Huduma ya kusambaza maji imewashinda mmeamua kufanya biashara ya kuuza mabomba kwa Wananchi

Huduma ya kusambaza maji imewashinda mmeamua kufanya biashara ya kuuza mabomba kwa Wananchi

MSHINO

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2013
Posts
1,069
Reaction score
713
Napenda kuishauri serikali kuu kuzuia taasisi zake kuacha biashara ndogo ndogo kwani kufanya hivyo ni kuzuia kukua kwa biashara na wajasiliamali kwa ujumla hivyo kupunguza mzunguko wa pesa na kuikosesha serikali kodi. Mfano shirika la kusambaza maji Morogoro MOROWASA linalazimisha wananchi kununua vifaa vya kuunganishia maji yaani mabomba na viunganishi vyake kutoka MOROWASA.

Iwapo mwananchi atafanya hivyo MOROWASA hawamuunganishi mteja maji japokuwa atakuwa amepewa ruhisa na michilo na MOROWASA. Imekuwa ikisababisha ukiritimba ambao unasababisha wananchi kuchelewa kupata huduma ya kuunganishiwa maji.

Kwa sasa ili mwananchi aweze kuunganishiwa maji anatakiwa kulipa gharama zifuatazo au Zaidi kulingana na umbali kutoka bomba kubwa:
  • Vifaa 250,000.00
  • Ada 50,000.00
  • Ufundi 20,000.00
  • Jumla 320,000.00
Iwapo wananchi watanunua kwa wafanya biashara wa kawaida serikali itapata mapato ya kodi huku gharama zikipungua. Au MOROWASA ifanye isiwe lazima mwananchi afanye maamzi mwenyewe wapi anunue mabomba.

MOROWASA wameshindwa kusambaza maji sasa wameamua kufungua biashara ya hardware na kuuza vifaa vya ujenzi. Sehemu nyingi maji hayatoki. Mfano Kihonda, kiyegea, mkundi na nk. hakuna hudima za amaji japo morowasa wanaendelea na huduma ya kuuza vifaa.
 
MOROWASA kuna tatizo kubwa
 
idara za maji karibu wilaya/mikoa yote ni wapuuzi huku katavi wanachaji tsh 2,500 kama pesa ya kufanyiwa service kila mwezi ila ukipata tatizo wanakutaka ununue tena mwenyewe vifaa ili hali kila mwezi wanakusanya pesa hiyo.

tanesco naona wanaelekea kuzuri.ila idara/mamlaka za maji ni hovyo mwanzo mwisho.
 
Muwasa Mwanza mbona hyo system inakarbia miaka miwili tangu kuanzishwa sehem zangu zote za biashara mwendo ulikua huo .
Wanakuja na ka kifaa kao ka ku detect Bomba lilipo kale ka kifaa kakishindwa kupata Bomba jitayarishe kutoa gharama za kusaka Bomba lilipo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom