Huu ni Usaliti kwa Taifa, Wahariri jitazamemi mara mbili

Wahariri wengi ni wachumia tumbo
 
Makamu mwenyekiti wa Chadema Tundu Lisu ameshauriwa kama mtu mzima aombe msamaha kwa watanzania kwani mtu mzima akivuliwa nguo huchutama na siyo kukimbia uchi.

Ni miaka sita sasa tangu Tundu Lisu aitabirie Tanzania mabaya ikiwemo kushitakiwa MIGA , ndege kukamatwa, uchumi kufilisika, kunyimwa misaada mbalimbali. Mpaka sasa hakuna hata kitu kimoja kilichotabiriwa na Lisu kilichotimia maaana yake aliwadanaganya watanzania, yani licha ya kusoma kwa kodi za watanzania yeye anakuja kufanya kazi ya kuwadanganya watanzania!!!
Kinyume na utabiri wa Lisu ,Tanzania ya sasa imeingia uchumi wa kati, hatujashitakiwa MIGA na viwanda vya kuchenjua dhahabu vimejengwa Mwanza. Mapato ya madini yamepanda kutoka billioni 100 hadi billion 500, ndege hazikamatwi na watanzania ni wamoja zaidi kinyume na utabiri wake.
Baada ya kuona aibu Tundu Lisu na Lema badala ya kuwaomba msamaha watanzania wao wamekimbilia Ulaya kwenda kulishwa bure na wazungu!!

Lema na Lisu rudini nyumbani muwaombe msamaha watanzania muanze kuishi kwa jasho lenu kwa kufanya kazi na siyo kulelewa.
 
"Msimamizi Mkuu wa Katiba na Sheria za nchi, ni Serikali. Mamlaka yote ya Serikali yapo mikononi mwa Rais. Hivyo, Msimamizi mkuu wa Utii wa Katiba na sheria ni Rais. ibara za 33 na 34 zipo wazi. Rais anawajibu kulinda sheria na katiba zisivunjwe na mhimili wa Bunge"
 
Walikuwa wanauza sura kutafuta nafasi ya kuwemo kwenye mkeka wa Ukurugenzi wa Halmashauri.
Wahariri wamethibisha kuwa wao ni aibu ya Taifa.
Shame on them.
 
Makanjanja, ndio maana magazeti yao sinunui tena, wakajaladie madaftari ya watoto wao ...
 
Wahariri wana matatizo na mahitaji yao.


CHADEMA na ninyi mna shida na matatizo yenu.

Kwanini unataka wahariri waaxhe mambo yao, wazungumze matatizo ya CHADEMA?
 
Pole sana jitahidi uwe mhariri ili siku wahariri wakiitwa uyaulize hayo maswali. Usilazimishe mawazo yafanane
 
Mwanangu una hoja hapa tena kubwa tu. Hata hivyo, siku hizi watu walio wengi wanafikiri kwa matumbo badala ya vichwa. Hata hivyo, nani angejibu maswali yako kwa ufasaha wakati akina Bashite wanaendelea kutukoga?
 
mkutano huu ulijulikana mapema utafanyika, chadema mulikuwa na jukumu moja tu la kimkakati kupenyeza watu wenu wa kuwasemea na kuuliza hayo maswali , na hii ingewaongezea credit chadema kwa namna moja
Hivi CHADEMA ni chombo cha habari? Rais aliwaalika wahariri/Waikiki wa vyombo vya habari, sasa hapo CHADEMA wangeingiaje?Forgery?
Nadhani Rais akiitisha mkutano wa vyama vya siasa halafu CDM wakashindwa kuhudhuria ama kuhoji hayo maswali au mengine,watastahili kulaumiwa na so vinginevyo.
Mshaurini Mh.SSH akutane na viongozi/vyama vya Upinzani na wajadiliane mustakabali wa Taifa letu na aache propaganda za u CCM.Tunataka Katiba ya Wananchi, Period.
 
Ndugu yangu wee, waandishi wa habari hapa Tanzania wako hoi tumboni mpk kichwani wamepungukiwa.

Yule nani nani wa TEF yule katumia muda mwingi kuomba safari za nje, ofa za matangazo ya serikali na stimulus package kwa vyombo vya habari. Unategemea mwandishi ombaomba wa aina hii anaweza kumuuliza swali gumu anayemtegemea kumfadhili???

Lkn pia kuna tatizo la asili la waandishi wa habari nchi hii. Mtu akikosa sifa za kujiunga na fani nyingine yoyote ile (akifeli kabisaaa) ndiyo anasomea uandishi wa habari. Nadhani unanielewa. Kwahiyo % kubwa ya waandishi wa habari wa nchi hii ni weupe sana vichwani.
 
CHADEMA ni mashujaa wazuri wa kudai katiba mpya ya nchi, lakini ni waoga wa kudai mabariko kwa katiba inayopa Mbowe umilele, tena ukigusia hilo wanatamani wakutafune mzima mzima.
Hawana tofauti na wafuasi wa hayati, Mbowe ni baba, hakuna kama Mbowe, Mbowe alishushwa na Mungu, utasikia mwamba tuvushe, oooh mwamba tuvushe, hawako tayari hata kuuliza ofisi makao makuu vipi haijengwi na ukigusa hilo utaporomoshewa matusi.
MWAMBA TUVUSHE.
 
Duh! Tusubiri tutaona mengi,ni suala la muda tu.
 
Nadhani tatizo moja kubwa ni mfumo wa kuuliza maswali. Unajuwa ilitakiwa swali linaulizwa na linajibiwa hapo hapo sio maswali yanaulizwa 20 halafu majibu yanakuja kama walivyofanya. Na sababu kubwa ya kusema hivi unajuwa swali likiulizwa linajibiwa hapo hapo ili kama jibu halijajitolesha kuwe na swali la kufuata unapokuwa unachukuwa note ya maswali inakuwa sasa sio maswali na majibu ila maelelezo tu. Nashauri twende katika system ya maswali na jibu kama kweli tuko serious tunataka kujibu masuala muhimu ya nchi. Ni bora kuwa na maswali machache lakini ya msingi na yakajibiwa kwa umakini. Tujifunje kwenye press confrence za wenzetu Swali-jibu-swali-jibu sio swali-swali-swali-swali then majibu inapoteza focus hasa kwa watazamaji maana hatuchukuwi note za maswali.
 
Umaskini una uhusiano mkubwa sana na jinsi watu wanavyofikiri na kuzungumza.
 
Mkuu Yericko, you have nailed it. Unapopata fursa adimu ya kuitumia, ni wakati pekee ambao unaweza kuuthibitishia umma wa Watanzania kuwa wewe ni mzalendo wa kweli kwa kujali maslahi mapana ya taifa, na wala siyo kujipendekeza!
Maslahi mapana ya taifa ni kuuliza kuhusu Tundu Lissu???

Watu waache kuuliza mambo ya msingi waulize kuhusu CDM?? Hivi nyie watu mkoje???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…