nchi" sasa wanasema amelia kisa "pombe". Kwa mtu mwenye hisia za kibaguzi baada ya kuona "mhindi" anachaguliwa one would definetly need a glass of ugimbi!
 
atuambie! wote wanatumia kiingereza wakati wa kujibu maswali? si kweli! kama sikosei mashindano ya 2005 au 2006 kuna mrembo alikuwa na mfasiri wake na nadhani alikuwa kwenye top 5, mnaokumbuka vizuri naomba mnisaidie. Kuhusu wahindi kuwa wabaguzi mi nina experience yangu mwenyewe, mdosi yule sintomsahau and i really hate indians kwa jinsi a(wa)livyonitendea, tena nikiwa ndani ya nchi yangu!ieleweke kuwa wahindi ni wabaguzi na kinachompata Richa sasa ni payback time, anadeserve - wahindi wote wanadeserve! kama wana akili safi waanze kujisahihisha/kujisafisha or else ..... i dont care about legacy ya Nyerere! its too much and we wont mouth it anymore ..... Hoyce kawasha moto! hata kama kakanusha kuwa hakuwa akipinga rangi(more precisely tabia chafu iliyojificha ndani ya rangi ya kihindi), nahisi alikuwa akifanya hivyo, mimi na jamii nyingine yenye mtazamo huo au inayoonja ubaguzi na maudhi ya wahindi tunamtaka asikanushe wala kuomba radhi ... yupo sahihi! tena mumwacheni!
 
atuambie! wote wanatumia kiingereza wakati wa kujibu maswali? si kweli! kama sikosei mashindano ya 2005 au 2006 kuna mrembo alikuwa na mfasiri wake na nadhani alikuwa kwenye top 5, mnaokumbuka vizuri naomba mnisaidie. Kuhusu wahindi kuwa wabaguzi mi nina experience yangu mwenyewe, mdosi yule sintomsahau and i really hate indians kwa jinsi a(wa)livyonitendea, tena nikiwa ndani ya nchi yangu!ieleweke kuwa wahindi ni wabaguzi na kinachompata Richa sasa ni payback time, anadeserve - wahindi wote wanadeserve! kama wana akili safi waanze kujisahihisha/kujisafisha or else ..... i dont care about legacy ya Nyerere! its too much and we wont mouth it anymore ..... Hoyce kawasha moto! hata kama kakanusha kuwa hakuwa akipinga rangi(more precisely tabia chafu iliyojificha ndani ya rangi ya kihindi), nahisi alikuwa akifanya hivyo, mimi na jamii nyingine yenye mtazamo huo au inayoonja ubaguzi na maudhi ya wahindi tunamtaka asikanushe wala kuomba radhi ... yupo sahihi! tena mumwacheni!

hakuna cha nini wala nini, hakuna cha kujifanya ati "miye walinibagua basi na miye nawabagua".. ubaguzi hauna sababu! Ubaguzi asili yake ni hisia ya kujiona bora kuliko mtu mwingine hata kama mtu yule mwingine hajakufanyia wewe jambo lolote lile baya! Angalau mnajitokeza ili tujue kuwa wabaguzi wapo hata wa rangi nyeusi! Na sumu yenu tutaendelea kuipinga kwa nguvu zote. Wabaguzi kama nyinyi ni hatari kabisa kwani hamuishii kwenye kuchukia tu, ubaguzi hauokomi na hasa ukipata nafasi ya kulipiza kisasi! Tunawapinga nyinyi wabaguzi mambo leo, hamna nafasi katika Tanzania na mawazo yenu ni ya hatari kama ukoma! Tutaendelea kuwapinga nyinyi wabaguzi ambao mnataka kutumia ushindi wa Richa kama kichocheo cha itikadi zenu potovu na za kibabe! Tunawapinga nyinyi wabaguzi mambo leo, ambao licha ya kukosa hata sababu moja ya msingi mnataka kumuadhibu binti huyu wa kitanzania kwa vile hafanani nanyi na kwa vile ati "wahindi walininyanyasa!".. Tunawapinga, tunaendelea kuwapinga, na tutazidi kuwapinga hadi pale mtakapotambua kuwa "binadamu wote ni sawa" na kila mtu "ana haki ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake"!

Tanzania tutakayoijenga ni Tanzania ile ambapo wana na mabinti wake wote bila ya kujali hali zao za kimaisha, rangi zao, dini zao, au mahali wanakotoka, au asili yao ya kitaifa, watakuwa na haki sawa, na nafasi sawa. Tuliupinga ubaguzi wa mtu mweupe dhidi ya watu weusi, tukaonesha makosa yake, na hatimaye ukaporomoka katika himaya yake ya mwisho kule Afrika ya Kusini, na sasa tumeanza mapambano mapya ya kuupinga ubaguzi wa watu weupe unaofanywa na watu weusi, hadi na wenyewe uporomoke kama vipande vya biskuti na uwe umesagika na kuwa tikitiki kama tikiti maji lililoangushwa kwenye mwamba!

Fikra zenu na vitendo si za kupuuzwa bali za kubezwa na si za kutweza! Kama vile wabaguzi wa Marekani walipata msemaji wao ndani ya Gavana Wallace, na wale wa Afrika ya kusini kupata msemaji wao kwenye P. W Botha, na nyinyi wa Tanzania inaonekana mmepata msemaji wenu kwenye Hoyce Temu, na waandishi ambao wanajifanya wanatetea usawa kumbe wanashiriki katika kupenyeza sumu yao ya kibaguzi! tunawapinga, tunaendelea kuwapinga na tutazidi kuwapinga!

Sumu yenu ya kibaguzi huwa haikomi, na hupenya kama mshale wa mwindaji, na kuwadunga wasiokuwa tayari na kuwafanya mateka wa fikra hizo mbovu!! Kwa ngao ya utambuzi wa usawa wa binadamu, tukisimama kidete kama majemedari wale waliopinga ubaguzi kwenye vilima vya Wamatumbi, na wale waliosimama kumwaga damu zao kulinda heshima ya mtu mweusi na haki ya watu weusi kuwa na haki sawa na binadamu mwingine yoyote! Tunawapinga kwa majina ya mababu zetu ambao walipigana kwa nguvu zote kupata nafasi ya kuishi kama binadamu wengine na kutambuliwa kama binadamu wengine na siyo kupigana ili wao wawe juu ya binadamu wengine! Kwa majina ya Mkwawa, na Ihunyo, kwa majina ya Songea na Mirambo! Tunawapinga, tunaendela kuwapinga, na tutaendelea kuwapinga!

Katika Tanzania hii kila Mtanzania atakuwa na haki sawa na nafasi sawa! Hata wabaguzi wetu na wenyewe wataheshimiwa na kuthaminiwa utu wao licha ya kwamba fikra zao mbovu zitapingwa kwa nguvu zote na hadi kwa masilio ya matone ya damu itiririkayo katika mishipa ya wale wapigania usawa na haki!

Tunawatangazia kuwa hamna nafasi ya kushinda, hoja zenu ni dhaifu, na mifano yenu ya kibaguzi imeporonyoka kama ndege aliyeruka mtego! Ni ninyi wenyewe mliotega mtego huo na mmnaswa wenyewe!
 
Mwanakijiji hebu mtafute huyu kisura umuhoji tumsikie ana ujumbe gani kwa hawa wabaguzi....
 
Ina maana kwamba watoto ambao baba zao hawana uwezo wa kupita njia za panya, hawawezi kupewa funguo ya gari lenye thamani ya sh milioni 45, huo ndiyo ukweli.

Jambo hili sasa liko wazi, tena halina kificho, hivyo machozi ya waliolia na kusononeka Inshallah Mola awapoze ila wakati umefika sasa kwa wazazi ambao wana mabinti zao wawapeleke shule za Kihindi, Kichina, Kijapan na hata Kirusi ili mradi tu mwanao aweze kutwaa taji la Miss Tanzania kwakuwa akizungumza Kiswanglish anaonekana mshamba, mwenye ukurutu usiotibika, hana sura ya kuonekana mbele ya watu na kuweza kuielezea nchi yake ambayo babu na mababu zake walizaliwa na kufia hapa, ama kweli waswahili walisema mdharau kwao au chake ni mtumwa, nimeamini.
Kumbe zile shepu za namba nane na mahips hazitakiwi ‘Miss World’, nasema hivyo kutokana na kwamba warembo walioshindana mwaka huu walikuwa mashallah, walijaaliwa, tulio kizani tukadhani kwamba taji litaenda Kanda ya Ziwa na kwingineko, lakini wapi, wenye nguvu na wajanja wa mjini wamelinyakua, tena kwa kutumia kisu butu chenye kutu na kuwaachia warembo wetu ukurutu wenye kutu.Hivyo basi, kilio kile kile kilichomwagwa hadharani na Hoyce, si cha bure, na nina hofu kwamba huenda ikawa sawa na sauti ya mtu aliae nyikani, akiomba msaada huku wengine wakimkebehi na kumwona kama hana jipya.

What a ridiculous comments!

Ikumbukwe kwamba, huyu aliwahi kuwa mrembo wa taifa na kuiwakilisha nchi, hivyo anafahamu nini huwa kinafanyika kule, hasa wanapokuwa kambini kuanzia kambi ya Miss Tanzania na ‘Miss World’ kwa ujumla.

So what? mbona aliboronga? if anything ni mfano mbaya si wa kufuatwa
 
Masatu.. yaani Hoyce ndiyo msemaji wao! Halafu hiyo article imejaa maneno ya kibaguzi ya chini chini kweli..
 
Richa huyo hapo anajichanganya na watu bila shida............au ndio mtasema ni PR(public relationship)campaign ya kupoza watu??? wabaguzi dunia nzima huwa wanaka-trait kama moja ka kuwa na uzembe uriokithiri ktk kufikiria.
 
Mwanakijiji hebu mtafute huyu kisura umuhoji tumsikie ana ujumbe gani kwa hawa wabaguzi....

Mzee Ngabu, haya yalikuwa sehemu ya mahojiano yake na Bongo Celebrity.com wakati huo ndio kwanza kashinda taji la miss Kinondoni, Miss Tanzania ilikuwa "mbado!"... Mzee Mwkjj nae akimpata huenda atayasema haya haya.

....;

BC: There is this issue of race. We have to say about it because people have raised concern about you being a Tanzanian of Asian origin and all that.

RICHA: It's sad that people have raised such an issue. I don't see why they should, because I am not the only Asian born in this Country. In fact both my parents were born here in Tanzania. My mother in Pemba and my father in Morogoro. I was born here in Dar and grew up in Mwanza so what does that make me? Definitely not an American nor a British not even an Indian. I am proudly Tanzanian and I know no other country but Tanzania. May be I am Afro Indian but I am still a born Tanzanian.

BC: Do you feel offended by the race issues raised?

RICHA: Not really, it doesn't offend me but it does surprise me. Our father of the Nation the late Julius Kambarage Nyerere himself said once that we should stop discriminating each other because we are all brothers and sisters. I totally agree with his words. Racial discrimination has long past its phrase and is considered history, so its high time Tanzanians bury the past.

Source; www.bongocelebrity.com/2007/07/12/i-am-proudly-tanzanian-miss-kinondoni-07/
 
hata ajieleze vipi, wabaguzi wetu wataendelea kuishikilia shoka ya rangi yake na kuielekeza kwenye shingo yake kisa na mkasa ati "wahindi wengine ni wabaguzi basi na sisitunambagua huyu"!
 
hakuna lolote zaidi ya chuki binafsi na ubaguzi tu. Richa ana sifa zote za kushinda miss tanzania lakini hao akina Hoyce naona wanajichanganya kukataa ushindi wake kwani wao wana sifa gani hata mwenzao azikose? na hao watanzania wenye kuendelea na ubaguzi watafute jengine lakini hata wakisema mchana na asubuhi na usiku walale na waamke basi ndio ameshachaguliwa na hawezi kuacha huo ushindi mpaka mwakani. panapo majaaliwa ndio amkabidhi mwengine kwa hivyo wabaguzi tunakupeni pole na mtafute jengine la kuzungumza ushindi anao Mhindi mkitaka msitake zamu yake mwaka huu msubiri mwakani labda atapata Mzungu au Mwarabu mzidi kusema zaidi.
 
Mwanakijiji siku zote mie nahiheshimu sana michango yako,hata tunapotofautiana bado naheshimu tofauti hizo.Mfano wa Marekani mie naona hapa haufai kwani wote hao wazungu na Waafrika hakuna aneyeweza kudai yeye ndiye mwenye asili.Wenye asaili walikuwa red Indians, na inawezekana tangu uingie huko hujawahi waona.
Mie sina tatizo na baadhi ya sehemu kuwa na watanzania wahamiaji, lakini kuna strategic places. Mfano Urais!! eti Tanzania tukapata rais "MHINDI" MWARABU au MZUNGU ina maana kuwa katika jamii nzima ya Mamilioni ya Watanzania asili hakuna mwenye ubongo au uwezo wa kutuongoza.Kwa upande wa Miss ni uwakilishi na kuitangaza nchi.Mwaka kesho tutawakilishwa na MZUNGU kesho kutwa MWARABU!!!!Mie sio kuwa nawaona Wahindi au Mwarabu au Mzungu sio bora, hapana nwaona ni bora kama mie.MH Mwanakijiji kila kitu kina mipaka.Hata Demokrasia ina mipaka yake.
 
Baada ya kuangalia posts nyingi hapa naona kuna tatizo.Kuna makundi makubwa mawili ambayo yamejitokeza,Kundi moja linalojiita la watanzania safi au la watu ambao kama sikosei pia linalojiita siyo lawabaguzi linasema kuwa Richa ni safi kama theluji na hakuna EVIDENCE au ushahidi wowote kuonyesha kuwa kuna connection yoyote ile ya upendeleo au ubaguzi katika ushindi wa Richa na kwa jamii yetu!.Kundi hili limeamua kufumbia macho na kuwanyamazisha wote ambao wanatoa malalamiko yao juu ya kuwepo kwa upendeleo wa makusudi kwenye ushindi miss TZ.
Kundi la pili linasema kuwa ushindi ule haukuwa wa haki na kuna matatizo ya kibaguzi katika jamii yetu ya Kitanzania na mara nyingi kuna upendeleo wa makusudi hasa kati ya jamii ya wahindi juu ya ile ya watanzani weusi.Na kwamba mara nyingi watanzania weusi wamekuwa victims wa sera hizi za kibaguzi za wahindi kwa MUDA MREFU TU na kuwa haijawahi kusikika hata siku moja mtu kutoka kwenye kundi la kwanza au kiongozi wa serikali akiwasahihisha au japo kuwakemea wahindi hao kwa sera zao za kibaguzi.
Kwa mtazamo wa kundi la kwanza hawa ni wabaguzi weusi! na ubaguzi kwao ni pale tu kundi la pili linapotoa malalamiko juu ya wahindi! hapo ndipo mlolongo wa neno EVIDENCE unapotakiwa! na kwao ni haki na ni sheria mtu mweusi akibaguliwa! na nikosa la jinai mhindi kukosolewa au kuhojiwa pindi kunapotokea malalamiko ya kibaguzi au upendeleo wa namna fulani! hii ni double standard! ubaguzi hauji tu kutoka upande mmoja!na kuhalalishwa upande mwingine!sisi wengine tunapinga ubaguzi au upendeleo kwa pande zote! tunataka haki itendeke bila ya kujali rangi.Na pale inapotokea malalamiko tunakuwa mstari wa mbele kuchunguza,kuchambua,na kukemea kwa nguvu zote ubaguzi au upendeleo wa aina yoyote ile.Richa ameibua malalamiko mengi kuwa hakustahili! na vigezo vilivyotumika havikuweza kuhalalishwa kushindwa kwa wale wengine.Sasa sisi kama wapenda haki tunaungana na wote kudai haki!hata kama tutaitwa wabaguzi.
Mpaka sasa tunao victims wengi weusi kwenye jamii yetu kuanzia majumbani,kwenye siasa,mahakamani,mahospitalini,mashuleni, madukani,michezoni,mitaani na hata kwenye huo Umiss Tanzania! na kwa miaka mingi watanzania hawa wamelazimishwa au kunyamazishwa kuwa hakuna ubaguzi wowote au upendeleo wowote kwa wahindi juu ya wale weusi.Watanzania hawa hawana mtetezi yeyote yule! wengi wao ama wameshazulumiwa haki zao za msingi au hata kubakwa! na kuitwa majina yasiyoweza hata kutamkwa na mtu mwenye akili timamu! hili pia kwa mtazamo wa kundi la kwanza ni sawa, nani haki mbele ya sheria! na ni makosa na ubaguzi pale tu watu kama akina Hoyce wanaposema jamani hebu tuangalie jinsi muenendo mzima wa ushindi wa huyu binti kama kweli alistahili au la? na kama ni kweli wale wengine walistahili kushindwa!!
Kundi la kwanza (linalojiita la watanzania safi au ambalo kama sikosei linajiita pia si la wabaguzi) kwa sababu ambazo hazijulikani limeshawahukumu na kuwashutumu vikali kundi la pili na kuwabatiza jina la wabaguzi weusi ati tu kwa sababu kundi la pili limeamua kufichua sera za ubaguzi na upendeleo juu ya tabaka moja juu ya jingine katika jamii yetu katika nyanja mbalimbali ikiwemo Umiss Tanzania.Kwa mtazamo wangu hawa nadhani wanachuki binafsi na Hoyce na kwa kweli ninaweza kuwaweka kwenye kundi la watu wenye ubaguzi wakibinafsi!
Tanzania kama nchi nyingi za kiafrika ina matatizo ya kibaguzi.Wapo wale ambao wanataka tuamini kuwa Tanzania ni safi na iliyotukuka! na kwamba hatuna victims wa ubaguzi wa Tabaka moja juu ya jingine.Mimi kwa sauti KUU NA YA JUU NINALIPINGA HILO! NANIKO TAYARI KUTETEA HAKI NA KUHAKIKISHA KUWA KAMWE HATURUDI KWENYE ZAMA ZA UKOLONI ambapo mtu mweusi alionekana kama bidhaa tu!
Ubaguzi unauwa na unauma na kamwe hauna nafasi katika jamii yetu. Na ubaguzi hauwezi kuhalalishwa tu pale kundi moja hasa la wahindi linapoachwa kuwabagua wale wa tabaka lingine yaani weusi na kushutumiwa vikali pale kundi la weusi linapoamua kueleza tatizo hili katika jamii yetu.
Hoyce Temu ameelezea tatizo kubwa kwenye jamii yetu! na chakushangaza ameshahukumiwa na kubatizwa majina ya kila aina! Hivi kweli tujiulize sisi wenyewe jamii yetu ya kitanzania ni safi? ni kweli hakuna ubaguzi ambao wahindi wanaufanya juu ya wale weusi? au ni kweli kuwa hakuna upendeleo wowote kweye mambo mbalimbali inapofika kwenye suala la wahindi? au ni sawa watu weusi kubaguliwa na ni nikosa na dhambi kuu wahindi kusahihishwa au kuchukuliwa hatua pindi wanapobagua au kupendelewa?
wale wanaotaka EVIDENCE walikuwa wapi miaka yote hiyo ambapo watanzania weusi wamekuwa wakibaguliwa??? wakitanzania weusi ambao kwa miaka nenda rudi wamekuwa wakinyanyaswa katika jamii yetu na wahindi, wamekuwa wakiachwa wao peke yao bila ya mtetezi yeyote na hakukuwa na mtu yeyote yule aliyejitokeza kumea ubaguzi huu au kutamka neno EVIDENCE! mambo yakibaguzi yako wazi kwenye jamii yetu!na victims tunao! na cha kushangaza hawa ambao wako kwenye kundi la kwanza walikuwa kimya kama maji mtungini! kana kwamba mambo yanayofanyika ni sawa! leo hii watanzania wanapotaka kujua ukweli kundi hili linaamka na kuwabatiza kila aina ya majina na kuweka neno EVIDENCE!
Wembe.
 
Nyangumi, nakubaliana kutofautiana, lakini kuna kutofautiana kwa msingi na kwingine kwa kwa kawaida. Tofauti yetu hapa ni ya msingi. Na msingi wake ni kuwa baadhi yetu wameamua kuvunja kanuni kubwa ya msingi na hapa hawana hoja. Ukiivunja hiyo kanuni (ya usawa wa raia wote) basi hiyo kanuni itakuvunja. Leo hii Ufaransa wana Waziri mwenye asili ya Morocco, Hivi majuzi US wamechagua mwakilishi Muislamu kwa mara ya kwanza, Uingereza nako sisemi mengi, leo hii kuna mwendesha mashtaka wa Kitanzania Australia (tena mweusi), n.k Kwanini wazungu waliokuwa wabaguzi sana leo hii wanaamini hii haki ya msingi ya usawa kuliko wale ambao walikuwa wanapinga sana ubaguzi ambao leo wamegeuka wabaguzi.

Tunaweza kutofautiana, lakini tunapotofautiana kwenye jambo la msingi namna hii, ni lazima tofauti hiyo ioneshwe na kumulikwa (highlighted) kwa nguvu zaidi ili wenye mitazamo ya kibaguzi wajulikane na wale wenye kutetea usawa wa binadamu wote na haki sawa kwa raia wote wajulikane. Katika hili msimamo wangu uko wazi kabisa na hauna kivuli cha kukengeuka (no shadow of ambiguity). Richa kama binti aliyezaliwa Tanzania, na aliyezaliwa na wazazi waliozaliwa Tanzania anastahili haki zote kama raia wa Tanzania. Hilo kwangu halina mjadala, hivi kweli mnafikiri kuwa sijawahi kukutana na wahindi wabaguzi? Hivi mnafikiri kuwa sijawahi kukutana na wahaya wabaguzi, sijakutana na Wazaramo wabaguzi? Hivi katika Tanzania wenye ubaguzi na wenye kuwatenda vibaya watanzania wenzao ni wahindi peke yao na wachagga, wanyakyusa, n.k wote ni watu wenye kupenda mafanikio ya watu wengine! Kwa vile niliwahi kubaguliwa na wahaya leo hii binti wa kihaya akishinda, nihoji kwanini alishinda!!?

Hoja hizi za kibaguzi ni za kipuuzi na lazima zioneshwe hivyo!
 
Baada ya kuangalia posts nyingi hapa naona kuna tatizo.Kuna makundi makubwa mawili ambayo yamejitokeza,Kundi moja linalojiita la watanzania safi au la watu ambao kama sikosei pia linalojiita siyo lawabaguzi linasema kuwa Richa ni safi kama theluji na hakuna EVIDENCE au ushahidi wowote kuonyesha kuwa kuna connection yoyote ile ya upendeleo au ubaguzi katika ushindi wa Richa na kwa jamii yetu!.Kundi hili limeamua kufumbia macho na kuwanyamazisha wote ambao wanatoa malalamiko yao juu ya kuwepo kwa upendeleo wa makusudi kwenye ushindi miss TZ.
Kundi la pili linasema kuwa ushindi ule haukuwa wa haki na kuna matatizo ya kibaguzi katika jamii yetu ya Kitanzania na mara nyingi kuna upendeleo wa makusudi hasa kati ya jamii ya wahindi juu ya ile ya watanzani weusi.Na kwamba mara nyingi watanzania weusi wamekuwa victims wa sera hizi za kibaguzi za wahindi kwa MUDA MREFU TU na kuwa haijawahi kusikika hata siku moja mtu kutoka kwenye kundi la kwanza au kiongozi wa serikali akiwasahihisha au japo kuwakemea wahindi hao kwa sera zao za kibaguzi.
Kwa mtazamo wa kundi la kwanza hawa ni wabaguzi weusi! na ubaguzi kwao ni pale tu kundi la pili linapotoa malalamiko juu ya wahindi! .

Nyangumi, binafsi yangu nakubali kabisa Tanzania kama nchi nyingine tuna Ukabili, Ubaguzi na Udini, japo Mwalimu alijitahidi sana kuupiga vita nasi miaka nenda rudi hatukuwa nayo mambo haya "hadharani", lakini sumu hii imeanza kurudi kwa kasi, na kama alivyohoji mzee Mwkjj nani alaumiwe, naweza jibu Wahandishi wa habari wa magazeti hasa ya udaku nao wanachangia kwa sasa.

Kwanini basi huyu binti kama alishinda kitongoji cha Kinondoni akaachiwa mpaka ashiriki Miss Tanzania ndio watu wakurupuke? Kwani Miss Tanzania kuna kigezo mbantu tu ndio ashiriki? mashindano ya Miss Tanzania 2005 alikuwemo chotara Lisa Jensen, hakusemwa!, wakati huo huo Miss World 2006-Poland, South Africa mwakilishi wao alikuwa Mhindi -Dhiveja Sondrum, mwaka huu Mzungu ndio mwakilishi wao. Tuseme sie ndio tuna uchungu kuliko kwa akina madiba walobaguliwa miaka nenda rudi??? Hakuna upendeleo wala nini, binti kawazidi IQ wenziwe thts all. Tena tukiendelea kulia lia eti mhindi/wahindi hata kina Madiba watatushangaa!
 
Mimi napinga kwa nguvu zote vitendo vya ubaguzi anavyofanyiwa huyu binti ! Nadhani ni jambo la aibu ambalo halina nafasi yoyote ile katika Tanzania yetu ya sasa . Huyu dada ni mtanzania kama watanzania wengine na kitendo chakumbagua kwa kutumia kigezo cha rangi yake ni cha kizandiki na kinatakiwa kupingwa na kila mtu.

Pili , Watanzania wenzetu wenye asili ya kihindi ni lazima watusaidie katika hili pia ! Ni lazima wajitahidi kuassimilate na jamii ya watanzania weusi .

Ni hayo tuu.
 
Rufiji hilo la pili ni la muhimu na nililionesha pia kwenye makala yangu. Hata hivyo kitendo cha wao kutoassimilate hadi sasa haihusiani kabisa na ushindi wa binti huyu. Hawa wabaguzi mambo leo wanataka kumuadhibu huyu binti kwa vile tu huko "rakesh" na "patel" fulani waliwahi kuwaita majina mabaya au kuwabagua, so kama mmoja alivyosema kwao this is "pay back"! This is the absurdity of all absurdities!
 
Back
Top Bottom