Nashukuru Mungu nilizaliwa miaka ile picha zinahifadhiwa kwenye kitabu maalum aka albamu na kuandikiana barua kwa kalamu na karatasi. Hivo kuondoa hasira nachukua albam zote za zamani naanza kuangalia picha moja baadae ya nyingine, kabla sijazimaliza nakuwa nshasahau kama nilikuwa na hasira au kuna mtu alinikasirisha.
Pia huwa nachukua boksi langu ninalohifadhia barua zangu na posti kadi. Naanza kusoma moja baadae ya nyingine najikuta naishia kucheka hasira kwishney.
Ingine natafuta muvi nzuri ya Mahaba au true story au vichekesho yaani nikitoka hapo mweupeeee.
Ingine naanza kuimba na kucheza kama nipo nyumbani,kama kazini ntaweka mziki masikioni au wa sauti ndogo au ntaimba kwa sauti ndogo huku naendelea kufanya kazi.
Ingine naingia kabatini, natoa nguo ambayo nikiivaa najua nimependeza aka bibi bomba. Najipa mtoko wa dinner na mziki hadi nichoke, huko ntayekutana naye ajue kunitabasamisha, makumbato yangu atayapata mengi tuu.
Nikishindwa kufanya vyote hivo kutokana na mazingira, naenda beauty parlour, nafanyiwa manikyua, pedikyua, masaji na shevingi ya pubiki hea....
Nikitoka hapo raahaaaa ndani ya rohooo,kwatuuuu.
K' Matata.