Huwezi kuzungumzia maendeleo ya teknolojia duniani bila kuitaja China

Huwezi kuzungumzia maendeleo ya teknolojia duniani bila kuitaja China

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
1665541952809.png


Na Gianna Amani
China ni nchi kubwa kiuchumi na yenye idadi ya watu wengi kuliko nchi zote duniani, na ni muumini mkubwa wa teknolojia katika shughuli zake mbalimbali. Miongoni mwa mambo ya kuvutia ni namna jinsi China inavyotumia teknolojia katika shughuli zake za bandari.

Bandari ya Qingdao iliyopo katika mkoa wa Shandong, ni miongoni mwa bandari nne kubwa duniani ikihudumia makontena zaidi ya milioni 5.3 kwa mwaka. Uwezo wa bandari hiyo kutoa huduma kwa idadi kubwa namna hiyo ya makontena, unatokana na matumizi ya teknolojia, kwani miaka kadhaa iliyopita kabla ya kuanza kutumia teknolojia za kisasa, bandari hiyo ilikuwa ikihudumia makontena 2.8 milioni.

Kwa sasa bandari hiyo ambayo huhudumia mizigo ya makontena pekee, imeachana na utegemezi wa watu zaidi katika utendaji wake, na sasa inategemea sayansi zaidi. Bandari hiyo sasa inatumia magari yasiyo na dereva kuchukua makontena yanaposhushwa kutoka kwenye meli na kuyapeleka sehemu ya maegesho, magari hayo hutumia umeme.

Licha ya kuwa magari hayo yanatumia umeme, hayahitaji kwenda kuchajiwa badala yake huchajiwa wakati yakiendelea na kazi zake. Lakini mbali na magari hayo, mitambo mingine ambayo hutumika kushusha na kupakia makontena, haiendeshwi na mwongozaji wa hapo hapo, bali waongozaji hutumia kompyuta wakiwa kwenye chumba maalumu hivyo kuongeza ufanisi.

Kwa mujibu wa viongozi wa bandari hiyo, kutokana na matumizi ya sayansi na teknolojia shughuli ambayo hapo awali ilikuwa inafanywa na watu 10, sasa inaweza kufanywa na watu watatu tu.
 
Bandari ya Qingdao inajiendesha vizuri sana tena kitaalamu nimekuwa mfuatiliaji wa hili kwa muda mrefu sasa hakika bandari ya Qingdao ina mengi ya kuzifunza bandari zetu za Dar es saalam, Tanga, Mtwara n.k
 
Kuna vijana huwa wanafikri msingi wa maendeleo nchini China ulijengwa wakati wa ujamaa, huwa wanakosea sana
 
View attachment 2384270

Na Gianna Amani
China ni nchi kubwa kiuchumi na yenye idadi ya watu wengi kuliko nchi zote duniani, na ni muumini mkubwa wa teknolojia katika shughuli zake mbalimbali. Miongoni mwa mambo ya kuvutia ni namna jinsi China inavyotumia teknolojia katika shughuli zake za bandari.

Bandari ya Qingdao iliyopo katika mkoa wa Shandong, ni miongoni mwa bandari nne kubwa duniani ikihudumia makontena zaidi ya milioni 5.3 kwa mwaka. Uwezo wa bandari hiyo kutoa huduma kwa idadi kubwa namna hiyo ya makontena, unatokana na matumizi ya teknolojia, kwani miaka kadhaa iliyopita kabla ya kuanza kutumia teknolojia za kisasa, bandari hiyo ilikuwa ikihudumia makontena 2.8 milioni.

Kwa sasa bandari hiyo ambayo huhudumia mizigo ya makontena pekee, imeachana na utegemezi wa watu zaidi katika utendaji wake, na sasa inategemea sayansi zaidi. Bandari hiyo sasa inatumia magari yasiyo na dereva kuchukua makontena yanaposhushwa kutoka kwenye meli na kuyapeleka sehemu ya maegesho, magari hayo hutumia umeme.

Licha ya kuwa magari hayo yanatumia umeme, hayahitaji kwenda kuchajiwa badala yake huchajiwa wakati yakiendelea na kazi zake. Lakini mbali na magari hayo, mitambo mingine ambayo hutumika kushusha na kupakia makontena, haiendeshwi na mwongozaji wa hapo hapo, bali waongozaji hutumia kompyuta wakiwa kwenye chumba maalumu hivyo kuongeza ufanisi.

Kwa mujibu wa viongozi wa bandari hiyo, kutokana na matumizi ya sayansi na teknolojia shughuli ambayo hapo awali ilikuwa inafanywa na watu 10, sasa inaweza kufanywa na watu watatu tu.
Je hao saba waliobaki wanapelekewa posho nyumbani maana umeondoa Tonge lao mdomoni

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom