Huu sio uungwana, Makomandoo wa Yanga wamshushia kichapo kikali shabiki wa Yanga

yaani sijui wanadhani kupitia kumpiga wanapunguza kelele wakati kelele ndio zinazidi
 
Huo ukomandoo kawatunuku nani, malofa wasiojielewa unapiga mtanzania mwenzako kisa mpira?

Watakuja kugusa pengine wale ngumi na visu vya fasta fasta.
 
Hakika Hapo vyurani fc wenye akili ni wawili tu.
 
Sasa Mtu anapigwa mnaishia kusema tu msimpige hata hamumsaidii? Huko wanakomkimbizia wakienda kumuumiza vibaya mtaishia kusema tu "alikuwa anatoa maoni akapigwa". Nchi bado sana hii. Sasa hii na lililokuwa linamkuta Bonge aliyekuwa anatekwa tofauti yake ni nini?.
 
Kwa matokeo ya jana mashabiki wa yanga watapata kweli nguvu za kwenda kupiga kura?
Au niachane nayo hayanihusu
 
Yanga walihujumiwa mechi ya jana,dube alipokuwa anataka kufunga kuna mtu alikuwa anapunguza mwanga wa jua,wabadilishe uwanja
Sijajua kwa huko Dar ni nani anahusika na ku control jua,kwa huku kwetu Chuga anaitwa palanjo naye ana michezo hiyo sana hivyo huenda hayo malalamiko yana mashiko.
 
Nimeshangazwa pia na hii kitu
 
Wamemuonea bure huyo kijana Hana kosa Kama walitaka kutafuta ufumbuzi wamuulize hersi kwanini amemfukuza gamondi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…