Huyo jamaa ni tapeli sana, anashindwa nini yeye kuratibu hiyo zoezi kupitia Wizara ya Afya?! Anatumika vibaya na waCuba. Utaratibu wa kuingiza Dawa nchini unajulikana na Sheria zipo lakini Polepole hataki kufuata Sheria ya nchi. Kama upo ulazima wa kuingiza hizo Dawa ambazo hazijasajiliwa nchini Serikali ndo ina uwezo wa kuingiza kwa njia ya dharura lakini siyo kama anavyofanya huyo Balozi.Kwa nini Polepole anataka atumiwe majina ya wagonjwa??
Sahihi kabisa.Polepole hafai kuendelea kuwa balozi.
Acheni kuaminishwa porojo za kijuha,Nyie ndio watu mnaojifikiria nyinyi tu badala ya kuwafikiria maelfu ya wananchi ambao wanateseka na maradhi ambayo hayana tiba nchini. Pole pole kwa maono yake anataka kuwasaidia wananchi hao na ndio maana anataka majina yao ili idadi Yao ifahamike. Idadi Yao ikifahamika itakuwa rahisi kujua kiasi cha dawa kinachoweza kuletwa nchini ; dawa zikiletwa itakuwa rahisi kuwasiliana na wagonjwa ambao majina yao yameorodheshwa.
Ikumbukwe kwamba hao waganga wanaotaka kuhujumu huu mpango wa dawa kutoka CUBA ni wale waliosomeshwa Kufuata ya western countries ambao hawataki kusikia kuwa nchi ya Cuba ina ubingwa wa kutibu kuliko mabwana zao wa America na Uingereza. Hao hao mabwana zao kutoka Ulaya na America wanazunguka kwa watindiga na wamasai wakitafuta madawa ya asili ambayo wanakwenda kuyafanyia utafiti na kuyauza as supplements!!
Mama Abdul ni lazima aje openly kuunga mkono initiative hii kwani wananchi wengi wa Visiwani wakiwemo ndugu zake wa karibu na viongozi wa Serikali wanasumbuliwa na maradhi ambayo dawa hizi zitawasaidia!!
Hizo dawa za Cuba zifuate utaratibu kama vile dawa nyingine zote mfano zinazotoka India na Ulaya zinavyofuata utaratibu kuuzwa nchini. Litakuwa taifa la kijuha na la kienyeji sana kuingiza tu dawa kwa kusikiliza maneno ya mtu au wawili watatu. Hamjachoka tu na utapeli wa kikombe cha babu na dawa za Madagascar alizokuwa anagawa Rais mwenyewe ambapo hadi ndege ilitumwa kuzichukua?!Kuja public kusudi lake ni kuona wananchi wa chini wanafahamu uwepo wa dawa hizi ili nao wafaidike!! Ama sivyo mafisadi wataingilia kati na walengwa wa Polepole hawatafaidika!!
Serikali haina sababu ya kuingilia na kuweka vikwazo ; waache dawa ziingie na wananchi wazijaribu kama zinafanya kazi na kuwasaidia wananchi. Kama hazitafanya kazi biashara itakufa naturally!
Watu wenye ufahamu kama wako ndio wanakwamisha maendeleo ya nchi; Polepole katimiza wajibu wake. Hospitali ya Kairuki umejiridhisha kwamba kuna tatizo na wenye matatizo wameelekezwa kuwasiliana na hospital ya Kairuki. Ninyi mnaojiona lazima mshirikishwe endeleeni kusoma sheria na taratibu.Huyo jamaa ni tapeli sana, anashindwa nini yeye kuratibu hiyo zoezi kupitia Wizara ya Afya?! Anatumika vibaya na waCuba. Utaratibu wa kuingiza Dawa nchini unajulikana na Sheria zipo lakini Polepole hataki kufuata Sheria ya nchi. Kama upo ulazima wa kuingiza hizo Dawa ambazo hazijasajiliwa nchini Serikali ndo ina uwezo wa kuingiza kwa njia ya dharura lakini siyo kama anavyofanya huyo Balozi.
Hivi Kiongozi anayevunja Sheria za nchi ni wa nini?! Hivi majukumu ya msingi ya Balozi ndiyo hayo kweli?
Kwahiyo wanaofaa ni wale wako kimya sio?Polepole hafai kuendelea kuwa balozi.
Upo sawa, ndiyo maana nikasema Wizara inashindwa nini kuagiza hiyo Dawa kwa njia ya dharura kama ulazima upo? Ninachoona hospitali binafsi zinataka kutelezea humo kwa Balozi kupindisha utaratibu wa nchi for his own interest.Watu wenye ufahamu kama wako ndio wanakwamisha maendeleo ya nchi; Polepole katimiza wajibu wake. Hospitali ya Kairuki umejiridhisha kwamba kuna tatizo na wenye matatizo wameelekezwa kuwasiliana na hospital ya Kairuki. Ninyi mnaojiona lazima mshirikishwe endeleeni kusoma sheria na taratibu.
Wagonjwa hawana shida na sheria wana shida na kupona maumivu na makovu yanayowasumbua. Nilitoa mfano wakati wa kikombe cha babu wanasiasa na wanasheria wote waliekea kwa babu na hakukuwa na pingamizi.
Wakati mnajiandaa kufuata sheria wapo watanzania tayari wana tiketi za kwenda Cuba kupata matibabu
Huyo lofa wako anatafuta cheap popularity. Atulize tako afanye kazi ya ubalozi. Kila jambo lina taratibu zake aache utoto. Polepole hajawahi kuwa na akili hafai kuwa kiongozi mkubwa. Enzi za kichaa mwenzake alikuwa anawapigia mawaziri na watendaji wa serikali saa 5 usiku eti kutatua matatizo ya wananchi. Hajui kuna muda wa kazi? Amejaa sifa za kijinga, ana IQ ndogo km Bashite.Pole pole anapiga kazi , ana uwezo wa kujenga hoja na anayo maono makubwa kuhusu kesho ya Tanzania.
Kwa akili alizonazo hawezi kukubalika ndani ya CCM kirahisi na mwisho wa siku watampiga Majungu hata nafasi yake ya Ubalozi apokonywe. Waliona akiwa Malawi anafaidi wakampeleka Cuba . Amefika Cuba ametulia na kufanya mazungumzo na mamlaka husika na zimemwelewa, amepata fursa ya kuleta dawa tiba kwa watanzania.
Kuonyesha wana CCM walivyo na wivu na chuki, imemlazimu yeye binafsi afanye mazungumzo na hospitali ya Kairuki na kuwaomba wenye hospital nyingine wamtumie majina ya wagonjwa. Wizara ya Afya hakuna Sehemu kwenye website wala mitandao ilipoonyesha kumuunga mkono. Maana yake wapo watu wanajadili namna yakumkwamisha kwa kisingizio cha taratibu za kuingiza dawa nchini.
Watafanya hivyo kumkwamisha kwa sababu wao siyo wahanga wa magonjwa haya manne anayowaza kutusaidia mdogo wetu Polepole. Wapo watu wizara ya Afya watataka waende Cuba kujiridhisha na dawa hizi kwa gharama za serikali au cuba , jiulize kama hizo dawa hazipo nchini wao walizosomea wapi hadi wakazifanyie uchunguzi?
Nimeandika haya kwa sababu kwenye moja ya droup la whatsapp nimeona kiongozi mmoja Mwanza mwenye taaluma ya dawa akisema Polepole hatofanikiwa kwenye mpango wake kwa sababu hizo dawa anqzosema hazijasajiliwa na Mamlaka za Tanzania na kwamba serikali haiwezi kuziruhusu ziingie nchini. Pia ameongeza hakuna dawa zinaingizwa nchini kwa sababu tu balozi kaomba, dawa zinatakiwa zifanyiwe utafiti na wataalam wetu aidha kwa wao kwenda Cuba au sample kuletwa Tanzania. Haya mawazo ndiyo mtizamo wa wasomi wengi wa Afya, ndio mtizamo wa washauri wa serikali kwamba wao dawa hawana lakini wanataka wapewe wazichunguz3....Pole pole usikate tamaa tunahitaji msaada huu wa tiba kwa ajili ya ndugu zetu. Ila fanyia utafiti vikwazo vinavyotarajiwa kuwekwa na wanasiasa wenzako kukuzina mdomo na kukufanya uonekane umewalaghai wananchi.
Wizara ina utaratibu wake wa kufanya kazi, inajua mahitaji yake siyo atokee mpumbavu moja kwa maslahi yake aanze kutumia mitandao kuwa anataka kuleta dawa. Pole×2 hakuwahi kuwa na akili, alikuwa hata hajui majukumu ya mwenezi wa chama. CCM sijui inamchekea wa nini arudishwe nyumbani.Upo sawa, ndiyo maana nikasema Wizara inashindwa nini kuagiza hiyo Dawa kwa njia ya dharura kama ulazima upo? Ninachoona hospitali binafsi zinataka kutelezea humo kwa Balozi kupindisha utaratibu wa nchi for his own interest.
Sasa mwehu km wewe utamtambuaje mwenye akili?Polepole ni very intelligent.
teh teh.Sasa mwehu km wewe utamtambuaje mwenye akili?
wewe ni special case, madaktari wasikupuuze.Sasa mwehu km wewe utamtambuaje mwenye akili?
Mimi kiuweli huyu Polepole ananishangaza sana. Hizo Sheria na Kanuni tumeziweka za nini kama hatuwezi kuheshimu?! Eneo sensitive kama la afya siyo ya kucompromise kirahisi namna hii. Tuna Wizara husika na Idara zake, nini kinashindikana yeye kupitia huko?! Balozi unabagaza Wizara ya Serikali yako?! Kweli?Wizara ina utaratibu wake wa kufanya kazi, inajua mahitaji yake siyo atokee mpumbavu moja kwa maslahi yake aanze kutumia mitandao kuwa anataka kuleta dawa. Pole×2 hakuwahi kuwa na akili, alikuwa hata hajui majukumu ya mwenezi wa chama. CCM sijui inamchekea wa nini arudishwe nyumbani.
Huko ndio afrika utaijua vizuri kwenye taratibu na sheria.Pamoja na kazi nzuri ya Polepole, lazima sheria, kanuni na taratibu zinazohusu uingizaji dawa zifuatwe.
Dawa zaweza kusababisha madhara zaidi ya kutibu, hivyo weledi unahitajika na siyo siasa.
Adui mkubwa wa taifa hili ni CCMNyerere alituambia kuwa maadui wakubwa wa taifa ni maskini, ujinga na maradhi.
Ila alisahau kuwa, kuna maadui wengine waliojificha ambao ni chuki na roho mbaya, hawa maadui wapya ndio sasa wanaliangamiza taifa kuliko chochote.
Adui wa Mwafrica huwa ni mwafrica mwenzie.
Lakini si zilikuja? Sasa hizi za Cuba mnazbania kwanini? Kwavile zinampandisha Chati Pole pole au mnataka kujipendekeza kwa Marekani kuwa nyinyi nanyi mnawawekea embargo Cuba? Acheni ujinga huo ; Rais wenu mstaafu “Kamando” pengine angewahi kupata dawa hizo saa hizi angekuwa anaona!!Hivi zile juice alizofuataga muokotwa jalalani
Hivi zile juice alizofuataga muokotwa jalalani kwa ndege yetu kule Madagascar ziliishia wapi mkuu?
Maana promo yake ilikuwa baabu kubwa.
Polepole ni kati ya watu wajinga ambao huwa wanaona Tanzania ni mali binafsiMimi kiuweli huyu Polepole ananishangaza sana. Hizo Sheria na Kanuni tumeziweka za nini kama hatuwezi kuheshimu?! Eneo sensitive kama la afya siyo ya kucompromise kirahisi namna hii. Tuna Wizara husika na Idara zake, nini kinashindikana yeye kupitia huko?! Balozi unabagaza Wizara ya Serikali yako?! Kweli?
Huyu ni Balozi wa hovyo kuweza kutokea Tanzania.
Taratibu na sheria zipo kila mahali, hata Mbinguni.Huko ndio afrika utaijua vizuri kwenye taratibu na sheria.