Hussein Bashe amechoka Uwaziri na kuamua kumchafua Rais Samia kwa Watanzania?

Hussein Bashe amechoka Uwaziri na kuamua kumchafua Rais Samia kwa Watanzania?

Mwandishi umeegamia upande mmoja haukumskiliza Mh. Bashe alivosema hadi mwisho, alisema hivi "ataenda kuonana na wananchi wa kisesa na kuwauliza kama zile tuhuma anazozitoa mbunge wao ni tuhuma ambazo na wao wanaziamini zipo basi serikali haitapeleka kweli hizo dawa lakini kama sio maoni yao bali ni ya mbunge binafsi basi serikali itapeleka huduma kama kawaida bila kujali maneno ya mh. Mpina"
Kwa hiyo hilo ndio jibu kutokupeleka? Ni wajibu au ni hisani? Ni takwa la kisheria serikali kuhudumia wananchi au ni fadhila? Maamuzi hayo ni msimamo wa serikali? Katumwa na nani kusema hivyo? Hekima ni ipi kati ya kwenda kufanya uchunguzi na kusema hupeleki Huduma? Je serikali itaacha kukusanya kodi eneo hilo au itaendelea?
 
Sasa anakuwa anamkomoa nani? Anayeathirika na kupoteza heshima na kuaminika kwa jamii atakuwa nani kama siyo yeye mwenyewe?
Si na yule mwingine alivyonusa alienda kuropoka kule BK? Ili Wazidi kumharibia
 
Nimejiuliza hivi Mheshimiwa waziri anaweza vipi kutamka maneno ya namna hiyo hadharani? Ndio uongozi huo? Nani kampa jeuri hiyo? Nani kamuagiza kutamka maneno hayo? Nani kamfundisha kuwa ndio serikali inavyofanya mambo yake hivyo?
Leo umechambua bombaaa, Hongera kwa kuanza kuyaona mwenyewe mamboziiii.

Ana kiongozi alogemchagua nae ni Mh. Rais, hivyo kwa mimi mwananchi ni kwamba alijua atayasema hayo na amependa maana hadi sasa kuna ukimya.

Wananchi ni Wananchi.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Nimesikitika sana, kusononeka sana,kushangazwa sana,kuumia sana ,kutoamini macho na masikio yangu kwa kile nilichokiona na kusikia maneno na kauli za waziri wa kilimo Mheshimiwa Hussein Bashe. Maneno ya Mheshimiwa Waziri yakisema kuwa serikali haitapeleka huduma za Dawa,mbegu na hata wanunuzi katika jimbo la kisesa kwa makosa ya mbunge wao ambaye alisema kuwa serikali hupeleka vitu feki hadi wanunuzi wa bei ndogo.

Nimejiuliza hivi Mheshimiwa waziri anaweza vipi kutamka maneno ya namna hiyo hadharani? Ndio uongozi huo? Nani kampa jeuri hiyo? Nani kamuagiza kutamka maneno hayo? Nani kamfundisha kuwa ndio serikali inavyofanya mambo yake hivyo? Vipi siku mbunge akisimama Bungeni na kusema kuwa serikali imepeleka Dawa za binadamu feki na wahudumu wasio na sifa jimboni kwake? Je, atatoa amri kuwa jimbo hilo lisipewe hata kidonge kimoja na kuwataka wahudumu waache kutoa huduma? Je Wagonjwa wangapi watakufa kwa kukosa dawa? Wagonjwa wangapi watafia wodini na milangoni kwa kushindwa kupokelewa na kupewa huduma? Kosa litakuwa la nani?

Vipi siku mbunge akisimama bungeni akasema kuwa jimboni kwake walimu hawafundishi vizuri na wanashinda wanaendesha bodaboda na wakike wanashinda wanauza vitambaa mitaani? Je waziri atafunga shule na kuondoa walimu wote jimbo hilo? Vipi mwingine mbunge akitokea akasema polisi wa jimboni kwake wanaonea Wananchi? Je waziri atafunga vituo vyote vya polisi na kuondoa askari wote katika jimbo hilo?

Hivi hiyo itakuwa ni serikali ya aina gani? Nani ataielewa? Nani ataiunga mkono? Nani atafurahishwa na maamuzi hayo? Nani ataelewa umakini wa serikali hiyo? Hivi maamuzi kama hayo ya Mheshimiwa Hussein Bashe ndio uongozi huo? Kwanini hajakwenda kufanyia kazi na kufanya uchunguzi wa tuhuma na malalamiko ya Mbunge na kisha kuja kupinga hadharani na kuwatoa hofu wananchi wake?

Je mbunge wa kisesa alichaguliwa na wananchi wote? Vipi wale ambao hawakumchagua na hawamuungi mkono na wala hawakubaliani na kauli zake? Wao unawasaidiaje? Je huduma kwa wananchi walipa kodi ni wajibu wa serikali au hisani? Ni takwa la kisheria au ni maamuzi ya waziri na hisia zake na maelewano yake na mbunge wa jimbo husika?

Halafu inakuwaje Mheshimiwa waziri aseme kwa kiburi kabisa kuwa AMEAMUA na kama mbaya na iwe mbaya.je yeye ni Rais? Amepoka madaraka ya Rais? Anapata wapi kiburi na majivuno ya kutamka kauli hiyo ambayo haiwezi kutamkwa hata na makamu wa Rais wala waziri Mkuu wala naibu waziri Mkuu? Kwa hiyo anaposema yeye ameamua anamaanisha kuwa yeye ndio alfu na omega na mwenye kauli ya Mwisho?yeye ndio Mkuu wa Nchi? Ndio Amiri Jeshi Mkuu wetu?

Kwanini anamshusha na kumvunjia heshima Mheshimiwa Rais na kuonekana kana kwamba siyo kitu? Kwanini anamchafua na kumdharau Mheshimiwa Rais na kuonekana kama hana uwezo wala nguvu ya kumfanya chochote kile na kwamba pasipo yeye haiwezekani mambo yakaenda? Hivi Mheshimiwa amejikwaa ulimi au ameteleza? Alidhamiria kusema hivyo au ni kujisahau?

Kwanini kiongozi ngazi ya Uwaziri ujidhalilishe na kuidhalilisha serikali na mamlaka ya uteuzi kiasi hicho? Nini kipo nyuma ya pazia ya kauli ya Mheshimiwa Waziri? Kwanini waziri ushindwe kudhibiti hisia zako? Kwanini ushindwe kuchunga ulimi wako? Kwanini ushindwe kutumia Busara,hekima na kuwa mtulivu uzungumzapo? Je hiyo ni kauli ya serikali nzima?

Soma Pia: Hussein Bashe: Luhaga Mpina uwe na shukrani kwa serikali, chezea sekta nyingine sio kilimo

Halafu inakuwaje Waziri aseme kuwa atakwenda kuwauliza wananchi wa kisesa kama wanamtuma mbunge wao kuzungumza azungumzayo? Je kwanini asingekwendwa kuzungumza kwanza na wananchi kabla ya kutoa maneno na kauli yake ambayo haikubaliki bila kujali itikadi za kisiasa? Na vipi kama wangesema kuwa wanaunga mkono kauli za mbunge wao? Je waziri angewanyima huduma au angepaswa kufanya uchunguzi wa madai na malalamiko ya Wananchi?

Napingana katika mambo mengi na Luhaga Mpina. Lakini pia nilikuwa namuunga mkono waziri katika mambo mengi Tangia akiwa mbunge mpaka waziri na hata hapa nimewahi kuandika kumpongeza ,lakini katika hili sikubaliani naye hata kidogo.

Mwisho mbona wabunge wa upinzani walikuwa kwa miaka yote wanapinga kila bajeti ya serikali inayopelekwa bungeni na ya kila wizara na bado wakawa wanapelekewa miradi mbalimbali ya maendeleo majimboni kwao na kupewa pesa za mfuko wa jimbo?

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Kama hata Ndugu Hebel Lucas Mwashambwa naye ameanza kusikitika na kusononeka kuhusu wenzie huko Chamani basi ujue huko Chamani kwafukuta kweli kweli 😳 !
Naona Bundi anavinjari pande ile au ni KARMA ??!

Ngoja Tusubiri tuone !
 
Ndugu zangu Watanzania,

Nimesikitika sana, kusononeka sana,kushangazwa sana,kuumia sana ,kutoamini macho na masikio yangu kwa kile nilichokiona na kusikia maneno na kauli za waziri wa kilimo Mheshimiwa Hussein Bashe. Maneno ya Mheshimiwa Waziri yakisema kuwa serikali haitapeleka huduma za Dawa,mbegu na hata wanunuzi katika jimbo la kisesa kwa makosa ya mbunge wao ambaye alisema kuwa serikali hupeleka vitu feki hadi wanunuzi wa bei ndogo.

Nimejiuliza hivi Mheshimiwa waziri anaweza vipi kutamka maneno ya namna hiyo hadharani? Ndio uongozi huo? Nani kampa jeuri hiyo? Nani kamuagiza kutamka maneno hayo? Nani kamfundisha kuwa ndio serikali inavyofanya mambo yake hivyo? Vipi siku mbunge akisimama Bungeni na kusema kuwa serikali imepeleka Dawa za binadamu feki na wahudumu wasio na sifa jimboni kwake? Je, atatoa amri kuwa jimbo hilo lisipewe hata kidonge kimoja na kuwataka wahudumu waache kutoa huduma? Je Wagonjwa wangapi watakufa kwa kukosa dawa? Wagonjwa wangapi watafia wodini na milangoni kwa kushindwa kupokelewa na kupewa huduma? Kosa litakuwa la nani?

Vipi siku mbunge akisimama bungeni akasema kuwa jimboni kwake walimu hawafundishi vizuri na wanashinda wanaendesha bodaboda na wakike wanashinda wanauza vitambaa mitaani? Je waziri atafunga shule na kuondoa walimu wote jimbo hilo? Vipi mwingine mbunge akitokea akasema polisi wa jimboni kwake wanaonea Wananchi? Je waziri atafunga vituo vyote vya polisi na kuondoa askari wote katika jimbo hilo?

Hivi hiyo itakuwa ni serikali ya aina gani? Nani ataielewa? Nani ataiunga mkono? Nani atafurahishwa na maamuzi hayo? Nani ataelewa umakini wa serikali hiyo? Hivi maamuzi kama hayo ya Mheshimiwa Hussein Bashe ndio uongozi huo? Kwanini hajakwenda kufanyia kazi na kufanya uchunguzi wa tuhuma na malalamiko ya Mbunge na kisha kuja kupinga hadharani na kuwatoa hofu wananchi wake?

Je mbunge wa kisesa alichaguliwa na wananchi wote? Vipi wale ambao hawakumchagua na hawamuungi mkono na wala hawakubaliani na kauli zake? Wao unawasaidiaje? Je huduma kwa wananchi walipa kodi ni wajibu wa serikali au hisani? Ni takwa la kisheria au ni maamuzi ya waziri na hisia zake na maelewano yake na mbunge wa jimbo husika?

Halafu inakuwaje Mheshimiwa waziri aseme kwa kiburi kabisa kuwa AMEAMUA na kama mbaya na iwe mbaya.je yeye ni Rais? Amepoka madaraka ya Rais? Anapata wapi kiburi na majivuno ya kutamka kauli hiyo ambayo haiwezi kutamkwa hata na makamu wa Rais wala waziri Mkuu wala naibu waziri Mkuu? Kwa hiyo anaposema yeye ameamua anamaanisha kuwa yeye ndio alfu na omega na mwenye kauli ya Mwisho?yeye ndio Mkuu wa Nchi? Ndio Amiri Jeshi Mkuu wetu?

Kwanini anamshusha na kumvunjia heshima Mheshimiwa Rais na kuonekana kana kwamba siyo kitu? Kwanini anamchafua na kumdharau Mheshimiwa Rais na kuonekana kama hana uwezo wala nguvu ya kumfanya chochote kile na kwamba pasipo yeye haiwezekani mambo yakaenda? Hivi Mheshimiwa amejikwaa ulimi au ameteleza? Alidhamiria kusema hivyo au ni kujisahau?

Kwanini kiongozi ngazi ya Uwaziri ujidhalilishe na kuidhalilisha serikali na mamlaka ya uteuzi kiasi hicho? Nini kipo nyuma ya pazia ya kauli ya Mheshimiwa Waziri? Kwanini waziri ushindwe kudhibiti hisia zako? Kwanini ushindwe kuchunga ulimi wako? Kwanini ushindwe kutumia Busara,hekima na kuwa mtulivu uzungumzapo? Je hiyo ni kauli ya serikali nzima?

Soma Pia: Hussein Bashe: Luhaga Mpina uwe na shukrani kwa serikali, chezea sekta nyingine sio kilimo

Halafu inakuwaje Waziri aseme kuwa atakwenda kuwauliza wananchi wa kisesa kama wanamtuma mbunge wao kuzungumza azungumzayo? Je kwanini asingekwendwa kuzungumza kwanza na wananchi kabla ya kutoa maneno na kauli yake ambayo haikubaliki bila kujali itikadi za kisiasa? Na vipi kama wangesema kuwa wanaunga mkono kauli za mbunge wao? Je waziri angewanyima huduma au angepaswa kufanya uchunguzi wa madai na malalamiko ya Wananchi?

Napingana katika mambo mengi na Luhaga Mpina. Lakini pia nilikuwa namuunga mkono waziri katika mambo mengi Tangia akiwa mbunge mpaka waziri na hata hapa nimewahi kuandika kumpongeza ,lakini katika hili sikubaliani naye hata kidogo.

Mwisho mbona wabunge wa upinzani walikuwa kwa miaka yote wanapinga kila bajeti ya serikali inayopelekwa bungeni na ya kila wizara na bado wakawa wanapelekewa miradi mbalimbali ya maendeleo majimboni kwao na kupewa pesa za mfuko wa jimbo?

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Naunga mkono hoja, umeandika mambo mazito sana, Je Mbunge wa Ilemela Mhe. Anjelina Mabula alivyolalamika Bungeni kwamba Kituo cha Afya Sangabuye kinalaza wagonjwa kwa kuwachanganya ndani ya chumba kimoja wanaume, wanawake na watoto basi Waziri wa Afya angesema hawatapeleka huduma za afya kituoni hapo lakini badala yake aliwatuma wataalam wa Wizara wakafanya uchunguzi na kurudi Bungeni na majibu ya tuhuma za Mbunge iweje Bashe ajione yeye ndo kila kitu wakati hayo ni mamlaka ya Rais ambaye pia hawezi kutoa kauli kama hizo. Isitoshe Bashe ni Msomali tu aliyejikuta yupo Tanzania kutokana na uharamia wa wazazi na babu zake waliokuwa maharamia wa pembe za ndovu.
 
Aombe radhi na kufuta kauli yake ,maana inaleta taswira mbaya na kuichafua serikali japo naamini hajaagizwa na Baraza la mawaziri kusema aliyoyasema.
Sio atumbuliwe ili ajifunze na kuwa onyo Kwa wengine kuwa makini wanapotoa kauli zao? Hasa ikizingatiwa wakati huu wa kampeni kuelekea uchaguzi 2025.
 
Sio atumbuliwe ili ajifunze na kuwa onyo Kwa wengine kuwa makini wanapotoa kauli zao? Hasa ikizingatiwa wakati huu wa kampeni kuelekea uchaguzi 2025.
Ni sahihi kabisa akitumbuliwa au yeye mwenyewe ilipaswa awe ameandika barua ya kujiuzulu
 
Kijana mzalendo, semaji la Taifa
Sio dhambi tukampatia nafasi ya usemaji "mitandaoni" wakapatikana na wengine wanne, kuungana naye, hata wakawa wanapatiwa posho fulani sio mbaya, "Nguvu ya mitandao ni kubwa mno, na ina nguvu kweli, na inafikiwa na watu 1000, kwa sekunde chache kabisa!
#A. Makalla, ngoja nimuone Bw. Makalla ili alifikirie suala hili.
 
Sio dhambi tukampatia nafasi ya usemaji "mitandaoni" wakapatikana na wengine wanne, kuungana naye, hata wakawa wanapatiwa posho fulani sio mbaya, "Nguvu ya mitandao ni kubwa mno, na ina nguvu kweli, na inafikiwa na watu 1000, kwa sekunde chache kabisa!
#A. Makalla.

Wazo zuri. Ila Sasa ajifunze kuwa mchumi wa maneno na kuelewa vizuri hadhira yake. Watu wengi hawapendi kusoma habari ndefu sana, aandike fupi lakini nondo mwanzo mwisho.
 
Yawezekana ndio mbinu zenu.
Unakumbuks Jiwe alisema hadharani hatopeleka miradi ya maendeleo kwenye majimno yanayoongozwa na upinzani.
Au umesahau ewe chawa?
Serekali katika kutawanya maendeleo mara nyingi huwa haingalii mbunge wa kiongozi wa mkoa au ras, yenyewe huwa na DATA za maeneo yote tanzania yenye kero, na huyafanyia kazi kwa mujibu wa bajeti iliyopo, ieleweke, mapping ya mahitaji yote nchini huwa ipo FRAMED, wapi panataka nini?, serekali huwa inafahamu kila kitu kwa undani kabisa, MASUALA YA CHUKI, huchelewesha tu, utekelezaji wa mradi husika!,
SEREKALI HUTENDA KWA USAWA KWA MIKOA YOTE KULINGANA NA MAHITAJI YA MKOA HUSIKA.
 
Back
Top Bottom