Huna Wajibu wa kumtunza au kumhudumia Mzazi wako akiwa chini ya miaka 60 kama haumwi

Huna Wajibu wa kumtunza au kumhudumia Mzazi wako akiwa chini ya miaka 60 kama haumwi

Mleta mada umeona mindset za watu weusi?

Mtu mweusi
anazaa watoto kama investment.

Lengo la mtu mweusi kuzaa watoto ni ili watoto waje wamhudumie.

Hapa umegusa shina halisi la maana ya maisha ya muafrika, utapingwa na kila mtu.
Hata ufanyeje huwezi kuikimbia asili yako na ndiyo umeshakuwa hivyo huna namna.

Kama yupo hapa mtu anayeweza kusema mzazi asisaidiwe kwa kigezo chochote kile eg:umri maradhi ni kusema hela anatafuta za kazi gani?wema atamtendea nani ikiwa hata yule aliyemzaa na kumsomesha anajiuliza ampe au asimpe huyu ataweza kweli kumsaidia hata mlemavu?
 
Mimi niliwahi kuwa na dada wa kazi binti mdogo tu wa miaka 18, mshahara nilikua namlipa elf.50 kwa mwezi. Kitu Cha kushangaza ikifika tarehe tu mshahara kulipwa mama wa yule Binti anampigia simu mwanae atumiwe hiyo pesa.

Yule binti hakuwahi kutumia pesa yake hata kidogo maana akipokea tu mama ake anampigia na kumwambia shida kibao alizonazo huko alipo. Aisee nilikua namuhurumia sana lkn hakua na uwezo wa kumkatalia mama ake.

Wazazi inabidi tujitafakari sana, tuwape muda watoto watafute maisha. Wakishajipata watarudi kusaidia nyumbani, hii kumbebesha mzigo mtoto ni kumdidimiza aendelee kuwa masikini.
 
Mzazi ni mungu wa duniani.

Kushukuru ni kufungua milango ya baraka.

Mawazo haya ya kujitenga na wazazi wako Mwanaume, lazima utakuwa Umepewa na mkeo ambaye pesa zote anapeleka kwao.
Mke amtoe wapi huyu chakubanga?

Bado maskini sana huyu na bado mdogo,kuanza tu kuona kumsaidia Baba yake nor mama yake siyo jukumu lake huyu hawezi ishi na binti wa mtu.na hawa ndiyo wanataka kusaidiana maisha na mke hata wakijua ametoka kudanga.
 
Nimesoma tu heading nikagundua mtoa mada ni mtu ambae hamnazo.!

Ni mtu ambae kila anachokifikiria kichwani kwake anakiona Cha kukileta mbele ya jamiii na kujiona genius.

Usipowapa furaha wazazi wako unataka kuwapa wakina nani.?? Maisha ni Nini kwako kama unajiweza na huku ukiwapa kisogo wazazi wako eti tu kisa wapo chini ya miaka 60.

saidia wazazi wako kwa kile ulicho nacho Wala hutapungukiwa chochote na zaidi baraka zitaongezeka katika utafutaji wako.!

Usisubiri mzazi afe ili uje kuonyesha fahari katika mazishi mbele ya jamii na marafiki WA kazini kwako

Note.
Maisha ni mafupi sana Miaka inaenda kama upepo siku si nyingi na sisi tutakuwa wazee kama walivyo wazazi wetu. Tusaidie ndugu na jamaa zetu

Nb.taikon WA fasihi ni mtoto mdogo Ambae hajui maisha yanataka nini. Yeye anajua mtu ukishapata Hela basi imeisha unafanya unavyoweza.kumbe sio kweli Kuna sehemu Hela na umaarufu havifiki

Be humble mzee sio Kila kitu Cha kuandika mtandaoni ' WE zombie.
Pole mkuu
 
Mke amtoe wapi huyu chakubanga?

Bado maskini sana huyu na bado mdogo,kuanza tu kuona kumsaidia Baba yake nor mama yake siyo jukumu lake huyu hawezi ishi na binti wa mtu.na hawa ndiyo wanataka kusaidiana maisha na mke hata wakijua ametoka kudanga.
Ulichoongea nini
utoto ndo unaomsumbua sababu unaweza ukawa na miaka hata 40 ila utoto ukawa unakusumbua

majukumu ya mwanaume ni pamoja na kusaidia wazazi wako ndo asili yetu wa afrika
Mada nyingi sana za huyu jamaa zinautoto mwingi sana na fantasy kama watu wakizifuata basi tutakua na jamii ya hovyo sana ya kila mtu abebe msalaba wake

Wanawake uwaonge na marafik zako uwanunulie bia ila iwe ni nongwa kumsaidia mzazi wako tunawatu wanafikra za hovyo sana
 
HUNA WAJIBU WA KUMTUNZA AU KUMHUDUMIA MZAZI WAKO AKIWA CHINI YA MIAKA 60 KAMA HAUMWI.

Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Mada hii inaweza kuwa ngumu kwa baadhi ya Watu. Lakini nitakachojadili hapa ni Haki, kweli, akili na upendo kama ilivyo kwa Watibeli wote.

Kama ilivyo kwa mzazi hana wajibu wa kukutunza na kukuhudumia pindi ufikishapo umri wa kujitegemea yaani kuanzia miaka 21 hivi kwa sisi Watibeli. Na kwa sheria za dunia ni miaka 18. Basi ndivyo hivyohivyo kuwa mtoto hana wajibu wa kumtunza na kumhudumia mzazi au mlezi ambaye yupo chini ya miaka 60 ambaye HAUMWI(hana tatizo la kiafya).

Kuna kijitabia fulani cha kinyonyaji, dhulma, uvivu, na ukandamizaji ambao unafanywa na wazazi kwenda kwa watoto wao. Ambapo mzazi anazaa watoto idadi fulani anawapa na kuwatunza(wajibu wake) alafu wakishafikisha miaka 20 tuu wakaenda kujitafutia basi inakuwa nongwa. Mzazi hata miaka 50 haujui, miaka 60 ndio kabisa hatarajii leo wala kesho kuifikia. Mzazi ananguvu kabisa lakini kutwa kusumbua watoto na kuwatia watoto katika shinikizo isivyostahili.

Sio jukumu la mtoto kukulea na kukutunza ukiwa na umri huo. Wewe bado upo umri wa kujitegemea na kujihudumia. Kwa nini umpe mtoto mzigo? Kwa nini umdhulumu mtoto haki zake?
Kama sababu ni kuzaa na kumtunza hata yeye atazaa na kutunza watoto wake.

Kama ishu ni wajibu basi subiri muda ukifika mtoto atekeleze wajibu wake. Na kama atakutunza au kukuhudumia iwe kwa uwezo na mapenzi yake kwako na shukran na sio shinikizo.

Ni laana kubwa kumhudumia mtu isivyo halali. Kuhudumia mzazi kwa kushinikizwa yaani kunyonywa na kudhulumiwa ni laana ambayo wengi inawatafuna.

Sio ajabu unakuta Watu wengi tangu wakiwa vîjana wanateseka kuhudumia wazazi isivyostahili wakifikiria ndio baraka lakini miaka inaenda maisha yao hayabadiliki zaidi ya kuzidi kuwa maskini na fukara zaidi.

Ni sawasawa na mzazi amuone mtoto keshafikia umri wa kujitegemea alafu bado awe anamhudumia na kumtunza huo ni umaskini wa akili na roho. Lazima kizazi hiki kiwe fukara.

Ninajua ndoa nyingi zilizoharibika na familia nyingi kuanguka kisa wazazi kushinikiza huduma. Ni laana tupu. Wakati huo wazazi wananguvu kabisa.
Ninajua mabinti wengi wanaoteseka kwenye ndoa kisa wazazi wao wamewashinikiza watoto wao wabaki kwenye mateso ili wao wanufaike au walishanufaika na kumuuza binti yao.

Wengine huwashinikiza binti zao waolewe na wanaume wenyewe pesa hata kama hawapendwi na binti zao kwa kulenga kuhudumiwa na pesa za mkwilima wao.

Wapo vibinti vya kazi za ndani wanalipwa mishahara kiduntu kama elfu 30 mpaka 60 na bado wazazi wanataka gawiwo licha ya kuwa wazazi hao bado kiumri wanauwezo wa kufanya kazi na kujitafutia.

Wapo wazazi kiumri ni wadogo lakini wanawakosea watoto wao haki kwa kuwashinikiza watoto wao kwa matusi na kejeli kuwa hawafanyi kazi huko mjini kisa tuu hawatumiwi pesa. Jambo ambalo sio Haki na sio Upendo.
Wapo watoto wanajitutumua kuhakikisha wanahudumia wazazi wao kiugumuugumu, kwa kujikamua, na malalamiko ya nafsi wazazi kwa ubinafsi wao huona ni sahihi lakini sio sahihi kabisa.

Acheni watoto wakiwa na umri wa kujitafutia watafute na kujitegemea alafu wao kwa roho ya upendo wawatumie kwa hiyari yao na sio kuwadhulumu maisha na nguvu zao.

Watoto pia, acheni kudhulumu nguvu za wazazi wenu huku mkujua kuwa tayari mmefikia umri wa kujitegemea na sio kuwapa wazazi wenu mzigo, kuwanyonya na kuwakatili.
Mzazi asifurahie utu uzima wake aanze kukufikiria mtu mzima na ndevu zako kisa ati ni mtoto wake. Hiyo sio HAKI

Kumhudumia mzazi wako aliyemzee sio hiyari yako wala sio mapenzi yako kwake. Hiyo ni lazima, wajibu.
Bahati nzuri wazee hawana mahitaji mengi kama ilivyo kwa watoto.

Lakini kuhudumia mzazi aliyechini ya miaka 60 na haumwi hiyo ni hiyari na mapenzi tuu na sio lazima/wajibu. Unaweza ukafanya au usifanye na hakuna lolote litakupata.

Kumhudumia mtu anayeweza kujitegemea ni laana na kurudisha nyuma kizazi na ukoo wenu.
Lazima Watu wafanyekazi na wawajibike kwa maisha yao na ya wale wanaowahusu.

Huo ndio Utibeli. Ukweli, haki, upendo na Haki
Mimi nimemaliza, mwenye maswali anaweza kuuliza.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Kwa asili mtu akizeeka anakuwa less productive,kuna wakati tu utahitaji jeki kama sio MALI basi jeki ya HALI,
Kama watoto wako wa kuzaa hawawezi kufanya lolote kati ya hayo basi hiyo ni PATAPOTEA.

Sent from my TECNO BE6 using JamiiForums mobile app
 
Kwa asili mtu akizeeka anakuwa less productive,kuna wakati tu utahitaji jeki kama sio MALI basi jeki ya HALI,
Kama watoto wako wa kuzaa hawawezi kufanya lolote kati ya hayo basi hiyo ni PATAPOTEA.

Sent from my TECNO BE6 using JamiiForums mobile app
Ukiwa kijana una-nguvu unaamini hizo nguvu utakua nazo milele kama mleta uzi anavyodhani
Ila kuna mda nguvu zinaisha inabidi uwe mpole
 
Soma vizuri mkuu unielewe.
Sijasema mtu asisaidie kwao au wazazi.
Afanye kwa hiyari au mapenzí kwa wazazi ambao hawajazeeka.

Kuna wazazi wanatumia vibaya uzazi wao kudhulumu haki za watoto.
Kama ilivyo kuna watoto wanatumia utoto wao kudhulumu haki za wazazi wao
Watanzania wengi hatuwezi kukuelewa kwa sababu fikra zetu zimegandishwa na ujamaa wa Mwalimu.

Chanzo kikuu cha umasikini Tanzania ni umasikini wa kurithi na siyo wa kipato.

Yaani unakuta mtu ana kipato kizuri lakini kwa kuwa nyuma yake ana msururu wa ndugu wategemezi basi automatically anakuwa masikini.

Yaani unazaliwa na ukikua tu ndugu wanaanza kukuganda uwasaidie na utatue shida zao.

Mimi niliwahi kupewa jukumu la kujenga nyumba kwa babu sehemu ambayo baba zangu na baba wadogo walishindwa kujenga kwa zaidi ya miaka 40.

Nikawaambia siwezi kujenga hapo wakati mimi bado kwangu.

Waafrika tuna mambo ya ajabu sana!
 
Mke amtoe wapi huyu chakubanga?

Bado maskini sana huyu na bado mdogo,kuanza tu kuona kumsaidia Baba yake nor mama yake siyo jukumu lake huyu hawezi ishi na binti wa mtu.na hawa ndiyo wanataka kusaidiana maisha na mke hata wakijua ametoka kudanga.
Kila mwaka wanaenda Moshi ukweni,

Unakuta watoto aliowazaa, hawajui Babu Yao wa kiumeni, ni ukweni tu,

Wanawake tuishi nao Kwa akili asee!!
 
Kama watoto wenyewe ndiyo hawa akina Mtibeli alafu ndiyo tuwategemee waje watusitiri tukizeeka tuhesabu maumivu tu Wazee wenzangu.

Ndiyo maana nimefungua akaunti yangu ya Siri, najiwekea hela zangu ili kuepusha aibu ya kudharilishwa na Watoto tunaotegemea watupe Faraja Uzeeni.

Kama nitakufa mapema bora wale watu wa Benki tu 🥲
Baba kumbe ndiyo tabia yako unatufanyia!?

Na ukipata tatizo usitusumbue; utumie hizohizo hela!

Na mama nitamwambia!
 
Mtoa mada katumia akili nyingi sana huenda ni Uzi mzuri zaidi ktk hii wiki.

Wachangiaji wengi hawana critical thinking na wanakurupuka kumkosoa mtoa mada bila kuwaza mara mbilimbili na kufanya analysis.

Binafsi nitashare experience yangu:

Baada ya kupata kazi tu.. nikaanza kujumuishwa ktk ishu za familia hasa kulipia ADA wadogo zangu (Hapo mwanzo walikuwa wanalipiwa na Wazazi na Shule waliyosoma wao ni ghali sana na wapo watatu) haya nikawa najibana nalipa angalau nusu ya ada kwa wote watatu.

Ikumbukwe mimi nimesoma shule ya kidumu na mfagio na wazee walikuwa nauwezo wa kunisomesha ktk mabas ya njano ila wakanitupa huko.

Wananyumba huwa wamepangisha na wanakusanya kodi kila mwisho wa mwezi, kama mtoto ktk swala la mgao wala sijawahi kupata hata mia.. na wakikusanya maokoto hata taarifa hupati ila ww utapata taarifa za majanga tu kuna hiki kimeharibika kuna kile kinataka hela etc.. ila.maswala positive hutosikia taarifa achilia mbali mgao (siutaki mgao wenyewe).

Haya ilifikia muda nataka kuoa, wakaniwekea ngumu nisioe (akili yangu ikawa imejiongeza na kujua nini sababu ya wao kunikataza kuoa wakisema ni mapema kwamba nina umri mdg hapo nina 28), jambo ambalo wao walikuwa hawataki ni mm kuwa na majukumu na familia yangu ntakayoanzisha hivyo sitaendelea kuwapa hivyo vihela vya hapa na pale..

Familia za kimaskini ukiziendekeza hupigi hatua sana sana unabaki palepale kila siku.. mshahara unaingia unapitiliza kusolve ishu zao sometimes ubinafsi unasaidia sana kupata maendeleo.

Wazazi wawaache wototo wajiimarishe kiuchumi ndio wafaidike na sio mtu kajipata kdg tu tyr majukumu mnamjazia hapo hata kujiweka sawa bado na mnaenda mbali kumzuia ishu za msingi kbs kama kuanzisha familia yake ili muendelee kula hela zake kwa uhuru..

Kwani nan kasema nikiwa na familia yangu sitawasaidia? Mawazo ya kimaskini sana..
 
Nimesoma tu heading nikagundua mtoa mada ni mtu ambae hamnazo.!

Ni mtu ambae kila anachokifikiria kichwani kwake anakiona Cha kukileta mbele ya jamiii na kujiona genius.

Usipowapa furaha wazazi wako unataka kuwapa wakina nani.?? Maisha ni Nini kwako kama unajiweza na huku ukiwapa kisogo wazazi wako eti tu kisa wapo chini ya miaka 60.

saidia wazazi wako kwa kile ulicho nacho Wala hutapungukiwa chochote na zaidi baraka zitaongezeka katika utafutaji wako.!

Usisubiri mzazi afe ili uje kuonyesha fahari katika mazishi mbele ya jamii na marafiki WA kazini kwako

Note.
Maisha ni mafupi sana Miaka inaenda kama upepo siku si nyingi na sisi tutakuwa wazee kama walivyo wazazi wetu. Tusaidie ndugu na jamaa zetu

Nb.taikon WA fasihi ni mtoto mdogo Ambae hajui maisha yanataka nini. Yeye anajua mtu ukishapata Hela basi imeisha unafanya unavyoweza.kumbe sio kweli Kuna sehemu Hela na umaarufu havifiki

Be humble mzee sio Kila kitu Cha kuandika mtandaoni ' WE zombie.
Wewe ndo HAMNAZO. Huyu Mtibeli yuko sahihi 100%. Tena hiki ni kilio cha wengi ila kimyakimya. Watu wanawasitiri tu wazazi wao ila ndani kwa ndani moto unawawakia. Mabinti wananyanyasika kwenye ndoa wazazi wanaishia kuwaambia NDOA NI UVUMILIVU kisa kuna maokoto wanapata kutoka kwa mkwe. Watu wengi imekuwa ngumu kuchomoka kwenye umaskini kwasababu ya kutumia muda na pesa zao kufanya majukumu ya wazazi wao kama vilw kusomesha wadogo zao. Watoto wa kwanza wengi huwa maskini na wale wa mwisho huwa na unafuu kwa kutokuwa na majukumu mengi. PUNGUZENI UNAFIKI tujiokoe kwenye umaskini.
 
Hata ufanyeje huwezi kuikimbia asili yako na ndiyo umeshakuwa hivyo huna namna.

Kama yupo hapa mtu anayeweza kusema mzazi asisaidiwe kwa kigezo chochote kile eg:umri maradhi ni kusema hela anatafuta za kazi gani?wema atamtendea nani ikiwa hata yule aliyemzaa na kumsomesha anajiuliza ampe au asimpe huyu ataweza kweli kumsaidia hata mlemavu?
Kinachonipa faraja ni kwamba, Ujinga wa muafrika hausababishwi na rangi yake, bali na vitu vingine hivyo basi,

Naikubali rangi yangu nyeusi ila naukataa Ujinga wa mtu mweusi.

Wewe kama unaamini ni jukumu lako kuhudumia wazazi wako hudumia, na kama unadhani ni jukumu la watoto wako kukuhudumia waambie wakuhudumie,

Kujaribu kukushawishi vinginevyo ni kupoteza muda, maana hata hujaelewa alichosema mleta mada.
 
Mleta mada umeona mindset za watu weusi?

Mtu mweusi anazaa watoto kama investment.

Lengo la mtu mweusi kuzaa watoto ni ili watoto waje wamhudumie.

Hapa umegusa shina halisi la maana ya maisha ya muafrika, utapingwa na kila mtu.

Lazima nilaaniwe na kupingwa na Watu humu.
Wakati hilo ni jambo lipo Wazi
 
Wewe ndo HAMNAZO. Huyu Mtibeli yuko sahihi 100%. Tena hiki ni kilio cha wengi ila kimyakimya. Watu wanawasitiri tu wazazi wao ila ndani kwa ndani moto unawawakia. Mabinti wananyanyasika kwenye ndoa wazazi wanaishia kuwaambia NDOA NI UVUMILIVU kisa kuna maokoto wanapata kutoka kwa mkwe. Watu wengi imekuwa ngumu kuchomoka kwenye umaskini kwasababu ya kutumia muda na pesa zao kufanya majukumu ya wazazi wao kama vilw kusomesha wadogo zao. Watoto wa kwanza wengi huwa maskini na wale wa mwisho huwa na unafuu kwa kutokuwa na majukumu mengi. PUNGUZENI UNAFIKI tujiokoe kwenye umaskini.

Upo mbele yangu kwa kunielewa
 
Sishangai Mtibel kutoeleweka!

Alichoandika taikuni wa fasihi ni akili kubwa na kinaeleweka kwa wenye akili kubwa pia.

Ukipata shida kuelewa huu uzi, unapaswa kutathimini akili yako na siyo kushambulia mwandishi. Kila kitu kipo wazi.
shida ni kwamba, hakuna anayesoma ndani ya uzi
mtu anavamia heading na ku comment povu
 
HUNA WAJIBU WA KUMTUNZA AU KUMHUDUMIA MZAZI WAKO AKIWA CHINI YA MIAKA 60 KAMA HAUMWI.

Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Mada hii inaweza kuwa ngumu kwa baadhi ya Watu. Lakini nitakachojadili hapa ni Haki, kweli, akili na upendo kama ilivyo kwa Watibeli wote.

Kama ilivyo kwa mzazi hana wajibu wa kukutunza na kukuhudumia pindi ufikishapo umri wa kujitegemea yaani kuanzia miaka 21 hivi kwa sisi Watibeli. Na kwa sheria za dunia ni miaka 18. Basi ndivyo hivyohivyo kuwa mtoto hana wajibu wa kumtunza na kumhudumia mzazi au mlezi ambaye yupo chini ya miaka 60 ambaye HAUMWI(hana tatizo la kiafya).

Kuna kijitabia fulani cha kinyonyaji, dhulma, uvivu, na ukandamizaji ambao unafanywa na wazazi kwenda kwa watoto wao. Ambapo mzazi anazaa watoto idadi fulani anawapa na kuwatunza(wajibu wake) alafu wakishafikisha miaka 20 tuu wakaenda kujitafutia basi inakuwa nongwa. Mzazi hata miaka 50 haujui, miaka 60 ndio kabisa hatarajii leo wala kesho kuifikia. Mzazi ananguvu kabisa lakini kutwa kusumbua watoto na kuwatia watoto katika shinikizo isivyostahili.

Sio jukumu la mtoto kukulea na kukutunza ukiwa na umri huo. Wewe bado upo umri wa kujitegemea na kujihudumia. Kwa nini umpe mtoto mzigo? Kwa nini umdhulumu mtoto haki zake?
Kama sababu ni kuzaa na kumtunza hata yeye atazaa na kutunza watoto wake.

Kama ishu ni wajibu basi subiri muda ukifika mtoto atekeleze wajibu wake. Na kama atakutunza au kukuhudumia iwe kwa uwezo na mapenzi yake kwako na shukran na sio shinikizo.

Ni laana kubwa kumhudumia mtu isivyo halali. Kuhudumia mzazi kwa kushinikizwa yaani kunyonywa na kudhulumiwa ni laana ambayo wengi inawatafuna.

Sio ajabu unakuta Watu wengi tangu wakiwa vîjana wanateseka kuhudumia wazazi isivyostahili wakifikiria ndio baraka lakini miaka inaenda maisha yao hayabadiliki zaidi ya kuzidi kuwa maskini na fukara zaidi.

Ni sawasawa na mzazi amuone mtoto keshafikia umri wa kujitegemea alafu bado awe anamhudumia na kumtunza huo ni umaskini wa akili na roho. Lazima kizazi hiki kiwe fukara.

Ninajua ndoa nyingi zilizoharibika na familia nyingi kuanguka kisa wazazi kushinikiza huduma. Ni laana tupu. Wakati huo wazazi wananguvu kabisa.
Ninajua mabinti wengi wanaoteseka kwenye ndoa kisa wazazi wao wamewashinikiza watoto wao wabaki kwenye mateso ili wao wanufaike au walishanufaika na kumuuza binti yao.

Wengine huwashinikiza binti zao waolewe na wanaume wenyewe pesa hata kama hawapendwi na binti zao kwa kulenga kuhudumiwa na pesa za mkwilima wao.

Wapo vibinti vya kazi za ndani wanalipwa mishahara kiduntu kama elfu 30 mpaka 60 na bado wazazi wanataka gawiwo licha ya kuwa wazazi hao bado kiumri wanauwezo wa kufanya kazi na kujitafutia.

Wapo wazazi kiumri ni wadogo lakini wanawakosea watoto wao haki kwa kuwashinikiza watoto wao kwa matusi na kejeli kuwa hawafanyi kazi huko mjini kisa tuu hawatumiwi pesa. Jambo ambalo sio Haki na sio Upendo.
Wapo watoto wanajitutumua kuhakikisha wanahudumia wazazi wao kiugumuugumu, kwa kujikamua, na malalamiko ya nafsi wazazi kwa ubinafsi wao huona ni sahihi lakini sio sahihi kabisa.

Acheni watoto wakiwa na umri wa kujitafutia watafute na kujitegemea alafu wao kwa roho ya upendo wawatumie kwa hiyari yao na sio kuwadhulumu maisha na nguvu zao.

Watoto pia, acheni kudhulumu nguvu za wazazi wenu huku mkujua kuwa tayari mmefikia umri wa kujitegemea na sio kuwapa wazazi wenu mzigo, kuwanyonya na kuwakatili.
Mzazi asifurahie utu uzima wake aanze kukufikiria mtu mzima na ndevu zako kisa ati ni mtoto wake. Hiyo sio HAKI

Kumhudumia mzazi wako aliyemzee sio hiyari yako wala sio mapenzi yako kwake. Hiyo ni lazima, wajibu.
Bahati nzuri wazee hawana mahitaji mengi kama ilivyo kwa watoto.

Lakini kuhudumia mzazi aliyechini ya miaka 60 na haumwi hiyo ni hiyari na mapenzi tuu na sio lazima/wajibu. Unaweza ukafanya au usifanye na hakuna lolote litakupata.

Kumhudumia mtu anayeweza kujitegemea ni laana na kurudisha nyuma kizazi na ukoo wenu.
Lazima Watu wafanyekazi na wawajibike kwa maisha yao na ya wale wanaowahusu.

Huo ndio Utibeli. Ukweli, haki, upendo na Haki
Mimi nimemaliza, mwenye maswali anaweza kuuliza.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Wazazi wengi wa kiafrika wanazaa watoto wengi ili wakishakuwa wakubwa waje kuwafanya watumwa nao wazazi wabaki kuwa mabwana wanaotumikiwa na watoto wao(hizi ni fikra za kimaskini na ufukara wa kutupwa); toka nimeligundua hilo na hali ya dunia iliyopo sasa nimejiapiza nitazaa watoto wachache hawatazidi wawili, ili nipate nafasi ya kujiimarisha kiuchumi na wao wakiwa wakubwa waendelee na maisha yao bila mimi kuwasumbua. am done.
 
Back
Top Bottom