Huu upepo wanaJF wa kurudisha watoto kayumba kutoka EM wala sio maamuzi binafsi ni basi tu ukata umekuwa mkali

Wazazi wengi wakishapiga hesabu ya kwamba anamsomesha mtoto kwa gharama alafu mwishowe anakosa ajira na status yake inakuwa sawa na aliyesoma Kayumba ndo huchukua maamuzi ya kuwapeleka watoto wao Kayumba.
Suala la kukosa ajira ni universal, hos nothing na kumsomesha mtoto international or kayumba
 
Duh wewe jamaa una akili nyingi sana mkuu. You are th true son of your father.
 
Kabisa kumsomesha mtoto EMs ukimlipia ada mamilioni halafu mwisho WA siku anakuja kufanya mitihani inayosimamiwa na NECTA, halafu elimu ya chuo kikuu anaenda kuitafuta kwenye chuo kinachosimamiwa na TCU ni sawa tu kujenga gorofa kwenye hifadhi ya barabara au kando kando ya mto mkubwa, mwisho WA siku utalipoteza tu Hilo gorofa na hatimae utakuwa sawa tu wale ambao hawana nyumba.

Huku mitaaan waliosoma EMs na waliosoma government schools a.k.a kayumba schools, tofauti Yao ni kingereza tu Cha ku-comment mitandaoni.

Mtu kama ameamua kumpa mtoto wake elimu iliyo Bora basi ampe kilicho Bora mwanzo mwisho, yaani mtoto Yuko kindergarten tayari wewe mzazi huko unamuandalia kuja kusoma Stanford university au akishindwa sana basi hata Witwatersrand hapo south Africa... Mtu akienda na huu mlolongo kielimu sio rahisi kuja kuteseka.

Sasa wewe leo hii unajinadi mtoto wako hasomi Kayumba anasoma EMs halafu mwisho WA siku anakuja kuishia Udom au Teofilo Kisanji, kisha akitoka hapo na yeye anaanza kugombania ajira za TRA na hao waliosoma Kayumba sasa ni akili hiyo???
 
100% Fact
 
Mtu anayeweza kumudu kusoma IST hawezi kubangaiza, mkuu.
Vilevile, kusoma shule hizo, kunapanua uelewa wako na kukufanya uwe mbunifu kwenye mambo makubwa.
Tazama trends za wanafunzi waliotoka shule za namna hiyo utapata jawabu.
 
Mtu anayeweza kumudu kusoma IST hawezi kubangaiza, mkuu.
Vilevile, kusoma shule hizo, kunapanua uelewa wako na kukufanya uwe mbunifu kwenye mambo makubwa.
Tazama trends za wanafunzi waliotoka shule za namna hiyo utapata jawabu.
Nabishana na maskini ukute hata hiyo IST hujui inapatikana wapi. Mmejaa na kujazana ujinga eti unapata connection.

Hivi wewe tukuweke katikati ya watoto wa kihindi na kiarabu tofauti na kijifunza kula kachori.Wewe mtoto wa MBANGAIZAJI ni connection gani utapewa na hao watu.

Gentleman kaa ukijua wenzako hao wa kihindi na kiarabu na baadhi ya watoto wa mawaziri,balozi na wafanyabiashara wale international( wakubwa akina MO,BAKRESA) achana na hawa wachuuzi.Ndo wapo huko IST ,wewe pangu pakavu ni bora ujikite kuondoa umaskini wa UKOO kuliko kuanza kuzungumzia ndoto.Maana wenye kusoma IST hata JAMII FORUM hawaijui.
 
100% Fact
 
Nitajie mtu aliyesoma IST na kaanzisha kampuni yake kubwa from the scratch au ni kiongozi serikalini.
Mo Dewji kasoma IST. Vilevile waliosoma IST wengi hawapo nchini au hawafanyi hizi kazi njaa huwezi waona.
 
Hawa wanafunzi wengine ambao hata majina yao wanashindwa kuandika ndio unasema watazame fursa Uturuki na Malaysia?
 
Wazazi wengi wakishapiga hesabu ya kwamba anamsomesha mtoto kwa gharama alafu mwishowe anakosa ajira na status yake inakuwa sawa na aliyesoma Kayumba ndo huchukua maamuzi ya kuwapeleka watoto wao Kayumba.
LIKUD
 
Ni kweli hadi vitukuu vya baresa vitafaidi labda litokee lijukuu jinga jinga litakaloua uchumi wa babu
 
Mo Dewji kasoma IST. Vilevile waliosoma IST wengi hawapo nchini au hawafanyi hizi kazi njaa huwezi waona.
Mo Dewji karithishwa yeye kaanzia alipoishia mzee wake(nilisema from the scratch). Nitajie aliyesoma IST na kafanya makubwa hao waliopo nje ya nchi wengi wao wana ndugu zao huko.
 
Watu wapo wamesoma IST na bado wanabangaiza
Kina nani wataje majina. Waliosoma international schools ndio hawa kina Benjamin Fernandez.
Mbona inawezekana waliosoma shule za kawaida kupeana connection, kuna ugumu gani waliosoma EM na IS kupeana connection. Sasa wanajuana kupitia wapi kama sio shule na vyuo, yani hawa waitane kwenye ubodaboda na kupaka kucha rangi ila wale washindwe kuitana kwenye partnership?
 
Hivi unafikiri hao decision makers wengi wao walisoma English Medium au International Schools? Angalia historia ya viongozi wengi wa serikali wengi wao wamesomea vijijini.
Zamani shiule za serikali ndio zilikuwa bora zaidi na waliofeli ndio walikimbilia private schools. Huwezi fananisha shule za kata na shule za wamisionari waliosoma kina Benjamin Mkapa kwa sababu utajidanganya tu mkuu

Kwa sasa ipo wazi, shule binafsi ni bora kuliko government. Haina mjadala, vingine ni kujifariji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…