Huduma za Uvushaji wa MV Kigamboni zasitishwa

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
1717698297937.png



KUSITISHA UTOAJI HUDUMA YA UVUSHAJI KWA KIVUKO MV. KIGAMBONI
Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) unawataarifu watumiaji wa kivuko Magogoni Kigamboni na wananchi kwa ujumla kuwa, Kivuko MV. KIGAMBONI kinachotoa huduma eneo hilo, kitasimama kutoa huduma kuanzia alfajiri ya siku ya Ijumaa Tarehe 07 Juni, 2024.

Kivuko MV. KIGAMBONI kinasimama kutoa huduma kwa ajili ya kwenda kufanyiwa ukarabati mkubwa ili kitakaporejea kiweze kutoa huduma kikiwa katika hali ya ubora na usalama.

TEMESA inawashauri abiria hasa wenye magari kwa sasa, kutumia njia mbadala ya Daraja la Mwalimu Nyerere ili kuepusha msongamano katika eneo la kivuko mpaka pale kivuko MV. KIGAMBONI kitakaporejea.

Aidha, shughuli za uvushaji katika eneo hilo, zitaendelea kutolewa kama kawaida kwa kutumia kivuko MV.KAZI pamoja na Sea Taxi.

TEMESA inawaomba radhi abiria wote kutokana na usumbufu watakaoupata wakati wote ambapo kivuko MV. KIGAMBONI hakitakuwepo na inawakumbusha kuendelea kufuata maelekezo ya mabaharia wakati wanapotumia vivuko ili kuendelea kuwa salama.

Imetolewa na Kitengo cha Masoko na Uhusiano
TEMESA
06/06/2024

PIA SOMA

- Abiria tunaovuka Kivuko cha Kigamboni leo ni kero tupu, kivuko kimoja tu ndio kinafanya kazi

- Changamoto ya Vivuko Kigamboni kwa sasa kunafanya kazi kivuko kimoja tu

- Vivuko vimekuwa kero, wanatoa taarifa za ghafla kuwa hamna huduma

- Huduma za Vivuko Kigamboni janga linaloenda kusababisha maafa nchini

- Huduma za Uvushaji wa MV Kigamboni zasitishwa
 
Nchi imekuwa shamba la bibi.mwezi wa tatu kilipelekwa Kenya kutengenezwa kikakomba bilioni saba na kimetumika miezi mitatu kimeharibika Tena.Nchi imeoza kabisa Hadi imezidiwa na Nchi ya nje ya Zanzibar
 
1.jpeg


Kigambo ni kama kisiwa ila si kisiwa, ni wilaya mpya iliyomegwa kutoka Temeke ili kuongeza nafasi za wanasiasa.
ni eneo la wahamiaji na makazi mapya, ilipokuwana mradi mkubwa wa nyumba za ECO, DEGE, NHC na NSSF.

Watumiaji wa kivuko Magogoni Kigamboni na wananchi kwa ujumla wanaarifiwa kuwa Kivuko MV. KIGAMBONI kinachotoa huduma eneo hilo, kitasimama kutoa huduma kuanzia alfajiri ya siku ya Ijumaa Tarehe 07 Juni, 2024.

Taarifa ya Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) imebainisha kuwa Kivuko hicho kinasimama kutoa huduma kwa ajili ya kwenda kufanyiwa ukarabati mkubwa ili kitakaporejea kiweze kutoa huduma kikiwa katika hali ya ubora na usalama.

“TEMESA inawashauri abiria hasa wenye magari kwa sasa, kutumia njia mbadala ya Daraja la Mwalimu Nyerere ili kuepusha msongamano katika eneo la kivuko mpaka pale kivuko MV. KIGAMBONI kitakaporejea.” imesema TEMESA

“Aidha, shughuli za uvushaji katika eneo hilo, zitaendelea kutolewa kama kawaida kwa kutumia kivuko MV.KAZI pamoja na Sea Taxi.”

“TEMESA inawaomba radhi abiria wote kutokana na usumbufu watakaoupata wakati wote ambapo kivuko MV. KIGAMBONI hakitakuwepo na inawakumbusha kuendelea kufuata maelekezo ya mabaharia wakati wanapotumia vivuko ili kuendelea kuwa salama.” TEMESA
 
Kazi imewashinda,kwa nini wasiwape watu binafsi waendeshe hiyo huduma hapo..UDART hoi,TRC hoi,TAZARA hoi,sasa nyie ni watu wa namna gani?
 
Kama ndo hivyo basi Sea Tax ziwe zinafanya kazi tatu na isiwe mwisho saa mbili usiku bali vifanye kazi mpaka saa nne au saa tano usiku
 
Tuna wabunge mizigo sana Kwa Nini wasiiyambie serikali iachene na hicho kivuko wapewe watu binafsi wakiendeshe

Kila siku kivuko kinatengenezwa Kwa kutumia mabilioni ya walipa Kodi hi nchi mda si mrefu itakuwa mufilisi
 
Nchi imekuwa ya ovyo sana. Wameondoa Mv Magogoni kwenda kuikarabati Mombasa, zaidi ya mwaka haijarudi. Sasa unaondoa kivuko kimoja cha maana kilichobaki. Kweli hawa watu huwa wanatumiamakili kufikiria au kiungo kingine? Wakati wa Magu hapo vivuko vitatu vilikuwa vinapiga kazi ukija na gari muda wowote hutumia zaidi ya 30 minutes ushavuka. Sawa toeni vivuko vikubwa acheni Mv Kazi ila bajeti ya mafuta iwe ile ile ya vivuko vitatu.
#shambalabibi
#kulakwaurefuwakamba
 
Back
Top Bottom