Huu ndo Ushahidi wa Nchi za Magharibi zinavyotusaidia. Anayewatukana na kuwasimanga muonee huruma sana!

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Kwa kifupi Nchi za Magharibi zinatusaidia kuanzia miradi ya Afya ikiwemo kupambana na magonjwa kama Ukimwi, Kifua kikuu, utapia mlo na mingine mingi. Zinatusaidia Kuokoa uhai wa Mama wajawazito na watoto kwa kutoa fedha nyingi sana tunazotumia kuboresha hospitali zetu!

Nchi hizi zinatusaidia hadi kutujengea vituo vya kupokea kupoza na kusambaza umeme. Miradi mingi inayoendelea ni fedha wanazotoa wao kama misaada!

Zinatusaidia hadi kwenye miradi ya uzalishaji chakula ili tuwe na chakula cha kutosha.

Zinatusaidia kwenye masuala ya ya nishati mbadala bila kusahau miradi ya ujenzi wa shule, maji , hospitali na maeneo mengi.

Sijawahi ona mchina akitusaidia miradi ya afya zetu na uhai wetu.

Sijawahi ona Urusi akitusaidia miradi ya afya zetu na uhai wetu.

Kusema ukweli namuonea sana huruma aliyewapiga biti hawa watu. Wakati ndo wanawasaidia wajisifu kwa wananchi kuwa wanatoa huduma bora.

Tuwaombe tu hawa wakubwa wamuonee huruma wasimchukulie hatua kali huyu aliyewatishia. Maana wakimchukulia hatua tu twafaaaaa🙌
 
Hakuna msaada wa bure, wao wanakomba mara kibao ya wanavyoleta.

Mfano mzuri Magufuli alipigwa biti asiwaguse Barrick la sivyo wanasitisha misaada.

Baada ya kuanza kushambuliana kuhusu misaada fikirieni ni vipi mtaji toa kwenye budget deficit,

Sio sifa kujisifia misaada.
 
Anzisha uzi wa namna tunaweza kujitoa huku.

Huu uzi unahusu mtu anayewatukana na kuwatisha wanaomlisha na kumfanya aonekane mtu!
 
Chawa + Wakaa kwa shemeji zao hawawezi elewa ulichoandika hapa.
 
Watakuja hapa chawa kubeza. Ila point inabali pale pale, siku nchi itakapojitegemea atleast 70% ndipo watakuwa na sauti kwa hawa jamaa until then hawana sauti yoyote
 
Anzisha uzi wa namna tunaweza kujitoa huku.

Huu uzi unahusu mtu anayewatukana na kuwatisha wanaomlisha na kumfanya aonekane mtu!
Mkuu mtu akija kwako anachuma mchicha wa 500 anauza halafu baadae anakuletea 200 jioni hakusaidii, hao wanahitaji Africa zaidi kuliko Africa inavyowahitaji wao. Mentality zenu hizo ndio za Kutojitegemea ndio zinafanya kila siku bara lipo gizani.
 
Unayohaki ya Kuomba Uraia wa US ukale bure shemeji.
Watanzania walitafuta uhuru ili wajiamulie mambo yao wenyewe sio kupangiwa nini cha kufanya na kila nchi inayoleta misaada.

Anzisha familia yako ujitegemee?
 
Si mkatae misaada yao kama mna jeuri?
 
Wewe ni kilaza kama walivyo vilaza wengine na ndio mmejaza Africa, Unategemea nini hapo ? Unajisifia umasikini kwenye nchi ya Ardhi tajiri , nyie wajinga ndio mnaturudisha Nyuma sana .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…