Uchaguzi 2020 Humphrey Polepole: Dkt. Magufuli atachukua fomu ya Urais 06 Agosti Dodoma. Mwanachama aliyepiga mazonge kwenye kura za maoni atashikishwa adabu

Uchaguzi 2020 Humphrey Polepole: Dkt. Magufuli atachukua fomu ya Urais 06 Agosti Dodoma. Mwanachama aliyepiga mazonge kwenye kura za maoni atashikishwa adabu

Katibu wa Itikadi na Uenezi (CCM), Humphrey Polepole,  amesema chama hicho kitaw ( 640 X 640 ).jpg


Hayo yamesemwa na Mzee Hamphrey pole pole ambaye ni Katibu wa Itikadi na uenezi wa chama hicho , Kwamba wale wote waliopita kimagumashi hawana nafasi ya kuteuliwa na chama hicho kugombea ubunge au udiwani.

Hakufafanua magumashi anayoyasema kama ni rushwa au jambo lingine , bali inafahamika kwamba 90% ya watia nia wa ccm walimwaga rushwa , wakiwemo wale waliotoa rushwa kwa kipindi cha miaka 4 mfululizo .
 
View attachment 1527776

Hayo yamesemwa na Mzee Haumphrey pole pole ambaye ni Katibu wa Itikadi na uenezi wa chama hicho , Kwamba wale wote waliopita kimagumashi hawana nafasi ya kuteuliwa na chama hicho kugombea ubunge au udiwani.

Hakufafanua magumashi anayoyasema kama ni rushwa au jambo lingine , bali inafahamika kwamba 90% ya watia nia wa ccm walimwaga rushwa , wakiwemo wale waliotoa rushwa kwa kipindi cha miaka 4 mfululizo .
Kumekucha
 
Katibu wa NEC - Itikadi na Uenezi ndugu Polepole ataongea na watanzania kupitia vyombo mbalimbali vya habari.
Mkutano utafanyika ofisi ndogo ya CCM - Lumumba, Dar es Salaam. Usipange kukosa kufuatilia.



Juzi tulikuwa na NEC ilituita vyama vyote, taarifa muhimu tumepewa, kikao kilichopita tulimaliza kikao cha maadili na tukasaini, sheria iko vizuri asiwadanganye mtu, tukikaaga na tume wote tunazungumza lugha moja ni unafiki tu wa wachache. Tena kuna menu na kuna wengine hawaondoki mpaka wale msosi.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetutangazia kuanzia leo tunaweza kuchukua fomu kwa ajili ya wagombea wa nafasi ya Urais, Mgombea Urais CCM ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Tanzania Dkt. Magufuli atachukua fomu wiki hii Dodoma

Hili sikutaka kulisema lakini limetuuma kama WaTZ, juzi wenzetu wamebadilisha maneno ya Wimbo wa Taifa wameweka maneno ya chama chao, najiuliza sisi CCM tuna nyimbo nzuri lakini huu tunauheshimu hatuwezi kuunajisi kwa kuweka mambo binafsi. Nchi hii inatambulishwa na vitu vitatu ambavyo ni jina yaani Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Pili inatambulishwa na Bendera ya Taifa na mwisho ni Wimbo wa Taifa.

Tufanye siasa lakini tusiguse vitu vinavyotambulisha taifa letu wimbo wa taifa huwa tunaimba tukiwa katikati ya vita, mapigano na ndio kiunganishi chetu kimaombi kati ya taifa letu na Mwenyezi Mungu, waombe radhi Watanzania kwa kuushushia hadhi.

Wawaombe radhi Watanzania ila mimi najua hawataomba radhi, kama mnabisha tu-bet hapa, ni desturi yao nimefanya nao chaguzi nyingi wanavunja sheria, juzi wamemsema vibaya kila mtu kwenye nchi hii, chama hiki ni tatizo kubwa

Siku amerudi jamaa yao, nakuambia siku ile watu hawakutembea barabarani, waliambiwa pita moja, wee wamepita zote na siyo kwamba walikuwa wengi ni kama walikuwa wanapita zigizaga, mimi nimekutana nao pale Kinondoni Studio wapo huku na huku

Unajua wamefika mpaka kwenye ofisi zao Mtaa wa Ufipa, wakaanza kusema mbona hawajatukamata, nikasema kumbe mpango wao ilikuwa kukamatwa sasa hawajakamatwa wanalalamika, hiki chama sikielewa hivi nidhamu ni zero na kutii sheria bila shuruti ni zero

Halafu wanajenga hoja wanasema tuambieni wapi tumevunja sheria, hivi kwenye nchi hii kuna sheria inasema usichukue Mke wa Kaka yako?, mimi nawaachia Watanzania hiki ndiyo chama kabla hakijaomba dhamana kishabadili Wimbo wa Taifa kishafanya wa chama.

Wana-CCM ambao mmeomba dhamana na mlizingatia katiba na kanuni hamkujishirikisha kwenye makatazo na miiko muwe na amani na sisi kama chama hatutawaangusha watu waaminifu na wanyenyekevu na wenye nidhamu, ila wale mlipiga mazonge tutafundisha watu adabu kipindi hiki. Kila mwanachama aliyeshiriki ‘uovu’ katika kura za maoni, atashikishwa adabu.

Nampa pole TID sababu hawa majamaa ni mazulumati wametudhulumu wimbo wa Taifa. TID anapambana mtu wa watu ametengeneza Ni Yeye na ile ilikuwa Magufuli, wale majamaa wameichomeka kule. Hawajamshirikisha hawajamuomba kwa kweli sisi kama Watanzania tutawachukulia hatua.

Mazoea hujenga tabia alisema wapinza nisawa na corona
 
Humphrey Polepole mnapoteza muda chama chenu kinazidi kupasuka :



''Wagombea Ubunge ARUSHA CCM Wampinga Mgombea Mwenzao ''

Wagombea Wawili walioshiriki kwenye mchakato wa uchaguzi wa kura za maoni wa ndani ya chama cha mapinduzi katika jimbo la Arusha wamejitokeza hadharani kumpinga mmoja wa wagombea walioshiriki mchakato huo kwa kusema alitoa rushwa.
 
Mambo ya Diamond na Alikiba kugombea penseli yameanza, Polepole anagombea wimbo wa Taifa na ni 'Yeyee' ya TID. Hivi chama kilichokufa kinawapa mchamchaka hivi?
 
Si ange ongelea kwenye lile kongamano la wadada Mh alio wapigia simu?
Huu ni mwrndelezo wa kuzuia vyombo vya habari visitangaze mkutano wa ACT WAZALENDO. Hawezi kuwaita waandishi muda ule ule ambao ACT wana anza mkutanobaao live..
Sijui anae wapa Ccm hizi mbinu za kizamani ana toka wapi kwenye hii dunia. Na tujiulize, Ccm wana ogopa nini???
Kwani waandishi wa habari wapo wangapi? Je kuna kanuni inazuia kufanya kikao wakati mmoja na mwenzio?
 
Waliopora nembo ya M4C mwaka 2015 walikuwa ni chama gani?

Na je,TID ana hati miiki ya hiyo slogan?

Na,wana uhakika gani kama wameiba?

Na,slogan hiyo imetumiwa na chama kama chama au imetumiwa tu na baadhi ya wanachama kwa mapenzi yao?
Wala usingepoteza muda kujibu
 
Tatizo linaanzia hapa: Hoja za CCM zinajibika kirahisi sana ila hoja za Upinzani CCM hawawezi kuzijibu kutokana na njia walizotumia kupita. Sasa options ni 2. Kuzima wapinzani wasiendelee kusikika au CCM kujibu hoja za wapinzani ambazo zitamfanya Rais mpendwa abadili muelekeo aliokuwa anakwenda.
 
h
Nimwombe, ajikite kwenye sera za Chama Chetu. Mambo ya kujibu mapigo au kuzungumzia vyama vingine "SIYO KAZI YAKE" ni kazi ya Msajili wa vyama na NEC.
historia ya lissu ipo wazi sana kwamba uchaguzi wowote kwake hushinda mkuu sera za chama mda wake ni kwenye majukwaa but kwa aliyoyaongea jana ulikua mda mhafaka wa kuyazungumzia maana kampen bado so ulitataka aanze kuzungumzia sera za chama chake wakati kampeni bado?

itoshe kusema Mh Mbowe mungu akubariki na vizazi vijavyo vitakukumbuka umepika vijana mfano wa wazi mh mwalim iyo ni hazina nyingine katika taifa hili ,hivyo kumteua kuwa mgombea mwenza wa urais nawapa asilimia 200 japo kimahesabu hua hamna
 
Tatizo linaanzia hapa: Hoja za CCM zinajibika kirahisi sana ila hoja za Upinzani CCM hawawezi kuzijibu kutokana na njia walizotumia kupita. Sasa options ni 2. Kuzima wapinzani wasiendelee kusikika au CCM kujibu hoja za wapinzani ambazo zitamfanya Rais mpendwa abadili muelekeo aliokuwa anakwenda.
mkuu upo sawa kabisa na lingune hoja za ccm ni zile zile ambanzo mwenyekiti wao amekua akizizungumza kila wakati kwa miaka mitano so wananchi wameisha zizoea na ikumbukwe prof mkandala kwenye kongamano moja aliema kitu wennda hata viongozi wa ccm hawakutilia mahanani sana japo ni jambo la msingi alilo sema ,kwamba.

Waweza kua baba mzuri katika familia na unawapa kila kitu familia ila kama hawana furaha moyoni ni kazi bure , ni maneno machache yenye wigo mpana wa kufikirisha sana na pamoja na kumlinganiasha baba wa taifa na mh rais wa sasa katika kujenga hoja zake alisema HATIMA YA CCM BADO HAIJULIKANI JAPO DALILI ZA MVUA NI MAWINGU ,VIPI ndugu zangu na viongozi wa ccm hua wanayatafakari maneno haya hata siku moja kwamba yana uzito wa kipekee na kuyafanyia kazi ?
 
Back
Top Bottom