Uchaguzi 2020 Humphrey Polepole: Dkt. Magufuli atachukua fomu ya Urais 06 Agosti Dodoma. Mwanachama aliyepiga mazonge kwenye kura za maoni atashikishwa adabu

Uchaguzi 2020 Humphrey Polepole: Dkt. Magufuli atachukua fomu ya Urais 06 Agosti Dodoma. Mwanachama aliyepiga mazonge kwenye kura za maoni atashikishwa adabu

Asante sana, huwa tunashindana na watoto wangu kila wakati kukiwa na kive event kwenye TV huwa tunashindana Elimu bure zimeenda shs ngapi, Zimejengwa zahanati ngapi, Wanafunzi wa Chuo pesa kiasi gani,. Uchumi unapanda kwa asilia ngapi, ndege ngapi. So predictable.

Kingine kwenye front line hakuna talkers. Hakuna watu watatu mfano wa Mzee Yusuf Makamba watapanda kwenye stage wafikishe msg kwa njia ya utani n.k Front line yote iko Serious and cold, eg Jafo, Lukuvi, Zungu, Majaliwa even Mama Samia sio mwongeaji japokuwa ana haiba ya kupendwa.

Watanzania wanapenda watu waongeaji, wachekeshaji n.k ukiwa mkali watanzania wana tabia ya kukuogopa na kukukwepa kwa sababu hawajui kumface mtu na kumwambia ukweli.
mkuu upo sawa kabisa na lingune hoja za ccm ni zile zile ambanzo mwenyekiti wao amekua akizizungumza kila wakati kwa miaka mitano so wananchi wameisha zizoea na ikumbukwe prof mkandala kwenye kongamano moja aliema kitu wennda hata viongozi wa ccm hawakutilia mahanani sana japo ni jambo la msingi alilo sema ,kwamba
Waweza kua baba mzuri katika familia na unawapa kila kitu familia ila kama hawana furaha moyoni ni kazi bure , ni maneno machache yenye wigo mpana wa kufikirisha sana na pamoja na kumlinganiasha baba wa taifa na mh rais wa sasa katika kujenga hoja zake alisema HATIMA YA CCM BADO HAIJULIKANI JAPO DALILI ZA MVUA NI MAWINGU ,VIPI ndugu zangu na viongozi wa ccm hua wanayatafakari maneno haya hata siku moja kwamba yana uzito wa kipekee na kuyafanyia kazi ?
 
Summary ya press ya Polepole:

1.kuwafokea wananchi waliompokea Lissu Airport.
2. kufokea chadema kuhusu ubeti wa nyimbo ya taifa.
3. Kupiga kampeni kabla ya uchaguzi.
4. kuwafokea chadema kwa kutumia neno ambalo yeye anasema ni mali ya T.I.D.
5. Kutaja list ya wasanii kama kivutio cha kuongeza wahudhuriaji kwenye kampeni za CCM (hapa kamtaja hadi man walter ambaye sio msanii)

My Take:
(a)CCM wamepanic baada ya ujio wa Lissu nchini hususani baada ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya Chadema.
(b) CCM wamepandwa na jazba kwa spana walizoonjeshwa kidogo kwenye vikao vya Chadema vilivyofanyika Mlimani City.

NB:
Mataga safari hii mmejiingiza kwenye kina kirefu chenye mamba wakali mnoo 🤣🤣🤣
 
Katibu wa NEC - Itikadi na Uenezi ndugu Polepole ataongea na watanzania kupitia vyombo mbalimbali vya habari.
Mkutano utafanyika ofisi ndogo ya CCM - Lumumba, Dar es Salaam. Usipange kukosa kufuatilia.



Juzi tulikuwa na NEC ilituita vyama vyote, taarifa muhimu tumepewa, kikao kilichopita tulimaliza kikao cha maadili na tukasaini, sheria iko vizuri asiwadanganye mtu, tukikaaga na tume wote tunazungumza lugha moja ni unafiki tu wa wachache. Tena kuna menu na kuna wengine hawaondoki mpaka wale msosi.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetutangazia kuanzia leo tunaweza kuchukua fomu kwa ajili ya wagombea wa nafasi ya Urais, Mgombea Urais CCM ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Tanzania Dkt. Magufuli atachukua fomu wiki hii Dodoma

Hili sikutaka kulisema lakini limetuuma kama WaTZ, juzi wenzetu wamebadilisha maneno ya Wimbo wa Taifa wameweka maneno ya chama chao, najiuliza sisi CCM tuna nyimbo nzuri lakini huu tunauheshimu hatuwezi kuunajisi kwa kuweka mambo binafsi. Nchi hii inatambulishwa na vitu vitatu ambavyo ni jina yaani Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Pili inatambulishwa na Bendera ya Taifa na mwisho ni Wimbo wa Taifa.

Tufanye siasa lakini tusiguse vitu vinavyotambulisha taifa letu wimbo wa taifa huwa tunaimba tukiwa katikati ya vita, mapigano na ndio kiunganishi chetu kimaombi kati ya taifa letu na Mwenyezi Mungu, waombe radhi Watanzania kwa kuushushia hadhi.

Wawaombe radhi Watanzania ila mimi najua hawataomba radhi, kama mnabisha tu-bet hapa, ni desturi yao nimefanya nao chaguzi nyingi wanavunja sheria, juzi wamemsema vibaya kila mtu kwenye nchi hii, chama hiki ni tatizo kubwa

Siku amerudi jamaa yao, nakuambia siku ile watu hawakutembea barabarani, waliambiwa pita moja, wee wamepita zote na siyo kwamba walikuwa wengi ni kama walikuwa wanapita zigizaga, mimi nimekutana nao pale Kinondoni Studio wapo huku na huku

Unajua wamefika mpaka kwenye ofisi zao Mtaa wa Ufipa, wakaanza kusema mbona hawajatukamata, nikasema kumbe mpango wao ilikuwa kukamatwa sasa hawajakamatwa wanalalamika, hiki chama sikielewa hivi nidhamu ni zero na kutii sheria bila shuruti ni zero

Halafu wanajenga hoja wanasema tuambieni wapi tumevunja sheria, hivi kwenye nchi hii kuna sheria inasema usichukue Mke wa Kaka yako?, mimi nawaachia Watanzania hiki ndiyo chama kabla hakijaomba dhamana kishabadili Wimbo wa Taifa kishafanya wa chama.

Wana-CCM ambao mmeomba dhamana na mlizingatia katiba na kanuni hamkujishirikisha kwenye makatazo na miiko muwe na amani na sisi kama chama hatutawaangusha watu waaminifu na wanyenyekevu na wenye nidhamu, ila wale mlipiga mazonge tutafundisha watu adabu kipindi hiki. Kila mwanachama aliyeshiriki ‘uovu’ katika kura za maoni, atashikishwa adabu.

Nampa pole TID sababu hawa majamaa ni mazulumati wametudhulumu wimbo wa Taifa. TID anapambana mtu wa watu ametengeneza Ni Yeye na ile ilikuwa Magufuli, wale majamaa wameichomeka kule. Hawajamshirikisha hawajamuomba kwa kweli sisi kama Watanzania tutawachukulia hatua.

 
Mbona kama ilikuwa ni press ya kuwachamba cdm?
 
Hisia zimeanza kuwa kali na kwa mara ya kwanza nasikia CCM wakikiri kupungukiwa uvumilivu. Polepole amekerwa na CHADEMA kuuchezea wimbo wa taifa na katika hilo amekiri hakuna uvumilivu wa kisiasa.

Naye Tundu Lissu amedai NEC hawawezi kumkata kwa sababu hajavunja sheria yoyote ya maadili na kwamba atamuwekea pingamizi Dr Magufuli.

Kiufupi dalili zote zinaonyesha kwamba kampeni za mwaka huu hazitakuwa za kitoto maana Polepole kaishiwa uvumilivu na kusema Maalim Seif amekomaa usoni ampishe kijana Mwinyi.

Maendeleo hayana vyama!
 
Muumba mbingu na nchi ampe afya njema na maisha marefu muheshimiwa Polepole kwa hekima na busara zake zilizotukuka.
 
Si ange ongelea kwenye lile kongamano la wadada Mh alio wapigia simu?
Huu ni mwrndelezo wa kuzuia vyombo vya habari visitangaze mkutano wa ACT WAZALENDO. Hawezi kuwaita waandishi muda ule ule ambao ACT wana anza mkutanobaao live..
Sijui anae wapa Ccm hizi mbinu za kizamani ana toka wapi kwenye hii dunia. Na tujiulize, Ccm wana ogopa nini???
tuendelee kulisha familia zetu hao jamaa mmhh achaneni nao tu..wanaumiza vichwa juzi tu lowassa tulikuwa nae ukawa leo anasema tumuunge mkono magufuli..ukiwa na hasira sana kunywa sumu ni jambo la dakika moja tu
 
kijana anaipenda ccm hata baada ya miaka 60 ta uhuru namuonea huruma
 
Fomu chukueni lakini Rais wa Tanzania ajaye ni Tundu Antipas Lissu, inyeshe isinyeshe. Hata kama mtaamua kumtangaza JPM kwa kutumia NEC na Polisi, mjue nguvu ya umma itatumika kumchomoa JPM Ikulu kama Ivory Coast walivyomchomoa Laurent Bbagbo mwaka 2012
 
Bwana Polepole muanzie na Jimbo la Rorya. Namba 1,2, na 3 nafasi zao zina walakini.
 
Hili eti ndiyo jembe la CCM. Ndiye katibu wa itikadi na uenezi. Kutoa taarifa tu za mgombea wao kwenda kuchukua fomu mpaka tukio lirushwe live na TV....

Ama kweli CHEMA CHAJIUZA, KIBAYA CHAJITEMBEZA CHENYEWE USIKU NA MCHANA ILI KIJIUZE...

å Chema ni CHADEMA na ACT - Wazalendo. Vinajiuza vyenyewe hivi...

å Kibaya ni CCM, kinajitembeza na kujiuza hiki mithili ya changudoa.....!
 
Polepole atuambie hapa alitolea tamko gani? Au kunya anye kuku, bata atakuwa kaharisha?

 
Summary ya press ya Polepole:

1.kuwafokea wananchi waliompokea Lissu Airport.
2. kufokea chadema kuhusu ubeti wa nyimbo ya taifa.
3. Kupiga kampeni kabla ya uchaguzi.
4. kuwafokea chadema kwa kutumia neno ambalo yeye anasema ni mali ya T.I.D.
5. Kutaja list ya wasanii kama kivutio cha kuongeza wahudhuriaji kwenye kampeni za CCM (hapa kamtaja hadi man walter ambaye sio msanii)

My Take:
(a)CCM wamepanic baada ya ujio wa Lissu nchini hususani baada ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya CDM.
(b) CCM wamepandwa na jazba kwa spana walizoonjeshwa kidogo kwenye vikao vya CDM vilivyofanyika Mlimani City.

NB:
Mataga safari hii mmejiingiza kwenye kina kirefu chenye mamba wakali mnoo [emoji1787][emoji1787][emoji1787]

[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2] ila Siasa Bana.
 
Back
Top Bottom