Hoyce Temu na Wabaguzi Mamboleo!

Hoyce Temu na Wabaguzi Mamboleo!

stonetown.. maneno ya hekima hayo... Kuna sifa nyingine si za kujivunia.
 
In any circumstances we can not justify racism. Even if they don't mingle with us but it doesn't matter. Fore sure if you have been discriminated in any way you can not inflict the same pain to any one.I think the whole issue hear is jealous.
 
Mwanakijiji hoja ni nzuri umeileta kwa namna nzuri na unapata mitizamo mingi sana kwa watu mbali mbali...huyu Richa..yeye kama yeye anaweza kuwa hana tatizo...na Hoyce kuria chozi mbele ya watu ilikuwa ni ishara mbaya sana...kwa msomi kama yeye na mwelewa.

Ila ni kwanini watu wengi walikurupuka kupinga uteuzi huo wa binti yule..hii ilikuwa kama vile imepagwa..aliyekuwa kwenye mchakato huo anaweza kuniunga...mkono..walitaka wafanye mabadiliko katika warembo wa tanzania..waonyeshe uko nje kuwa hata tanzia kuna mataifa na watu walihamia na kuwa watanzania japo wana asili ya mbali na hapa.

Na wanaweza pewa haki sawa katika kila kitu...tatizo ni kwamba wamefanya faster sana...

Wahindi kwa ujumla mimi binafsi siwakubali kabisa...hawa leo ukiwaambia kuwa ni watanzania kama hakuna wanalopata kutokana na kukubali kuwa ni watanzania jibu utakalo pata utapigawa na butwaa mwenyewe..tukiongea na ukweli kabisa wako hapa kuchuma na mambo yakigoma wanabaki tanzania ila yakikubali wanarudi kwao..si wenzetu hawa...si yakubali tunabaki yakatae tunabaki.

Labda kama umeandika kupata population na kuongeza article zako kwenye JF ila tukikutana wewe face to face kutoka moyoni wewe wahindi huwakubali.

Angalia hata maisha ya wafanyakazi wao utaona the different ya treatment katika maisha.....leo hii wamekabidhiwa shirika la reli..i hope umesikia habari ya jana watu wamekwama wapi?

Wako hapa kuchuma pesa tu...

Good day

Buswelu
 
Jamani mkiangalia tatizo sio rangi. Tatizi liko katika mgawanyo wa mali. Wanaolalamika majority ni walalahoi. wanaona wahindi kama Gabacholi(Mtikila version). Kwa hiyo wana wa Tnzania weusi wanaona wamebanwa kila nyanja ya maisha na wahindi. Chuki inaanzia hapo. wahindi wankuwa treated vipi na a kina maganga wanakuwa teated vipi. Weusi ni indegneous more than wahindi. wanaonaona nchi inaondoka. Pili watu wengi wanaamini wahindi wengi wana dual au tripple citizeship. Tanzania plus Canada au UK, usa AU India au USA. Kwa hiyo wanaonekana kama si wazalendo halisi. Huyo miss Tanzania ahana Passport ya nchi ingine? tusione matokeo ya watu kulaumu bali chunguza source. Ukifika hapo then you can propose a good mitigating ways kuondoa hali hiyo.
 
Hata hivyo, watetezi hawa wa ubaguzi mamboleo wanashindwa kutuambia ni nani Mtanzania ambaye ana asili ya ardhi hii. Wangoni wanatoka wapi? Wachagga wanatoka wapi? Wamakonde je? Na Wahaya asili yao wapi? Tutawauliza hawa wabaguzi mamboleo (neo-segregationists) je, kama Richa wazazi wake wangekuwa ni Watanzania ambao asili yao ni Nigeria, nao ni weusi, ingekuwa sawa kwa binti huyo kushinda?

Vipi kama ingekuwa ni mtoto wa Wamarekani weusi waliohamia Tanzania miaka ya 60 na licha ya kuwa ni weusi, lakini familia zao zimekaa miaka mia tatu huko Marekani, angestahili kushinda?

Wanasema si hilo tu la wapi anatoka, wanatuambia kuwa Richa hawakilishi rangi ya Watanzania. Kwa hawa wabaguzi mamboleo, rangi ya Watanzania wote ni nyeusi na kama wewe si mweusi, basi Utanzania wako ni robo au theluthi (kutegemea na weusi wako).

Sasa anapotokea binti ambaye ni Mtanzania (kiuraia), lakini si mweusi, wabaguzi wetu wanataka tumtenge kwa vile si Mtanzania kamili? Watu hawa wanashindwa kwa moyo mweupe kuelezea mbona tuna wabunge wenye asili ya Uhindi, tunawafadhili wa klabu wenye asili ya Uhindi, tuna madaktari wa Kihindi, n.k ambao ni Watanzania kwa kuzaliwa.


One of those masterpieces of Tanzanian genius...rare but as all can see always there in people with views such as these. Mwanakijiji, the future of Tanzania needs to built on minds like yours...a true scion of Mwalimu Kambarage.

Lest Richa's detractors forget....it is a Tanzanian of Indian descent who scooped the "UDSM Intellectual of the Millenium Award". None other than the stout widely respected Professor of Law, Issa Shivji. Two other most prolific intellectuals who have put Tanzania on the international map of the Humanities are also of Indian descent. ie. Professor Abdul Sherrif of Zenj and the novelist Moyez Gulamhussein Vassanji. Richa is following a tradition of great Tanzanians of Indian descent envied by their kinsmen even in Kenya and Uganda. Committed Asian Africans whose hearts are in Africa and quite the opposite of the so-called "native Tanzanians" eyeing a US Green Card so that they can escape the Dark Continent and find new lives in the West.

Kudos Mwanakijiji and Kudos Richa. 21st century Africa's destiny lies not in homogenous pasts but heterogenous future
 
Jamani mkiangalia tatizo sio rangi. Tatizi liko katika mgawanyo wa mali. Wanaolalamika majority ni walalahoi. wanaona wahindi kama Gabacholi(Mtikila version). Kwa hiyo wana wa Tnzania weusi wanaona wamebanwa kila nyanja ya maisha na wahindi. Chuki inaanzia hapo. wahindi wankuwa treated vipi na a kina maganga wanakuwa teated vipi. Weusi ni indegneous more than wahindi. wanaonaona nchi inaondoka. Pili watu wengi wanaamini wahindi wengi wana dual au tripple citizeship. Tanzania plus Canada au UK, usa AU India au USA. Kwa hiyo wanaonekana kama si wazalendo halisi. Huyo miss Tanzania ahana Passport ya nchi ingine? tusione matokeo ya watu kulaumu bali chunguza source. Ukifika hapo then you can propose a good mitigating ways kuondoa hali hiyo.

It is not legal to have dual citizenship when one of those citizenships is Tanzanian. Kwa hiyo nadhani hapo hamna ukweli. Katiba ya TZ inasisitiza kwamba mtu ambaye ana citizenship ya nchi yenu, hawezi kuwa na citizenship nyingine.

Dual citizenship can only happen where the two countries you want to belong each has constitutional provisions for dual citizenship.

For example mimi ni mTZ nusu na Mkenya nusu. I could not have both citizenships though I desired such. I had to choose one of the two when I attained 18 years. I chose the Kenyan one.

Kenya like Tanzania only allows one citizenship.

India on the other hand and Canada allow dual citizenship. So you can be a Canadian/Indian citizen. But you cannot be a Tanzanian/Indian or Tanzanian/Canadian citizen. Because although Tanzania and India accept dual citizenship, Tanzania (the other citizenship mtu angependa kwa mfano) does not accept such a legal status.

Kwa hiyo kuna asilimia ndogo tu ya wahindi wetu ambao wanahold dual citizenship eti ya TZ na kwengineko. Na wanafanya hivyo wakijua hilo ni makosa kisheria.

Richa Adhia na maprofesa Abdul Sherrif na Issa Shivji ni waTanzania kamili na hamna haja ya kujaribu na kuweka scapegoats kwamba ni wahindi ndio wanaoleta umaskini wa waafrika asilia Tanzania. The question of Tanzanian poverty is multifaceted. Politics, economics, history na vingine vingi vinachangia.

In my opinion the Jew and the Indian are just cogs in the unjust structure of Capitalist societies. The problem lies with the economic system and it is political will and praxis that can alter this. Nyerere did his best. You saw the benefits. Its time for the likes of Mh. Rais Kikwete and his generation to do their bit. I am glad that Jitto has emerged and one of the unfair arenas of the Tanzanian economy, ie Mineral Industry is now in critical political focus.

Maoni yangu Wakuu.

Shukran
 
Mimi linaniumiza jambo moja kuhusu huu ubaguzi wa rangi. Katika sehemu zote ninakoona au kusikia ubaguzi wa rangi, ni mtu mweusi ndiye anayebaguliwa na kunyanyaswa. Sijaona popote ambapo mtu mweusi anabagua na kunyanyasa watu wa rangi nyingine. Je hii inatokana na wema wa watu weusi (kwamba kamwe hawana tabia ya kumnyanyasa tu yeyote), au unyonge wao (kwamba hata wangetaka kunyanyasa, hawana ubavu huo, kwa hiyo wanateswa tu). Yaani sisi tuna nini kwenye hizi rangi nyeusi zetu, au kuna zaidi ya rangi? Weusi wa Amerika, Australia, India, Afrika, kila mahali tunabaguliwa tu sisi, nini hii bana? Kwa nini tusiamue siku moja ku-revolt, potelea mbali tubaki na umaskini wetu? Ah!
 
Richa adhia out.......,Je angeshinda miss world ingekuwaje??wahindi wangejaa airport kumpokea na weusi wasingepata nafasi ya kumshika hata mkono??Kabla ya kuondoka alifanyiwa pati kubwa sana na wahindi.
 
Jambo la Msingi hapa ni Je kubaguana ni vema ? la hasha si jambo la busara kabisi na halipaswi kuendelezwa na wote wenye hekima.
Je kama jirani yako anafanya mabaya nawe ushindane naye kwa ubaya ? nadhani hupaswi kufanya hivyo ama sivyo wote mtainngia katika kundi moja la wasio na hekima. Kama wahindi wao wanijibagua na kubagua wengine sisi tusiwaige,tuendeleze kuhuhubiri na kutenda tunachoamini ni chema ."Si vema kujifunza kutoka kwa wajinga"
 
mzee mwanakijiji anauliza ninani ameishawahi kutongoza binti wa kihindi akakataliwa,kwanza utamuona wapi,muda wote wamefungiwa getini,na akijaribu kukubali familia itamtenga.achana na wale wanaojiuza Q BAR,Bilicanas nk.hao ni wahindi-koko.siyo siri wahindi ni wabaguzi,ebu waulize dada zetu kutoka Iringa,wanaofanya u-house girl kwa wahindi watakueleza wanavyobaguliwa,wanatupiwa chakula kama mbwa.
 
Mimi nadhani kutumia mfano wa Richa Adhia kuzungumzia ubaguzi si sahihi.
- Watanzania wengi hawakulalamika kwa sababu alikuwa mhindi, ile ilikuja kama issue baada ya kushindwa kwa wengi kuexpress kile walichoona ni upendeleo. Angekuwa mchagga wangesema mchagga huyooo! It doesn't matter. Wao walichoona ni ule upndeleo ulioendelea stejini, kwamba walipobaki Victoria na Richa lile bakuli lenye masuali lilitolewa wakasimama kwa muda. Bakuli iliporudi, Victoria alivuta swali na akakuta ni swali ambalo hawakupangiwa (can you imagine warembo wamepewa maswali in advance matano ukiingia top 5 these are the 5 possible questions!? Ni viini macho tu!) Kwa hiyo Victoria alikuta swali ambalo alipata halikuwa miongoni mwa yale matano waliopewa! Na kusema Richa alijibu vizuri zaidi, jamani binti huyu anaongea primarily English na Kiswahili chenyewe kinampiga chenga. So of course atajibu kwa kiingereza fasaha. Anyway to make the long story short, alishinda katika mazingira ya kutatanisha.
- Suala la rangi ya ngozi aliliibua Lundenga aliposema kwamba Richa ataenda kufanya maajabu kwa sababu 'amefanana nao' Yaani mimi niko against not only racism but prejudice na sentensi hii ilinitia hasira! He was playing the race card when convenient.
- Richa hakuwa the best miongoni mwa wasichana siku hiyo, na Hoyce alieleza kwa nini. Haya sasa someni Lundenga anavyojitetea kwenye magazeti baada ya Richa kuanguka vibaya Miss World. Eti anasema 'ni jukumu la kila mtanzania kutafuta mwakani mrembo anayefaa kwani wameweza kuona kwenye luninga warembo wanaotakiwa hivyo mshindi mwakani afanane nao' (kwenye gazeti la Mtanzania)!
Mmh! Hii kali! Sasa ameona baada ya mchina, mwangola (ambaye ni shombe but looks black) na mexican (hispanic) kushinda anasema sasa wafanane na washindi? Huyo hajui kazi.

Tanzania na watanzania sio wabaguzi nimekataa! Suala hili la Richa is a result of Lundenga and company kubangaiza matokeo na kuongea pumba na kusababisha mtafaruku katika jamii. Nahoji tena, mbona alipoenda Miss Earth mwaka 2006, watu hawakumsema Richa? Think!
I am against racism, but Tanzanians are not racists generally. Individuals may be but this is true of all races kuna wabaguzi wahindi, wabaguzi waafrika, wabaguzi wazungu, wabaguzi wachina n.k. But generally Tanzania is NOT a racist society.
 
HUU NI UBAGUZI!
Bango la nafasi za kazi ya muuzaji kwenye famasia lililobandikwa katika moja ya maduka ya Shoppers Plaza, Dar es Salaam, likionesha sifa mojawapo ya mwombaji ni kuwa Mtanzania mwenye asili ya Asia. (Picha na Emmanuel Kwitema)

5357.jpg


Hili Tangazo la kibaguzi la ajira linapaswa kulaaniwa na kila Mtanzania
Chanzo, Majira 18/01/72007
 
5357.jpg


Hili Tangazo la kibaguzi la ajira linapaswa kulaaniwa na kila Mtanzania
Chanzo, Majira 18/01/72007

Sio kulaaniwa tu, kuchukuliwa sheria na hiyo biashara iwe boycotted. Nimeona matangazo yanayosema mwombaji lazima ajue kigujarati au kihindi! Ni watu kama hawa ndio wanaopakazia jamii nzima ya waTanzania wenye asili ya uhindini. Hivi leo unaweza kuweka tangazo kuwa nafasi hiyo ni ya wamakonde tu? Kama unataka mhindi au mmakonde mweke bila kuweka matangazo kama haya!Hivi hatuna sheria inayopinga ubaguzi? Hivi jina la hiyo famasi limetajwa?
 
Kwanza nitaongelea kundi la watu, najua mara zote unapoongelea kundi la watu kunakuwa na "exception to the rule"

Sina nia ya kumtetea mbaguzi yeyote, na ninaelewa kwamba makosa mawili yanayokinzana hayafanyi mambo kuwa sawa.Nakemea kauli au vitendo vyo vyote vya kibaguzi mahala popote, regardless.Baada ya kusema hivyo ningetaka pia kuweka vitu katika "context".

Hakuna mtu mbaguzi kama muhindi, ubaguzi wa muhindi umekuwa institutionalized katika dini na jamii nzima kwa mpango wa caste system.Muhindi anawabagua hata wahindu wenzake wasio "caste" moja, itakuwa mswahili? Hata hapa Marekani ni nadra sana kuona muhindi ameoana na mtu wa asili nyingine.

Watanzania hawana ubaguzi kiasi hicho, ukitaka kujua ona watu wanavyowachangamkia wageni kutoka sehemu mbali mbali.Wahindi wanataka kula keki yao halafu ibaki.Wanataka uraia wa Tanzania lakini hawapo kwenye majeshi ya ulinzi, hawataki kuchanganyika na Watanzania wengine, hawataki kujifunza Kiswahili.

Sasa nani mbaguzi hapo?
 
Watanzania hawana ubaguzi kiasi hicho, ukitaka kujua ona watu wanavyowachangamkia wageni kutoka sehemu mbali mbali.Wahindi wanataka kula keki yao halafu ibaki.Wanataka uraia wa Tanzania lakini hawapo kwenye majeshi ya ulinzi, hawataki kuchanganyika na Watanzania wengine, hawataki kujifunza Kiswahili.

Hatuwezi katika nchi huru kulazimisha raia wetu kufanya kazi fulani au kuchanganyikana na wengine. Tunachoweza kufanya ni kuweka sheria ambazo zitaweka bayana ni vitendo gani vitaeleweka kama ubaguzi na kuwa havina nafasi katika jamii. Vitendo kama vilivyowekwa hapo juu kwenye bango wala havihitaji sheria. Ni wananchi wote (waswahili,wahindi na wazungu n.k) kuungana na kuonyesha kutovikubali. Mimi naamini kama watu watafanya campaign ya kutokununua dawa katika duka hilo, wenye tabia kama hii watajifunza. Hii campaign iwahusishe na wale wageni waishio kwetu. Wakae vijana na mabango nje ya famasi husika(kama haiwezekani basi nje ya geti la Shoppers Plaza), media na yenyewe ilivalie njuga suala hili kwa kupanua wigo na kuangalia maduka mangapi ambayo yameajiri kwa misingi hii, pamoja na wale wamatumbi wenzetu. Tukionyesha wenyewe kuwa tumechoka na hatutakubali kubaguliwa na yeyote nchini mwetu, tutafanikiwa.

Kama tunaona ni muhimu kwa mtu yeyote anyetaka uraia wa Tanzania kujua kiswahili basi na yenyewe tuiweke kwenye sheria. Maana yake ni kuwa mtu yeyote anayeomba uraia ni lazima ashinde mtihani wa kiswahili. Kwa wale waliozaliwa na wazazi walio tayari ni raia hatuna jinsi. Wengine watakuwa wamezaliwa nje ya nchi na hawakupata nafasi ya kujifunza lugha hii. Hao tuwaache walivyo.
 
Tina kuna msichana alishinda huko nchini Belgium na akashindwa kuongea ki-native chao na ilkuwa scandal sana..Kwa hiyo i will feel proud kama miss Tz akaongea ki Swahili.Jamani imefika wakati wa jujivunia lugha yetu
 
hii lugha ambayo inavunjwa vunjwa Bungeni? Haionekani tutawabagua "waswahili" wenzetu ambao lugha ya Kiswahili kwao bado ni ya kigeni...?
 
Kama inavunjwa vunjwa kemea kuvunjwa vunjwa pia, usitumie mapungufu kuhalalisha mapungufu mengine.
 
hii lugha ambayo inavunjwa vunjwa Bungeni? Haionekani tutawabagua "waswahili" wenzetu ambao lugha ya Kiswahili kwao bado ni ya kigeni...?

Pengine kuvunjwa vunjwa huku ni katika kuonyesha kuwa muongeaji madarasa yamepanda ndio maana anachanganya lugha!
 
Back
Top Bottom