Huwezi amini lakini ukweli bila NATO, Marekani anaiogopa Sana Urusi

Ila dunia inaenda kasi sana ...Sio dunia ya miaka 90 na mwanzoni mwa miaka 2000...
Tunakoelekea inaonyesha ni ngumu sana kudhibiti ( Monopoly) technology kama zamani....Ona uwezo wa silaha wa Nchi zinazonyanyuka kama KOREA KZ,. IRAN, TURKEY, India nk....
Itafika mahali kumiliki silaha fulani haitoshi wewe kuweza kuishambulia tu nchi bila ya wewe kupata madhara..
Hata Russia anawaza mara 2 kuushambulia UKRAINE...
Issue sio tu kushinda bali damages baada ya vita....Hilo ndio maana US anahangaika na ': Nuclear deal"' na IRAN
Ndo maana Israel anaumiza kichwa kwa IRAN, vivyo hivyo IRAN kwa ISRAEL..
Korea kz ana test silaha kila siku watu wanaangalia tu.
Zile zama za WEST na US kutamba pekee zinayoyoma...Silaha pekee wanayotegemea ni UCHUMI,. kitu ambacho Mchina anakuja ku- ibalance dunia Ktk kutegemea West na US...
Nawaza miaka 30 ijayo Geo politic itakavyokuwa . Je US ataendelea kumudu kuilinda Taiwan, UKRAINE , Israel nk...au zitasimama zenyewe?...Je kwa utawandawazi ulivyo na usiri wa technology nchi ngapi zitainuka Ktk ujuzi wa vitu mbalimbali ikiwemo silaha..?
 
Tatizo lako wewe unalinganisha nchi yenye watu bil 1.4 na USA yenye watu million 370+ au hizo nchi za ulaya zenye watu milioni 10+

Bila uteam China kuja kuipata USA hizo ni ndoto za mchana kumbuka USA na Ulaya ndio wameifanya china ifike hapo ilipo

Gdp zisiwazingue mimi ukiniuliza kati ya Switzerland na china ipi iliyoendelea nitakujibu Switzerland coz pato la taifa+idadi ya watu inatosha kusema nchi nyingi za ulaya ni pepo za hapa dunian
 
Jitahidi utumie akili.
 
Wewe lini tajiri akamuogopa maskini, wewe una akili kweli, unajua unachoongea.
 
Turudi kwenye achievements alizopiga, siyo kwamba china ina population tu, ila ina skilled population. Ingekuwa ina population tu ungekuwa mzigo kwake ila ina skilled population.
Pia population yake ni soko. We hujiulizi kwanini makampuni yote ya marekani kuanzia apple, tesla, na mengine bado wanahitaki soko la china? Kwakuwa population ya china ina afford kununua hizo bidhaa, why not Africa.
Ukiongelea per capital income hata US siyo sidhani kama iko kwenye top 5.
Kwahiyo hicho kigezo tukiweke pembeni tunapokuwa tunazungumzia usuper power wa nchi.
China hajamzidi US ila kamkaba koo. 30 years ago, alikuwa hajamkaribia hata kidogo, leo anazidi kupunguza gap, so tujiulize miaka 20 ijayo itakuaje?
 
That why anatumia mgongo wa NATO kuisajili Ukraine ili apate ushawishi wa kuidhibiti Urusi kupitia Uanachama wa Ukraine.
Kitu ambacho kitaleta Vita ya Urusi na Ukraine ni USA kushawishi NATO kuijoin Ukraine.
 
China sijui hii teknolojia ya haraka wamejifunza wapi, kiukwel wale jamaa ni wana balaa kubwa. Saizi wana barabara inapita chini ya bahari hatari sana wale jamaa
 
China sijui hii teknolojia ya haraka wamejifunza wapi, kiukwel wale jamaa ni wana balaa kubwa. Saizi wana barabara inapita chini ya bahari hatari sana wale jamaa
Hawa watu kwasasa ni balaa sana. Wanacopy wanafyatua vyao tena kama ni kwa matumizi yao ni ubora haswaa. Wana vituo vya utafiti vingi. Juzi juzi wamezindua kituo cha kufanya vipimo vya aerodynamics kikubwa kuliko kituo chochote duniani. Lengo ni kitumike katika fesigning ya rockets zao na ndege.
Wamewekeza sana katika utafiti na elimu yenye application.
 
Wewe bado haujanielewa... tafuta wafanyabiashara wa kibongo huko china na sio hawa wanaofata tu mizigo trust me china inasafari kubwa sana aiseee

China haiwezi kua superpower ipo siku utanitafuta kwanza nchi yenyewe haina mifumo mizuri ya kiutawala raia wanakomaa kivyao vyao pia skilled labor upo sahihi kabisa jamaa jamaa hawajui kutegemea tu kabisa nayogovernment ikiamua kujenga jengo refu hadi mwezi wananchi watashangaa mjengo ushainuka

Tabia za china ni nchi masikini tu ndio zinaweza kuiwaza china kwenye usuperpower

Tatizo la USA kila kitu anataka kua yeye huu ni ujinga

Ushasikia nchi kama Netherland inafanya ujinga kama USA kiongoz kunachi zinasubiri tu dunia ifike mwisho

Mwisho USA ni mkuda[emoji38][emoji38]
 
Nchi maskini ndiyo zinaiwaza china kwenye usuperpower? Bloombergy imeitabili kufikia 2050, hope unaifahamu bloombergy, kuna analyst wengine wanaitabili kufikia 2030 itakuwa ndiyo nchi yenye ukwasi zaidi.
Huo mfumo wa uongozi unaoukandia, ndiyo umeitoa ilipo ambapo wanadai miaka ya 60 ilikuwa kundi na sisi leo ni ya pili kwa uchumi duniani. Sasa unasemaje ni mfumo mbovu mbovu?
State controlled economy imeifikisha hapo. Wakati covid imeathiri uchumi wa US, wa china umekua. Serikali inaweza kucontrol kila aspect ya maisha ya wananchi china.
Hii no advantage kwao katoka kuset ukuaji wao wa kiuchumi.
Narudia, siyo nchi maskini zinazosema china inakua kwa kasi, bali ni world bank, bloombergy and et el.
Ela anayomwaga mchina pale asia na africa siyo mchezo.
Ulisikia alichokifanya pale singapore?
 
Kwani urusi wametangaza kuivamia Ukraine 😳😳😳😳😳?
 
Maana yangu ni kwamba Marekani hawezi kuikabili Urusi bila NATO na anachoweza kuikabili Urusi ni vikwazo tu.
Unasema kwamba, Marekani haiwezi kuikabili Urusi bila NATO, hapohapo unasema inaweza kuikabili Urusi kwa vikwazo! Sijakuelewa!
 
Sijui nikuite Punguani au Layman?

Bila NATO Urusi ataifanya Nini Marekani?

NATO ina jumla ya Wanajeshi 450,000. Kati ya hao Wanajeshi wa Marekani ni 370,000. Nchi 29 zilizobaki Zina Wanajeshi 80,000 ndani ya NATO.

NATO ina Aircraft Carrier 27. Kati ya Hizo 22 ni za Marekani. Nchi 29 zilizobaki Zina Aircraft Carrier 7 tu.

NATO ina Combat Tanks 27,000. Kati ya Hizo, 19,000 ni za Marekani. Nchi 29 zilizobaki kwa pamoja Zina Combat Tanks 8,000.

Bajeti ya NATO kwa mwaka ni $ 1,019,000,000,000.($ 1.019T). Kati ya Hizo, $ 760,000,000,000 ni za kutoka Marekani. Nchi 29 zilizobaki zinachangia Nusu ya Marekani kwa pamoja $ 300,000,000,000.

NATO ina Jumla ya Nuclear Waepons 7,200. Kati ya hizo, 6,500 ni kutoka Marekani. Nchi zingine 29 kwa pamoja Zina Nuclear Waepons 700 tu.

NATO ina Jumla ya Fighter jets 3,500. Kati ya Hizo, 2,700 ni Kutoka Marekani. Nchi zingine 29 zinachangia Jumla ya Jets 800 tu.

Huwa mnaposema sijui eti Marekani bila NATO hawezi kupigana wakati mnajua kabisa Marekani ndio NATO kwenye Kila Kitu,bila Marekani hakuna NATO.

Lengo la Marekani kwenye NATO sio kutafuta Support ya nchi za Ulaya Kijeshi bali ni Hofu ya Marekani kwamba Urus atazimeza nchi za Ulaya Mashariki tangu USSR kusambaratika. Ndio maana kwenye huu mgogoro wa URUS na UKRAINE,Mataifa madogo ya Ulaya Mashariki Kama LATVIA,LITHUANIA,ROMANIA na ESTONIA ambao ni wanachama wa NATO wameiomba Marekani iongeze Wanajeshi wake kwenye Mataifa hayo na Siraha nzito ili kuyalinda dhidi ya Urusi.

Ndio Maana Marekani imeahidi kwamba endapo Urus itaivamia Ukraine kijeshi basi Marekani haitatuma Wanajeshi wake kwasababu Ukraine sio Memba wa NATO. Lakini ikaahidi Urus itajutia kitendo chake make Marekani itaongeza idadi ya vikosi vyake na Siraha nzito kwenye Mataifa ya Ulaya Mashariki ili kuyalinda dhidi ya uvamizi wa URUS. Ndio Maana mpaka Sasa Putin kagoma Kuvamia Ukraine.
 
Putin kagoma kuvamia Ukraine?.

Urusi inatia presha Ukraine isijiunge na NATO na sio kwamba anavamia tu kama Mmasai anavyovamia mashamba ya wakulima.

Ngoja tuone ni nini kitatokea endepo Ukraine itajiunga na NATO.
 
Putin kagoma kuvamia Ukraine?.

Urusi inatia presha Ukraine isijiunge na NATO na sio kwamba anavamia tu kama Mmasai anavyovamia mashamba ya wakulima.

Ngoja tuone ni nini kitatokea endepo Ukraine itajiunga na NATO.
Kipindi LITHUANIA na ESTONIA wanajiunga na NATO mwaka 2004 URUS sio tu alitishia Bali alipeleka Makombora ya ISKANDER Beralus na Karzakhstan. Alitia Pessure kubwa Sana eti zisijuinge na NATO kwasababu ziko Mpakani na URUS lakini yako wapi mpaka Leo?

This time URUS hatavamia Ukraine direct,atatumia mbinu nyingine. Consequences ya Urusi Kuvamia ni kubwa sana. Ujeruman ilikataa kusitisha NORD STRING 2 Lakini imeapa kusitisha Ujenzi wa Bomba Hilo endapo Urus itaivamia Ukraine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…