Huwezi na Hutoweza Kuongea / Kuandika Kiswahili fasaha

Huwezi na Hutoweza Kuongea / Kuandika Kiswahili fasaha

Kiswahili ni lugha ya wenyeji wa pwani ya Afrika mashariki, ni lugha iliyotokana na nasibu ya kiarabu kwa wingi wa maneno yake na kibantu kadhalika , , wenyeji wa pwani ya Afrika mashariki ndiyo hasa walioitwa "asswahili"na pwani hiyo ilijaa waarab ambao ndiyo walioitumia sana pwani hiyo kibiashara.
Hivyo ni sawa kusema ili uwe na lafudhi nzuri ya kiswahili, hakuba budi kujua kiarabu au matamshi yake
 
Kwani wasemaji wa kiswahili wanashindana hivyo hivyo mara nyingi...

Kama inabidi kweli kujua kiarabu ili kutumia kiswahili kwa fasaha pia eti itabidi kujua kilatini au kifaransa ili kutumia kiingereza kwa fasaha. Pia naweza kujua maana ya kustaarabu bila kujua kiarabu vilevile mtu wa kiingereza anaweza kujua neno ya "bureau" bila kujua kifaransa.

Bila shaka itasaidia kujua lugha zinazohusika na lugha yako lakini si lazima. Yaani yeyote anaweza kuelewa maana ya neno kabisa akipata neno kwa etymology (yaani maelezo ya maneno kwa historia). Tuangalie kiingereza - Wasemaji wa kiingereza wangapi wanajua kifaransa? lugha ambayo inahusika na zaidi ya 30% ya maneno yote. Zamani kingereza kilibadilika sana wakati wafaransa wakivamia ungereza.
 
Si kwamba sijui/sijuwi, lakini nahisi inaweza kuwa tafsiri yako na yangu zikawa tofauti na hivyo tunaweza kubishana kwa tunalinganisha chungwa na parachichi.

Kwako wewe pengine lugha sio 'nasibu' na haibadiliki (static), na hivyo 'kiswahili fasaha' ni kile kilichozungumzwa kabla ya wakoloni kutoka Uropa na kinachotumia lafudhi/lafidhi ya kiarabu.

Nisome post namba moja, halafu ujione ulivyo "stagnant" kichwani mwako.
 
Kwani wasemaji wa kiswahili wanashindana hivyo hivyo mara nyingi...

Kama inabidi kweli kujua kiarabu ili kutumia kiswahili kwa fasaha pia eti itabidi kujua kilatini au kifaransa ili kutumia kiingereza kwa fasaha. Pia naweza kujua maana ya kustaarabu bila kujua kiarabu vilevile mtu wa kiingereza anaweza kujua neno ya "bureau" bila kujua kifaransa.

Bila shaka itasaidia kujua lugha zinazohusika na lugha yako lakini si lazima. Yaani yeyote anaweza kuelewa maana ya neno kabisa akipata neno kwa etymology (yaani maelezo ya maneno kwa historia). Tuangalie kiingereza - Wasemaji wa kiingereza wangapi wanajua kifaransa? lugha ambayo inahusika na zaidi ya 30% ya maneno yote. Zamani kingereza kilibadilika sana wakati wafaransa wakivamia ungereza.

Soma tena post namba moja, hakuna mahala nimeandika "kujuwa" sasa wewe kwanini ubadilishe maandiko yangu?

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?

Inasikitisha sana uelewa na ufahamu wa Watanzania, kila anaekuja kujibu hoja yangu anaibadilisha maana, sijaona moaka sasa aliye i "tackle" hoja na hat kuja na jibu ya nililouliza.

Dr. Mp Kalix2 kajaribu kujibu swali lakini kakosea jibu. At least kajitahidi kwa kuliona swali.
 
Mtoa Hoja..kwa maelezo yako inamaana kiswahili ni kiarabu...na kwako kiswahili fasaha ni kiarabu ndio maana unazihusiahanisha hizi lugha kwa ukaribu hivyo...hivyo hakuna kiswahili bila kiarabu ndivyo unavyotaka kutuaminisha..labda kwa maana rahisi tuambie kiswahili fasaha ni kipi?..kiarabu ni lugha iliyo athiri kiswahili tu kama lugha zingine zilivyo kiathiri kiswahili hivyo mantiki yako kuwa uweze kiswahili fasaha ni hadi ukijue kiarabu me nakataaa kwa miguu yote na mikono

Kwanini utie maana yako ambayo haipo kwenye andiko langu na ufikirie tu kuwa mimi nnamaanisha hiyo? mimi nnamaanisha nilichokiandika, huwa sichezi na akili ya mtu, kama unajichezea akili yako ni wewe mwenyewe tu.

Hii inaonesha ni vipi Tanzania watu badala ya kuwa na reality wana "hallucinate". Mmoja tu au wawili mpaka sasa ambao sijaona kuwa wamebadili maana ya nilichokiandika, Watanzania wachache sana wako kama hao wawili. Wanaelewa wanachokisoma na hawabadili maana.

Ni nani leo hii anaekataa kuwa Kiswahili hakipo kama nilivyoandika kwenye post yangu namba moja para ya kwanza?
 
Kiswahili ni lugha ya wenyeji wa pwani ya Afrika mashariki, ni lugha iliyotokana na nasibu ya kiarabu kwa wingi wa maneno yake na kibantu kadhalika , , wenyeji wa pwani ya Afrika mashariki ndiyo hasa walioitwa "asswahili"na pwani hiyo ilijaa waarab ambao ndiyo walioitumia sana pwani hiyo kibiashara.
Hivyo ni sawa kusema ili uwe na lafudhi nzuri ya kiswahili, hakuba budi kujua kiarabu au matamshi yake

Umenielewa kabisa point yangu na mpaka hapo juu nimeweka mfano wa Wazungu Waalimu wa awali wa Kiswahili wa vyuo vikuu huko nje walivyoona huo umuhimu wakujifunza Kiswahili kwa kujuwa maandiko na matamshi ya Kiarabu, sijuwi hawa ndugu zangu ambao hawalioni hilo na wanalipinga wanapinga nini haswa?

Mimi kuileta hii mada nna maana yangu pana sana, ni juzi juzi tumesikia kuwa Tanzania imetowa maamuzi kuwa lugha ya kufundishia masomo yote iwe Kiswahili. Ni jambo jema sana hilo. Ni wakati muafaka tukatambuwa kuwa inabidi na watu wafundishe kukijuwa Kiswahili fasaha kwa matamshi ya Kiarabu ili wawe na ufasaha na kina cha kuelewa maana ya maneno mengi ya Kiarabu yaliyomo kwenye Kiswahili.

Itakuwa ni rahisi sana kwa mwanafunzi kuwa na ufasaha wa hali ya juu na au Mwalimu atakuwa na kina cha kufundisha ikiwa tu atakielewa Kiswahili kwa herufi za Kiarabu kuliko yule ambae atabaki na kukielewa kwa herufi za Kilatini tu.

Leo hii utashangaa mtu anakuja na jina la kiajabu ajabu la kutunga hata halina kina wala halina uhusiano wowote na ubaridi wala historia eti "jokofu", wakati neno hilohilo kwa Kiswahili fasaha lipo "barada", ambalo lina historia, lina kina na lina uhusiano na ubaridi.

Nnawashauri Waalimu wa Kiswahili, wa kuanzia shule za msingi mpaka juu kabisa huko, waanze kujifundisha herufi za Kiarabu na waone wakisha zijuwa kuandika na kuzisoma herufi hizo watavyoona raha kufundisha Kiswahili kwa ufasaha na kina zaidi.

Fikiri.
 
Kwanini utie maana yako ambayo haipo kwenye andiko langu na ufikirie tu kuwa mimi nnamaanisha hiyo? mimi nnamaanisha nilichokiandika, huwa sichei na akili ya mtu, kama unajichezea akili yako ni wewe mwenyewe tu.

Hii inaonesha ni vipi Tanzania watu badala ya kuwa na reality wana "hallucinate". Mmoja tu au wawili mpaka sasa ambao sijaona kuwa wamebadili maana ya nilichokiandika, Watanzania wachache sana wako kama hao wawili. Wanaelewa wanachokisoma na hawabadili maana.

Ni nani leo hii anaekataa kuwa Kiswahili hakipo kama nilivyoandika kwenye post yangu namba moja para ya kwanza?
Kwa majibu yako wewe ni mbishi tu na hata tukeshe autakubali....ivi kiswahili kina Asilimia ngapi ya misamiati ya kiarabu? Na unashindwa kueleza maana yako ya kiswahili fasaha......tatizo ni kukariri eti mtu akiwa anaongea kwa lafudhi ya kipwani ndio anajua kiswahili teh....yahe kheri akhsante taarabu...aya baki maana zako izo
 
Kwa majibu yako wewe ni mbishi tu na hata tukeshe autakubali....ivi kiswahili kina Asilimia ngapi ya misamiati ya kiarabu? Na unashindwa kueleza maana yako ya kiswahili fasaha......tatizo ni kukariri eti mtu akiwa anaongea kwa lafudhi ya kipwani ndio anajua kiswahili teh....yahe kheri akhsante taarabu...aya baki maana zako izo

Tafuta maandiko yoyote ya Kiswahili yenye maneno zaidi ya elfu moja halafu chambuwa maneno ya Kiarabu, Ki Uropa na Ki bantu, utapata jibu "roughly".

Hapa sipo kubishana nipo kupanuana mawazo.

Nisome tena post namba moja kwa utuvu. Utanielewa tu.
 
Tafuta maandiko yooyote yenye maneno zaidi ya elfu moja halafu chambuwa maneno ya Kiarabu, Ki Uropa na Ki bantu, utapata jibu "roughly".

Hapa sipo kubishana nipo kupanuana mawazo.

Nisome tena post namba moja kwa utuvu. Utanielewa tu.

Utuvu = utulivu (bila shaka ni kuteleza kwa kidole).
 
Tafuta maandiko yooyote yenye maneno zaidi ya elfu moja halafu chambuwa maneno ya Kiarabu, Ki Uropa na Ki bantu, utapata jibu "roughly".

Hapa sipo kubishana nipo kupanuana mawazo.

Nisome tena post namba moja kwa utuvu. Utanielewa tu.

Skia nikuambie kitu kimoja...lugha hizi hata kisarufi ni tofauti...jaribu kuchukua hata mfano mdogo tu wa mkazo wa lugha ya kiswahili na ule wa lugha ya kiarabu...alafu nipe jibu faster nakusubiria...nambie mazingira ya mkazo ya lugha ya kiarabu na ule wa kiswahili....chukua maneno ya mkopo kama tathmini, barabara, hukumu...alafu yasiyo ya mkopo kucheza kuimba kupika kupiga alafu ndio tuje katika ufasaha
 
Tafuta maandiko yoyote ya Kiswahili yenye maneno zaidi ya elfu moja halafu chambuwa maneno ya Kiarabu, Ki Uropa na Ki bantu, utapata jibu "roughly".

Hapa sipo kubishana nipo kupanuana mawazo.

Nisome tena post namba moja kwa utuvu. Utanielewa tu.

Ni chini ya asilimia 30 tu ya msamiati wa kibantu katika kiswahili kama malcon Guthrie na meinhof wanavyosema...athari ya kiarabu ipo kwa kiswahili lakini sio hadi kuathiri ufasaha wa kiswahili...lugha hizi zingekuwa zinafanana kisarufi kama muundo wa sentensi..mwishilizo wa vitenzi ..uambishaji... unyambulishaji kidogo ningekubali...lakini lugha hizi ni tofauti kabisa...chunguza kwa umakini usitangulize ujasiri...angalia mwisho wa maneno mengi ya kiswahili hamna coda ila kiarabu maneno kama sahel Allah yanaishia na konsonati sasa nashindwa kuelewa ufasaha wa kiswahili kusababishwa na kiarabu unakujaje hapa....kiswahili fasaha sio utamkaji wa kheri...taaratibu ila ni kuheshimu taaratibu za kisarufi....
 
Skia nikuambie kitu kimoja...lugha hizi hata kisarufi ni tofauti...jaribu kuchukua hata mfano mdogo tu wa mkazo wa lugha ya kiswahili na ule wa lugha ya kiarabu...alafu nipe jibu faster nakusubiria...nambie mazingira ya mkazo ya lugha ya kiarabu na ule wa kiswahili....chukua maneno ya mkopo kama tathmini, barabara, hukumu...alafu yasiyo ya mkopo kucheza kuimba kupika kupiga alafu ndio tuje katika ufasaha

Hata hilo neno ulilotumia ni la Kiarabu sasa sijuwi unamaanisha nini ukisema "lugha hizi"?

Hakuna maneno ya "mkopo" kama umeyakopa utayarudisha lini? unarudi kule kule ambako swali hilo limeshajadiliwa.

Mmoja juu huko alikuja na maneno ya "kuazima", cha kuazima chako? sasa wewe umebadili unakuja na kukopa, cha kukopa hurudishwa, wewe utarudisha lini? Fikiri.

Hayo maneno yanatokana na Kiarabu na yanaunda Kiswahili. Hakuna kukopana wala kuazimana. Na ndiyo maana ukinisoma vizuri post namba moja, para ya kwanza, sentensi ya kwanza kabisa, nimeandika hivi:

"Kiswahili ni lugha ambayo imetokana na Kiarabu na Kibantu na maneno mengine machache yaliongezeka kidogo kidogo kutoka lugha zingine za Afrika, Uropa na Asia"

Sasa ni nini usichokielewa hapo? sasa rudi post namba moja, ujibu swali langu, lipo mwisho kabisa wa maandiko yangu.

Hujalisoma au limekuwa gumu kwako na unalikwepa?

 
Ni chini ya asilimia 30 tu ya msamiati wa kibantu katika kiswahili kama malcon Guthrie na meinhof wanavyosema...athari ya kiarabu ipo kwa kiswahili lakini sio hadi kuathiri ufasaha wa kiswahili...lugha hizi zingekuwa zinafanana kisarufi kama muundo wa sentensi..mwishilizo wa vitenzi ..uambishaji... unyambulishaji kidogo ningekubali...lakini lugha hizi ni tofauti kabisa...chunguza kwa umakini usitangulize ujasiri...angalia mwisho wa maneno mengi ya kiswahili hamna coda ila kiarabu maneno kama sahel Allah yanaishia na konsonati sasa nashindwa kuelewa ufasaha wa kiswahili kusababishwa na kiarabu unakujaje hapa....kiswahili fasaha sio utamkaji wa kheri...taaratibu ila ni kuheshimu taaratibu za kisarufi....

Kiarabu haukijuwi. Ndiyo maana umekuja na "argument" ya kijinga kabisa. Kwanza jifunze Kiarabu halafu utaona kwanini nimesema "argument" yako ya kijinga.

Viunganishi muhimu kabisa vya Kiswahili vinatokana na Kiarabu, ufasaha wa lugha ni viunganishi na matamshi.

Mfano; "taka kuja" na "Na" taka kuja. Hiyo "na" inatokana na Kiarabu.

"Amma hivi Amma vile" = hiyo "amma" inatokana na Kiarabu.

"Wewe au mimi" = hiyo "au" inatokana na Kiarabu.

Mahari na Mahali ni maneno mawili tofauti na yote yanatokana na Kiarabu na ukiyakosea kuandika au kuyatamka kiufasaha basi umeharibu maana ya sentensi nzima.

Nisome post namba moja para ya kwanza utanielewa tu.

Hiyo "tu" inatokana na Kiarabu.

Jifunze Kiswahili kwa herufi za Kiarabu utapanuka hata mawazo yako.
 
Kama unaamini Kiswahili kimeazima maneno, jee neno swahili ambalo ni kiashiria cha kwanza cha lugha ya Kiswahili nalo limeazimwa pia? limeazimwa kutoka wapi? na kabla ya hali neno Kiswahili kulikuwa kuna neno lipi?

Unajuwa kitu kimoja, wewe unataka kulazimisha kuwa Kiswahili hakikutkana na Kiarabu lakini wakati huohuo unajisahau kuwa hata neno Kiswahili ni la Kiarabu.

Maatizo uliyonayo ni madogo sana, yanayokufanya usifikirie kwa mapana na marefu zaidi yahpo ulipofikia. Tatizo la kwanza ni unataka kuongelea luga wakati historia hauijuwi. Kwanza anza kuchambuwa historia ndipo utapoielewaa vizuri lugha ya Kiswahili imetokana na nini, kwa kuanzia:

Nifahamishe, nini maana ya neno Swahili? na Waswahili ni akina nani? ili twende vyema, kwani Kiswahili ni lugha ya Waswahili. Kumbuka, kama hauwajuwi Waswahili ni akina nani na historia yao ni ipi hutoweza kujuwa Kiswahili kimetokea wapi.

Kujitosheleza kwa lugha au kutojitoshelezza kwa lugha hakumaanishi kuwa "imeazima" maneno ya lugha nyingine. Mimi nnaona ni vyema tukasema "imechukuwa" maneno ya lugha nyingine kwa maana chakuazima hurudishwa, wewe umeshindwa kueleza Kiswahili kitarudisha lini maneno "iliyoazima". Mimi nnasema; Nisome post namba moja sentensi ya kwanza.
1:hili
2:hakikutokana
3:matatizo
4:ya hapo
5:lugha
6:kuchambua
7:naona
8:nasema
 
Hata hilo neno ulilotumia ni la Kiarabu sasa sijuwi unamaanisha nini ukisema "lugha hizi"?

Hakuna maneno ya "mkopo" kama umeyakopa utayarudisha lini? unarudi kule kule ambako swali hilo limeshajadiliwa.

Mmoja juu huko alikuja na maneno ya "kuazima", cha kuazima chako? sasa wewe umebadili unakuja na kukopa, cha kukopa hurudishwa, wewe utarudisha lini? Fikiri.

Hayo maneno yanatokana na Kiarabu na yanaunda Kiswahili. Hakuna kukopana wala kuazimana. Na ndiyo maana ukinisoma vizuri post namba moja, para ya kwanza, sentensi ya kwanza kabisa, nimeandika hivi:

"Kiswahili ni lugha ambayo imetokana na Kiarabu na Kibantu na maneno mengine machache yaliongezeka kidogo kidogo kutoka lugha zingine za Afrika, Uropa na Asia"

Sasa ni nini usichokielewa hapo? sasa rudi post namba moja, ujibu swali langu, lipo mwisho kabisa wa maandiko yangu.

Hujalisoma au limekuwa gumu kwako na unalikwepa?


Shuka uhusiano wa sarufi ya kiswahili na asilimia ya maneno kiarabu ya kiswahili yaliyokwisha fanyiwa tafiti sio kelele za misamiati 50...nmekuuliza tu mazingira ya mkazo na coda...jibu kwanza hili....tumia sarufi kunisahwishi na sio misamiati nichache..ata misamiati ya kilatini ipo kwenye kiingereza ila wanasarufi sjawai kuwaskia wakiongelea ufasaha unaouzungumzia... naomba kama huna Hoja za kisarufi rudi shule...
 
Bado unarudi pale pale ambapo nilikueleza kuwa unaandika bila kuijuwa historia.

Swali langu moja tu, sijuwi kama unalikumbuka, soma post namba moja mstari wa mwisho, nijibu hilo kwanza ili tuendelee vyema.

Ukishajibu hilo, sasa jibu na hili kwa kuwa umelianzisha pazuri kabisa, kwenye historia, Ubantu ulikuja lini pwani ya Afrika ya Mashariki ambako ndiyo chimbuko la Kiswahili?

Naona "argument" yako ya "kuazima" sasa haipo tena na umekubaliana nami kuwa ni kuchukuwa na si kuazima.

Kwa hiyo hapo ukumbuke, ni kuchukuwa na si kuazima kama ulivyofikiria awali.


Kabla ya kuendelea kujaza kurasa ningekuomba unijibu swali moja tu, Je Kiswahili kiko ktk familia gani ya lugha? Yaani Je Kiswahili ni Kibantu au afrosemitic language?
Naomba unijibu hilo swali tu kama ukipenda bila na wewe kuniuliza swali nipe jibu tu basi halafu sasa tuanzie hapo hatua kwa hatua Historia kwa Historia!
 
Back
Top Bottom