Huku Zanzibar kuna mambo ya ajabu sana

Hiyo wikipedia sio ushahidi kaka, tukubaliane hapo kwanza, hata wewe unaweza kuingia na kuandika, ndio maana kwenye hilo uliloleta kuna makosa mengi mno ,mwanzo waliandika Ali Hasan Mwinyi alizaliwa Zanzíbar, jambo ambalo sio kweli (sasa weshabadilisha). Kuna wakati Zanzíbar pia ilisemwa ni visiwa vikubwa (Pemba, Unguja na Máfia) jambo sio kweli , wamerekebisha .... Hayo ni baadhi tu. Je Kiswahili ni kibantu au kingozi ? (Ulishawahi kusikisia hii kauli ? ) Wangozi ni watu waliotokea Uhabeshi na kuja kuishi ufuo wa Áfrika uchejua .....
Kuhusu L R nitakupa mifano watu mashuhuri waliozaliwa / lelewa Zanzíbar , yupi Kati yao ana matatizo hayo ya L R .... Mwinyi baba na Mtoto, Samia Suluhu, Ali Shein , Seif Sharif, Charles Hilari , Khadija Kopa , (hatuwataji wanawe ) , Mzee Yusuf, Salim Ahmed Salim, je unaweza kunipa wabara mashuhuri wasio na matatizo ya L R (tena inasikitisha mpaka waswahili wa mrima wanaanza kuchanganya) ....
 
Umemuandikia maneno magumu sana ya Kiswahili halisi ambayo hawezi kuelewa maana yake:
Uchejua
Ufuo
Naongezea na Urejua[emoji106]
[emoji120] Mkuu umenikumbusha Kiswahili.
 
So kila kitu kwenye wikipedia kipo unavyodai, kwahiyo hata serikali chini ya wizara ya elimu inavyofundisha kiswahili ni kibantu inakosea?
 
So kila kitu kwenye wikipedia kipo unavyodai, kwahiyo hata serikali chini ya wizara ya elimu inavyofundisha kiswahili ni kibantu inakosea?
Sasa wewe unashangaa hilo wakati kuna waziri kabisa alishawahi kusema Tanzania ni Muungano wa Pemba na Msumbiji.
 
Sasa wewe unashangaa hilo wakati kuna waziri kabisa alishawahi kusema Tanzania ni Muungano wa Pemba na Msumbiji.
Usifananisha misspelling na kitu kilochofanyiwa utafiti kwa makumi ya miaka Africa nzima, halafu huu ndio wakati wenu Zanzibar kudai haki yenu kupitia wawakilishi wenu wapeleke muswada wa kujitenga na Tanganyika, changamkeni msikubali.
 
Wewe ni TISS ulienda Zanzibar kwa ajili ya kuiba uchaguzi.
 
So kila kitu kwenye wikipedia kipo unavyodai, kwahiyo hata serikali chini ya wizara ya elimu inavyofundisha kiswahili ni kibantu inakosea?
Vitu vingi tukichukulia mtizamo wa serikali unakuwa na mrengo fulani, mfano, vita vya Biafra, Nyerere aliwaunga mkono (baadae akajua kuwa kakosea na kukiri) , je unaamini hadithi za Idi Amini ? Sisemi kuwa alikuwa malaika ila vita Ilê haikuwa na ulazima kwetu kuingia, Nyerere aliingia vitani kwa sababu zake mwenyewe, migogoro ya mipaka ilikuwepo na ipo ( hata baina ya Zanzíbar na bara - bara wanalitaka fungu Latham / mbaraka ilhali wanajua kuwa ni la Zanzíbar) , je tuimaini serikali ipi Kati ya Malawi na Tanzania ? Mimi sikusomeshwa kuwa Kiswahili ni kibantu, niliambiwa kuna falsafa nyingi , ipi sahihi na tukawa tunajadili ( ila mwalimu alituambia tukikata tupate, basi tuandike Kiswahili ni kibantu) dhana zilizopo ni ... Je Kiswahili ni kibantu? Je Kiswahili ni Kingozi ? Je Kiswahili ni kiarabu ? Au Kiswahili ni krioli ?
 
LI-PAULO[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Usifananisha misspelling na kitu kilochofanyiwa utafiti kwa makumi ya miaka Africa nzima, halafu huu ndio wakati wenu Zanzibar kudai haki yenu kupitia wawakilishi wenu wapeleke muswada wa kujitenga na Tanganyika, changamkeni msikubali.
Kwa akili yako waziri mzima kweli asijue kuwa Tanzania ni Muungano wa Zanzibar na Tanganyika? Unatetea eti misspelling!! Mbona unaongea utopolo? Nijuavyo mimi kama angeandika Tanzania ni Muungano wa Zanzibare na Tanganyika:
Zanzibar kuiandika kama Zanzibare hiyo ndio misspelling! Lakini kaandika kabisa eti Pemba na Msumbiji unasema misspelling kweli! [emoji38][emoji38][emoji38][emoji23][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji377][emoji377][emoji377][emoji2445][emoji2445][emoji2445]
 
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
 
Kwanza wanapenda kutumia neno "Alifiriwa" wakiwa na maana ya "Alifiwa"....... Yalikua yananipa kiwewe, ila labda wako sahihi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…