Huu ni Usaliti kwa Taifa, Wahariri jitazamemi mara mbili

Huu ni Usaliti kwa Taifa, Wahariri jitazamemi mara mbili

We kweli Huna Akili Kila Siku mnapiga kelele Rais aheshim katiba leo unataka Rais aingilie Mhimili wa Bunge kisa Mna Wivu na Wabunge wanawake..
Hujui Bunge ni Mhimili unaojtegemea?..
Kwann Rais aingilie mhimili mwengne?..
Mmelalamika sana Rais kainglia mahkama leo Rais wetu Mpendwa kaacha kila Mhimili Peke ake eti Mnataka awafukuze wabunge kwan wabunge wa Ccm wale?....

Kama hawajafata sheria Kwann msiende mahkaman haki itendeke kutupgia kelele humu kisa wivu tu Hatutaki..
Wanamuonea wivu halima mdee??
 
Hivi CHADEMA ni chombo cha habari? Rais aliwaalika wahariri/Waikiki wa vyombo vya habari, sasa hapo CHADEMA wangeingiaje?Forgery?
Nadhani Rais akiitisha mkutano wa vyama vya siasa halafu CDM wakashindwa kuhudhuria ama kuhoji hayo maswali au mengine,watastahili kulaumiwa na so vinginevyo.
Mshaurini Mh.SSH akutane na viongozi/vyama vya Upinzani na wajadiliane mustakabali wa Taifa letu na aache propaganda za u CCM.Tunataka Katiba ya Wananchi, Period.
Hivi unajua kwamba Mheshimiwa rais ana kazi nyingi na za muhimu za kufanya??
 
Kama mama angeomba kuulizwa maswali kutoka mitandaoni mfano JF naamini kabisa maswali hayo yote na mengine mengi ya msingi yangeulizwa,Ila hao waandishi wamefeli vibaya
You know what guys?
Rejea UTEUZI WA ABDULLAH MWAIPAYA wa ITV kuwa DC wa wilaya ya Mwanga. This was very calculated by Mama Samia kabla hajakutana na media!!
Mama alijua kuwa atakutana na media hivo akaingia huko kuwateua ili akikutana na Wahariri wasipige kettle kwa maans ya kuuliza MASWALI MAGUMU wasije wakakosa teuzi huko mbeleni!!!
Inanikumbusha cartoon ya GADO wa Kenya aliyeonesha Wahariri wa Media WAKIRAMBA MIGUU YA JK enzi za utawala wake!
Hicho ndicho kilichofanyika juzi kati ya Samia na Wahariri/Media!! It's really a disgrace to Tanzania.
 
Mkuu kwa kifupi tu, hawa waandishi wa hbari itakuwa walipigwa bit,na kuambia aina gana ya maswali wanayo paswa kuuliza. najaribu kuwaza kwa ukimya tuu.

Unless otherwise kama uwezo wao ndo huu basi hii tasinia ya habari imevamiwa kwa kasi sana na wasiyo na Ueledi na kazi hii
 
a tata juu ya wasiojulikana, juu ya wabunge tata, juu ya mambo mengi yasiyo na majibu. Lakini mategemeo yametegea.

Wasaliti wakubwa nyie! Hamfai Msikitini, Hamfai Kanisani.... Wala kwenye dini yangu ya Mizimu hamfai.

Au juice za Ikulu ziliwasahaulisha? Ok kivuli cha Dikteta Magufuli bado kimetanda baadhi ya maeneo.
Wewe sio yule unayempigia pambio kisu kikali? Kwanini wewe hukuenda kuuliza maswali hayo wakati ni mwandishi? Kwanini unawalaumu waandishi wenzio ambao tangu mwanzo mliingia kichwa kichwa mkaanza kucheza mdundo cha mwenye kisu kikali sifa za umalkia?

Kwanini mwenyekiti wako wa CDM hukumshauri amwandikie hayo maswali mwenye kisu kikali ayajibu kwa vitendo kuliko tazamio lako la kujibiwa kwa maneno yasiyo na tija?

Punguza kuwa na rangi nyingi zenye kubadilikabadilika.
 
Hivi unajua kwamba Mheshimiwa rais ana kazi nyingi na za muhimu za kufanya??
Acha majibu rahisi kwa maswali magumu!
Unnaposema Mh. Rais ati ana kazi nyingi za kufanya what do you really mean? Unataka kutuambia Katiba mpya, mikutano ya hadhira, kupotea kwa Azory Gwanda, Ben Saanane, shambulio la Tundu Lissu na WASIOJULIKANA na upuuzi mwingine wote ulliofanyika chini ya mtangulizi wake SIYO MUHIMU??
You're really talking nonsense!
 
Maslahi mapana ya taifa ni kuuliza kuhusu Tundu Lissu???

Watu waache kuuliza mambo ya msingi waulize kuhusu CDM?? Hivi nyie watu mkoje???
Mkuu kamwe usimsaidie mtu kufikiri kama unavyofikiri wewe binafsi ikiwa kama ndiyo njia sahihi kwako ya kuwakilisha hisia zako. Nani hapa amezungumzia kuhusu CDM ama Tundu Lissu kuwa ndivyo vitu pekee ambavyo vingetawala katika mkutano ule ili vipate kutambulika kuwa ni maslahi mapana ya taifa?
 
Hivi kweli wahariri zaidi ya 50 mliohudhuria mkutano wa Rais Samia suluhu Hassan mmeshindwa kuuliza maswali mazito yanayotesa taifa kwa miaka mitano mizima ambayo mwenye majibu ni Rais wa Nchi ya Tanzania? Mfano hata hili la kikatiba juu ya Wabunge waliopo bungeni bila kuwa na chama cha siasa mmeshindwa kuuliza?

Enyi Wahariri ni kweli hamjui ama kulikuwa na maelekezo ya kuzuia baadhi ya maswali? Hamjui kuwa Kwamjibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano, "Msimamizi Mkuu wa Katiba na Sheria za nchi, ni Serikali. Mamlaka yote ya Serikali yapo mikononi mwa Rais. Hivyo, Msimamizi mkuu wa Utii wa Katiba na sheria ni Rais. ibara za 33 na 34 zipo wazi. Rais anawajibu kulinda sheria na katiba zisivunjwe na mhimili wa Bunge"

Je kuwepo na Wabunge wasio na vyama vya siasa Bungeni wahariri hili hamkulioni ama hamkukumbuka?

Wahariri wa Tanzania mkashindwa kuuliza Watu wasuojulikana wameshughulikiwaje? Mkashindwa kuuliza aliko Azory Gwanda, Ben Saanane, na wengine? Mkashindwa kuuliza nani alimpiga risasi Tundu Lussu?

Wahariri wa Tanzania Mkashindwa kuuliza kauli na msimamo wa Rais kuhusu Watanzania walioikimbia nchi kunusuru maisha yao katika utawala wa Magufuli mfano Lissu, Ngurumo, Lema nk?

Nafasi mliyoipata jana ilikuwa ni ya dhahabu na umma uliwategemea kuondoa mtanziko wa miaka 5 iliyopita, Mmeipoteza na mmesaliti umma. Umma hautapata tena nafasi ya aina hii. Umma ulitegemea uondoe zile dhana tata juu ya wasiojulikana, juu ya wabunge tata, juu ya mambo mengi yasiyo na majibu. Lakini mategemeo yametegea.

Wasaliti wakubwa nyie! Hamfai Msikitini, Hamfai Kanisani.... Wala kwenye dini yangu ya Mizimu hamfai.

Au juice za Ikulu ziliwasahaulisha? Ok kivuli cha Dikteta Magufuli bado kimetanda baadhi ya maeneo.
Niliweka uzi humu nikionya juu ya hatari ya tabia iliyojengeka ya kuwasifia kupitiliza marais waliopo madarakani, mods nao waliuondoa haraka. Sijui ulikuwa na shida gani
 
Kama mama angeomba kuulizwa maswali kutoka mitandaoni mfano JF naamini kabisa maswali hayo yote na mengine mengi ya msingi yangeulizwa, ila hao waandishi wamefeli vibaya.
Watu wanapambania fursa nyie mnawletea mambo magumu magumu
 
Hivi CHADEMA ni chombo cha habari? Rais aliwaalika wahariri/Waikiki wa vyombo vya habari, sasa hapo CHADEMA wangeingiaje?Forgery?
Nadhani Rais akiitisha mkutano wa vyama vya siasa halafu CDM wakashindwa kuhudhuria ama kuhoji hayo maswali au mengine,watastahili kulaumiwa na so vinginevyo.
Mshaurini Mh.SSH akutane na viongozi/vyama vya Upinzani na wajadiliane mustakabali wa Taifa letu na aache propaganda za u CCM.Tunataka Katiba ya Wananchi, Period.
chadema si chombo cha habari, ila kama chama kinajukumu lakuwa na mapandikizi kila sector ili kupata infomation ambazo ni ngumu kupatikana. maana yangu ni kwamba hata kwenye vyombo vya habari wanatakiwa kuwa na ma informer wao mfano tulikuwaga na kubenea na alitumikaga vizuri sana kumchafua lowasa lakini pia najua kuna waandishi wenye mrengo wa kiharakati na niwafuasi wa chadema je chadema inawatumia ipasavyo nyakati kama hizi na katika mikutano kama hii je inakutana nao kabla nakuwapa mikakati na maswali fikirishi yatakayo ibua hoja za kumfungua rais aonekane ameegemea wapi ili wao wapate pa kuendelea kujiimarisha kimkakati zaidi. katiba ni jambo la msingi tuendelee kuidai.
 
Back
Top Bottom