Elections 2015 Humphrey Polepole: CCM ilifanya maamuzi ya kiume, Majizi na hasa kubwa lao yakakatwa...

Elections 2015 Humphrey Polepole: CCM ilifanya maamuzi ya kiume, Majizi na hasa kubwa lao yakakatwa...

Kwani nayeye(jpm) katajwa kwenye hyo rist ya mafisadi.
Mbna hamuweki ninyi upawa.. cc tunazungumzia kutowapa uongozi hawa mafisadi..na ninyi mnatetea ...
Kwa hyo na ninyi mnatumia hoja ya kwamba kma wao wana mafisadi na ninyi muwe naye fisadi???
 
Bwana Polepole wewe kama msomi, mzalendo na muungwana, unapowaita watanzania wenzako tena pengine wenye umri sawa na wazazi wako unao wajibu pia na uwezo wa kuwafungulia mashtaka mahakamani. Thats what courageous and brave people do in modern civilised world. Haitoshi Bwana Polepole kupayuka kila siku bila kuchukua hatua muafaka. Ni mahakama peke yake yenye jukumu la kikatiba kuhukumu watanzania, vinginevyo unataka tuishi katika mazingira ya utamaduni wa porini/ushenzini!

Ni wazi sasa Polepole umejitishwa mzigo wa uchunguzi, mwendesha mashtaka na hakimu dhidi ya Lowasa. Sina hakika pia kama unao mpango na dhamira ya kuwashughulikia watuhumiwa wengine hasa kwa misingi ya Ripoti za CAG ambazo zimeweka bayana upotevu wa fedha za umma nyingi zaidi kuliko zile unazoshupalia kila uchao!

Kiu ya Watanzania ni kuleta mabadiliko ya dhati ili pamoja na mambo mengine kuziba mianya ya ufisadi na kuimarisha taasisi zenye uwezo wa kuchukua hatua kila matendo ya ufisadi yanapojitokea. Watanzania hawana tatizo na watu binafsi au fisadi mmojammoja, bali mifumo ya utawala ambayo kimsingi imedumu zaidi ya miaka 50 sasa ikiwemo - "imperial presidency". This is the essence of the Change we yearn for. Sasa madhalo Lowasa amekubali kutekeleza sera ya UKAWA ya kutupatia katiba mpya kwa misingi ya maoni ya wananchi, huyo ndiye anastahili kuwa Rais wa Tanzania baada ya uchaguzi wa 25th Oktoba, 2015.

Samahan mkuu, huyo Polepole unaemwita "msomi" ana level gani ya elimu kuwa accredited kama "msomi"? Mtazamo wangu ni kwamba huyu mtoto anatumiwa tu wala hana lolote analoljua. kama ni swala la wezi mbona CCM kuna wezi ambao hata idadi haijui. Mi nahisi kama angetaka kuwa na dhamira ya kweli angezungumzia wizi na uizo kwenye system na sio kuelekeza vita yake kwa Lowassa! Ufisadi tunaoshuhudia leo ina maana EL ndo anauendeleza?!

Polepole ni mihemko tu inamsukuma, sio mtu "rational" hata siku moja. Huwezi kuwa rational ukawa subjective kama polepole.
 
polepole nakushauri hata kama unayafaham mengi nakushauri kipindi hiki ungekaa kimya, swala la ufisadi siyo la uyo mmoja tu unaemwandama kila uchwao, na elewa kama kwel kuna watu wanakumia ipo siku haohao hutawaona upande wako. Kumbuka aliyoyasema zitto kua siasa haina adui wa kudumu! Kwa maana leo wanaokutuma kuna siku watakua nyuma ya huyo unae mtukana kila siku, na pia kwanini ujitwike jukumu ambalo si lako sana, kwa maana kuna vyombo vinavyopaswa kushuhurika na uyo bwana je vimetoa ushirikiano kisa gani kwako kusudi uyo bwana ashitakiwe, au utaishia hongea pale channel ten afu hakuna kitu, mwisho japo sio kwa umuhim kwa kua wewe upendi ufisadi tunaomba uongelee juu ya uzwaji wa nyumba za serikali uliosimamiwa na bwana magufuli. Hapo ndo tutaamini kua kweli wewe upendi ufisadi.
 
Kwani ninyi(mtatiro) mchakato wenu wa kumpta rais ulikuwaje????.
Kuna haki hapo ww uliona au ushabiki usiokuwa na tija...siasa za maji taka...???
Hakukuwa na mchakato huru baada ya kulambishwa mabilioni, Mgombea urais kupitia UKAWA kanunua vyama vyote vinavyounda umoja huo na ndio maana ukaona waliokuwa wanajielewa kama Slaa na Lipumba wakaamua kukaa pembeni.
 
Wakuu nina maswali yafuatayo, Mr Polepole anasema katika uteuzi wa mgombea uraisi kwa tiketi ya ccm, walikatwa mafisadi akabaki mtu mmoja msafi Mh Magufuli.Jambo linalo ni tatiza ni kuwa miongoni mwa waliokatwa ni makamu wa raisi, waziri mkuu mzee Pinda na hata jaji mkuu msataafu, je inamaana Magufuli ni msafi kuliko hawa? Kama ni hivyo mbona asiteuliwe yeye kuwa hata waziri mkuu. Mr Polepole, mbona haelezi ufisadi wa hawa wengine waliokatwa. Mzee lowasa ilikuwaje akaweza kupewa nafasi ya juu na mkuu wa nchi, kuwa waziri mkuu kama hafai kiasi hicho. Mr Polepole mbona hatukumsikia hata mara moja kumshambulia mzee Lowasa, tangu ilipoibuliwa tuhuma ya Richmond, na hata baada ya kujiuzulu uwaziri mkuu. Mbona Mr Polepole hatukumsikia hata mara moja kushinikiza Lowasa kwenda mahakamani? Hizi kelele za Mr polepole kwa nini zinasikika kwa sasa ambapo mzee Lowasa kahamia ukawa? Je hii haidhihirishi kuwa agenda kuu ya Mr Polepole ni kudhoofisha ushindi, kwa vyama vya ukawa? Kwa maoni yangu Mr Polepole baada ya kutofautiana na chama chake cha CCM, anajaribu kujikomba ili apate huruma ya kusamehewa na wana CCM.
 
Nimefuatilia kwa makini sana hoja za Hamfrey pole pole.Nathubutu kusema mwanzo nilidhani ni kijana mzalendo anaeipenda nchi yake tena mkweli lakini nimegundua yafuatayo kutoka kwa Polepole.

1. H Polepole ana chuki binafsi na Mgombea wa upinzani.kwa nini nasema hivyo kabla ya uteuzi wa wabunge Polepole alisema ccm inapaswa kuwakata wote wanaotuhumiwa kwa ufisadi na kama hawatafanya hivyo alikuwa tayari kuisema ccm nchi nzima.Mara baada ya uteuzi kupita na wale wote wanaotuhumiwa kwa ufisadi kupita Polepole amegeuka na kuacha hoja hiyo.hiyo inaonyesha ana chuki na mgombea wa Ukawa.

2. Katika nchi ufisadi uliofanyika ni mkubwa sana na waliofisadi nchi wako wengi sana na pole pole anawajuwa lakini hajawahi hata siku moja kuwataja kwa Polepole ufisadi ni Richmond pekee vipi kuhusu EPA, Kagoda, meremeta, Escrow.uuzaji wa nyumba za serikali, uuzaji wa viwanda. Tukitaka kuiokoa nchi yetu basi tuwe wa kweli bila upendeleo.Chuki anayoionyesha pole pole ni ya wazi mno.

3. CCM ni chama chetu lakini kuna mambo mengi mabaya yaliyofanyika tuyaseme ili tukiokoe chama chetu.
Mgombea wetu ametoa hotuba inayoonyesha udhaifu mkubwa katika mambo mengi yanayohitaji kurekebishwa tuyaseme kwa uwazi kama Dr Pombe anavyosema. Mgombea wetu hashambulii mtu anaongelea hoja.polepole jikite kwenye hoja za kujenga nchi si kila siku unamshambulia mtu mmoja kama vile wewe huna dhambi Acha chuki haijengi.

Target kubwa ya Polepole kuhusu wagombea wenye kashfa iliegamia kwenye Urais na sio ubunge wala udiwani na ndio maana baada ya Magufuli kupita ile hoja ikawa mfu. Tatizo watanzania tuna ile hali ya kumchukia mtu kwasababu yupo against na matakwa yako, hatupimi hoja.

Polepole alijua vyema kuwa Lowassa aliutaka urais kwa udi na uvumba, punda afe mzigo ufike.Na mtu wa namba hiyo ni wa kuogopa kama ukoma.Hakuna mtanzania asiyejua ufisadi wa EL, labda uwe na mapenzi binafsi na EL ndio utapumbazika kwa hilo.
 
Hoja ya Polepole eti "...wengine wanadhibitika" ni upotoshaji, ubabaishaji na ufinyu wa mawazo. Taasisi zetu za utawala bora ni dhaifu na tegemezi! hazina meno ya kuuma! Uteuzi na uwajibikaji wa taasisi za utawala bora (good governance) ndiyo tatizo la ufumbuzi wa ufisadi na maradhi mengine yanayokabili taifa. Tunahitaji katiba inayo tupatia vyombo huru na mchakato wa upatikanaji wa viongozi wake ulio wazi na vigezo mahsusi. Bunge lazima lihusike katika mchakato huo na ku-oversee utekelezaji wa majukumu yake. Hatutaki kusikia wahalifu/watuhumiwa wanaambiwa warejeshe mali/fedha waliyoiba hala yaishe, wala utendaje wa taasisi kuingiliwa na mihimili tofauti ya dola. Haya ndiyo mabadiliko tunayotaka kama taifa, ambayo yaelekea Bwana Polepole hajaelewa pamoja na kuhusika kwenye kamati ya katiba mpya - pengine ni ukada wa CCM?. Na mataifa yote yaliyofanikiwa duniani yaliimarisha mifumo ya utawala bora na siyo kuhangaika na mtu mmojammoja. Mwalimu Nyerere aliwahi kusema katiba iliyokuwepo ingesababisha awe dikteta wa kutupwa hata kama alikuwa hapendi. The ultimate solution was to change the basi law.
 
Pole pole kwa mjibu maelekezo usichukue SHERIA mkononi mbona wewe unachukukua sheria kumhukumu mtu hivyo unapingana na mahakama umetuhumiwa laki sita na umejitahidi kujibu
 
pole pole hata ccm hatukuamini maana una ndimi mbili na ni mnafiki!

mkuu umenifurahisha kweli...kwamba dogo hata kwenu hamumuelewi...anauma na kupuliza.....mwambieni dogo kuchamba kwingi mwishowe unatoka na nnya mkononi....dogo anasahau mtaka nyingi nasaba hufikwa mwingi msibaaa....

Polepole humphrey...hebu nenda polepole kijana....utajaumbuka ukose wa kukulilia msiba wako.

The public enemy..ahahahahahaaha.
 
Sitaki kuamini kama mdogo wangu Polepole nae kanunuliwa but kilicho dhahiri kwake ni kwamba Polepole ana chuki binafsi na Lowassa; nitafafanua.
1. Polepole amepata umaarufu kupitia tume ya katiba ile ya mzee Warioba, msimamo wake ju ya katiba pendekezwa upo dhahiri, mgombea mwenza wa ccm alikua msaidizi wa mwenyekiti wa bunge la katiba, huyu mama pamoja na chama chake walikataa kataka kuipitisha ile rasmu yao, Polepole haoni kama kuna tatizo kwake, tatizo analiona kwa Lowassa tu.
2. Nchi ina kashfa kadhaa za ufisadi, nitaja chache, IPTL, Rada, ndege ya raisi, uuwaji holela wa wanyama kama Tembo, Faru na Twiga, Richmond/Dowans/Symbion, Epa, Deep green finance, Meremeta, ujenzi wa minara pacha pale BOT bila kusahau Escrow, yooote hayo jina la Lowassa linatajwa kwenye Ricmond/Dowans peke yake. Sitaki pia kuamini kama Polepole hamjui Mr. Richmond ni nani? Dr. Mwakyembe aliisha twambia mule mule Bungeni; hapa napo macho ya Polepole yana muona Lowassa tu ya dealers wengine hayaoni.
3. CCM wameuza nchi (ccm kama chama na sio mtu) nina hakika Polepole anajua vizuri sana uuzwaji holela wa mashirika yaliokua yakifanya vizuri kibiashara kama NBC bank n.k, uuzwaji wa nyumba za serikali na hasara tunayoipata sasa hvi kama wananchi, yipo mwingine aliyeratibu zoezi hilo akampa na girl friend wake nyumba 1 na mtu huyo sasa hvi ndio mgombea wa chama chake kwenye nafasi ya uraisi (sitaki kuamini kama polepole halijui hili) but YES, still macho ya Humfrey yamepigwa upofu upande huo yana ona kwa Lowassa tu.

Namshauri mdogo wangu huyu (narudia, sitaki kuamini kama na yeye kanunuliwa) aanze kuvaa miwani ili macho yake yawe yanaona pande zote na sio upande mmoja tu.
 
Kwa mjibu wa viongozi na wafuasi wa cdm ,kama lowasa angekuwa fisadi basi angekuwa kashafungwa.na wanakwenda mbali zaidi na kusema aliye na ushaidi kuwa lowasa ni fisadi auweke hadharani au aende mahakamani.kwa sababu hizo,hata chenge,mhongo,ngereja,tibaijuka,rostam,karamagi n.k sio mafisadi pia,kwa sababu nao hawajashitakiwa mpaka sasa.Hivyo ccm hakuna fisadi hata mmoja.
Unachoshindwa kujua ni kwamba hawa wote walifikishwa kwenye tume ya maadili. Sihawahi kusikia Lowasa alihojiwa mahali popote kwa kukosa maadili. Km unajua utusaidie wakina siye!
 
Lowassa wanamtukana kwa kumuita maneno yote mabaya kwakuwa tu hayuko kwenye Maslahi ya MKAPA babalao... Lowassa amemtaja Mmiliki wa Richmond ambaye waliitumia kumtuhumu na kumuita maneno yote mabaya dhidi yake... Hadi Leo Ikulu haijakanusha hivyo LOwassa kumbe hakuwa JIZI, FISADI kama ambavyo Mr Clean Mmiliki wa Kiwira ... Tumejua kuwa Ugomvi Mkubwa wa Lowasa na Mr Clean alietuita Malofa kuwa ilikuw ni Uamuzi wa Lowassa kurejesha Kiwira Serikalini .. Mtahangaika sna lakini Ukweli Utabaki kuwa Pole Pole ni Mvatican mwenye kulinda Maslahi ya Mabwana zake ...
 
Polepole kama Amon Anastaz Mpanju tu, hakuna tofauti, labda tu kwamba huyu anaona, na huyu haoni.

Ngoja nikuonyeshe tofauti ya Lowasa wa CCM na Lowasa wa UKAWA:

Lowasa wa CCM yuko radhi kujiuzuru uwaziri mkuu kuliko kumtaja mwenye mradi wa Richmond.

Lowas wa UKAWA amemtaja fisadi wa Richmond kuwa ni aliyekuwa na mamlaka ya Juu kuliko Waziri Mkuu wa wakati huo.

Sasa kweli bwana Polepole huoni kuwa Lowasa wa Ukawa amekombolewa kutoka katika dhambi alizokuwa nazo akiwa CCM?

Sisi Walokole huwa tunatoa ushuhuda tunapookoka kutoka kwenye dhambi kwa kutaja dhambi zetu na wale tuliotenda nao maovu. Hii haina maana kwamba tunaendelea kuwa na maovu yanyuma. Staili hii ilitumiwa pia na Saul ambaye ndiye Mtume Paul. Alikuwa mkatili sana akiua wafuasi wa Yesu, lakini baadae amempigania Kristu kuliko hata akina Petro, Yohana, Andrew, Yakobo, Yuda n.k. Hivi Pole pole kinachokufanya usiamini katika wokovu ninini? Wewe ni Mkristu ingawa sijui wa dhehebu gani, lakini huamini katika sakrament la kitubio? au unadhani tuna sali ili tuendelee kuwa wenye dhambi? We unaamini kuwa unaweza samehewa dhambi katika dini, lakini katika siasa haiwezekani?

Mbona Kenyata alikuwa KANU leo anaongoza nchi vizuri tu kutokea chama pinzani? Mbona Yeye tajiri yuko radhi kukatwa mshahara wake lakini aliyeingia maskini Kikwete leo ni tajiri na anaogonza kuwa na mshahara mkubwa wa Sh. milioni 480 nilizosoma juzi kwenye magazeti? Kuna sababu gani ya kuingia maskini ukatoka tajiri, si bora uingie tajiri utoke maskini? Hii usiikatae maana hatujaijaribu, ndio sasa tunataka kuianza!
 
Pole pole hata CCM hatukuamini maana una ndimi mbili na ni mnafiki!

THANKS MKUU, PAMOJA NA KWAMBA HUWA SIKUBALI HOJA ZAKO ILA NASHUKURU LEO AKILI ZIMEKURUDI UMECHANGIA VYEMA....

And this is just a minor complement 2 u...
 
Hapo wote wachafu si hao chadema wala ccm....woote wachafu tena mnatia aibu...hapa ukomboz kamwe hauwez kupatikan kwa njia ya siasa ya sasa ya tanzania nilazim tufikiri nje ya box...kam itawezekan tuongoz nchi kwa demokrasi ya kupokezana tupate vyam viwili tu....nikionacho mim chadem mkipata hii nchi na nyie mtakuw kam hawa mnawatuhumu ila kwasabab hamjapat mnatak muonekan ni wakomboz kumbe nanyinyi ni wachumia tumbo kama hao nduguzenu
 
pole pole kama unajua lowassa nijambazi kwa nini usimriport police tuone uzalendo wako
 
Back
Top Bottom