Huu unyonge wa kushindwa kuongea mnapokereka wanaume unasababishwa na nini?

Huu unyonge wa kushindwa kuongea mnapokereka wanaume unasababishwa na nini?

Mwanaume mke wako amechelewa kurudi kazini unashindwa kuongea nae na kujua kilichotokea unanuna na kwenda kulala. Masikini binti wa watu hajui hata kama umekasirika.

Huyu hapa pichani anakereka kumuona mke wake ana chart kwenye simu, anashindwa kumwambia hisia zake amebaki kujikunyata huku akichemka kwa hasira.

Matatizo mengi ya mahusiano yanasababishwa na mawasiliano mabovu. Mdomo unepewa ili uweze kuwasiliana kirahisi. Kama mwenzako ana hasira tafuta jinsi ya kufikisha ujumbe umpate na aelewe kuwa ana kukera.

Kama unashindwa kuongea nae tumia texted massage, tumia mtu unae muamini afikishe ujumbe au hata barua. Tujifunze kuwasiliana katika mahusiano.
Mara nyingi wanawake wengi wanavichwa vizito sana kupitiliza.Mara nyingine mwanaume anaamua kujikalia kimya kwa sababu ameshajua mkewe mzito kuelewa hivyo atamsha malumbano yasiyo ya msingi.mwisho ataitwa ana GuBu
 
Mara nyingi wanawake wengi wanavichwa vizito sana kupitiliza.Mara nyingine mwanaume anaamua kujikalia kimya kwa sababu ameshajua mkewe mzito kuelewa hivyo atamsha malumbano yasiyo ya msingi.mwisho ataitwa ana GuBu
Hao wanaume wa kukaa kimya wanapatikana wapi? Huyu wakwangu ataongea tu hata iwe saa kumi usiku atahitaji maelezo yaliyo kamilika.
 
Mwanaume hajaumbiwa maneno mengi kama mwanamke. Mwanamke huchukua jambo, hulitafakari na kuchukua hatua thabiti.Nadhani ndiyo sababu ya wanaume wengi kifa mapema. Maana wanaume hawapo tayari kuonyesha udhaifu au kuyumba yumba katika maumivu,Huvumilia na kuugulia moyoni.Ila atakapochukua hatua, basi ujue hiyo ni final.
 
Wanaume tumeumbwa na uwezo mkubwa wa kuvumilia mateso, maumivu na hata kunyamzia mambo yanayotukera,
Tumeumbwa na maneno machache na kuwa na upendo mwingi na huruma sana kwa wanawake.......
BRETHREN, INABIDI TUJITAFAKARI SANA....KAMA HATUNA HIZI SIFA BAC TUZITAFUTE SISI KAMA WANAUME
Mkuu tunaambiwa wadhaifu kwa upole wetu
 
Mwanaume mke wako amechelewa kurudi kazini unashindwa kuongea nae na kujua kilichotokea unanuna na kwenda kulala. Masikini binti wa watu hajui hata kama umekasirika.

Huyu hapa pichani anakereka kumuona mke wake ana chart kwenye simu, anashindwa kumwambia hisia zake amebaki kujikunyata huku akichemka
Sisi tuna namna yetu ya kuongea ambayo ni very effective kuliko mdomo.
 
Inategemea, kuna wanawake wengine, wewe una neno moja yeye elfu moja,kuna mambo mengine mtu anavunga kuepusha kelele.. na sababu nyingije kedekede.

Unaposema hivyo maana yake umejumuisha kuwa wanaume woote tuna tabia moja, kitu ambacho hakipo hivyo
 
Mkuu tunaambiwa wadhaifu kwa upole wetu
Kuwa mpole au mvumilivu au mtu mwenye upendo au mtu mwenye kusamehe sio udhaifu, hii ni ideology ambayo Lucifer(ibilisi) ametupandikizia kichwani ili tushindwe kufanana na muumba wetu

Note; the more unapofanana na MUNGU the more u become strong not weak....
Na kufanana na MUNGU sio topic ya kujifunza wiki nzima, hapana ni kuwa na upendo tuu(ila kupata huo upendo sio rahic kama tunavofikiria)

-sisi kama wanaume kiumbe cha kwanza kufinyangwa na mikono ya Muumba wetu.... tumeumbwa katika ukamilifu wa upendo, sema kwa Bahati mbaya ubinasfi uliingia moyoni mwa Adam baada ya kumuona Eva amekula tunda na kutenda dhambi, baada ya hapo mambo yakawa sio mambo tena
 
Kuna ishi ya kutojiamini,lakini pia kuna suala la kukwepa kuonekana una gubu kwa kusema kitu kimoja mara nyingi nyingi.
Mara nyingi wanaume( hususan mimi) tukianza kukaa kimya kwa vitu vile vile ambavyo mwanzo tulikua tukipigia kelele ujue tumepata "alternative" 😉
 
Mwanaume mke wako amechelewa kurudi kazini unashindwa kuongea nae na kujua kilichotokea unanuna na kwenda kulala. Masikini binti wa watu hajui hata kama umekasirika.

Huyu hapa pichani anakereka kumuona mke wake ana chart kwenye simu, anashindwa kumwambia hisia zake amebaki kujikunyata huku akichemka kwa hasira.

Matatizo mengi ya mahusiano yanasababishwa na mawasiliano mabovu. Mdomo unepewa ili uweze kuwasiliana kirahisi. Kama mwenzako ana hasira tafuta jinsi ya kufikisha ujumbe umpate na aelewe kuwa ana kukera.

Kama unashindwa kuongea nae tumia texted massage, tumia mtu unae muamini afikishe ujumbe au hata barua. Tujifunze kuwasiliana katika mahusiano.
Chart [emoji409]

Chat [emoji3581]
 
Mbona iko viseverser cc tunajua KE ndo wanapenda kukaa na dukuduku moyoni unaweza ufanye kitu ambacho hakimfrahishi badala ya kukwambia utaona anavuta midomo kama kenge kwa kununa tu na inaweza pita miaka na miaka anakaa na kinyongo moyoni ila wanaume anakuchana apoapo au nasema uongo ndugu zangu??
Kweeeeeeeeeeeeeliiiiiiiii hasa hapo uliposema mdomo kama kenge.
 
Mwanaume ni kujikausha

Mwanaume ni kuivilia ndani kwa ndani [emoji16][emoji16][emoji16]
 
Aisee huu uzi umeupenda, ingawa sijapata jibu sahihi kuwa uanaume bora ni ule wa kumchana makavu au ni ule wa kunyamanzia vitu na kuchukua hatua kimnya kimnya, asanteni kwa michango yenu leo nimejitambua kwa kiasi vile inanipasa mimi kuwa.
 
Aisee huu uzi umeupenda, ingawa sijapata jibu sahihi kuwa uanaume bora ni ule wa kumchana makavu au ni ule wa kunyamanzia vitu na kuchukua hatua kimnya kimnya, asanteni kwa michango yenu leo nimejitambua kwa kiasi vile inanipasa mimi kuwa.
 
Kuna wanawake wenye matatizo haya pia. Hasa mwanaume anapokuwa main breadwinner anatoa tu amri hamna muda wa kujadiliana.
Katika vitu sipendi ni sijui majadiliano na wife au sijui nn nn aisee bora uitwe mkoloni
 
Kuna wanawake wenye matatizo haya pia. Hasa mwanaume anapokuwa main breadwinner anatoa tu amri hamna muda wa kujadiliana.
Katika vitu sipendi ni sijui majadiliano na wife au sijui nn nn aisee bora uitwe mkoloni
 
Daaah, wale tulio moja kwa moja tunaambiwa tuna mfumo dume ujue! Wanasema hatuko romantic and caring.

Sijui nachanganya mambo hapa au vipi, ila ukivaa ovyo, nakutimua on the spot, uko kitandani una-chat mi nijikunyate? Pengine na taa inawaka, ninune? Daaah
Wanawake wana vitabia vya kupenda kujaribu jaribu ukinyamaza inakuwa tabia halali Kwa kudai mbona siku Ile nilikuwa nafanya hivi hukusema
 
Back
Top Bottom