Huwa sielewi watu wanatoa wapi Uhalali wa kumfananisha Mwanamuziki Fally Ipupa na Feregola!

Sure
 
Ferre golla ni habari ingine.
 
Fere Golla nyimbo maarufu na nzuri ni hizo 2 tu (100 Kilos & Kamasutra) lakini Fally Ipupa nyimbo zote ni hatari na nusu!.


Uzuri wa fally ipupa nyimbo za taratibu na sebene ni gwiji
Fally Ipupa Rhumba zake kali ni "Associe" (Nyimbo ya taifa ya walevi wote bongo) kuna ile "Nidja" pamoja na "Chaise Electrique" ukiachana na hizo zingine sebene sebene
 
jamaa katelekeza uzi baada ya kuishiwa pumzi ngoja niweke kamasutra alafu ifate 3 em doigt na maria fally ipupa namsikiliza sana tu lakini hawezi kumfikia feregola, fally ipupa kwa mauno sawa ila sauti yake kumfikia feregola bado sana,
Wote wazuri ila Ferre Gola hatari mno
 
Eti ukmtoa Papa wemba na 'mimi'
Huyu mimi ni jina la mwanamziki wa Kongo au mimi hii ni wewe mwandishi kutoka viunga vya sitaki shari😆
 
Utakuwa na kichaa sio Bure, Fally ipupa huyu huyu ambae album yake ya Formule 7 yenye nyimbo kama MAYDAY na SE-YO inazidi kuvunja recodi huko Spotify!


FAlly ipupa tarehe 25 November 2023 amevunja rekodi ya kujaza PARIS LA DEFENSE ARENA Pale Paris. Ticket zilikuwa sold out!


There 8 December 2023 akajaza Wembley Arena


Tarehe 16 December 2023 yaani kesho anapiga show pale ING ARENA Belgium. Na Kwa taarifa yako ticket zimeshakuwa sold out! ... La huelew maana ya SOLD OUT kaangalie kwe ye dictionary yako! Halafu nakuomba fuatilia hizo arena zinachukua IDADI ya watu wangapi.


Naomba unitajie show yoyote ya ferre Gola amewahi kusold out arena yoyote ulaya. Usilete maneno yako ya kujaza arena sio kuimba muziki mzuri.


Kabla ya December Kuna show aka kopo la fally ipupa litapigwa pale Kwa Biden!

 
Kuwa superstar na kupendwa sio kigezo cha kua msanii bora kuliko wengine hata burnaboy alijaza arena lakini sio msanii bora kuliko wote naigeria, diamond ni superstar bongo lakini sio msanii bora kuliko wote Tz kuna watu wanavipaji kuliko yeye wengi tuu, fally ipupa ana funbase kubwa duniani kuliko ferre gola ila hamzidi ferre gola kwa ubora, maisha haya na bahati hua inachangia.
 
Juzi nilikua na mcongoman nikamwambia feregola anajua kuliko fally Ipupa, akanambia simjui Fally Ipupa, nikiwa congo nikatamka feregola anamzidi Fally Ipupa wanaweza nipiga wakaua😃
 
Achana na wimbo huo mmoja tu wa mazingaombwe mkuu,sasa ukisema 100 kilos na Ambao tunaujua ASSOCIE tusemeje!

Hivi unaujua ALLIANCE,MAYDAY au MARIA?
Malizia kabisa Maria Pm....Fally ni hataree sana ila mzee wangu nikiwaga mahali nishakula serengeti Lite zangu likapigwa Lumba la 100kg..walah nasahau shida zangu zoote.
 
Nitakuja kuanzisha mpambano wa songs tu siyo maneno kati ya wawili hawa kila mtu atasikia utofauti na kipenda roho
 
Yaani wewe unaleta mambo ya Redio one ya Nani zaidi kati ya Madonna na Hadija kopa , Hadija Kopa alishinda kwa kishindo , kwa sababu wapiga kura walitoka Mbagala
Hii kiboko na aliyeandaa huo mpambano alikua analipwa mshahara Kwa Kodi za watanzania masikini.... Hahhaha so sad
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…