Huu ni mwaka wa kusafiri sana kuifaidi dunia

Huu ni mwaka wa kusafiri sana kuifaidi dunia

Mwaka 2020 unagawanyika kwa mbili. Ni mwaka mzuri. Usikubali ukaishi maisha ya dhiki na kutofurahia maisha. Unafanya kazi ili iweje kama huwezi kutenga siku kadhaa za kufurahia maisha?

Dhamiria kuufanya mwaka huu kuwa mwaka wa kujipa nafasi binafsi. Au kama uwezo unaruhusu, basi jipe nafasi na wale uwapendao muizunguke dunia japo kwa nchi chache.

Kwa mfano, kama upo Tanzania. Unashindwaje kwenda Misri hapo kushangaa shangaa uzuri wa Cairo? Dubai kuona kufuru za Waarabu? Kusini mwa Afrika kuwehuka na maporomoko ya Viktoria? Au hata kule Instabul-Uturuki kwa 'akina Sultana kufurahia miji ya kihistoria? Basi hata Kenya tu hapo ukazunguke Masai Mara kubadilisha mazingira?

Januari achana nayo, unaweza kuanza kuweka mipango ya kuanza kuzunguka Februari sababu ni msimu wa sikukuu hivyo bei ziko chini sana kuanzia tiketi za ndege hadi maeneo ya kula maisha.

Uhai ni zawadi. Ufurahie!
Mwaka 2020 au 2022?mkuu kuwa makini basi na safari zako
 
Kiukweli tatizo sio kibunda bali ni taarifa mkuu Joseverest. Watanzania wengi hawajui kuwa baadhi ya safari za kutalii nje ya nchi ni cheap zaidi kuliko hata za hapa ndani.

Mfano katika Msimu huu zipo packages za kwenda Uturuki na gharama inaanzia laki 5 tu ($230) kwa siku 4 hadi 5. Utashindwaje hapo?
we jamaa acha utani na vitu serious basi, hiyo laki 5 si nakulipa sasa hivi uniongeze kwenye list..
 
Tunaelewa huu mtazamo, wengi wako nao lakini kiuhalisia gharama za kusafiri kwa baadhi ya nchi ni nafuu sana. Ushajiuliza kwanini siku hizi warembo wengi waTanzania wanaruka sana kwenda Uturuki kwa masuala yao ya urembo? Ni nafuu.

Packages zetu tunazipandisha muda wowote kutoka sasa. Baki nasi.
Hii ni yetu sote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiukweli tatizo sio kibunda bali ni taarifa mkuu Joseverest. Watanzania wengi hawajui kuwa baadhi ya safari za kutalii nje ya nchi ni cheap zaidi kuliko hata za hapa ndani.

Mfano katika Msimu huu zipo packages za kwenda Uturuki na gharama inaanzia laki 5 tu ($230) kwa siku 4 hadi 5. Utashindwaje hapo?
gharama ya tiketi ya ndege sh ngapi?
 
Kwamba nikiweka laki tano mezani mm nafika, nalala,nakula na kurudi kwa laki tano ?

Yes, ukiweka kiasi tajwa unapokelewa Airport (bure), unapelekwa hoteli ya nyota 3 (bure), unaanza tours zote kesho yake na siku zinazofuata (bure), viingilio na watakaokuzungusha (bure), chakula cha mchana huko kwenye tours (bure).

Kwa ufupi gharama za Hoteli, Usafiri kutoka Airport na Tours zote ni BURE baada ya kulipia hicho kiasi cha package.

Gharama PEKEE zitakazokuhusu ni Tiketi ya Ndege, Vipimo vya Uviko na Visa tu!
 
Yes, ukiweka kiasi tajwa unapokelewa Airport (bure), unapelekwa hoteli ya nyota 3 (bure), unaanza tours zote kesho yake na siku zinazofuata (bure), viingilio na watakaokuzungusha (bure), chakula cha mchana huko kwenye tours (bure).

Kwa ufupi gharama za Hoteli, Usafiri kutoka Airport na Tours zote ni BURE baada ya kulipia hicho kiasi cha package.

Gharama PEKEE zitakazokuhusu ni Tiketi ya Ndege, Vipimo vya Uviko na Visa tu!
JUMLA YA GHARAMA ZOTE NI TZS NGAPI AU DOLLAR NGAPI
 
Uhai ni zawadi. Ufurahie!
Hakika, hapa umenena vyema sana sana!

IMG_20220115_160830.jpg
 
Asanteni WanaJF kwa utayari. Pia maoni na mapendekezo kuwa tuweke packages tulizonazo msimu huu, japo lengo letu lilikuwa kuambizana tu na haikuwa na ulazima msafiri kupitia huduma zetu. Ni heshima kubwa mmetupatia.

Kwa bahati nzuri, tuliandaa posters za package ambazo zina taarifa za kutosha. Tutaweka moja baada ya nyingine na kuzifafanua kwa uchache ili mtu awe na chaguo lake.

1. ISTANBUL - VALENTINE's PACKAGE

View attachment 2089317


Package hii gharama yake inaanzia Dola 230 sawa na takribani laki 5 na elfu 30 za Kitanzania.

Yaliyomo:

1. Siku nzima kutembelea majengo ya kihistoria ya utawala wa Ottoman. Utapatiwa na chakula cha mchana.
2. Siku nzima Kubarizi katika njia asili ya maji inayotenganisha bahari mbili. Njia hii ni maarufu kwa jina la Bosphorus. Utapatiwa chakula cha mchana.
3. Utalala siku 4 kwenye hoteli ya nyota 3 na kushinda siku moja. Kifungua kinywa ni bure kuanzia siku ya 2 hadi 5.
4. Ziara zote zilizotajwa hapo juu HUTOLIPIA ikiwemo viingilio katika maeneo ya utalii na mizunguko yote.

Na mengine mengi.

NB: Ofa hii imeanza Januari 15 hadi Machi 31, 2022.
Mbona Tangazo halina mawasiliano? Wala address ya kampuni, wala jina la kampuni. Hebu kuweni serious asee
 
Hebu tangaza biashara vizuri.

Weka packages zenu na huduma mnazotoa pamoja na gharama zake kwa ukamilifu na uwazi kabisa.

Weka Jina la kampuni na physical location pia anonymity ya JF usiilete kwenye biashara.

Relief Mirzska muda wa kuzurura unakaribia.

Jamaa anazidiwa hadi na wapitisha michicha ambao hupayuka bei la fungu jero, ukinunua mafungu 3 kwa buku...

Plus majira haya ya sasa kuna Covid-19, angeambatanisha na vipeperushi nchi gani ina masharti yapi japo kwa uchache, maana kuna watu hawataki kichanjwa na wapo wanaopenda safiri hawana shida kuchanjwa...
 
Yes, ukiweka kiasi tajwa unapokelewa Airport (bure), unapelekwa hoteli ya nyota 3 (bure), unaanza tours zote kesho yake na siku zinazofuata (bure), viingilio na watakaokuzungusha (bure), chakula cha mchana huko kwenye tours (bure).

Kwa ufupi gharama za Hoteli, Usafiri kutoka Airport na Tours zote ni BURE baada ya kulipia hicho kiasi cha package.

Gharama PEKEE zitakazokuhusu ni Tiketi ya Ndege, Vipimo vya Uviko na Visa tu!
Si unaona sasa umeanza kufunguka taratibu. nyie ni matepeli kwa kuwa hamuweki taarifa wazi mpaka mbanwe banwe
 
kuweni makini. binafsi sioni reality yoyote kwenye hilo tangazo.

Ni kweli mkuu. Umakini ni muhimu sana. Ndiyo maana hatutachukua pesa ya mtu yeyote mpaka atakapojiridhisha na kuthibitisha. Na hili ombwe la taarifa ndio sababu tukaja kutoa elimu. Unamaanisha nini kusema huoni reality yoyote?
 
Back
Top Bottom