Huwa unaruhusu mtoto wako kupigwa picha na watu mbalimbali ikiwemo ndugu? Unajua madhara yake?

Huwa unaruhusu mtoto wako kupigwa picha na watu mbalimbali ikiwemo ndugu? Unajua madhara yake?

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2021
Posts
590
Reaction score
1,648
Wakuu kwema?

Inaweza kutokea ndugu yako akaomba kumpiga picha mtoto wako akisema mtoto amependeza au mtoto wako mzuri picha zitatoka vizuri, wakati mwingine inaweza kuwa hata kwa majirani au watu ambao huwajui kabisa.

Dunia imebadilika, huwezi kujua unayemruhusu ampige picha mtoto wako ameficha nini moyoni.

Picha hizo zinaweza kutumiwa kwa namna tofauti kama vile;

  • Matangazo ya Biashara: Mtoto anapigwa picha na picha zake zinaenda kutumiwa kwenye matangazo mbalimbali bila ridhaa yako.
  • Picha hizo kuuzwa kwa watu wenye 'fantancy' za kingono zinazohusu watoto.
  • Picha hizo kutumika kama sampuli za kwenda kuonesha bidhaa (mtoto wako) kwa watu wanaojihusisha na biashara haramu za binadamu (human trafficking). Mteja akipenda mtoto wako itatafutwa mbinu itakayoweza kufanikisha kupatikana mtoto wako na atakachoenda kufanywa huko ni chochote atakachoamua mnunuzi, sababu tayari anamiliki 'bidhaa' hiyo.

Mambo haya yanatokea kwa wingi kuliko vile tunavyofikiria, hivyo mzazi kuwa makini na mtoto wako, usiruhusu mtoto wako apigwe picha ovyo ukawa njia ya mtoto wako kwenda kufanyiwa ukatili.

Unaweza kusema unamuamini mtu anayempiga picha ni kaka yake, mjomba wake, shangazi yake, jirani mwema nk, lakini matukio mengi yameonesha si kila unayesema unamjua yupo hivyo kweli. Pamoja na hayo yote, kwanini apige picha ya mtoto wako, ili iweje?

Nini maoni yako kuhusu hili?
 
Kuna watu wanabeza na kuona kama unachekesha.

Ni kawaida ya watanzania hasa tanganyika ujuaji, ila kama unataka kujua ni kosa kumpiga picha mtu hasa mtoto bila ridhaa emu kaishi nje ya tanzania kwa wenzetu uyafanye hayo.

Tatizo wasiokuwa na exposure waliokulia na kuzaliwa mbwinde ndo wanajifanya wajuaji.

Kaza fuvu na uendeleee na kuruhusu watu wapige picha za mwanao
 
Wakuu kwema?

Inaweza kutokea ndugu yako akaomba kumpiga picha mtoto wako akisema mtoto amependeza au mtoto wako mzuri picha zitatoka vizuri, wakati mwingine inaweza kuwa hata kwa majirani au watu ambao huwajui kabisa.

Dunia imebadilika, huwezi kujua unayemruhusu ampige picha mtoto wako ameficha nini moyoni.

Picha hizo zinaweza kutumiwa kwa namna tofauti kama vile;

  • Matangazo ya Biashara: Mtoto anapigwa picha na picha zake zinaenda kutumiwa kwenye matangazo mbalimbali bila ridhaa yako.
  • Picha hizo kuuzwa kwa watu wenye 'fantancy' za kingono zinazohusu watoto.
  • Picha hizo kutumika kama sampuli za kwenda kuonesha bidhaa (mtoto wako) kwa watu wanaojihusisha na biashara haramu za binadamu (human trafficking). Mteja akipenda mtoto wako itatafutwa mbinu itakayoweza kufanikisha kupatikana mtoto wako na atakachoenda kufanywa huko ni chochote atakachoamua mnunuzi, sababu tayari anamiliki 'bidhaa' hiyo.

Mambo haya yanatokea kwa wingi kuliko vile tunavyofikiria, hivyo mzazi kuwa makini na mtoto wako, usiruhusu mtoto wako apigwe picha ovyo ukawa njia ya mtoto wako kwenda kufanyiwa ukatili.

Unaweza kusema unamuamini mtu anayempiga picha ni kaka yake, mjomba wake, shangazi yake, jirani mwema nk, lakini matukio mengi yameonesha si kila unayesema unamjua yupo hivyo kweli. Pamoja na hayo yote, kwanini apige picha ya mtoto wako, ili iweje?

Nini maoni yako kuhusu hili?
Sawa asante
 
FB_IMG_16872352747111555.jpg
 
Mimi napinga tu vichanga kupigwa picha, yaani katoto hakajaleta hata nuru ya uangavu...picha zipo status
...anyways, kila mtu aishi atakavyo!!
 
Kuna watu wanabeza na kuona kama unachekesha.


Ni kawaida ya watanzania hasa tanganyika ujuaji, ila kama unataka kujua ni kosa kumpiga picha mtu hasa mtoto bila ridhaa emu kaishi nje ya tanzania kwa wenzetu uyafanye hayo.

Tatizo wasiokuwa na exposure waliokulia na kuzaliwa mbwinde ndo wanajifanya wajuaji.

Kaza fuvu na uendeleee na kuruhusu watu wapige picha za mwanao
Kisa ushirikina..

Wewee..
Em komaa akili..
 
Kisa ushirikina..

Wewee..
Em komaa akili..
Unawaza ushirikina tu....hapo kwenye uzi hujaona kingine cha kukuelimisha. Matukio mangapi umesikia yametokea kwa mkoa mmoja tu watoto kufanyiwa vitendo vya ukatili? unafikiri njia pekee ni mpaka mtu awe anaishi na wewe karibu? Hata wa mbali anaweza kumpata mtoto wako kirahisi ikiwa unaweka taarifa za mtoto wako mtandaoni.

Mtoto akienda shule unapiga picha, siku ya birthday unaweka picha, akiwa na marafiki zake, ndugu unaweka picha, sehemu mkitoa out picha, yaani kutoka kwenye mtandao mtu anajua jina kamili la mtoto wako, mnakoishi, chumba chake kinafananaje, shule anayosoma, vyakula anayopenda/asivyopenda, marafiki zake nk. mwenye nia ya kumdhuru unafikiri ni ngumu kumpata. Na watoto ni rahisi kurubuni. Kuwa makini na uwaelimishe wengine pale unapopata nafasi
 
Back
Top Bottom