Huwa mnapiga story gani siku ya kwanza kukutana na ndugu yako ambaye hujaongea nae zaidi ya mwaka


Tuna ndugu wa aina tofauti, kuna mwingine anakusaidia huku akitegemea umlipe fadhila kwa kumpa chance ya kukuendesha na mwingine anafanya kwa upendo Tu. Japo katika situation hizo mbili, kinachohitajika zaidi ni kujitambua na kuweka mipaka katika mahusiano yako


Whoever feeds you, owns you. Huu ni ukweli mchungu lakini uupokee, huwezi kutaka freedom kama haupo financially independent kwa hiyo, jifunze kuweka mipaka na kuwa na aibu ya kuomba pesa au misaada kirahisi. Kuwa na marafiki hata wawili watatu ili wakuondolee dependency kwa mtu mmoja mambo yanapoenda mrama ili usimpe mtu mmoja impression kuwa bila yeye, wewe huwezi..

Kingine wewe ni mdogo wake, kama ulitumia njia mbaya sio mbaya ukasuluhisha maana ugomvi wa familia hata kama ni wa kijinga hurithishwa kizazi hadi kizazi hivyo, jitahidi kujishusha myamalize bila ya kuumiza ego yake maana haikugharimu chochote haswa kwa mtu aliyekufaa kwa tough times nyingi "kuwa na shukrani maana hujui alijinyima vingapi ili akukwamue".

halafu baada ya hapo Weka mipaka yako kama mwanaume.
 
Ni kweli kujifunza kuweka mipaka ni muhimu saan Nashukuru kwa ushauri wako bora mkuu.
 
Umasikini unakusumbua

Umekosa mtu wa kumpiga vizinga, unajishobokesha ili umuingize kwenye mfumo uanze kumpiga vizinga.

Tafuta hela kijana.
 
Ushauri wangu ACHA SHOBO.

Mtoto wa kiume wewe ,kaza.
 
Hapo ndio pombe inapoingia sasa. Pombe inauwezo wa kusuluhisha hilo jambo lenu once & for all na wote mkawa na amani milele. Ukikutana na binaadamu asiyetumia mvinyo kuwa naye makini sana kwa asilimia kubwa ni lazima awe na chembechembe za unafiki
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Mualike mle gambe mtajikuta mmejenga undugu upyaa pombe huunganisha watu basi tu watu wanaizereu,
Lazima tuizereu. We kinywaji gani kinavuruga akili?. Ukizingatia kwamba utimamu wa akili ndio engine ya kuendeshea haya maisha.
 
Lazima tuizereu. We kinywaji gani kinavuruga akili?. Ukizingatia kwamba utimamu wa akili ndio engine ya kuendeshea haya maisha.
Pombe haivurugi akili bana mbona watu hawavui nguo mbon mdoctor hawakosei
 
Pombe haivurugi akili bana mbona watu hawavui nguo mbon mdoctor hawakosei
Mjomba kwa ninayoyashuhudia huku hiyo kitu ni ya kuizereu tu hamna namna. Uzuri sijawahi hata kuonja na huo mpango sina. Kijana ana miaka 29 lakini utadhani ana 50. Mambo gani haya?[emoji3]
 
Uyo
Mjomba kwa ninayoyashuhudia huku hiyo kitu ni ya kuizereu tu hamna namna. Uzuri sijawahi hata kuonja na huo mpango sina. Kijana ana miaka 29 lakini utadhani ana 50. Mambo gani haya?[emoji3]
Anakkunywa pombe kali chafu kula Kulasafar zAko 3 nnec
 
Mi ndugu zangu upande wa mama ukoo wake hatuwasiliani kila mtu hana habari na mwenzie
Tunakutanaga misiban tu sijui kwanin wakubwa hawakuanzisha upendo toka chini naonaga koo zingine wanapenda kweli wana magroup ya whatsapp huwa natamani niwaunganishe ila nasema muda ushapita kila mtu maisha yake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…