Hoyce Temu na Wabaguzi Mamboleo!

Hoyce Temu na Wabaguzi Mamboleo!

Nyani Luther, alikuwa amemalia PhD yake mwaka huo na ilikuwa hadi December 1955 (5th to be precisely), hata hivyo at the time alikuwa bado hajadevelop nadharia yake ya usawa wa watu wote kama alivyofanya Mwalimu earlier that year. Ilikuwa ni 1959 ndipo Luther alipoanza kupata mwelekeo ambao unamfanya akumbukwe sana leo hii.

Ok, nilidhani kwa vile mgomo wa Birmingham ulianza mwaka huo huo...na mwaka '57 alikuwa mmoja wa wageni waalikwa huko Accra kwenye sherehe za uhuru which means tayari alikuwa ameshajijengea jina!
Hata hivyo...nadhani wote walitoa hiyo nadharia kwa Gandhi...na wengineo kama akina W.E.B. DuBois, Garvey, n.k.
 
Mwanakijiji

Unaweza kunitajia ni nchi gani ulimwenguni ambayo haina ubaguzi? Naomba unipe nchi moja tu.

Blacks aren't sacrificial lambs?

So what?? It is still wrong and it doesn't justify it
 
Ok, nilidhani kwa vile mgomo wa Birmingham ulianza mwaka huo huo...na mwaka '57 alikuwa mmoja wa wageni waalikwa huko Accra kwenye sherehe za uhuru which means tayari alikuwa ameshajijengea jina!
Hata hivyo...nadhani wote walitoa hiyo nadharia kwa Gandhi...na wengineo kama akina W.E.B. DuBois, Garvey, n.k.

sawasawa kabisa. Still utaona kuwa Mwalimu alikuwa mbele kidogo, Gandhi alichofanya ni kudhihirisha kuwa kufanya nadharia hiyo kuwa kweli inawezekana na hapo ndipo Mwalimu na wengine walijifunza sana kutoka kwa Gandhi. Sijui wao Wahindi kule wanafikiri vipi siku hizi kuhusu watu wenye nasaba tofauti kuishi na kufanikiwa kule.
 
Pamoja na kwamba imeshatokea kuwa safari hii tunawakilishwa na mtanzania mwenye asili nyingine, na ingawa mlio wengi mnamtetea na kusema kuwa kumpinga ni sawa na kuunga mkono ubaguzi. Ila mimi ingawa msimamo wangu upo palepale kuwa nampinga miss mpya kwa mishipa yangu yote ya fahamu...
Ninachosimamia ni kwamba opportunities iwe kwa wenyeji wenye uasili, yaani wabantu...
siwapingi mnaounga mkono kwani ni haki ya kila mtu kuamini anachokiwaza na kusema anachokiamini.
Nakubali kuwa kosa tumelianza kwenye siasa na sidhani kama tutaweza kujisahihisha...

Labda niseme kwanini ninapinga, Ni kwa vile ambavyo ndugu zetu hawa waasia (wahindi) walivyo-wabaguzi huko kwao na jinsi wanavyothubutu kuendesha maisha ya kibaguzi hata ndani ya nchi yetu. Sio kwamba naongea nadharia ila hebu tafiti na unieleze kuwa ni watanzania wangapi ni waumini wa dini za kihindu, sio kwamba hawapendi ial Dini inawabagua wazelendo kushiriki, Pia hebu fuatilia namna ambavyo waasia hawa wanavyoendesha viwanda na biashara zao hapa nchini. Ninawafahamu baadhi ya watanzania wanaofanya kazi kwa wahindi na walah malalamiko ni jinsi wanavyobaguliwa is shame and sorrow....
Jeee, mtataka niunge mkono??? je niunge mkono kwa kipi au kwa uhalali upi????
Naomba kuungwa mkono
 
Ninachosimamia ni kwamba opportunities iwe kwa wenyeji wenye uasili, yaani wabantu...
siwapingi mnaounga mkono kwani ni haki ya kila mtu kuamini anachokiwaza na kusema anachokiamini.
Nakubali kuwa kosa tumelianza kwenye siasa na sidhani kama tutaweza kujisahihisha...

Ni nani alikuambia kuwa wenye uasili ni "wabantu"? Hivi unajua kuwa kuna watu wengine weusi ambao siyo "wabantu" usichanganye weusi na ubantu!!


Labda niseme kwanini ninapinga, Ni kwa vile ambavyo ndugu zetu hawa waasia (wahindi) walivyo-wabaguzi huko kwao na jinsi wanavyothubutu kuendesha maisha ya kibaguzi hata ndani ya nchi yetu. Sio kwamba naongea nadharia ila hebu tafiti na unieleze kuwa ni watanzania wangapi ni waumini wa dini za kihindu, sio kwamba hawapendi ial Dini inawabagua wazelendo kushiriki, Pia hebu fuatilia namna ambavyo waasia hawa wanavyoendesha viwanda na biashara zao hapa nchini. Ninawafahamu baadhi ya watanzania wanaofanya kazi kwa wahindi na walah malalamiko ni jinsi wanavyobaguliwa is shame and sorrow....

Hii inahusiana vipi na Richa? je Richa ni mhindu? Richa kwao wapi? wazazi wamezaliwa Tanzania, yeye kazaliwa Tanzania, hajawahi kwenda India wala nini, kwanini leo umlazimishe kuwa "kwake" ni India?

Jeee, mtataka niunge mkono??? je niunge mkono kwa kipi au kwa uhalali upi????
Naomba kuungwa mkono

Hakuna anayetaka uunge mkono!
 
We hold these Truths to be self-evident, that all Men are created equal, That they are endowed by their Creator with certain unalienable Rights, that among these are Life, Liberty, and the Pursuit of Happiness. That to secure these Rights, Governments are instituted among Men, deriving their just Powers from the Consent of the Governed, that whenever any Form of Government becomes destructive of these Ends, it is the Right of the People to alter or abolish it, and to institute a new Government, laying its Foundations on such Principles and organizing its Powers in such Form, as to Them shall seem most likely to effect their Safety and Happiness.

AMERICAN DECLARATION OF INDEPENDENCE

NAONGEZA YA KWANGU HAPA CHINI

That to secure these rights men in their individuality or using their institutions will have the right to take steps to abolish or alter any activity of anybody or group of people which shall be destructive on such principles without themselves to break the same principles
 
Tupo wengine tunahitaji mabinti zetu wawe Miss France, Miss UK, Miss Germany Miss USA, Miss Canada etc. kwa hiyo ni lazima tupige kona zote ili kuhalalisha lolote lile na iwe. Kwa hiyo basi kila mtu akili mkichwa.
 
Tupo wengine tunahitaji mabinti zetu wawe Miss France, Miss UK, Miss Germany Miss USA, Miss Canada etc. kwa hiyo ni lazima tupige kona zote ili kuhalalisha lolote lile na iwe. Kwa hiyo basi kila mtu akili mkichwa.

Wabaguzi ni vipofu, lakini upofu wao ni mbaya zaidi ya upofu wa kawaida kwani unaandamana na ujuaji. Nafikiri wengi wamejaribu kuonyesha ubaguzi na madhara yake "clearly" lakini bado hawaoni. Kipofu haoni, lakini anaweza kushikwa mkono akaongozwa...vipofu tulionao hapa, hawaoni na hawataki kuonyeshwa njia, waacheni gizani!

Taji lile lilikuwa ni la MISS TANZANIA. Sio Miss Bantu, Sio Miss Black, Sio Miss Blue, Sio Miss Pink.

[FONT=arial,helvetica,sans-serif][FONT=Arial, Helvetica, sans-serif]This is the official text. The Act, No. 6 of 1995, was passed in the National Assembly on 18 April 1995 and assented by the President on 10 October 1995.

[FONT=arial,helvetica,sans-serif][FONT=Arial, Helvetica, sans-serif]PART II ATTAINMENT OF CITIZENSHIP ON OR AFTER UNION DAY[/FONT][/FONT]
[/FONT]
[/FONT]
[FONT=arial,helvetica,sans-serif][FONT=Arial, Helvetica, sans-serif]5. Persons born in the United Republic on after Union Day[/FONT]

[FONT=arial,helvetica,sans-serif](1)Subject to the provisions of subsection (2), every person born in the United Republic on or after Union Day shall be deemed to have become and to have continued to be a citizen of the United Republic with effect from the date of his birth, and with effect from the commencement of this Act shall become and continue to be a citizen of the United Republic, subject to the provisions of section 30.[/FONT]

[FONT=arial,helvetica,sans-serif][FONT=arial,helvetica,sans-serif](2)A person shall not be deemed to be or to have become a citizen of the United Republic by virtue of this section if at the time of his birth-[/FONT]

[FONT=arial,helvetica,sans-serif][FONT=arial,helvetica,sans-serif](a)neither of his parents is or was a citizen of the United Republic and his father possesses the immunity from suit and legal process which is accorded to an envoy of a foreign sovereign power accredited to the United Republic; or[/FONT]

[FONT=arial,helvetica,sans-serif][FONT=arial,helvetica,sans-serif](b)any of his parents is an enemy and the birth occurs in a place then under occupation by the enemy.[/FONT]

[FONT=arial,helvetica,sans-serif]Mtalia sana na huyu Miss LAKINI ukweli unabakia pale pale, yeye ni Miss Tanzania 2007![/FONT]
[/FONT]
[/FONT]
[/FONT]
[/FONT]
 
Insurgent, kumbuka kuwa wabaguzi wetu hawahoji uraia wa Richa wanahojia rangi yake, kwani kwao msingi wa kuangalia uraia siyo sheria hiyo bali ni rangi ya mtu mwenyewe. Ndio maana hawawezi kuhoji uraia wake isipokuwa rangi yake.
 
Jamani ningeshauri kuanzishwa kwa thread nyingine inayozungumzia Ubaguzi rangi na Ukabila Tanzania.Kwa nini ninashauri hivyo?

1)Tanzania tunayo matatizo ya ubaguzi wa rangi hasa
kati ya waasia hasa jamii ya wahindi na ile ya watanzania
weusi.Suala la Richa ni punje tu juu ya mambo yanavyosokota
chini kwa chini katika jamii yetu na wote tumeshuhudia
hilo!.Kwa hiyo naona si vibaya kuwa na thread nyingine
ambayo itaweza kulijadili na kulitafutia
ufumbuzi au kupendekeza majibu.

2)Tuichukulie Tanzania kama Tanzania na siyo nchi kama
Marekani au South Africa na kwingineko.Nchi yetu ina
utamaduni na historia tofauti na nchi nyingine. Kwa mfano
Nchini Marekani suala hili walilijadili na kulitafutia
ufumbuzi karibu miaka arobaini iliyopita ingawa nao haikuwa
rahisi,ilibidi wamwage damu ndipo kieleweke!na mpaka leo
bado wanaendelea kuondoa kasoro zilizobaki ingawa bado kuna
maeneo mengi ya kuyafanyia kazi.Nchini Afrika kusini ni
kweli kwa nadharia tu kuwa ubaguzi umekwisha ila nao bado
mambo si shwari.

3) Kuna baadhi ya wenzetu ambao wanatumia suala la Richa ili kutaka kuondoa au kuipumbaza jamii kuwa hakuna ubaguzi ambao waasia hasa wa jamii ya wahindi wanaoufanya kwa wenzao weusi.Kila mara watu wanapotaka kujadili suala la ubaguzi wa rangi,hawa wenzetu wanalipotosha na kuweka lile la ukabila au la weusi juu ya wahindi.Sasa nadhani thread hiyo inaweza kuyachambua mambo hayo kwa KINA ingawa yote yanaelekea kuwa na dhana moja.

4) Tanzania bado ina matatizo ya ukabila,ingawa mambo haya yanaendelea kupungua siku hadi siku kutokana na jinsi watu wa makabila mbalimbali yanavyojichanganya pamoja na kujiona ni taifa moja.Hali hii si hivyo kwa ndugu zetu wahindi,bado ni taifa la wahindi ndani ya taifa lingine likiwa na passport ya Tanzania. Hii ni tofauti na wahindi walioko marekani ambao hujichanganya na wengine bila ya matatizo yoyote!! mifano tunayo.

5)Mzee wetu Mwl.Nyerere alipambana sana na ukabila na ubaguzi, ingawa naye alielekea kuwaadhibu weusi kuliko wahindi pindi wanapofanya makosa hayo.Karibu hotuba zake zote tangu miaka ya sitini alifokea sana weusi walipotaka kubaguana wenyewe kwa wenyewe au kuwabagua wahindi au waasia lakini sijawahi kuona pale alipodiriki kusema kuwa jamii ya wahindi inakosea inapoamua kujitenga au kuwabagau au kuwanyanyasa wenzao weusi!.Tafadhali mwenye mifano naomba awasilishe hapa tuone!

Ninaomba tu kuwasilisha!

Wembe.
 
Jamani ningeshauri kuanzishwa kwa thread nyingine inayozungumzia Ubaguzi rangi na Ukabila Tanzania.Kwa nini ninashauri hivyo?

1)Tanzania tunayo matatizo ya ubaguzi wa rangi hasa
kati ya waasia hasa jamii ya wahindi na ile ya watanzania
weusi.Suala la Richa ni punje tu juu ya mambo yanavyosokota
chini kwa chini katika jamii yetu na wote tumeshuhudia
hilo!.Kwa hiyo naona si vibaya kuwa na thread nyingine
ambayo itaweza kulijadili na kulitafutia
ufumbuzi au kupendekeza majibu.

2)Tuichukulie Tanzania kama Tanzania na siyo nchi kama
Marekani au South Africa na kwingineko.Nchi yetu ina
utamaduni na historia tofauti na nchi nyingine. Kwa mfano
Nchini Marekani suala hili walilijadili na kulitafutia
ufumbuzi karibu miaka arobaini iliyopita ingawa nao haikuwa
rahisi,ilibidi wamwage damu ndipo kieleweke!na mpaka leo
bado wanaendelea kuondoa kasoro zilizobaki ingawa bado kuna
maeneo mengi ya kuyafanyia kazi.Nchini Afrika kusini ni
kweli kwa nadharia tu kuwa ubaguzi umekwisha ila nao bado
mambo si shwari.

3) Kuna baadhi ya wenzetu ambao wanatumia suala la Richa ili kutaka kuondoa au kuipumbaza jamii kuwa hakuna ubaguzi ambao waasia hasa wa jamii ya wahindi wanaoufanya kwa wenzao weusi.Kila mara watu wanapotaka kujadili suala la ubaguzi wa rangi,hawa wenzetu wanalipotosha na kuweka lile la ukabila au la weusi juu ya wahindi.Sasa nadhani thread hiyo inaweza kuyachambua mambo hayo kwa KINA ingawa yote yanaelekea kuwa na dhana moja.

4) Tanzania bado ina matatizo ya ukabila,ingawa mambo haya yanaendelea kupungua siku hadi siku kutokana na jinsi watu wa makabila mbalimbali yanavyojichanganya pamoja na kujiona ni taifa moja.Hali hii si hivyo kwa ndugu zetu wahindi,bado ni taifa la wahindi ndani ya taifa lingine likiwa na passport ya Tanzania. Hii ni tofauti na wahindi walioko marekani ambao hujichanganya na wengine bila ya matatizo yoyote!! mifano tunayo.

5)Mzee wetu Mwl.Nyerere alipambana sana na ukabila na ubaguzi, ingawa naye alielekea kuwaadhibu weusi kuliko wahindi pindi wanapofanya makosa hayo.Karibu hotuba zake zote tangu miaka ya sitini alifokea sana weusi walipotaka kubaguana wenyewe kwa wenyewe au kuwabagua wahindi au waasia lakini sijawahi kuona pale alipodiriki kusema kuwa jamii ya wahindi inakosea inapoamua kujitenga au kuwabagau au kuwanyanyasa wenzao weusi!.Tafadhali mwenye mifano naomba awasilishe hapa tuone!

Ninaomba tu kuwasilisha!

Wembe.

...Richa asiwe kisingizio cha wewe kutaka ubaguzi uangaliwe. Waliposhinda wa rangi yetu hukulalamika ubaguzi na wahindi hawakulalamika ubaguzi. Wandugu...tuache DOUBLE STANDARDS. Ubaguzi hautatufikisha mahali. Hii thread imeshakuwa exhausted na points na counter points...kweli kama unataka kuendeleza Ubaguzi/Ukabila anzisha thread nyingine...Nafikiri hii itakuwa post yangu ya mwisho ma'nake wenye hekima walishasema, Don't Argue With A Fool...
 
Wembe, huhitaji ruhusa kuanzisha mada kuhusu Ubaguzi.. ile ya Ukabila ipo na ni mojawapo ya mada motomoto za JF. Na kama ukiangalia post zangu tangu mwanzo wa hili nilisema kama mnataka tuzungumzia kujitenga kwa wahindi, au ubaguzi wa aina yoyote ile anzisheni mada hiyo, lakini msimnyime au kumkatalia Richa ushindi wake wa wazi na dhahiri! Kama umekubali kuwa Richa anastahili kuwa Miss Tanzania kama mabinti wengine wowote wale wa Kitanzania, basi tutakuwa tumefikia mwisho wa mada hii halafu twende kwenye suala la Wahindi kujitenga na unyanyasaji wao wa watu weusi, utashangaa kuwa tuko karibu sana kwenye mtazamo kwenye hilo.
 
Wembe, huhitaji ruhusa kuanzisha mada kuhusu Ubaguzi.. ile ya Ukabila ipo na ni mojawapo ya mada motomoto za JF. Na kama ukiangalia post zangu tangu mwanzo wa hili nilisema kama mnataka tuzungumzia kujitenga kwa wahindi, au ubaguzi wa aina yoyote ile anzisheni mada hiyo, lakini msimnyime au kumkatalia Richa ushindi wake wa wazi na dhahiri! Kama umekubali kuwa Richa anastahili kuwa Miss Tanzania kama mabinti wengine wowote wale wa Kitanzania, basi tutakuwa tumefikia mwisho wa mada hii halafu twende kwenye suala la Wahindi kujitenga na unyanyasaji wao wa watu weusi, utashangaa kuwa tuko karibu sana kwenye mtazamo kwenye hilo.

Nadhani wengi wetu tuko karibu sana kimawazo kuhusu jambo hilo...
Tofauti iliyopo kati ya baadhi yetu ni kuwa kuna wale tunaopinga ubaguzi wa aina yoyote ile kwa mtu yoyote na kuna wale wanaopinga ubaguzi wa kubaguliwa mtu mweusi lakini wanaona sawa mtu mweusi kumbagua mtu asiye mweusi kwa kisingizio weusi wamebaguliwa na wanaendelea kubaguliwa sana.
 
Nyani, kwa namna fulani ndugu zetu hawa wanafikiri sisi sote hatujawahi kuishi na Wahindi au hatujui vitendo vya kiudhalilishaji ambavyo baadhi yao wamekuwa wakivifanya. Tofauti yetu na ndugu zetu hawa ni kuwa wakati wao wanataka kulipiza kisasi sisi tunataka vikome na visituambukize. Ndugu zetu hawa wanasema kimsingi kuwa kwa vile baadhi ya wahindi wana tabia hii ya kibaguzi basi sasa hivi ni zamu yao na sisi tutawabagua na tutaanzia na Richa Adhia ambaye ndiyo kwa wakati huu ndiye mhindi anayeonakana zaidi mbele ya watu. Wakiendeleza mawazo hayo wanasema kuwa wahindi wakigundua jinsi tulivyompiga vita Adhia basi watajua kuwa tumechoshwa na vitendo vyao vya kibaguzi. Kwa mtu mwenye maono mafupi mkakati huo unaweza kufaa, hata hivyo ukweli unabakia kuwa kwa kumbagua Richa kutokana na rangi yake ili kuonesha kuwa wanapinga ubaguzi wa watu weusi unaofanywa na baadhi yawahindi, watu hao wanashuka chini na kuwa na wao ni wabaguzi na hivyo hawakomeshi ubaguzi bali wanauhamisha na kuundeleza kwa upande mwingine.

Ndio maana wewe, insurgent, na baadhi ya watu wachache hapa wanaonesha msimamo usiotetereka nao ni kuupinga ubaguzi wa Mtanzania mmoja kwa mwingine kwa mising yoyote ile ya rangi, dini, kabila, asili ya utaifa au tofauti nyingine. Hili ndugu zetu bado hawajaelewa kwani wao wanataka tukubali watu weusi wawabague wahindi ili liwe fundisho kwao wahindi!
 
Jamani ningeshauri kuanzishwa kwa thread nyingine inayozungumzia Ubaguzi rangi na Ukabila Tanzania.Kwa nini ninashauri hivyo?

1)Tanzania tunayo matatizo ya ubaguzi wa rangi hasa
kati ya waasia hasa jamii ya wahindi na ile ya watanzania
weusi.Suala la Richa ni punje tu juu ya mambo yanavyosokota
chini kwa chini katika jamii yetu na wote tumeshuhudia
hilo!.Kwa hiyo naona si vibaya kuwa na thread nyingine
ambayo itaweza kulijadili na kulitafutia
ufumbuzi au kupendekeza majibu.

2)Tuichukulie Tanzania kama Tanzania na siyo nchi kama
Marekani au South Africa na kwingineko.Nchi yetu ina
utamaduni na historia tofauti na nchi nyingine. Kwa mfano
Nchini Marekani suala hili walilijadili na kulitafutia
ufumbuzi karibu miaka arobaini iliyopita ingawa nao haikuwa
rahisi,ilibidi wamwage damu ndipo kieleweke!na mpaka leo
bado wanaendelea kuondoa kasoro zilizobaki ingawa bado kuna
maeneo mengi ya kuyafanyia kazi.Nchini Afrika kusini ni
kweli kwa nadharia tu kuwa ubaguzi umekwisha ila nao bado
mambo si shwari.

3) Kuna baadhi ya wenzetu ambao wanatumia suala la Richa ili kutaka kuondoa au kuipumbaza jamii kuwa hakuna ubaguzi ambao waasia hasa wa jamii ya wahindi wanaoufanya kwa wenzao weusi.Kila mara watu wanapotaka kujadili suala la ubaguzi wa rangi,hawa wenzetu wanalipotosha na kuweka lile la ukabila au la weusi juu ya wahindi.Sasa nadhani thread hiyo inaweza kuyachambua mambo hayo kwa KINA ingawa yote yanaelekea kuwa na dhana moja.

4) Tanzania bado ina matatizo ya ukabila,ingawa mambo haya yanaendelea kupungua siku hadi siku kutokana na jinsi watu wa makabila mbalimbali yanavyojichanganya pamoja na kujiona ni taifa moja.Hali hii si hivyo kwa ndugu zetu wahindi,bado ni taifa la wahindi ndani ya taifa lingine likiwa na passport ya Tanzania. Hii ni tofauti na wahindi walioko marekani ambao hujichanganya na wengine bila ya matatizo yoyote!! mifano tunayo.

5)Mzee wetu Mwl.Nyerere alipambana sana na ukabila na ubaguzi, ingawa naye alielekea kuwaadhibu weusi kuliko wahindi pindi wanapofanya makosa hayo.Karibu hotuba zake zote tangu miaka ya sitini alifokea sana weusi walipotaka kubaguana wenyewe kwa wenyewe au kuwabagua wahindi au waasia lakini sijawahi kuona pale alipodiriki kusema kuwa jamii ya wahindi inakosea inapoamua kujitenga au kuwabagau au kuwanyanyasa wenzao weusi!.Tafadhali mwenye mifano naomba awasilishe hapa tuone!

Ninaomba tu kuwasilisha!

Wembe.

Hayo yote uliyoyasema yana ukweli,tunahitaji kuyafanyia kazi.
 
Hoaja zote zilizoelezwa na wenzangu zina msingi kwa mitazamo mbalimbali.lakini tujiulize jee tanzania ndiyo tunayoitaka kuijenga?Ni kweli kwenye nafasi fulanifulani akiipata mtu mweupe au aliyochanganya uzawa maneno yanaanza bila kutazama tunahoji nini.Jee hao weupe walioshika nafasi kubwa kwenye chama na bunge mbona hatuwahoji au pesa zao zinatufanya tusihoji.Kuna ukweli kidogo kuwa baadhi ya watu weupe ambao ni raia hawajichanganyi katika jamii ya watanzania weusi labda kutokana na imani zao za dini au tamaduni za babu zao.Lakini kuanza kushiriki katika mashindano ya urembo na mengine ambayo hapo awali yalichukuliwa kama ni uhuni yameanza kukubalika katika jamii hizo na ni mwanzo wa kujichanganya katika jamii ya kitanzania. Badala ya kupiga kelele za kibaguzi ninadhani tungeshangilia.Pamoja na hayo alistahili.tuacha kelele za kiswahili bila hoja za mzingi na zenye mtazamo mfupi.
 
Ngoja nimsaidie mwana kijiji. kwa question ya kuwa nci gani hakuna ubaguzi. jawabu ni kuwa pengine hakuna nchi isiyokuwa na ubaguzi so what? kwani ni sifa nzuri kuwa wabaguzi hata kama nch zote zina ubaguzi ndio tuwaige au? kwani sisi hatuwezi kujitafautisha na nchi zote tukawa tuna sifa ya pekee duniani? mbona tunaweza tukijaribu? kwa sababu kuwa wabaguzi sio sifa nzuri na tunalazimika kuacha ubaguzi kwa hali yoyote ila kwani vitabu vya dini vyote vinaelezea ubaya wa ubaguzi na dini zinaeleza wazi wazi namna ya watu kuishi pamoja bila ya kubaguana. ingawa ubaguzi unakuwa ndani ya damu ya binaadamu lakini kama utafata mafundisho ya dini yako yataweza kuondoka maana kitendo vya ubaguzi kinaambatana na shetani tu. bila ya shaka utakuwa umefahamu.
stonetowner
 
Back
Top Bottom