Dodoma leo
JF-Expert Member
- Jan 7, 2021
- 1,336
- 1,658
Mbwa hawaaminiki kama hawakujui, wale mbwa wa Kingunge wangemuua kabisa. Imagine mtu anaewalisha na wamemgeuka, itakuwa wewe wasiokujua?Hawaaminiki mbwa! Mzee Kingunge aling'atwa na mbwa wake kabisa.
KifuaniMwanamke atashka nni mkuu
Alijua ni mwizi[emoji23]Kuna mshkaji wangu nilikua naendaga kwao na wana mbwa ila wanasema ni coco yani mchana hana madhara mpaka usiku na pale kwa mshkaji naendaga mara nyingi tu na mbwa huwa ananiona ila hanaga ile kumfuata mtu miguuni kama wanavyofanya mbwa wengine wakiona tu mgeni kaingia haoo wanamkimbilia
Huyu hakua na hizo mambo yani wewe ukiingia utamkuta kalala zake hana time na wageni,sasa siku moja usiku nilienda tena kwa mshkaji wangu tukawa tunacheki movie ndani baadae muda wa kuondoka tumetoka nje mbwa yupo kibarazani na pale nje kulikua na mabox mawili jamaa akaniambia nimsaidie kuingiza ndani yeye akabeba box moja akaingia ndani sasa ile nataka kubeba box mara simu yangu ikaita hapo mbwa ananichora tu,nilivomaliza kuongea na simu ndo nikabeba box niingize ndani yani ile nakaribia mlango tu naskia mbwa ananikimbilia anabweka akapeleka mdomo wake karibu na mguu dah nilikimbilia ndani mwili unasisimka yan ilibaki kidogo tu achomoe mnofu
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Mbwa hafai, kuna nyumba moja iko jirani na tunakoishi kuna Mzungu alikuwa anaishi hapo na anafuga mbwa wakubwa tu. Na yana sauti kubwa yakibweka, na yeye huwa anatoa kauli hiyo hiyo. Sasa kuna siku nilikatiza hapo kwake mchana, na nilikua nimejisahau kama kuna mbwa wakali, sijui nilikua nawaza nini!! Ghafla mbwa wanaunguruma pembeni yangu, kugeuka kuangalia, naona mbwa wawili wako spidi wananifuata. Sikujiuliza mara mbili, nilifyatua mbio huku napiga mayowe. Na ndala niliziacha palepale getini kwake!! Ila nilishangaa kuona watu wananicheka, halafu wala hawana mpango na mimi. Baadaye nikasimama baada ya kuona kimya, kuja kufuatilia, kumbe wako ndani ya fence, zile za waya, kwa nje kumepandwa michongoma. Kwahiyo ukicheki kwa haraka, utaona michongoma tupu. Nikazirudia ndala zangu, nikasepa.
Sijui ni nini kilimfanya atake kunijeruhi maana kabla ya kufanya hivo pale nimeenda zaidi ya mara kumi na alikua ananiona vizuri tu[emoji28][emoji28]Alijua ni mwizi[emoji23]
Hiyo ni mbinu moja wapo ya kukufanya uingie ndani kwa lazimaKatika ujinga ambao sipendagi kuusikia ni huo. Huwa namuona Mwenye nyumba ni kama tapeli hivi.
Kama unanitarajia nakuja kwako basi cha muhimu fungia Mbwa wako kwenye Banda lao.
Haha hapa mbwa alikuwa anacheza na mzee tu ila ndo hivyo mzee hofu imemjaaπ
Tuseme tu mbwa hanaga urafiki,mbwa wako anaweza kukung'ataSijui ni nini kilimfanya atake kunijeruhi maana kabla ya kufanya hivo pale nimeenda zaidi ya mara kumi na alikua ananiona vizuri tu[emoji28][emoji28]
HehehHiyo ni mbinu moja wapo ya kukufanya uingie ndani kwa lazima
Mimi mwenyewe nina mpango wa kufunga mbwa sio kwa ajir ya ulinz ila kwa ajil ya wageni wa kike tu ambao sina udugu nao
Hahaha [emoji23][emoji23]Mimi hata mbuzi kama simjui simwamini sembuse mbwa.Kuna beberu alitakaga kunivunja goti.
Watu waoga sanaHahaha [emoji23][emoji23]
Asilimia 0.00Karibu sana mgeni! Usiogope Mbwa wangu hawang'ati!
Hii kauli huwa unaiamini asilimia ngapi ? Kuwa tu mkweli kabla sijakwambia jambo!
View attachment 2453454
πππMimi huwa namuamini asilimia 2%...
Alikuwa mbwa kokoKwa uzoefu wangu mbwa hata aweje huchukua siku chache kuzoea harufu mpya
Niliwahi kupanga nyuma moja ina mbwa mkali asee, tena nilikua nasotea kazi sehemu flani miaka hiyo.
Yule mbwa mchana huwezi kumuona mpaka saa tano usiku ndo anafunguliwa
Mara ya kwanza nilitoka nje usiku akaja na kasi ya ajabu ila hakufanya kitu, kesho tena nikajaribu kutoka nje mpaka akanizoea nikawa namfungulia mwenyewe na kumfungia bandani
Mkuu usije rudia tena kushika mbwa kichwani kama hauna urafiki nae, kuna baadhi ya mbwa atakufanya vibaya sana, mie shahidi, kuna wengine ukimshika masikioni umetangaza vita.Kuna jamaa nilienda kumtengenezea gari kwake. Kufika kwake nikakuta anafuga mbwa wawili, yan pit bull wakubwa walioshiba.
Akanambia wewe fanyakazi tu wala usiogope. Kwa vile ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika kwake, nikajifanya sina uoga na viumbe wale.
Nikiwa katika harakati zangu za kazi mara jamaa akanifuata na kuniambia kuwa anatoka mara 1 kwenda kumfuata mtoto shuleni (sio mbali sana na anapoishi) akasema wewe usiwe na wasi wasi hao hawawezi kukufanya chochote.
Dah kukataa nikashindwa na kukubali pia nikashindwa nikabaki kumeza fundo la mate huku nikijifanya sina wasi wasi na viumbe wale. Jamaa akaniachia funguo 1 ya gate la nje akafungua gate akatoka na kutuacha sisi watatu, yani mimi na ile mi pit bull miwili, basi ikawa inaniangalia huku inanikazia macho kama vile inataka nijichanganye kidogo tu inichane chane, maana tayari ulimi uko nje, huku mijino kama vidole vya mtu mzima.
Kitu cha kwanza nikatoka chini ya gari na kuingia ndani ya gari. Sasa wakati nikiwa ndani ya gari nikasikia honi ya gari inaita kwa nje ya nyumba, nikajiuliza huyo ni mshikaji amerudi anataka nikamsaidie vitu au ni mtu mungine anapiga honi nyumba ya pili, honi ikaendelea wale mbwa wakakurupuka na kukimbilia mlangoni wakawa wanabweka ile mbaya.
Hapo nikajua anaepiga honi yuko mlangoni na pia inaonesha sio mwenyeji wa nyumba ile maana ingekuwa ni mwenyeji wasingebweka vile, kidogo simu inaita jamaa ananambia nichukue funguo alioniachia nikamfungulie mgeni wake.
Hapo ndio palikuwa patamu maana jamaa nilikuwa nishamuonesha kuwa wale mbwa siwaogopi, sasa naanzaje tena kumwambia kuwa naogopa kwenda kufungua? Ikabidi nimwambie kuwa niko msalan nakata gogo, akasema poa fanya fasta basi ukamfungulie.
Jamaa akampigia akamwambia mgeni asubiri nikimaliza kukata gogo nitamfungulia. Baadae akanipigia tena bado tu, nikabidi nimwambia ndo najisafisha natoka sasa hivi.
Nikasema potelea mbali wakinivamia atanilipa, nikaanza kulifuata gate la nje kwa kunyata kumbe washanisikia ghafla nikaona hao wanakuja mbio upande wangu, nikaona nikikimbia watanivamia, ikabidi nioneshe ukakamavu ghafla hawa miguuni, sasa nilichofanya nikamshika yule dume kichwani kama nampalaza palaza likatulia huku likionesha kuelewa ninachokifanya nikawa natembea mdogo mdogo kuelekea getini huku wakinifuata kama vile ni mtu wanaenifahamu, ile kufika getini nafungua na mwenyeji namuona yule kwa mbali anakuja. Basi wakaingia wote mwenyeji, mtoto na mgeni tukafunga geti.
Aisee siku ile sintoisahau.
Kwa wale wasiomjua pit bull, huyu hapo pichani kulaleki π