Huduma za kufanyiwa mchakato wa hati, kufanyiwa uthamini (Valuation) na masuala yote ya ardhi

Huduma za kufanyiwa mchakato wa hati, kufanyiwa uthamini (Valuation) na masuala yote ya ardhi

Mkuu naomba utupe process zako zote kuanzia mwanzo hadi mwisho ili mtu akikufuata awe anajua procedure zote.Mfano mm kuna shamba langu nataka nilitafutie hati km heka kadhaa na nimeona eneo lipo humu kwenye hyo attachment yako.Ninaanzia au ww utaanzia wapi had kuishia wapi mpaka nipate hati yangu na gharama zinaweza kuwa kias gani?Nenda kwa mfano tu ili niweze kujua naimudu au vp?
Hapa inategemeana kama eneo lako limepimwa au halijapimwa.

a) Kama eneo halijapimwa inatakiwa lipimwe na kusajiriwa.Upimaji unaweza ukafanywa na kampuni binafsi au wapimaji wa halmashauri husika.

Baada ya kupimwa,kupitishwa na kusajiriwa hatua ya ufatiliaji hati inaweza kuendelea (nitaelezea chini hatua za kufuata)

b) Kama eneo lako limepimwa na kusajiriwa kinachofuata hapo ni kufatilia mchakato wa hati ambao unahusisha hatua zifuatazo

i)Kujaza Fomu ya maombi ya kupatiwa hati

ii) Uhakiki wa taarifa za kiwanja na muhusika.Hatua hii inajumuisha kufanyika kwa uhakiki wa kiwanja kinachoombewa hati kama kimepimwa na kusajiriwa lakini pia kuhakiki umiliki wa muombaji wa hati

iii)Hatua inayofuta ni kupewa gharama ambazo
utakiwa ulipie ili kufanikisha zoezi la kupata hati.Gharama hizo ni

Premium fee: Eneo la kwanja x Gharama ya kiwanja kwa mita mraba x 0.025

Registration Fee: Hii inatozwa 20% ya kodi ya ardhi ya mwaka

Survey Fees: Hii hutegemea na hamashauri husika

Certificate of Preparation

Deed Plan Fee

Stamp Duty

iv) Utatakiwa pia uwasilishe picha za pasipoti saizi za rangi za hivi karibuni.
 
Binafsi, nimekutana na Wapimaji Ardhi wa Private ni watu ambao wanajitambua sana kwa kweli. Kwa maana ya kwamba wana customer care nzuri kwa wateja wao. Ila usiombe ukutane na Maafisa Ardhi walioko Serikalini hasa kwenye Halmashauri za Wilaya, Manispaa na Majiji yaani ni waongo, wala rushwa na hawajali muda wanaotumia wateja wao kufuatilia masuala ya ardhi. Hawa Wapimaji Ardhi wa Private kidogo kwenye gharama huwa nao hawana gharama rafiki.
Kwanza niwapongeze kwa kitu huduma mnayofanya. Mna nafasi kubwa sana ya kufanikiwa na kujitanua iwapo mtazingatia huduma bora na za uhakika. Kwa exeperience yangu ya Tanzania ni kwamba sehemu/kampuni/watu wote wanaohusika na kutoa huduma wamejijengea utamaduni wa kutanguliza tamaa mbele na kutokuwa waaminifu. Naomba niwape ushauri ufuatao:
1: Ongezeni (hama hamna) huduma ya kusaidia wateja kuhakiki viwanja wanavyotaka kununua kama ni halali au vina mgogoro. Hili ni jambo gumu kidogo lakini mkitengeneza network nzuri na mamlaka husika mnaweza kuwa na taarifa sahihi, hivyo kwa mfano mtu anapotaka kununua kiwanja, atumie huduma yenu ya kitengo cha upelelezi kujua kama kiwanja husika kina uhalali.
2. Pamoja na hili nawashauri pia jaribu kufanya huduma zenu ziwa za kuaminika na customer care iwe nzuri. Tanzania sehemu nyingi za huduma wanatoa kauli mbovu na wanatanguliza tamaa mbele.
 
Okay Mkuu karibu sana
Vilevile usivunjwe moyo na hao wanaokutishia. Maana hujavunja Sheria yoyote katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Watu wenye taaluma kama yako ambao ni wachoyo wapo wengi. So, wewe Songambele, sisi tutawafikishia ujumbe mamia na maelfu ili wapate huduma yako.
 
Vilevile usivunjwe moyo na hao wanaokutishia. Maana hujavunja Sheria yoyote katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Watu wenye taaluma kama yako ambao ni wachoyo wapo wengi. So, wewe Songambele, sisi tutawafikishia ujumbe mamia na maelfu ili wapate huduma yako.
Shukrani sana mkuu
 
Nawezaje kutumia hati ya kiwnja kupata mkopo kama sina salary slip wala biashara?
Kwa benki au taasisi nyinginezo za kifedha ukiwa na hati ni rahisi kupewa mkopo.Huwa mara nyingi wanapendelea mali isiyohamishika ambapo hii inahusisha nyumba au kiwanja.

Baada ya kujaza form za maombi ya mkopo,watafanya uthamini wa nyumba/kiwanja chenye hati husika kwa ajili ya dhamana.

Baada ya kufanya uthamini na kupata thamani ya dhamana,utapata mkopo ambao ni chini ya thamani ya dhamana.Mfano kama nyumba yako ina thamani ya milion 50 hautopewa mkopo wa milioni 50 yote bali utapewa chini ya hapo lets say 40m.
 
This is nothing but an act of selfishness and greed. Hakuna ubaya wow one wa mtu mwingine kutuelimisha na huenda siku za usoni tukafanya biashara, hiyo VRB unategemea tungeijua vipi?

Na pia sasa tupo kwenye uchumi wa huduma kuwafuata wateja hivyo so dhambi akifanya hivyo.

Mkuu hawa watu ndio wanafanya hii nchi inaendelea kuwa maskini bila matumaini kwa mambo ya kizamani kabisa kama haya.

Wanajua kbs elimu ni investment, mtu anaenda kusoma kwa kulipa mamilioni ya pesa kwa cash au mkopo ambao baada ya hapo unahaingaika kulipa maisha yako yote hawana msaada hawa, unalipia leseni (professional), unalipia mibodi fees yao, nk nk halafu wanakuja kuleta masharti ya kishamba kbs wakati watu wanataka kurudisha investment zao walizofanya (RoI). Wanajifanya wanajua usimamizi wakati hamna tija yoyote wanayoleta eti taaluma yetu, my ass!!. Mnasimamia nini wakati nchi zaidi ya 80% haijapimwa? wanajifanya wana taaluma, wakati waanzilishi wa hii mifumo mabeberu walishaacha ushamba wa namna hii karne nyingi kule na kila taaluma ilishakuwa biashara (industry) sijui wanavosikia uchumi wa viwanda wanaelewa nini? Au ndo uzee wa kizazi cha miaka ya 60 kurudi nyuma wanakwamisha sana hii nchi kwa mapokeo yaliyopitwa na wakati! na uselfish pia

Mtu anatangaza huduma na watu wanataka huduma wanakwamishwa na mifumo iliyojaa watu wa namna hii eti wanatisha kbs tunakujua tutakufuatilia, ushamba mkubwa, bora kafuta post yake. Huduma zenyewe maofisini kwao mbovu kama nini halafu watu wakiibuka kusaidia na kucapitalize kwenye udhaifu wao wanakuja hapa kwa vitisho. Hopeless.

Watu wamechoka na Rais anasema kila siku sera na sheria zilizopitwa na wakati zifutwe/ziboreshwe unakuta ndo hawa watu wanahusika na kukwamisha hadi wanakuja kujionyesha hapa kwenye jukwaa! Pissed off. Sasa bila watoa huduma kutangaza watu watajuaje kuna huduma, hata chanjo zinatangazwa itakuwa kupima ardhi? Halafu tunalalamika umaskini hatukopesheki na bank zinataka ardhi iliyopimwa huku board inataka watu wasijitangaze, mtu ajisomeshe, alipe leseni, anunue vifaa vya upimaji, matotal station, RTK, alipe ofisi, na mijikodi ya kutosha halafu asubiri wateja waletwe na nani? wanakuja kama mvua?
 
Back
Top Bottom