Huwa unamuamini asilimia ngapi mwenyeji wako anapokwambia usiogope, Mbwa wake hang'ati?

Huwa unamuamini asilimia ngapi mwenyeji wako anapokwambia usiogope, Mbwa wake hang'ati?

mbwa ambaye haumi wenyeji ulio nao hawezi kukuuma wewe,kosa la kwanza ni kuanza wenge kama unachomoka mabawa mgongoni na kukimbia hovyo ukitengana na wenyeji wako,atakuuma.

saikolojia ya mbwa hubadilika anapoona mgeni,lakini mgeni salama ni yule aliye na mwenyeji wake au aliye mtulivu hata baada ya yeye kubweka.

kuna mpuuzi nilienda naye nilipopanga kulikuwa na geti na mbwa,nikamtahadhalisha mbwa haumi,awe mtulivu heee,kufungua tu geti mbwa akamsogelea jamaa akaanza kutuka ruka kama kuku kavaa mvuko mguuni😂😂,mpaka ananirukia mimi,yaani nilimind sijui alikuwa na majini mjinga yule.
 
Hapana kwakweli ni asilimia 0.000% maana mimi Mbwa au Ng'ombe bora nikutane na simba au chatu.
 
Mimi ile wanakuja kwangu tu, ningeludi ndani ya gari mbio hahahaha
Mbwa akishakuwa karibu yako hautakiwi kukimbia, maana kitendo cha kugeuka ili ukimbie mwenzako atakichukulia kama vile unapanga shambulizi dhidi yake, so atakuwahi na atakuchana chana vibaya sana.

Unapomuona ashakufikia karibu, unachotakiwa kufanya ni kuuvaa ujasiri kwa kujifanya umemzoea, unampenda na uko tayari kucheza nae. Kwa kuwa mbwa wamepewa fahamu, basi ataweza kufahamu kuwa wewe sio adui yake bali ni rafiki yake, na hapo ule mpango wake wa kukuvamia ili akudhuru utakuwa umekufa kibudu.
 
Wewe ni jasiri sana kwa hapo mimi ningeliwa tu mana ningetoka mbio na hili ni kosa. Mbwa sinaga urafiki nao kabisa wakati mtoto waliwahi kuniumiza hadi leo hii hawa viumbe hatuna ukaribu kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
🤣🤣🤣 Mkuu pamoja na kwamba niliogopa ujio wao, lkn niliona sina njia nyingine ya kufanya ili nijinusuru ikabidi nijifanye tunafahamiana. Na wao kwa bahati nzuri wakanielewa.
 
Kuna jiran yetu kipind tupo watoto alikuwa anafuga mbwa mbuzi na mifug mingi tuka agizwa kufwata mbolea kwa jirani yetu tulipofika tukagonga akasema piteni mimi na kihelehele kuingia ndani mbwa alikotokea sijui mpka leo akawa nakuja kwa kasi nikawa napiga kelel yeye mwenye mbwa anaangalia tu alipo ona anakalibia kabisa ndio akamuita jina lake akaondoka tulipo ludi nyumban nikawahadithia wakatukataza kwenda tena mpka leo siamin mtu kwenye hiyo kauli
 
Katika viumbe ambao huwa siwaogopi ni mbwa na nyuki nimecheza nao muda mrefu najua tabia zao sana nyuki akikutana na mimi huwa anageuka kipepeo na mbwa anageuka mbuzi
Mkuu nipe tip hyo ya nyuki
 
Ntamuamini nikiwa nna Zana mkononi... Mbwembwe kdg R.I.P
+255 679 645 515 20200704_153946.jpg
 
mbwa ambaye haumi wenyeji ulio nao hawezi kukuuma wewe,kosa la kwanza ni kuanza wenge kama unachomoka mabawa mgongoni na kukimbia hovyo ukitengana na wenyeji wako,atakuuma.

saikolojia ya mbwa hubadilika anapoona mgeni,lakini mgeni salama ni yule aliye na mwenyeji wake au aliye mtulivu hata baada ya yeye kubweka.

kuna mpuuzi nilienda naye nilipopanga kulikuwa na geti na mbwa,nikamtahadhalisha mbwa haumi,awe mtulivu heee,kufungua tu geti mbwa akamsogelea jamaa akaanza kutuka ruka kama kuku kavaa mvuko mguuni😂😂,mpaka ananirukia mimi,yaani nilimind sijui alikuwa na majini mjinga yule.
Hahaaaaa
 
Aisee! Hakuna mnyama rafiki kama mbwa,mnyama yeyote ukurarua tu pale anaposikia harufu ya uoga wa MTU....kutikisika kwingiii...lakini ukijiamini nae anaogopa hawezi kukugusa.

Na kuhusu kuamini kauli ya mwenyeji ni kwamba kama aliongopa tu ili kuniaminisha bas nikiguswa ajiandae kuzika mbwa wake.
 
Aisee! Hakuna mnyama rafiki kama mbwa,mnyama yeyote ukurarua tu pale anaposikia harufu ya uoga wa MTU....kutikisika kwingiii...lakini ukijiamini nae anaogopa hawezi kukugusa.

Na kuhusu kuamini kauli ya mwenyeji ni kwamba kama aliongopa tu ili kuniaminisha bas nikiguswa ajiandae kuzika mbwa wake.
Mkwara huo
 
Wenyeji wengine ukizongwa na mbwa wao wanacheka tu[emoji1787],

Mie mbwa akitaka kunizongo nakuwa mkali zaidi yake,tena kama kuna mawe nampiga,

Home nachekaga tu usiku watu wanavyokimbia kuogopa mbwa,wangejua mijibwa yenyewe inabweka tu wala haing'ati[emoji16]
 
Kuna nyumba moja niliwashangaa sana, niliingia nimefika uwani mbwa akakurupuka huko akanifata huku anabweka, nikaamua kutumia ujanja wangu, nikainama chini kama naokota jiwe mbwa anashituka kidogo ila tena asogea, wao wananiangalia tu, mbwa nae alikuwa jasiri sana nikimtishia kama namponda anatulia kidogo afu anasogea, eti baadae ndio wanakuja kumshika wakati huo nimeshachoka balaa nawaza sijui akinifikia kabisa itakuwaje
[emoji1][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]kiumbe ambae huwa ctakiii hata anisogeleee
 
Kuna jamaa nilienda kumtengenezea gari kwake. Kufika kwake nikakuta anafuga mbwa wawili, yan pit bull wakubwa walioshiba.

Akanambia wewe fanyakazi tu wala usiogope. Kwa vile ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika kwake, nikajifanya sina uoga na viumbe wale.

Nikiwa katika harakati zangu za kazi mara jamaa akanifuata na kuniambia kuwa anatoka mara 1 kwenda kumfuata mtoto shuleni (sio mbali sana na anapoishi) akasema wewe usiwe na wasi wasi hao hawawezi kukufanya chochote.

Dah kukataa nikashindwa na kukubali pia nikashindwa nikabaki kumeza fundo la mate huku nikijifanya sina wasi wasi na viumbe wale. Jamaa akaniachia funguo 1 ya gate la nje akafungua gate akatoka na kutuacha sisi watatu, yani mimi na ile mi pit bull miwili, basi ikawa inaniangalia huku inanikazia macho kama vile inataka nijichanganye kidogo tu inichane chane, maana tayari ulimi uko nje, huku mijino kama vidole vya mtu mzima.

Kitu cha kwanza nikatoka chini ya gari na kuingia ndani ya gari. Sasa wakati nikiwa ndani ya gari nikasikia honi ya gari inaita kwa nje ya nyumba, nikajiuliza huyo ni mshikaji amerudi anataka nikamsaidie vitu au ni mtu mungine anapiga honi nyumba ya pili, honi ikaendelea wale mbwa wakakurupuka na kukimbilia mlangoni wakawa wanabweka ile mbaya.

Hapo nikajua anaepiga honi yuko mlangoni na pia inaonesha sio mwenyeji wa nyumba ile maana ingekuwa ni mwenyeji wasingebweka vile, kidogo simu inaita jamaa ananambia nichukue funguo alioniachia nikamfungulie mgeni wake.

Hapo ndio palikuwa patamu maana jamaa nilikuwa nishamuonesha kuwa wale mbwa siwaogopi, sasa naanzaje tena kumwambia kuwa naogopa kwenda kufungua? Ikabidi nimwambie kuwa niko msalan nakata gogo, akasema poa fanya fasta basi ukamfungulie.

Jamaa akampigia akamwambia mgeni asubiri nikimaliza kukata gogo nitamfungulia. Baadae akanipigia tena bado tu, nikabidi nimwambia ndo najisafisha natoka sasa hivi.

Nikasema potelea mbali wakinivamia atanilipa, nikaanza kulifuata gate la nje kwa kunyata kumbe washanisikia ghafla nikaona hao wanakuja mbio upande wangu, nikaona nikikimbia watanivamia, ikabidi nioneshe ukakamavu ghafla hawa miguuni, sasa nilichofanya nikamshika yule dume kichwani kama nampalaza palaza likatulia huku likionesha kuelewa ninachokifanya nikawa natembea mdogo mdogo kuelekea getini huku wakinifuata kama vile ni mtu wanaenifahamu, ile kufika getini nafungua na mwenyeji namuona yule kwa mbali anakuja. Basi wakaingia wote mwenyeji, mtoto na mgeni tukafunga geti. Aisee siku ile sintoisahau.
Ungekimbia tu ungeisoma namba [emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom