Hata ufanyeje huwezi kuikimbia asili yako na ndiyo umeshakuwa hivyo huna namna.Mleta mada umeona mindset za watu weusi?
Mtu mweusi anazaa watoto kama investment.
Lengo la mtu mweusi kuzaa watoto ni ili watoto waje wamhudumie.
Hapa umegusa shina halisi la maana ya maisha ya muafrika, utapingwa na kila mtu.
Mke amtoe wapi huyu chakubanga?Mzazi ni mungu wa duniani.
Kushukuru ni kufungua milango ya baraka.
Mawazo haya ya kujitenga na wazazi wako Mwanaume, lazima utakuwa Umepewa na mkeo ambaye pesa zote anapeleka kwao.
Pole mkuuNimesoma tu heading nikagundua mtoa mada ni mtu ambae hamnazo.!
Ni mtu ambae kila anachokifikiria kichwani kwake anakiona Cha kukileta mbele ya jamiii na kujiona genius.
Usipowapa furaha wazazi wako unataka kuwapa wakina nani.?? Maisha ni Nini kwako kama unajiweza na huku ukiwapa kisogo wazazi wako eti tu kisa wapo chini ya miaka 60.
saidia wazazi wako kwa kile ulicho nacho Wala hutapungukiwa chochote na zaidi baraka zitaongezeka katika utafutaji wako.!
Usisubiri mzazi afe ili uje kuonyesha fahari katika mazishi mbele ya jamii na marafiki WA kazini kwako
Note.
Maisha ni mafupi sana Miaka inaenda kama upepo siku si nyingi na sisi tutakuwa wazee kama walivyo wazazi wetu. Tusaidie ndugu na jamaa zetu
Nb.taikon WA fasihi ni mtoto mdogo Ambae hajui maisha yanataka nini. Yeye anajua mtu ukishapata Hela basi imeisha unafanya unavyoweza.kumbe sio kweli Kuna sehemu Hela na umaarufu havifiki
Be humble mzee sio Kila kitu Cha kuandika mtandaoni ' WE zombie.
Ulichoongea niniMke amtoe wapi huyu chakubanga?
Bado maskini sana huyu na bado mdogo,kuanza tu kuona kumsaidia Baba yake nor mama yake siyo jukumu lake huyu hawezi ishi na binti wa mtu.na hawa ndiyo wanataka kusaidiana maisha na mke hata wakijua ametoka kudanga.
Kwa asili mtu akizeeka anakuwa less productive,kuna wakati tu utahitaji jeki kama sio MALI basi jeki ya HALI,HUNA WAJIBU WA KUMTUNZA AU KUMHUDUMIA MZAZI WAKO AKIWA CHINI YA MIAKA 60 KAMA HAUMWI.
Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.
Mada hii inaweza kuwa ngumu kwa baadhi ya Watu. Lakini nitakachojadili hapa ni Haki, kweli, akili na upendo kama ilivyo kwa Watibeli wote.
Kama ilivyo kwa mzazi hana wajibu wa kukutunza na kukuhudumia pindi ufikishapo umri wa kujitegemea yaani kuanzia miaka 21 hivi kwa sisi Watibeli. Na kwa sheria za dunia ni miaka 18. Basi ndivyo hivyohivyo kuwa mtoto hana wajibu wa kumtunza na kumhudumia mzazi au mlezi ambaye yupo chini ya miaka 60 ambaye HAUMWI(hana tatizo la kiafya).
Kuna kijitabia fulani cha kinyonyaji, dhulma, uvivu, na ukandamizaji ambao unafanywa na wazazi kwenda kwa watoto wao. Ambapo mzazi anazaa watoto idadi fulani anawapa na kuwatunza(wajibu wake) alafu wakishafikisha miaka 20 tuu wakaenda kujitafutia basi inakuwa nongwa. Mzazi hata miaka 50 haujui, miaka 60 ndio kabisa hatarajii leo wala kesho kuifikia. Mzazi ananguvu kabisa lakini kutwa kusumbua watoto na kuwatia watoto katika shinikizo isivyostahili.
Sio jukumu la mtoto kukulea na kukutunza ukiwa na umri huo. Wewe bado upo umri wa kujitegemea na kujihudumia. Kwa nini umpe mtoto mzigo? Kwa nini umdhulumu mtoto haki zake?
Kama sababu ni kuzaa na kumtunza hata yeye atazaa na kutunza watoto wake.
Kama ishu ni wajibu basi subiri muda ukifika mtoto atekeleze wajibu wake. Na kama atakutunza au kukuhudumia iwe kwa uwezo na mapenzi yake kwako na shukran na sio shinikizo.
Ni laana kubwa kumhudumia mtu isivyo halali. Kuhudumia mzazi kwa kushinikizwa yaani kunyonywa na kudhulumiwa ni laana ambayo wengi inawatafuna.
Sio ajabu unakuta Watu wengi tangu wakiwa vîjana wanateseka kuhudumia wazazi isivyostahili wakifikiria ndio baraka lakini miaka inaenda maisha yao hayabadiliki zaidi ya kuzidi kuwa maskini na fukara zaidi.
Ni sawasawa na mzazi amuone mtoto keshafikia umri wa kujitegemea alafu bado awe anamhudumia na kumtunza huo ni umaskini wa akili na roho. Lazima kizazi hiki kiwe fukara.
Ninajua ndoa nyingi zilizoharibika na familia nyingi kuanguka kisa wazazi kushinikiza huduma. Ni laana tupu. Wakati huo wazazi wananguvu kabisa.
Ninajua mabinti wengi wanaoteseka kwenye ndoa kisa wazazi wao wamewashinikiza watoto wao wabaki kwenye mateso ili wao wanufaike au walishanufaika na kumuuza binti yao.
Wengine huwashinikiza binti zao waolewe na wanaume wenyewe pesa hata kama hawapendwi na binti zao kwa kulenga kuhudumiwa na pesa za mkwilima wao.
Wapo vibinti vya kazi za ndani wanalipwa mishahara kiduntu kama elfu 30 mpaka 60 na bado wazazi wanataka gawiwo licha ya kuwa wazazi hao bado kiumri wanauwezo wa kufanya kazi na kujitafutia.
Wapo wazazi kiumri ni wadogo lakini wanawakosea watoto wao haki kwa kuwashinikiza watoto wao kwa matusi na kejeli kuwa hawafanyi kazi huko mjini kisa tuu hawatumiwi pesa. Jambo ambalo sio Haki na sio Upendo.
Wapo watoto wanajitutumua kuhakikisha wanahudumia wazazi wao kiugumuugumu, kwa kujikamua, na malalamiko ya nafsi wazazi kwa ubinafsi wao huona ni sahihi lakini sio sahihi kabisa.
Acheni watoto wakiwa na umri wa kujitafutia watafute na kujitegemea alafu wao kwa roho ya upendo wawatumie kwa hiyari yao na sio kuwadhulumu maisha na nguvu zao.
Watoto pia, acheni kudhulumu nguvu za wazazi wenu huku mkujua kuwa tayari mmefikia umri wa kujitegemea na sio kuwapa wazazi wenu mzigo, kuwanyonya na kuwakatili.
Mzazi asifurahie utu uzima wake aanze kukufikiria mtu mzima na ndevu zako kisa ati ni mtoto wake. Hiyo sio HAKI
Kumhudumia mzazi wako aliyemzee sio hiyari yako wala sio mapenzi yako kwake. Hiyo ni lazima, wajibu.
Bahati nzuri wazee hawana mahitaji mengi kama ilivyo kwa watoto.
Lakini kuhudumia mzazi aliyechini ya miaka 60 na haumwi hiyo ni hiyari na mapenzi tuu na sio lazima/wajibu. Unaweza ukafanya au usifanye na hakuna lolote litakupata.
Kumhudumia mtu anayeweza kujitegemea ni laana na kurudisha nyuma kizazi na ukoo wenu.
Lazima Watu wafanyekazi na wawajibike kwa maisha yao na ya wale wanaowahusu.
Huo ndio Utibeli. Ukweli, haki, upendo na Haki
Mimi nimemaliza, mwenye maswali anaweza kuuliza.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Ukiwa kijana una-nguvu unaamini hizo nguvu utakua nazo milele kama mleta uzi anavyodhaniKwa asili mtu akizeeka anakuwa less productive,kuna wakati tu utahitaji jeki kama sio MALI basi jeki ya HALI,
Kama watoto wako wa kuzaa hawawezi kufanya lolote kati ya hayo basi hiyo ni PATAPOTEA.
Sent from my TECNO BE6 using JamiiForums mobile app
Watanzania wengi hatuwezi kukuelewa kwa sababu fikra zetu zimegandishwa na ujamaa wa Mwalimu.Soma vizuri mkuu unielewe.
Sijasema mtu asisaidie kwao au wazazi.
Afanye kwa hiyari au mapenzí kwa wazazi ambao hawajazeeka.
Kuna wazazi wanatumia vibaya uzazi wao kudhulumu haki za watoto.
Kama ilivyo kuna watoto wanatumia utoto wao kudhulumu haki za wazazi wao
Kila mwaka wanaenda Moshi ukweni,Mke amtoe wapi huyu chakubanga?
Bado maskini sana huyu na bado mdogo,kuanza tu kuona kumsaidia Baba yake nor mama yake siyo jukumu lake huyu hawezi ishi na binti wa mtu.na hawa ndiyo wanataka kusaidiana maisha na mke hata wakijua ametoka kudanga.
Jambo la hekima hiliNdiyo maana nimefungua akaunti yangu ya Siri, najiwekea hela zangu ili kuepusha aibu ya kudharilishwa
Baba kumbe ndiyo tabia yako unatufanyia!?Kama watoto wenyewe ndiyo hawa akina Mtibeli alafu ndiyo tuwategemee waje watusitiri tukizeeka tuhesabu maumivu tu Wazee wenzangu.
Ndiyo maana nimefungua akaunti yangu ya Siri, najiwekea hela zangu ili kuepusha aibu ya kudharilishwa na Watoto tunaotegemea watupe Faraja Uzeeni.
Kama nitakufa mapema bora wale watu wa Benki tu 🥲
Wewe ndo HAMNAZO. Huyu Mtibeli yuko sahihi 100%. Tena hiki ni kilio cha wengi ila kimyakimya. Watu wanawasitiri tu wazazi wao ila ndani kwa ndani moto unawawakia. Mabinti wananyanyasika kwenye ndoa wazazi wanaishia kuwaambia NDOA NI UVUMILIVU kisa kuna maokoto wanapata kutoka kwa mkwe. Watu wengi imekuwa ngumu kuchomoka kwenye umaskini kwasababu ya kutumia muda na pesa zao kufanya majukumu ya wazazi wao kama vilw kusomesha wadogo zao. Watoto wa kwanza wengi huwa maskini na wale wa mwisho huwa na unafuu kwa kutokuwa na majukumu mengi. PUNGUZENI UNAFIKI tujiokoe kwenye umaskini.Nimesoma tu heading nikagundua mtoa mada ni mtu ambae hamnazo.!
Ni mtu ambae kila anachokifikiria kichwani kwake anakiona Cha kukileta mbele ya jamiii na kujiona genius.
Usipowapa furaha wazazi wako unataka kuwapa wakina nani.?? Maisha ni Nini kwako kama unajiweza na huku ukiwapa kisogo wazazi wako eti tu kisa wapo chini ya miaka 60.
saidia wazazi wako kwa kile ulicho nacho Wala hutapungukiwa chochote na zaidi baraka zitaongezeka katika utafutaji wako.!
Usisubiri mzazi afe ili uje kuonyesha fahari katika mazishi mbele ya jamii na marafiki WA kazini kwako
Note.
Maisha ni mafupi sana Miaka inaenda kama upepo siku si nyingi na sisi tutakuwa wazee kama walivyo wazazi wetu. Tusaidie ndugu na jamaa zetu
Nb.taikon WA fasihi ni mtoto mdogo Ambae hajui maisha yanataka nini. Yeye anajua mtu ukishapata Hela basi imeisha unafanya unavyoweza.kumbe sio kweli Kuna sehemu Hela na umaarufu havifiki
Be humble mzee sio Kila kitu Cha kuandika mtandaoni ' WE zombie.
Kinachonipa faraja ni kwamba, Ujinga wa muafrika hausababishwi na rangi yake, bali na vitu vingine hivyo basi,Hata ufanyeje huwezi kuikimbia asili yako na ndiyo umeshakuwa hivyo huna namna.
Kama yupo hapa mtu anayeweza kusema mzazi asisaidiwe kwa kigezo chochote kile eg:umri maradhi ni kusema hela anatafuta za kazi gani?wema atamtendea nani ikiwa hata yule aliyemzaa na kumsomesha anajiuliza ampe au asimpe huyu ataweza kweli kumsaidia hata mlemavu?
Mleta mada umeona mindset za watu weusi?
Mtu mweusi anazaa watoto kama investment.
Lengo la mtu mweusi kuzaa watoto ni ili watoto waje wamhudumie.
Hapa umegusa shina halisi la maana ya maisha ya muafrika, utapingwa na kila mtu.
Wewe ndo HAMNAZO. Huyu Mtibeli yuko sahihi 100%. Tena hiki ni kilio cha wengi ila kimyakimya. Watu wanawasitiri tu wazazi wao ila ndani kwa ndani moto unawawakia. Mabinti wananyanyasika kwenye ndoa wazazi wanaishia kuwaambia NDOA NI UVUMILIVU kisa kuna maokoto wanapata kutoka kwa mkwe. Watu wengi imekuwa ngumu kuchomoka kwenye umaskini kwasababu ya kutumia muda na pesa zao kufanya majukumu ya wazazi wao kama vilw kusomesha wadogo zao. Watoto wa kwanza wengi huwa maskini na wale wa mwisho huwa na unafuu kwa kutokuwa na majukumu mengi. PUNGUZENI UNAFIKI tujiokoe kwenye umaskini.
shida ni kwamba, hakuna anayesoma ndani ya uziSishangai Mtibel kutoeleweka!
Alichoandika taikuni wa fasihi ni akili kubwa na kinaeleweka kwa wenye akili kubwa pia.
Ukipata shida kuelewa huu uzi, unapaswa kutathimini akili yako na siyo kushambulia mwandishi. Kila kitu kipo wazi.
Wazazi wengi wa kiafrika wanazaa watoto wengi ili wakishakuwa wakubwa waje kuwafanya watumwa nao wazazi wabaki kuwa mabwana wanaotumikiwa na watoto wao(hizi ni fikra za kimaskini na ufukara wa kutupwa); toka nimeligundua hilo na hali ya dunia iliyopo sasa nimejiapiza nitazaa watoto wachache hawatazidi wawili, ili nipate nafasi ya kujiimarisha kiuchumi na wao wakiwa wakubwa waendelee na maisha yao bila mimi kuwasumbua. am done.HUNA WAJIBU WA KUMTUNZA AU KUMHUDUMIA MZAZI WAKO AKIWA CHINI YA MIAKA 60 KAMA HAUMWI.
Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.
Mada hii inaweza kuwa ngumu kwa baadhi ya Watu. Lakini nitakachojadili hapa ni Haki, kweli, akili na upendo kama ilivyo kwa Watibeli wote.
Kama ilivyo kwa mzazi hana wajibu wa kukutunza na kukuhudumia pindi ufikishapo umri wa kujitegemea yaani kuanzia miaka 21 hivi kwa sisi Watibeli. Na kwa sheria za dunia ni miaka 18. Basi ndivyo hivyohivyo kuwa mtoto hana wajibu wa kumtunza na kumhudumia mzazi au mlezi ambaye yupo chini ya miaka 60 ambaye HAUMWI(hana tatizo la kiafya).
Kuna kijitabia fulani cha kinyonyaji, dhulma, uvivu, na ukandamizaji ambao unafanywa na wazazi kwenda kwa watoto wao. Ambapo mzazi anazaa watoto idadi fulani anawapa na kuwatunza(wajibu wake) alafu wakishafikisha miaka 20 tuu wakaenda kujitafutia basi inakuwa nongwa. Mzazi hata miaka 50 haujui, miaka 60 ndio kabisa hatarajii leo wala kesho kuifikia. Mzazi ananguvu kabisa lakini kutwa kusumbua watoto na kuwatia watoto katika shinikizo isivyostahili.
Sio jukumu la mtoto kukulea na kukutunza ukiwa na umri huo. Wewe bado upo umri wa kujitegemea na kujihudumia. Kwa nini umpe mtoto mzigo? Kwa nini umdhulumu mtoto haki zake?
Kama sababu ni kuzaa na kumtunza hata yeye atazaa na kutunza watoto wake.
Kama ishu ni wajibu basi subiri muda ukifika mtoto atekeleze wajibu wake. Na kama atakutunza au kukuhudumia iwe kwa uwezo na mapenzi yake kwako na shukran na sio shinikizo.
Ni laana kubwa kumhudumia mtu isivyo halali. Kuhudumia mzazi kwa kushinikizwa yaani kunyonywa na kudhulumiwa ni laana ambayo wengi inawatafuna.
Sio ajabu unakuta Watu wengi tangu wakiwa vîjana wanateseka kuhudumia wazazi isivyostahili wakifikiria ndio baraka lakini miaka inaenda maisha yao hayabadiliki zaidi ya kuzidi kuwa maskini na fukara zaidi.
Ni sawasawa na mzazi amuone mtoto keshafikia umri wa kujitegemea alafu bado awe anamhudumia na kumtunza huo ni umaskini wa akili na roho. Lazima kizazi hiki kiwe fukara.
Ninajua ndoa nyingi zilizoharibika na familia nyingi kuanguka kisa wazazi kushinikiza huduma. Ni laana tupu. Wakati huo wazazi wananguvu kabisa.
Ninajua mabinti wengi wanaoteseka kwenye ndoa kisa wazazi wao wamewashinikiza watoto wao wabaki kwenye mateso ili wao wanufaike au walishanufaika na kumuuza binti yao.
Wengine huwashinikiza binti zao waolewe na wanaume wenyewe pesa hata kama hawapendwi na binti zao kwa kulenga kuhudumiwa na pesa za mkwilima wao.
Wapo vibinti vya kazi za ndani wanalipwa mishahara kiduntu kama elfu 30 mpaka 60 na bado wazazi wanataka gawiwo licha ya kuwa wazazi hao bado kiumri wanauwezo wa kufanya kazi na kujitafutia.
Wapo wazazi kiumri ni wadogo lakini wanawakosea watoto wao haki kwa kuwashinikiza watoto wao kwa matusi na kejeli kuwa hawafanyi kazi huko mjini kisa tuu hawatumiwi pesa. Jambo ambalo sio Haki na sio Upendo.
Wapo watoto wanajitutumua kuhakikisha wanahudumia wazazi wao kiugumuugumu, kwa kujikamua, na malalamiko ya nafsi wazazi kwa ubinafsi wao huona ni sahihi lakini sio sahihi kabisa.
Acheni watoto wakiwa na umri wa kujitafutia watafute na kujitegemea alafu wao kwa roho ya upendo wawatumie kwa hiyari yao na sio kuwadhulumu maisha na nguvu zao.
Watoto pia, acheni kudhulumu nguvu za wazazi wenu huku mkujua kuwa tayari mmefikia umri wa kujitegemea na sio kuwapa wazazi wenu mzigo, kuwanyonya na kuwakatili.
Mzazi asifurahie utu uzima wake aanze kukufikiria mtu mzima na ndevu zako kisa ati ni mtoto wake. Hiyo sio HAKI
Kumhudumia mzazi wako aliyemzee sio hiyari yako wala sio mapenzi yako kwake. Hiyo ni lazima, wajibu.
Bahati nzuri wazee hawana mahitaji mengi kama ilivyo kwa watoto.
Lakini kuhudumia mzazi aliyechini ya miaka 60 na haumwi hiyo ni hiyari na mapenzi tuu na sio lazima/wajibu. Unaweza ukafanya au usifanye na hakuna lolote litakupata.
Kumhudumia mtu anayeweza kujitegemea ni laana na kurudisha nyuma kizazi na ukoo wenu.
Lazima Watu wafanyekazi na wawajibike kwa maisha yao na ya wale wanaowahusu.
Huo ndio Utibeli. Ukweli, haki, upendo na Haki
Mimi nimemaliza, mwenye maswali anaweza kuuliza.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam