HR, Waajiri walalamika wahitimu ni weupe vichwani

HR, Waajiri walalamika wahitimu ni weupe vichwani

HR flani alilalamika wahitimu wengi Ni weupe vichwani na kuuliza Nini kifanyike

Nilikuwa na haya yakujibu!
Ushauri chakufanya Ni kwanza wakufunzi hasa wa vyuo vikuu waanze kufundishwa maarifa ya kisasa
Pili tujaribu kuchukua wakufunzi kutoka vyuo Bora vya nje inaweza kuwa kwa mpango wa kubadilishana.
Tatu : tuangalie tunapokwama kwenye mitaala yetu
Nne: Muda wa mafunzo ya vitendo angalau uwe muda mrefu kuliko ule wa kusoma darasani ,, badala ya mtu kwenda field miezi 3 mwanafunzi aende mafunzo ya vitendo angalau miaka miwili.
Tano : ipo mifumo inayomruhusu mwanafunzi kujifunza zaidi ya kile anachopewa darasani Yani maswali yanayochochea upimaji na sio yanayomlazimisha mwanafunzi kukariri kitini Cha notes
Waajiri wamekuwa wabinafsi sana, ni kweli vijana wanamaliza vyuoni wakiwa na distinction kwenye vyeti ila vichwani hawana ubunifu lakini ni mwajiri gani ametumia muda kumoatia induction course hata ya wiki mbili mwajiriwa mpya? Policy zao zinatoa hiyo nafasi?
Wakati mwingine ndio maana vijana wanaona mwajiri mzuri ni serikali maana wanalea watu kwa vikozi kadhaa mara kwa mara kuongeza ujuzi ila waajiri binafsi anataka mfanyakazi mzuri ila ambaye hajamtengeneza no wonder hauwezi kupata mtu mwenye uzoefu kazini.
 
Tatizo si wahitimu kuwa na uwezo mdogo..

Tatizo ni expeditions kubwa walizonazo waajiri ambazo akikuajiri anataka uzifikie kwa muda mfupi, na wakati huo ukiangalia ni jambo ambalo haliwezekani...

Tatizo pia waajiri wengi (hasa maboss/wamiliki wa makampuni na taasisi) kupenda pesa zaidi kuliko kutoa huduma... Kunamfanya afocus kwenye utendaji wa kuchakata pesa zaidi kuliko huduma... Hapa sasa unakuta boss ana mipango yake kichwani ambayo haiendani na mipango kazi... Unajikuta anakuforce ufanye anavyotaka na sio taaluma inavyotaka, mwisho wa siku inapoteza hamu ya ufanyaji kazi... Unaamua kwenda tu ilimradi Liwale na liwe

Tatizo lingine maHR wengi siku hizi hawajisumbui kutafuta watu, badala yake wanawatumia ma agent kupata watu, huko unakutana na mtu ambaye pengine wala hana taaluma ya hiyo kazi, ana experience ya kughushi... Akiingia kazini ndio matatizo yanaanza

Yapo mengi sana, ila mengi yanatokana na maboss wenyewe na sio wahitimu
Well stated.
 
Back
Top Bottom