Huwa unamuamini asilimia ngapi mwenyeji wako anapokwambia usiogope, Mbwa wake hang'ati?

Huwa unamuamini asilimia ngapi mwenyeji wako anapokwambia usiogope, Mbwa wake hang'ati?

Kuna mshkaji wangu nilikua naendaga kwao na wana mbwa ila wanasema ni coco yani mchana hana madhara mpaka usiku na pale kwa mshkaji naendaga mara nyingi tu na mbwa huwa ananiona ila hanaga ile kumfuata mtu miguuni kama wanavyofanya mbwa wengine wakiona tu mgeni kaingia haoo wanamkimbilia


Huyu hakua na hizo mambo yani wewe ukiingia utamkuta kalala zake hana time na wageni,sasa siku moja usiku nilienda tena kwa mshkaji wangu tukawa tunacheki movie ndani baadae muda wa kuondoka tumetoka nje mbwa yupo kibarazani na pale nje kulikua na mabox mawili jamaa akaniambia nimsaidie kuingiza ndani yeye akabeba box moja akaingia ndani sasa ile nataka kubeba box mara simu yangu ikaita hapo mbwa ananichora tu,nilivomaliza kuongea na simu ndo nikabeba box niingize ndani yani ile nakaribia mlango tu naskia mbwa ananikimbilia anabweka akapeleka mdomo wake karibu na mguu dah nilikimbilia ndani mwili unasisimka yan ilibaki kidogo tu achomoe mnofu
 
Asilimia 100 Kwa maana hata mbwa awe wa wapi mimi hawezi ningata mbwa ni kiumbe rahisi sana kumtawala ukishaijua saikolojia ambayo ni simple tu kuonyesha humuogopi na kutulia hata akikutishia
 
Wenyeji wengine ukizongwa na mbwa wao wanacheka tu[emoji1787],

Mie mbwa akitaka kunizongo nakuwa mkali zaidi yake,tena kama kuna mawe nampiga,

Home nachekaga tu usiku watu wanavyokimbia kuogopa mbwa,wangejua mijibwa yenyewe inabweka tu wala haing'ati[emoji16]
Hahah
 
Kuna mshkaji wangu nilikua naendaga kwao na wana mbwa ila wanasema ni coco yani mchana hana madhara mpaka usiku na pale kwa mshkaji naendaga mara nyingi tu na mbwa huwa ananiona ila hanaga ile kumfuata mtu miguuni kama wanavyofanya mbwa wengine wakiona tu mgeni kaingia haoo wanamkimbilia


Huyu hakua na hizo mambo yani wewe ukiingia utamkuta kalala zake hana time na wageni,sasa siku moja usiku nilienda tena kwa mshkaji wangu tukawa tunacheki movie ndani baadae muda wa kuondoka tumetoka nje mbwa yupo kibarazani na pale nje kulikua na mabox mawili jamaa akaniambia nimsaidie kuingiza ndani yeye akabeba box moja akaingia ndani sasa ile nataka kubeba box mara simu yangu ikaita hapo mbwa ananichora tu,nilivomaliza kuongea na simu ndo nikabeba box niingize ndani yani ile nakaribia mlango tu naskia mbwa ananikimbilia anabweka akapeleka mdomo wake karibu na mguu dah nilikimbilia ndani mwili unasisimka yan ilibaki kidogo tu achomoe mnofu
Na waking'ata na sumu ndo baas
 
Ukiambiwa hivyo usiamini kwa asilimia 100 nakumbuka niliambiwa hivyo na mwenyeji wangu baadae wakati naongea na simu nikashangaa yule dogi kanipiga jino kalioni tena kwa kuvizia ni dog anayeng'ata kimyakimya mwanzoni nilikuwa nashangaa huyu dog mbona anazungukazunguka nyuma yangu kumbe anatataka kuning'ata kalio hii leo hata nikienda kwa jamaa yule dog simpi nafasi ya kukaa nyuma yangu
 
Kuna nyumba moja niliwashangaa sana, niliingia nimefika uwani mbwa akakurupuka huko akanifata huku anabweka, nikaamua kutumia ujanja wangu, nikainama chini kama naokota jiwe mbwa anashituka kidogo ila tena asogea, wao wananiangalia tu, mbwa nae alikuwa jasiri sana nikimtishia kama namponda anatulia kidogo afu anasogea, eti baadae ndio wanakuja kumshika wakati huo nimeshachoka balaa nawaza sijui akinifikia kabisa itakuwaje
Mradi utesek tu [emoji1787][emoji1787]
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kuna jamaa nilienda kumtengenezea gari kwake. Kufika kwake nikakuta anafuga mbwa wawili, yan pit bull wakubwa walioshiba.

Akanambia wewe fanyakazi tu wala usiogope. Kwa vile ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika kwake, nikajifanya sina uoga na viumbe wale.

Nikiwa katika harakati zangu za kazi mara jamaa akanifuata na kuniambia kuwa anatoka mara 1 kwenda kumfuata mtoto shuleni (sio mbali sana na anapoishi) akasema wewe usiwe na wasi wasi hao hawawezi kukufanya chochote.

Dah kukataa nikashindwa na kukubali pia nikashindwa nikabaki kumeza fundo la mate huku nikijifanya sina wasi wasi na viumbe wale. Jamaa akaniachia funguo 1 ya gate la nje akafungua gate akatoka na kutuacha sisi watatu, yani mimi na ile mi pit bull miwili, basi ikawa inaniangalia huku inanikazia macho kama vile inataka nijichanganye kidogo tu inichane chane, maana tayari ulimi uko nje, huku mijino kama vidole vya mtu mzima.

Kitu cha kwanza nikatoka chini ya gari na kuingia ndani ya gari. Sasa wakati nikiwa ndani ya gari nikasikia honi ya gari inaita kwa nje ya nyumba, nikajiuliza huyo ni mshikaji amerudi anataka nikamsaidie vitu au ni mtu mungine anapiga honi nyumba ya pili, honi ikaendelea wale mbwa wakakurupuka na kukimbilia mlangoni wakawa wanabweka ile mbaya.

Hapo nikajua anaepiga honi yuko mlangoni na pia inaonesha sio mwenyeji wa nyumba ile maana ingekuwa ni mwenyeji wasingebweka vile, kidogo simu inaita jamaa ananambia nichukue funguo alioniachia nikamfungulie mgeni wake.

Hapo ndio palikuwa patamu maana jamaa nilikuwa nishamuonesha kuwa wale mbwa siwaogopi, sasa naanzaje tena kumwambia kuwa naogopa kwenda kufungua? Ikabidi nimwambie kuwa niko msalan nakata gogo, akasema poa fanya fasta basi ukamfungulie.

Jamaa akampigia akamwambia mgeni asubiri nikimaliza kukata gogo nitamfungulia. Baadae akanipigia tena bado tu, nikabidi nimwambia ndo najisafisha natoka sasa hivi.

Nikasema potelea mbali wakinivamia atanilipa, nikaanza kulifuata gate la nje kwa kunyata kumbe washanisikia ghafla nikaona hao wanakuja mbio upande wangu, nikaona nikikimbia watanivamia, ikabidi nioneshe ukakamavu ghafla hawa miguuni, sasa nilichofanya nikamshika yule dume kichwani kama nampalaza palaza likatulia huku likionesha kuelewa ninachokifanya nikawa natembea mdogo mdogo kuelekea getini huku wakinifuata kama vile ni mtu wanaenifahamu, ile kufika getini nafungua na mwenyeji namuona yule kwa mbali anakuja. Basi wakaingia wote mwenyeji, mtoto na mgeni tukafunga geti. Aisee siku ile sintoisahau.
 
Husimuangalie mbwa macho Kwa macho na dhibiti uoga mwili wako hisije kutema Adrenaline , atasikia harufu
 
Ungekimbia tu ungeisoma namba [emoji23][emoji23]
Aisee sio tu ningeisoma namba bali pengine leo hii ningekuwa naitwa marehem fulani, au wangeniachia ulemavu wa kudumu, maana hakuna mbwa mkali, hatari na mwenye nguvu kama pit bull. Huyo german shepherd mwenyewe akikutana na pit bull ujue siku hiyo hata wenye mbwa wao wenyewe watashindwa kuwaamua.

Na isitoshe walikuwa wakubwa last namba afu wameshiba haswa, wakitembea unasikia chini ti ti ti ti.
 

Attachments

  • images (64).jpeg
    images (64).jpeg
    21.5 KB · Views: 5
Mbwa hafai, kuna nyumba moja iko jirani na tunakoishi kuna Mzungu alikuwa anaishi hapo na anafuga mbwa wakubwa tu. Na yana sauti kubwa yakibweka, na yeye huwa anatoa kauli hiyo hiyo. Sasa kuna siku nilikatiza hapo kwake mchana, na nilikua nimejisahau kama kuna mbwa wakali, sijui nilikua nawaza nini!! Ghafla mbwa wanaunguruma pembeni yangu, kugeuka kuangalia, naona mbwa wawili wako spidi wananifuata. Sikujiuliza mara mbili, nilifyatua mbio huku napiga mayowe. Na ndala niliziacha palepale getini kwake!! Ila nilishangaa kuona watu wananicheka, halafu wala hawana mpango na mimi. Baadaye nikasimama baada ya kuona kimya, kuja kufuatilia, kumbe wako ndani ya fence, zile za waya, kwa nje kumepandwa michongoma. Kwahiyo ukicheki kwa haraka, utaona michongoma tupu. Nikazirudia ndala zangu, nikasepa.
 
Mbwa ukimjua jina hakupi shida.
Sisi kwetu ilikuwa lazima utambulishwe kwa mbwa, la siivyo hukai kwa raha.
Kwaiyo kama ni mgeni unaenda bandani kwa nje, anaitwa Max huyu ni mgeni atakuwa pamoja nasi siku zote la siovyo mgeni unacho. Sema mama alimuuzaga maana ilikuwa kero kwa wenyeji hawaji home kwa raha na mtaa mzima wanamuita mama Bibi Max, na mm dada Max.

Nyingine nilikuwa Njombe olevel sasa likizo naenda kwa Uncle, na pale kwao kuna mbwa. Sasa shida mchana hakuna wenyeji mbwa anakuwa tu around home mpaka wenyewe warudi ndy wanamfunga, kwaiyo kwao mchana hamna hata mwenyeji anaenda kuwasalimia mpaka jioni hiyooo.
Me nilikuwa nikienda nasimama barabarani naitaaa Kunjiiiiiiiiiii basi anakuja nacheza naye lakini kwa taadhari, then naingia ndani. Wenyeji wakija utasikia jaman Kunji hajakung'ata me naona jau tu watu gani niliwapa taarifa kwamba nitaenda kesho na bado wanamuacha Kunji nje.
 
Ukiambiwa hivyo usiamini kwa asilimia 100 nakumbuka niliambiwa hivyo na mwenyeji wangu baadae wakati naongea na simu nikashangaa yule dogi kanipiga jino kalioni tena kwa kuvizia ni dog anayeng'ata kimyakimya mwanzoni nilikuwa nashangaa huyu dog mbona anazungukazunguka nyuma yangu kumbe anatataka kuning'ata kalio hii leo hata nikienda kwa jamaa yule dog simpi nafasi ya kukaa nyuma yangu
Kalio alizani linadondoka nahisi
 
Back
Top Bottom