Uchaguzi 2020 Humphrey Polepole: Dkt. Magufuli atachukua fomu ya Urais 06 Agosti Dodoma. Mwanachama aliyepiga mazonge kwenye kura za maoni atashikishwa adabu

Uchaguzi 2020 Humphrey Polepole: Dkt. Magufuli atachukua fomu ya Urais 06 Agosti Dodoma. Mwanachama aliyepiga mazonge kwenye kura za maoni atashikishwa adabu

Ule mswada wa waandishi wa habari angalau wawe na elimu yenye ngazi Advanced Diploma leo ndio nimeona uhalisia wake , Waandishi wa Habari mnakwama wapi? Duh yani mpaka aibu.... ndio vitu gani mlikuwa mkiuliza , yaani mda wote wa propaganda za PRO mlishindwa kutunga maswali yenye afya?
Kamuulize Pascal Mayala walimnyanganya leseni/kibali cha kurusha matangazo kule Sabasaba/Nanenanr mpk alivyoanza kuwalamba miguu,kwa hio hata hao waandishi wanajua sana watakachofanywa na ndio maana pia Mkapa aliwaitaga ni makanjanja.
 
CCM imetoa taarifa kuwa tarehe 15/08/2020 kutakuwa na jambo kubwa sana la kisiasa katika uwanja wa Uhuru.

Tukio hilo litahusisha wasanii wote wa muziki, bongo movie, kandanda, basketball na sanaa nyingine zote.
Bwashee usipange kukosa.

Kuna Jambo Uhuru

Maendeleo hayana vyama!
 
Polepole amenichekesha sana leo hasa alipokuwa anawaambia ukweli chama kilichobadilisha wimbo wa Taifa.
 
Makene aitishe press, pamoja na Mambo mengine pia akiite chama cha mapinduzi ni cha kihuni na viongozi wake ni wahuni. Yaani wakiweka kigingi tunaweka jiwe, wakiweka ugoko tunaweka chuma, tit for tight wataelewa tu.
 
Makene aitishe press, pamoja na Mambo mengine pia akiite chama cha mapinduzi ni cha kihuni na viongozi wake ni wahuni. Yaani wakiweka kigingi tunaweka jiwe, wakiweka ugoko tunaweka chuma, tit for tight wataelewa tu.
Hahah Msajili atatoka huko aliko fasta kumkemea Makene na Chadema.
 
Katibu wa NEC - Itikadi na Uenezi ndugu Polepole ataongea na watanzania kupitia vyombo mbalimbali vya habari.
Mkutano utafanyika ofisi ndogo ya CCM - Lumumba, Dar es Salaam. Usipange kukosa kufuatilia.



Juzi tulikuwa na NEC ilituita vyama vyote, taarifa muhimu tumepewa, kikao kilichopita tulimaliza kikao cha maadili na tukasaini, sheria iko vizuri asiwadanganye mtu, tukikaaga na tume wote tunazungumza lugha moja ni unafiki tu wa wachache. Tena kuna menu na kuna wengine hawaondoki mpaka wale msosi.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetutangazia kuanzia leo tunaweza kuchukua fomu kwa ajili ya wagombea wa nafasi ya Urais, Mgombea Urais CCM ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Tanzania Dkt. Magufuli atachukua fomu wiki hii Dodoma

Hili sikutaka kulisema lakini limetuuma kama WaTZ, juzi wenzetu wamebadilisha maneno ya Wimbo wa Taifa wameweka maneno ya chama chao, najiuliza sisi CCM tuna nyimbo nzuri lakini huu tunauheshimu hatuwezi kuunajisi kwa kuweka mambo binafsi. Nchi hii inatambulishwa na vitu vitatu ambavyo ni jina yaani Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Pili inatambulishwa na Bendera ya Taifa na mwisho ni Wimbo wa Taifa.

Tufanye siasa lakini tusiguse vitu vinavyotambulisha taifa letu wimbo wa taifa huwa tunaimba tukiwa katikati ya vita, mapigano na ndio kiunganishi chetu kimaombi kati ya taifa letu na Mwenyezi Mungu, waombe radhi Watanzania kwa kuushushia hadhi.

Wawaombe radhi Watanzania ila mimi najua hawataomba radhi, kama mnabisha tu-bet hapa, ni desturi yao nimefanya nao chaguzi nyingi wanavunja sheria, juzi wamemsema vibaya kila mtu kwenye nchi hii, chama hiki ni tatizo kubwa

Siku amerudi jamaa yao, nakuambia siku ile watu hawakutembea barabarani, waliambiwa pita moja, wee wamepita zote na siyo kwamba walikuwa wengi ni kama walikuwa wanapita zigizaga, mimi nimekutana nao pale Kinondoni Studio wapo huku na huku

Unajua wamefika mpaka kwenye ofisi zao Mtaa wa Ufipa, wakaanza kusema mbona hawajatukamata, nikasema kumbe mpango wao ilikuwa kukamatwa sasa hawajakamatwa wanalalamika, hiki chama sikielewa hivi nidhamu ni zero na kutii sheria bila shuruti ni zero

Halafu wanajenga hoja wanasema tuambieni wapi tumevunja sheria, hivi kwenye nchi hii kuna sheria inasema usichukue Mke wa Kaka yako?, mimi nawaachia Watanzania hiki ndiyo chama kabla hakijaomba dhamana kishabadili Wimbo wa Taifa kishafanya wa chama.

Wana-CCM ambao mmeomba dhamana na mlizingatia katiba na kanuni hamkujishirikisha kwenye makatazo na miiko muwe na amani na sisi kama chama hatutawaangusha watu waaminifu na wanyenyekevu na wenye nidhamu, ila wale mlipiga mazonge tutafundisha watu adabu kipindi hiki. Kila mwanachama aliyeshiriki ‘uovu’ katika kura za maoni, atashikishwa adabu.

Nampa pole TID sababu hawa majamaa ni mazulumati wametudhulumu wimbo wa Taifa. TID anapambana mtu wa watu ametengeneza Ni Yeye na ile ilikuwa Magufuli, wale majamaa wameichomeka kule. Hawajamshirikisha hawajamuomba kwa kweli sisi kama Watanzania tutawachukulia hatua.

nilikuwa sijui ni kwa nini watu wamempachika huyu jamaa jina la la Chaku.

kumbe sababu yenyewe ndiyo hii!
 
Hujasikia kuhusu mambo ya rushwa?
Sasa Polepole anapata wapi ujasiri wa kukemea rushwa wakati ndani ya Chama chake rushwa imetamalaki kuanzia mashinani mpaka ngazi kuu ya chama!!

Huyo Polepole anatetea ugali wake tu ila CCM haiwezi kukemea rushwa sababu CCM ni rushwa na rushwa ni CCM.

CCM na rushwa ni mapacha wa kufanana ( identical twins).
 
Tufanye siasa lakini tusiguse vitu vinavyotambulisha taifa letu wimbo wa taifa huwa tunaimba tukiwa katikati ya vita, mapigano na ndio kiunganishi chetu kimaombi kati ya taifa letu na Mwenyezi Mungu, waombe radhi Watanzania kwa kuushushia hadhi.
Naunga mkono hoja.
 
Panic mode hivi huyo si muenezi wa chama? au ndio anafanya kazi yake apo LOL!!
 
Back
Top Bottom