Hussein Bashe, Waziri wa Kilimo: Waagizaji hawakupaswa kuleta mchele wa Msaada kutoka Marekani kwani Tanzania ina hazina ya mchele

Hussein Bashe, Waziri wa Kilimo: Waagizaji hawakupaswa kuleta mchele wa Msaada kutoka Marekani kwani Tanzania ina hazina ya mchele

Usihadaike na maneno ya huyo Msomali. Hii nimkshifa kubwa na inamhusu, uungwana ni Kujiuzulu tu tena haraka mno
Hakuna kashfa yoyote, acha fikra za kijuha.
 
Homeless wa kule mbona hawaonei huruma. Chakula bongo kingi sana. Walete hizo pesa tununue kyela wakapewe dodoma
Mnalalamika ujinga mtupu mbona tunaagiza ngano nje,sukari nje nk. Mchele bongo bei ghali ndomana huko Dodoma wali kwao ilikuwa ni anasa Sasa wanakuletea kutoka kwao maana ni msaada kwao umewazidia Sasa hapo unalialia Nini...
Waafrika wengi wanaujinga wahali ya juu mmno ukae ukijua kunawatu wanashinda na kulala njaa kwa kukosa chakula Sasa huo Mchele mwingi ukowapi?? SI bei zingeshuka na kilamtu angenunua!! Ujinga sana ninyi
 
Marekani ndio mtoa msaada mkubwa zaidi kwa DRC, kwa mwaka anaipa DRC msaada wa zaidi ya dola bilioni 1.
Sawa je vipi somalia au sudani kusini? Mbona asipeleke zambia na nchi ina janga la ukame?
 
Hata vifaru na zana za kijeshi vinapitisha nchini .

Jana nimekutana na msafara wa magari ya Uganda ukitokea bandari ya Tanga, kupitia huko Arusha na Kilimanjaro kuelekea Uganda.

Mizigo iliyokuwa imebebwa ni mungu anajua, tena escort ya police wa TANZANIA ilikuwa mbele kulinda na kusindikiza huu mzigo.
Sasa unafikiri mzigo wa kijeshi wa Uganda utaachwa upite tu kama mahindi au mchele?? Halafu badala ufurahi Uganda inatumia bandari yetu unalalamika!
 
Mh. Hussein Bashe Waziri wa kilimo ametoa kauli ya serikali kuhusu mchele ulioingizwa nchini toka Màrekàni Kwa lengo la kugawiwa mashuleni kama msaada. Mchele huo ulioongezwa virutubisho tayari uko Dodoma Kwa lengo la kusambazwa mashuleni. Baada ya picha za mchele huo kusambaa Watanzania wakaanza kuhoji sababu ya kupokea msaada wa mchele tena ulioongezwa virutubisho ambavyo hatujaelezwa vinarutubisha nini. Ghafla Jana kama ilivyo kawaida ya viongozi wa nchi hii, na yeye akajifanya kushangaa na kutoa tamko kwamba Tanzania ina akiba ya kutosha ya mchele na kama NGO husika inataka kutoa msaada ilete fedha mchele ununuliwe nchini kisha hivyo virutubisho viongezwe hapa hapa nchini.
Swali langu kwake ni kwamba, taratibu mpaka msaada huo tena wa chakula unaingia nchini kupitia mahali popote lazima mamlaka ikiwemo wizara yake zijue. Imekuwaje mpaka mchele unaingia nchini Waziri, Katibu, Wakurugenzi wizarani, mamlaka ya chakula, Bandari, uwanja wa Ndege wote hao hawakiona Hadi umefika Dodoma?
Kusiasisha (politicise) Kila kitu imekuwa kansa inayolitafuna Taifa. Mchele ulilenga kuboresha ustawi wa watu kisiasa na msingepiga kelele tungeambiwa ni Mchele wa "Mama Kimbo".
Hebu Bashe tusaidie kujua kama mchele wenye rutuba umeingia kupitia Bandari bubu?
View attachment 2936878
 
Sawa je vipi somalia au sudani kusini? Mbona asipeleke zambia na nchi ina janga la ukame?
Huna hoja, mtoa msaada anaamua pa kupeleka msaada wake, wakati na aina ya msaada. Hata matajiri unaowajua wewe nina uhakika unafahamu wanasaidia wanapojisikia kusaidia. Pia Marekani sio mtoa misaada pekee katika hii dunia.
 
kitu muzuri sana H.e Bashe. Babu yangu anaeleza alikula ugali ya njano ilikuwa hakuna Vitamini.
Labda babu yako angekosa huo ugali wa njano angekufa kabisa kwa njaa au angeshindwa hata kufanya mapenzi kuzaa na hata leo hii wewe usingekuwepo.
 
Kiburi chanini wakati watoto wetu wanaanguka njaa mashuleni huku walimu wakipepesuka kwa njaa??

Wizara ipime kama Mchele hauna shida upelekwe mashuleni, Mchele wenyewe bei ghali shule gani inaweza kununua ikalisha watoto wake???

Waziri anakaa Dar anaamini watuwote tunakula Kila tunapojiskia...huku vijijini kunawatoto hupigwa kipigo kikali kisa kudokoa wali kutokana na njaa kali waliyonayo. Tunakula mlo mmoja tuu labda siku ya bahati ndiyo tule milo miwili.

Msiweke kiburi kisa ninyi mnakula mnashiba na kuvimbiwa, chamuhimu Mchele unaenda liwa shule ambamo hawawezi nunua Mchele wetu ambao bei ni yajuu.

Nilini tutapata viongozi wazalendo wenye akili nzuri na wanaojua nchi yao na watu wake wanavyoumia hasa huku vijijini??
Hopeless leaders kabisa!!
Kwamba wizara ipime. Hivyo vipimo vimezalishwa wapi? Usimuamini mtu kizembe hivyo.
 
Mkuu umeshatembea huko vijijini ukawaona watoto wanavyoteseka na njaa na walivyodumaa. Lishe duni ni tatizo kubwa Tanzania. Kama wewe na watoto wako mnajitosheleza hapo ulipo shukuru Mungu, kuna watu huko hawajui mchana watakula nini. Cha msingi hapo Serikali ijiridhishe usalama wa hicho chakula kama Kipo Sawa mm sioni shida. Mchele na chakula kilichopo tz ni Kwa wanaojiweza Tu.
Unataka kusema huko kijijini kwenu wananjaa sana kuliko somalia sudani na palestina
 
Kwamba wizara ipime. Hivyo vipimo vimezalishwa wapi? Usimuamini mtu kizembe hivyo.
Vyakula vingapi vinatoka nje wewe hivi kwanini akili zenu huwa kunasaa zinahama? Mnakuwaje navichwa vigumu hivyo?
Hatuna taasisi inahusika na kupima vyakula na dawa?? Hao tissue hawawezi kuchunguza uhalali wa vyakula vinavyoingia nchini? Au kaziyao ni kuchunguza wapinzani tuu?
Elimu yetu inashida saaana tunawajinga wengi saana mitaani!!
 
334934260_157849730463871_4645662194721568443_n.jpg
 
Vyakula vingapi vinatoka nje wewe hivi kwanini akili zenu huwa kunasaa zinahama? Mnakuwaje navichwa vigumu hivyo?
Hatuna taasisi inahusika na kupima vyakula na dawa?? Hao tissue hawawezi kuchunguza uhalali wa vyakula vinavyoingia nchini? Au kaziyao ni kuchunguza wapinzani tuu?
Elimu yetu inashida saaana tunawajinga wengi saana mitaani!!
Kwanini usinijibu tu swali langu? Mbona maelezo mengi yenye hasira? Usifananishe vituo,jibu jambo uliloulizwa. Unaijua tiss unayoisema?
Wewe mwenye kichwa chepesi tuambie ni wapi Tanzania kuna njaa ya kitu kilicholetwa? Easy wala hatulumbani
 
Kwanini usinijibu tu swali langu? Mbona maelezo mengi yenye hasira? Usifananishe vituo,jibu jambo uliloulizwa. Unaijua tiss unayoisema?
Wewe mwenye kichwa chepesi tuambie ni wapi Tanzania kuna njaa ya kitu kilicholetwa? Easy wala hatulumbani
Tembeaa vijijini kijana, usikae mjini ukadhani kilamtu anakula na kushiba!! Kunavijiji hali ni mbaya mmno kushinda njaa nikawaida mmno watu wanakunywa ujii siku nzima!! Tembeaa nimejionea ndomana napata hasira!!
Wewe hujawahi saidia watu chakula hata siku moja?? Ndomana hujui kama Kuna wenyeshida...shameless!!
 
Hamjui hakuna USD nchini?
Pokeeni vya Bure Sasa!
Vya kununua mtatumia fedha za nchi Gani kununulia!
 
Back
Top Bottom