Mkuu Robert,
Suala la mtoto kumsaidia mzazi sidhani kama linahitaji sana sheria. It’s all about LOVE.
sababu kuingiza sheria kwenye upendo ni jambo gumu sana.
mtoto wa miaka 18 ni mtu mzima anaweza kujitegemea, lakini wazazi wanaendelea kulea watoto hao mpaka pale wanapoona sasa anaweza kujisimamia.
sihitaji wazee wangu wafike 60+ ili niwahudumie sababu sidhani kama ipo sheria ya kusema ni lazima uwahudumie wazazi wakiwa 60+
ILA hayo yote ni upendo wetu kwa wazazi na ile bond tuliyotengeneza.
Ukiona unaona ni mzigo kuhudumia mzazi aliyekulea nafikiri kuna shida mahali mimi huwa najisikia furaha hasa mama anapodeka akisema mwanangu nipo sehemu fulani Embu ntumie kiasi kadhaa nitatuma zaidi ya ile.
Mama namuungia banda la kuongea na mb za wiki nzima, baba yangu lazima niwe nampelekea gazeti la kusoma kila nitapoenda nyumbani, anafurahi sana na huwa napata kumbukumbu nzuri pindi alipokuwa akirudi nyumbani na gazeti mkononi.
Mzazi anatunzwa katika umri wowote ule.