Huduma ya Kipimo cha MRI katika Taasisi ya Mifupa MOI ni kero kwa Wagonjwa

Black Butterfly

Senior Member
Joined
Aug 31, 2022
Posts
130
Reaction score
368
Niende moja kwa moja kwenye hoja yangu.

Oktoba 9, 2023 nilikwenda kumpeleka Ndugu yangu pale MOI kwaajili ya kupata vipimo kutokana na hali yake kiafya kusumbua kwa muda mrefu. Kufika pale Daktari akamwandikia kipimo cha Magnetic Resonance Imaging (MRI) ili kubaini tatizo lake. Balaa likaanza kufika Lab, kuna foleni ndefu kuzidi mwendokasi za Kimara.

Ikabidi tuchague siku za mbele ambazo zinakuwa hazina watu wengi. Tukachagua Alhamisi Oktoba 12, 2023, Ndugu yangu alikuwa kama mtu wa 10 katika list ya watakaofanyiwa uchunguzi siku hiyo, sasa licha ya kufika mapema kwenye muda tuliopangiwa tumekuja kupata Kipimo masaa 10 baadaye. Na tulipohoji kwanini inakuwa hivyo majibu yao ni mashine ilikuwa mbovu kwa siku 2 hivyo Wagonjwa wa siku hizo mbili wameingizwa kwenye siku hii.

Hilo sio tatizo sana, issue ni kwanini Hospitali kubwa kama Moi inayohudumia Wagonjwa wa karibu Nchi nzima kwenye masuala ya Mifupa iwe na Mashine moja tu ya kufanya Vipimo? Yaani pamoja na Kodi na Tozo zote tunazopigwa na Serikali inashindwa kununua mashine hata 5 kuzifunga pale MOI kweli? au ni kupuuza Afya za wananchi kwasababu hawana la kuwafanya?

Hebu fikiria Mashine moja ihudumie Wagonjwa wa Ndani (Waliolazwa, na wengine wanatoka ICU kila muda na kusababisha Wagonjwa kusubirishwa au kuondolewa kwenye mashine ili mgonjwa wa ICU aingia, what a shame), bado hiyo hiyo ihudumie Wagonjwa wa nje na wengine wenye Rufaa zao. Ni aibu kwa Nchi inayotumia mabilioni ya Fdha kutangaza vitu vya ajabu ikiwemo Royal Tour wakati Mahospitali hakuna Vifaa Tiba na Wahudumu Wachache.

Ni hayo. Badilikeni
 
Mwaka 2014 kikwete alinunua gari zaidi ya 10 za polisi zile za kumwaga maji kwa presha na udambwiudambwi mwingine wa kumtesa atakayeandamana

Nia ni kumtisha MWANANCHI atakayejaribu kuleta fyoko kwenye UCHAGUZI kukiona
tena wenyewe walikuwa wanatamba na kuzipamba ni kwa ajiri ya UCHAGUZI ujao 2015

Miaka miwili mbele nikazikuta zile gari chang'ombe polisi zimeotaa kutu hata zingine kutumika hazijawahi kutumika
Na gari 1 walisema wamenunua milioni 700
Wakati hicho kipimo cha MRI na CT SCAN Bei yake ilikuwa milioni 500
Nilivyoyaona yale magari ya mln 700 yameota kutu
nikawaza MUHIMBILI kipimo cha MRI CT scan vinakaa hata mwezi vibovu dah niliumia sana pesa iliopotezwa pale nikajiuliza WHY wasingeongeza CT SCAN au MRI pale muhimbili
 
Karma is a bitch. Kwa kiburi kile cha kikwete kununua yale magari ili yaje yatese watanzania wasio na hatia kwa bei ya 700 we are still watching.
 
 
Nchi hii kwenye mambo mengi ya msingi ni bora liende!

Ukisikia press zao za kupandikiza mara uboho,figo,ini etc unaweza fikiri tupo serious sasa.

Nawasikitikia hao watakaoenda hapo kufanya hizo operation za kurekebisha maumbile sijui "shape".

Ku-risk maisha yako kwa ajili ya urembo tu kwa nchi kama hii ni ujinga
 
Karma is a bitch. Kwa kiburi kile cha kikwete kununua yale magari ili yaje yatese watanzania wasio na hatia kwa bei ya 700 we are still watching.
Mwisho wa siku aliyeweka yeye!
 
hii ni bei ya MRI ya kisasa kabisa ndizo zilizofungwa taasisi za serikali ni pesa ya India milion 130 ambayo ni sawa na bilion 4+
Hiyo nayo ni pesa sasa kwa serikali tena kwenye suala nyeti la afya?

Gari analotembelea DED Kahama MC pekee ni 460M huku yule wa Geita TC aliyefutwa kazi lilikuwa 400M.

Na yote yalinunuliwa nje ya utaratibu.
 
Amna CT SCAN na MRI kwa macho kama sio mjuzi huwezi jua kipi ni kipi
Kiumbo kila kitu sawa ila vina utofauti mdogo sana ambaye kma sio mambo ysko hutaweza kutofautisha mpk uambiwe
Tofauti kwa asiyefahamu ni ndogo sana
 
Muhimbili ni rushwa hadi kwenye kifungua faili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…