Huwa unamuamini asilimia ngapi mwenyeji wako anapokwambia usiogope, Mbwa wake hang'ati?

Huwa unamuamini asilimia ngapi mwenyeji wako anapokwambia usiogope, Mbwa wake hang'ati?

Katika viumbe ambao huwa siwaogopi ni mbwa na nyuki nimecheza nao muda mrefu najua tabia zao sana nyuki akikutana na mimi huwa anageuka kipepeo na mbwa anageuka mbuzi
Nilikua na rafiki yangu tunatembea, ghafla kuna mwanamke mmoja akapiga ukelele, tukashtuka kuna nini? "nyokaa" "nyokaa", tukasogea pale, jamaa wakaanza kumpiga yule nyoka mawe, nyoka akaingia kwenye kimti kwa chini amejificha, basi akatokea jamaa mmoja hivi mlevi na mwenzie anasema "msimpige macheni, nyoka mimi haniumi, nyoka wananijua muacheni nimkamate", basi tukaona ngoja leo tuone miujiza.

Ila tukamtahadharisha yule mlevi asifanye mchezo ile ni hatari.

Jamaa akasogea pale nyoka ameacha mkia, jamaa akamkamata mkiani kamnyanyua hakuwa mkubwa sana, yule nyoka akawa kichwa kipo chini jamaa kashika mkiani, yule nyoka akageuza kichwa kuelekea kwenye mkono wa jamaa, jamaa si akaona anang'atwa, hajamrushia huku tulipokua, acha watu wasambae , asee yule jamaa tulimfukuzaje?

Kama mwizi, jamaa pombe iliisha alikuwa anakanyaga kibati hatukumkamata yule nyoka sijui alipotelea wapi...
Hio kauli yako imenikumbusha hio moment, hizo kauli siziamini kabisa...😂🤣
 
Mkuu usije rudia tena kushika mbwa kichwani kama hauna urafiki nae, kuna baadhi ya mbwa atakufanya vibaya sana, mie shahidi, kuna wengine ukimshika masikioni umetangaza vita.
Story yako imenivunja mbavu, Pitbull wanaogofya...
Hawa jamaa pitbul wanatisha kimuonekano, lakini hata kivitendo, na pia wana nguvu sana. Niliona video flani ya kweli huko USA polisi walikwenda kumkamata jamaa fulan, wakati wanamkamata ile wanamfunga pingu basi pitbul wake hata alipotokea mi na wewe hatujui akamvaa askari mmoja ambae na yeye huyo askari alikuwa ameshika bonge la mbwa germansheffield, basi na yule germansheffield na yeye akamvaa pitbull hapo ndo palipokuwa patam kuwaachanisha ilibidi mtuhumiwa afunguliwe pingu na kuombwa amtulize pitbul wake huku na yule polisi akipambana kumtuliza germanffield wake ambae alikuwa ashaonesha kutokumtii kabisa. Kila apokuwa anamwambie aache kupambana na yule pitbul ndo kama vile alikuwa anamzidisha hasira huku pitbul nae akikataa kudhalilishwa mbele ya boss wake (mtuhumiwa mwenye mbwa)
 
Hawa jamaa pitbul wanatisha kimuonekano, lakini hata kivitendo, na pia wana nguvu sana. Niliona video flani ya kweli huko USA polisi walikwenda kumkamata jamaa fulan, wakati wanamkamata ile wanamfunga pingu basi pitbul wake hata alipotokea mi na wewe hatujui akamvaa askari mmoja ambae na yeye huyo askari alikuwa ameshika bonge la mbwa germansheffield, basi na yule germansheffield na yeye akamvaa pitbull hapo ndo palipokuwa patam kuwaachanisha ilibidi mtuhumiwa afunguliwe pingu na kuombwa amtulize pitbul wake huku na yule polisi akipambana kumtuliza germanffield wake ambae alikuwa ashaonesha kutokumtii kabisa. Kila apokuwa anamwambie aache kupambana na yule pitbul ndo kama vile alikuwa anamzidisha hasira huku pitbul nae akikataa kudhalilishwa mbele ya boss wake (mtuhumiwa mwenye mbwa)
Kuna chance ndogo ya Shepherd kumkabili pitbull, lakini shepherd ni mbwa ana akili nyingi, mjanja na mtiifu sana, shepherd anapoona mmiliki wake yupo hatarini atajaribu awezalo kusaidia, ndio maana huyo mbwa wa askari alikuwa mbishi.

Shepherd kwa ulinzi wapo vizuri.
 
Kuna chance ndogo ya Shepherd kumkabili pitbull, lakini pitbull ni mbwa ana akili nyingi, mjanja na mtiifu sana, shepherd anapoona mmiliki wake yupo hatarini atajaribu awezalo kusaidia, ndio maana huyo mbwa wa askari alikuwa mbishi.

Shepherd kwa ulinzi wapo vizuri.
Kwa maelezo yako haya, nimeamini kama wewe unawajua mbwa vizuri.
 
Mkuu usije rudia tena kushika mbwa kichwani kama hauna urafiki nae, kuna baadhi ya mbwa atakufanya vibaya sana, mie shahidi, kuna wengine ukimshika masikioni umetangaza vita.
Story yako imenivunja mbavu, Pitbull wanaogofya...
 
Hawa jamaa pitbul wanatisha kimuonekano, lakini hata kivitendo, na pia wana nguvu sana. Niliona video flani ya kweli huko USA polisi walikwenda kumkamata jamaa fulan, wakati wanamkamata ile wanamfunga pingu basi pitbul wake hata alipotokea mi na wewe hatujui akamvaa askari mmoja ambae na yeye huyo askari alikuwa ameshika bonge la mbwa germansheffield, basi na yule germansheffield na yeye akamvaa pitbull hapo ndo palipokuwa patam kuwaachanisha ilibidi mtuhumiwa afunguliwe pingu na kuombwa amtulize pitbul wake huku na yule polisi akipambana kumtuliza germanffield wake ambae alikuwa ashaonesha kutokumtii kabisa. Kila apokuwa anamwambie aache kupambana na yule pitbul ndo kama vile alikuwa anamzidisha hasira huku pitbul nae akikataa kudhalilishwa mbele ya boss wake (mtuhumiwa mwenye mbwa)
Duh noma noma,nilionaga video flani jamaa anashambuliwa na mbwa wawili huko marekani kati kati ya mitaa,jamaa yupo chini anaburuzwa tu,wale mbwa walikua wakorofi sana,wananchi walijaribu kuingilia lakini walishindwa na wengine wakaishia kung'atwa

Bahati nzuri waliwapigia askari simu,na askari wakawahi chap ndani ya muda mfupi sana wakawa wamefika,na wakajaribu kuwazuia wale mbwa ila wapiii na jamaa anavuja damu yupo hoi bin taaban

Polisi wakaona hapa tutampoteza jamaa kwa uzembe,wakachomoa bastola wakawapiga chuma wale mbwa wotee wakafa ndo wakamkimbiza mchizi hospitali
 
Aisee sio tu ningeisoma namba bali pengine leo hii ningekuwa naitwa marehem fulani, au wangeniachia ulemavu wa kudumu, maana hakuna mbwa mkali, hatari na mwenye nguvu kama pit bull. Huyo german shepherd mwenyewe akikutana na pit bull ujue siku hiyo hata wenye mbwa wao wenyewe watashindwa kuwaamua.

Na isitoshe walikuwa wakubwa last namba afu wameshiba haswa, wakitembea unasikia chini ti ti ti ti.
hao mbwa c ndo chotara wa simba hao?

Yaani Mimi toka nipigwe mtama na mbwa nikaangukia uso Sina hamu tena na wala Sina urafiki na mbwa kabisa .
 
Duh noma noma,nilionaga video flani jamaa anashambuliwa na mbwa wawili huko marekani kati kati ya mitaa,jamaa yupo chini anaburuzwa tu,wale mbwa walikua wakorofi sana,wananchi walijaribu kuingilia lakini walishindwa na wengine wakaishia kung'atwa

Bahati nzuri waliwapigia askari simu,na askari wakawahi chap ndani ya muda mfupi sana wakawa wamefika,na wakajaribu kuwazuia wale mbwa ila wapiii na jamaa anavuja damu yupo hoi bin taaban

Polisi wakaona hapa tutampoteza jamaa kwa uzembe,wakachomoa bastola wakawapiga chuma wale mbwa wotee wakafa ndo wakamkimbiza mchizi hospitali
Mbwa ni mmoja wa wanyama ambao ni hatari sana japo tunaishi nao kama walinzi wetu na marafiki zetu.
 
hao mbwa c ndo chotara wa simba hao?

Yaani Mimi toka nipigwe mtama na mbwa nikaangukia uso Sina hamu tena na wala Sina urafiki na mbwa kabisa .
Ilikuaje mkuu mpaka ukachotwa mtama? Aisee kuishi kwingi ni kuona mengi 🤣🤣🤣
 
Nisivyowapenda mbwa na paka uwafungie tu bandani. Sitaki habari za kuniambia usiogope hang'ati.
 
Mbwa hawaaminiki kama hawakujui, wale mbwa wa Kingunge wangemuua kabisa. Imagine mtu anaewalisha na wamemgeuka, itakuwa wewe wasiokujua?
Hata mbwa wa Kingunge hawakuwa wanamjua Kingunge kama ndio boss wao. Hii ni kwa sababu Kingunge aliajiri kijana ambae ndie aliekuwa anawalisha na kuwapa huduma zote walizozihitaji kupitia mfuko wa Kingunge, sasa mbwa wakajua kuwa yule kijana ndio boss wao, afu Kingunge wakamchukulia kama ni mpita njia tu ndo maana wakamvamia na kumchana chana vibaya.
 
7E45CD5F-9E29-471A-BB0A-2AC9960F5C54.jpeg

Mwanangu sana huyu anaitwa JUMBO hang’ati akiwa around na mwenyeji wake ila ukimpa respond ya kuattack ni hatari atakuweka chini ya ulinzi hadi afike mwenyeji wake..
 
Kuna jamaa nilienda kumtengenezea gari kwake. Kufika kwake nikakuta anafuga mbwa wawili, yan pit bull wakubwa walioshiba.

Akanambia wewe fanyakazi tu wala usiogope. Kwa vile ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika kwake, nikajifanya sina uoga na viumbe wale.

Nikiwa katika harakati zangu za kazi mara jamaa akanifuata na kuniambia kuwa anatoka mara 1 kwenda kumfuata mtoto shuleni (sio mbali sana na anapoishi) akasema wewe usiwe na wasi wasi hao hawawezi kukufanya chochote.

Dah kukataa nikashindwa na kukubali pia nikashindwa nikabaki kumeza fundo la mate huku nikijifanya sina wasi wasi na viumbe wale. Jamaa akaniachia funguo 1 ya gate la nje akafungua gate akatoka na kutuacha sisi watatu, yani mimi na ile mi pit bull miwili, basi ikawa inaniangalia huku inanikazia macho kama vile inataka nijichanganye kidogo tu inichane chane, maana tayari ulimi uko nje, huku mijino kama vidole vya mtu mzima.

Kitu cha kwanza nikatoka chini ya gari na kuingia ndani ya gari. Sasa wakati nikiwa ndani ya gari nikasikia honi ya gari inaita kwa nje ya nyumba, nikajiuliza huyo ni mshikaji amerudi anataka nikamsaidie vitu au ni mtu mungine anapiga honi nyumba ya pili, honi ikaendelea wale mbwa wakakurupuka na kukimbilia mlangoni wakawa wanabweka ile mbaya.

Hapo nikajua anaepiga honi yuko mlangoni na pia inaonesha sio mwenyeji wa nyumba ile maana ingekuwa ni mwenyeji wasingebweka vile, kidogo simu inaita jamaa ananambia nichukue funguo alioniachia nikamfungulie mgeni wake.

Hapo ndio palikuwa patamu maana jamaa nilikuwa nishamuonesha kuwa wale mbwa siwaogopi, sasa naanzaje tena kumwambia kuwa naogopa kwenda kufungua? Ikabidi nimwambie kuwa niko msalan nakata gogo, akasema poa fanya fasta basi ukamfungulie.

Jamaa akampigia akamwambia mgeni asubiri nikimaliza kukata gogo nitamfungulia. Baadae akanipigia tena bado tu, nikabidi nimwambia ndo najisafisha natoka sasa hivi.

Nikasema potelea mbali wakinivamia atanilipa, nikaanza kulifuata gate la nje kwa kunyata kumbe washanisikia ghafla nikaona hao wanakuja mbio upande wangu, nikaona nikikimbia watanivamia, ikabidi nioneshe ukakamavu ghafla hawa miguuni, sasa nilichofanya nikamshika yule dume kichwani kama nampalaza palaza likatulia huku likionesha kuelewa ninachokifanya nikawa natembea mdogo mdogo kuelekea getini huku wakinifuata kama vile ni mtu wanaenifahamu, ile kufika getini nafungua na mwenyeji namuona yule kwa mbali anakuja. Basi wakaingia wote mwenyeji, mtoto na mgeni tukafunga geti.
Aisee siku ile sintoisahau.

Kwa wale wasiomjua pit bull, huyu hapo pichani kulaleki [emoji23]
Mbna inatisha sanaaaaaa, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom