Huu umilikishwaji wa vitega uchumi muhimu vya nchi kwa waarabu, ni uwekezaji au uvunaji?

Huu umilikishwaji wa vitega uchumi muhimu vya nchi kwa waarabu, ni uwekezaji au uvunaji?

Vp kwa hivyo vingine vilivyo binafsishwa maana unabinafsisha kitu manake anaye kuja atakiimprove ktk nyanja zote za kiteknolojia. Sawa vip vingine.......

Sawa mfano waliopewa Vitalu uwindaji ww unavyo ona wata improve nini?
Hunting siyo privatisation bali ni biashara na kuna sheria na taratibu zinazofuatwa. Usifikiri kule Loliondo ambako Ortello Business Corporation amebinfasishiwa. Ni kwamba kile ni kitalu ma kinatangazwa kwenye zabuni ya wazi na hiyo kampuni inashinda. What is wrong with this one Watanzania?
 
Ni sawa unachosema
Kumbuka enzi za Magu walikamata mpaka watu wamechepusha mafuta mpka kwenye nyumba binafsi na malori yanabeba mafuta hapo

Kwa mfano wewe ni muwekezaji na umepewa sehemu lazima utaziba mianya yote ya wizi ingawa unawalipa TRA na kwenda BOT
Kweli ni yale yale ila utakuwa umeziba moja na hao wengine kwa sababu huwezi kubinafsisha basi watafute the finest wa kuzilinda hizo hela

Kila sehemu ni uozo, najua hata zinapokwendwa zinapigwa
Ina maana tutalalama hivi mpaka kiyama?
Hoja yako nimeielewa
Umeongea huko juu kwa kuonyesha ubora wa uwekezaji, mwisho chini umerudi kuwa yatakua yaleyale.

Kuna sehemu hapo unasema watatafutwa the finest hapa nchi kuzilinda hizo pesa zinazokusanywa huko TRA na huko BOT? Hapa una maana kuwa sio watanzania wote ni wezi na wazembe kama ulivyosema mwanzo? Hao the finest wanaweza kutafutwa TRA na BOT Ila kwa bandari haiwezekani?

Mwisho unasema kila sehemu ni uozo. Umeniconfuse sana sana
 
Sina takwimu halisi, nadhani wizara ya mawasiliano itakuwa nazo. Tumeondoka kutoka kwenye ule mfumo wa kizamani wa ushushaji na upakiaji wa meli moja kuchukua siku mbili au tatu.
Vizuri ingekua tunaenda na takwimu kuliko hisia, naomba mjadala ukae kitakwimu ili ulete maana nzuri
Mfano mm nikisema imeshuka? Utaniprove vipi kuwa imeshuka?
 
Uzembe, wizi, ufisadi, huko bandarini, kama ilivyo kwenye Serikali nzima na taasisi zake, hakuna anayepinga wala kukataa. Lakini tusitafute suluhisho linalotupeleka kwenye matatizo makubwa zaidi kupitia ufisadi mkubwa unaofanywa na watawala wetu kupitia mikataba.

Kama dhamira ni njema, kwa nini tusiingie kwenye JV kwa kupitia mkataba mzuri bila ya kupoteza sovereignity yetu? Kama hatuna watu wenye akili na uwezo huko Serikalini kwenye masuala ya mikataba kwa nini hata tusi-copy na ku-paste e.g.mkataba wa Uingereza na DPW? Kwa nini tunaruka majivu na kukanyaga moto?

Uchafu uliopo bandarini na taasisi nyingine za Serikali ni picha halisi ya Serikali nzima ilivyo. Je, tuwape DPW waendeshe na serikali yetu kwa sababu imejaa mafisadi, majizi, wala rushwa, wazembe na walaghai? Polisi na mahakama, kupitia reports za kila mwaka, ni taasisi zinazoongoza kwa rushwa. Je tuwape DPW wasimamie polisi na mahakama zetu?

Kushamiri kwa rushwa, wizi, uzembe na ufisadi ndani ya Serikali na taasisi zake, kama bandari, ndiyo ushahidi halisia kuwa Serikali imefeli kabisa, kwa sababu hizo taasisi zote, msimamizi mkuu ni Serikali. Na inafeli kwa sababu na yenyewe ni sehemu ya huo uchafu.
Ilibidi tugawe Mahakama tutagawa tu kwa namna Watanzania ambavyo hawa simamii haki na mwenye rushwa ndiyo anashinda kesi. Mbona MWENDOKASI mumeiuwa na INABINAFSISHWA
 
Nimetoa mfano tu kuwa unaweza kutumia mfano kama huo wa mashirika haya makubwa ambayo ni national flag carriers lakini majority shareholding iko kwa kampuni binafsi
Hapa tunakubaliana sasa kuwa serikali zinafanya biashara?
Ungesema serikali flani ya nchi zilizoendelea haifanyi biashara ndio ungekua mfano halisi

Ulikua na confidence serikali haipaswi kufanya biashara, jambo ambalo ni la uongo mkubwa sababu serikali hufanya biashara kwa nchi zote
 
Umeongea huko juu kwa kuonyesha ubora wa uwekezaji, mwisho chini umerudi kuwa yatakua yaleyale.

Kuna sehemu hapo unasema watatafutwa the finest hapa nchi kuzilinda hizo pesa zinazokusanywa huko TRA na huko BOT? Hapa una maana kuwa sio watanzania wote ni wezi na wazembe kama ulivyosema mwanzo? Hao the finest wanaweza kutafutwa TRA na BOT Ila kwa bandari haiwezekani?

Mwisho unasema kila sehemu ni uozo. Umeniconfuse sana sana
Taifa zima liko confused boss
 
Hunting siyo privatisation bali ni biashara na kuna sheria na taratibu zinazofuatwa. Usifikiri kule Loliondo ambako Ortello Business Corporation amebinfasishiwa. Ni kwamba kile ni kitalu ma kinatangazwa kwenye zabuni ya wazi na hiyo kampuni inashinda. What is wrong with this one Watanzania?
Nina swali: zabuni ilitangazwa lini ya obc?
 
Ilibidi tugawe Mahakama tutagawa tu kwa namna Watanzania ambavyo hawa simamii haki na mwenye rushwa ndiyo anashinda kesi. Mbona MWENDOKASI mumeiuwa na INABINAFSISHWA
Hapo bado umeonyesha hakuna hataaana ya huo uwekezaji sababu wasimamizi wa uwekezaji ni serikali ambayo Ina hao hao watanzania ambao ww huwatakk. Swali langu kwako huo uwekezaji utakua na maana gani ikiwa serikali inayoongozwa na hao hao watanzania ndio wasimamizi wa uwekezaji?
 
Hunting siyo privatisation bali ni biashara na kuna sheria na taratibu zinazofuatwa. Usifikiri kule Loliondo ambako Ortello Business Corporation amebinfasishiwa. Ni kwamba kile ni kitalu ma kinatangazwa kwenye zabuni ya wazi na hiyo kampuni inashinda. What is wrong with this one Watanzania?
Mimi yangu issues je tunapata nini? Tuancho kipata kinareflect maisha ya hao Watanzania wanaoishi karibu na hyo mazingira? Vp future ya vizazi vijavyo watanufaika na huo ubinafsishwaji......?

Ujue iwe ubinafsishwaji iwe sijui kuuzwa kwa kitalu, at the of the day kama nchi tukacho angaliwa tunanufaika vipi. Ndicho inacho hoji TEC kwani wametumia vifungu kujenga hoja zao na experience kwa tuliyo ya pitia na hata kuhamishwa kwa wale Wamasai Ngorongoro TEC wapinga kwa hoja bila kusahau hoja za bandari,tena wameweka na vifungu.

Hamna mtu anayepinga sijui kuuzwa vitalu, ubinafsishwaji wa mali za serikali (kwa style yoyote),ila watu wanataka kujua nchi itapata nini, hao wanaokuja watafanya nini na wasipofanya watafanywa nini.Mkapa mwenyewe kenye kitabu chake alikiri kuwa alitoa boko upande wa ubinafsishaji wa mali za uma.

Iwe kubinafsisha,kuuza,kukodisha at the of the day tutangalia nchi inafaidika vipi. Ndicho wasomi wengi na wanasheria wanahoji sana.
 
Taifa zima liko confused boss
Kweli kabisa, swali langu lilikuja pale nilipoona unasema uwekezaji huu utakua na maana kwetu. Maswali ndio yalikuja hapo, hiyo maana itatoka wapi ikiwa mamlaka za kusimamia na kukusanya mapato ya hao wawekezaji bado yatakua chini ya watanzania
Tunasema hatuna ufanisi, sisi ni wezi na wazembe hivyo tunampa mwekezaji, lakini Happ hapo taasisi kubwa za kumsimamia mwekezaji bado tunazo sisi, tunakua tumefanya nn?
 
Hivi Dangote ni dini gani? Kuna mtu amewahi kumsema vibaya kutokana na uwekezaji wake kwa vile ni muislam? Mkiishiwa hoja na akili, mnakimbilia kwenye dini.
Ndo maana huwa nasisitiza. ISRAEL DON'T SORT THEM JUST KILL THEM ALL.

MAAMAEE
 
Ni sekta nyeti lakini bado zi zinaendeshwa na watanzania ambao ww umesema hawawezi hawana ufanisi na wezi.

Au tunakubaliana kuwa huko TRA BOT hakuna wezi na wazembe?
Wazembe na wezi hata BOT hawakosekani. Lakini namna Serikali inavyotupia jicho sekta hizo kupitia TISS inatumia nguvu nyingi.

Ni bora Serikali ibakie na sekta chache strategic izisimamie kulikko kuwa kila mahali. Kwa mfano kwa nini Serikali ifanye biashara ya clearing and forwarding kupitia TASAC? Trivialities
 
Kukataaa ule ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo yalikuwa makosa makubwa mno ya kimkakati
Exactly, yule hayati wa Chato aliwafanganya Watanzania kwa husda zake tu dhidi ya JK. Akaishia kwenda kujenga Airport kwao Chato ambayo imebakia white elephant
 
Serikali ingeweza au isingeweza hilo sifahamu. Nimekujibu uliposema mashirika mengine yaliyobinafsishwa yalikufa sababu ya kutoendana na teknolojia mpya. Hapo ndio nikahliza huyo mwekezaji kama ameshindwa kuendana na teknolojia mpya tafsiri yake uwekezaji huo haukua na maana na umefeli. Maswali yakaja kwako ni mashirika mangapi yalifanikkwa kufanya vizuri na mangapi yalianguka ili tuweze kupima kama tulifanikiwa kwenye ubinafsishaji
Hata yale ambayo hayajukufanya vizuri at least yalitoka mikononi mwa Serikali na yakapunguza mzigo wa Serikali kutoa subsidy kila mwaka kwa ajili ya kuyaendesha. Mashirika kama NMC, RTC, NBC etc
 
Mbwembwe humu ndani kila mtu anazo na huo ushamba wa kujitapa kwamba ni mtu wa maana kila mtu pia anap humu tunatumia ID zenye majina ya kubuni hakuna anayemjua mwenzake hivyo kila mtu anakuja na uongo wake.

Hakuna namna yoyote ile IGA ya DPW ikaingilia uwekezaji mwingine wowote unaofanyika hapo TPA, hakuna namna IGA iliyosainiwa kwa ajili ya biashara za magati namba 3-7 ikazuia biashara nyingine ya bandari katika eneo lolote iwe ni bandari ya kule Mtwara iwe ni ile ya Bagamoyo au iwe ni ya kule Tanga.

Mnachosahau ni kuwa kipengele kimoja au viwili haviwezi kusomeka kwa ujumla eti vikiwa ndio kila kitu kwenye mkataba wa biashara,. Ukisoma mkataba usome kwa ujumla usidanganye watu kwa kuegemea kwenye kifungu kimoja au viwili.

Naona unapoteza muda kuongelea DPW nakukumbusha bandari bado haijamaliza katika suala zima la ubia na waendeshaji wengine na hakuna dhambi yoyote kuwa na waendeshaji kutoka kona yoyote ya dunia.

Pale Uwanja wa ndege kuna kampuni inaitwa DAHACO ipo kuanzia mwaka 1995 mpaka leo, kuna kitu gani cha ajabu kimetokea kwa wao kuwepo mahali pale?.

Utaendelea kuwapata wajinga wajinga tu.
Hii umempiga Bams kisawasawa. Kama atakujibu itakuwa ni kiburi cha kuwa na bando tu. Lakini umepiga msumari
 
Tujipe muda hadi 2030 tuone kama kweli hawa DP WORLD inaowaponda ni matapeli. Namba hazitadanganya na maybe tutakuwa na serikali mpya.
Sijasema DP World ni matapeli. Tatizo kubwa lipo upande wetu. Kwa nini DPW hao hao kwenye nchi nyingine kuwe na mikataba mizuri ila kweti wawe na mkataba wa hovyo?

Wakati wa utawala wa Mwinyi, tuliwapa Waarabu mbuga yetu ya wanyama. Mpaka sasa ni zaidi ya miaka 30, ile mbuga ina nini cha pekee, zaidi ya kumnufaisha huyo mwarabu na familia yake, na labda mafisadi waliomsaidia kwenye huo uporaji.
 
Back
Top Bottom