Huwezi na Hutoweza Kuongea / Kuandika Kiswahili fasaha

Huwezi na Hutoweza Kuongea / Kuandika Kiswahili fasaha

Hiyo post ya kwanza ni kiroja tu. Zaidi ya udini wako inaonesha hujui Kiswahili wala Kiarabu, ndio sababu unafikiri kuzungumza Kiswahili fasaha ni lazima ujue Kiarabu (what a shame!).

Hivi ni waislamu wangapi wa Tanzania wanaweza kuongea kiarabu (acha hicho mnachofunza huko madrasa)? Wangapi wanaweza kwenda Riyadh, Madina au Mecca na kuwasiliana na Waarabu bila kuhitaji mkalimani? Kiswahili ni lugha kamili inayojitegemea kama ilivyo kwa Kiarabu. Zote mbili zinakua na kubadilika kwa kadri ya wakati na hazitegemeani. Ufasaha wa lugha moja hauwezi kuletwa na lugha nyingine. Lugha ni sauti za nasibu na ni jamii husika ndio inaamua kipi ni fasaha na kipi si fasaha kulingana na wakati.

Kwa hivyo hoja kuwa mtu hawezi na hatoweza kuzungumza au kuandika kiswahili fasaha kama hajui lugha ya kiarabu, ni hoja unayoweza kuitoa kwenye vijiwe vyenu vya kahawa nje ya misikiti kule kariakoo tu.

Sasa huo "udini" ulioukazania uko wapi? Unanshangaza.

Wewe inaonesha hata maana ya dini hauelewi. Unajuwa kuwa neno "dini" linatokana na Kiarabu? Hata hiyo "nasibu" unaishadidia pia inatokana na Kiarabu. Unalijuwa hilo?

Sijuwi utakikwepa vipi Kiarabu katika Kiswahili. Na ili uwe na lafdhi na kina cha kuelewa maneno basi kama haujuwi kusoma na kuandika kwa herufi za Kiarabu unapitwa na mengi sana.

Hao Waswahili uliowataja wanaanza kufundishwa kusoma na kuandika Kiarabu kabla hawajaenda mashuleni, Hulijuwi hilo? au ni gumu kulimeza?

Utabeza sana lakini mwisho wa siku hutamsikia au kumuona aliyesoma herufi na irabu za Kiarabu kukosea "L" akaweka "R" na aongeapo, utajuwa tu, kuwa huyu ana ustaarabu.

Jee, unajuwa maana ya Ustaarabu?
 
Tehehe unataka kutuaminisha yakuwa inatupasa kujua kiarabu ili tu "fit" kwenye kicha cha Uzi wako.

Naam na hata nimeweka mifano ya Waalimu wa vyuo vikuu vya Ujerumani waliofundisha Kiswahili walifanya kila njia kujifundisha herufi na kusoma Kiarabu ili wafundishe Kiswahili kwa kina.
 
Tehehe unataka kutuaminisha yakuwa inatupasa kujua kiarabu ili tu "fit" kwenye kicha cha Uzi wako.

Naam na hata nimeweka mifano ya Waalimu wa vyuo vikuu vya Ujerumani waliofundisha Kiswahili walifanya kila njia kujifundisha herufi na kusoma Kiarabu ili wafundishe Kiswahili kwa kina. Na ushahidi nimeweka. pitia post namba 33 ufaidike.
 
Siyo maana yake kwa lugha gani?


Kumbuka kuna maana ya neno/maneno na kuna matumizi ya neno/maneno. Mimi sijauliza matumizi yake, nimeuliza maana yake.

Mfano; Kichwa ni neno la Kiswahili lenye maana yake lakini lina matumizi tofauti tofauti. Fikiri.

Si ndiyo maana hata mada imewashinda kuelewa.
 
Kumbuka kuna maana ya neno/maneno na kuna matumizi ya neno/maneno. Mimi sijauliza matumizi yake, nimeuliza maana yake.

Mfano; Kichwa ni neno la Kiswahili lenye maana yake lakini lina matumizi tofauti tofauti. Fikiri.

Si ndiyo maana hata mada imewashinda kuelewa.


Wewe usitake kutuzingua na kutuchota akili hapa kama umeanzisha mada ili ujaze kurasa bila kuwa na data zozote bora useme kwa maana hata haueleweki hasa unachotaka kusema ni kipi!
Mwanzoni umesema kiswahili kimetokana na kiarabu nikakupinga nikakwambia ya kwamba Kiswahili ni Lugha ya Kibantu kwa 100% iliyoazima maneno ktk kwenye lugha ya Kiarabu na nyinginezo na haina uhusiano wowote ule na Kiarabu kwenye muundo ya wake kitu ambacho ndiyo kinaamua kama lugha mbili zina uhusiano ama la wewe ukapinga!
Nikakuuliza kama Kiswahili ni sehemu ya Afrosemitic languages hautoi jibu unaniuliza maana ya neno ustaarabu nimekupa maana ya neno Ustaarabu kama tuijuavyo kwa Kiswahili wewe unasema siyo hivyo wakati kamusi ya Kiswahili (Ustaarabu - Wikipedia, kamusi elezo huru) inasema hivyo wewe unapinga sasa sijui hata unachotaka kusema ni kipi?

Kama unataka kuongelea kuhusu lugha na asili yake basi unapaswa kwanza uanzie kwenye familia ya lugha yenyewe, kama vile kiingereza ni familia ya germanic languages Kifaransa ni Latin languages hizo ni lugha mbili tofauti na hazina uhusiano wowote ule isipokuwa maneno ya kuazima ambapo Kiingereza kimeazima zaidi ya 50%, Sasa wewe unasema Kiswahili kimetokana na Kiarabu lkn hautaki kusema Kiarabu kama lugha kiko familia gani na Kiswahili familia gani sasa kama huwezi/hautaki kusema hilo kuna haja gani hata kuendela kujadiliana kuhusu lugha? Kwa maana msingi wa lugha uko hapo!
 
Naam na hata nimeweka mifano ya Waalimu wa vyuo vikuu vya Ujerumani waliofundisha Kiswahili walifanya kila njia kujifundisha herufi na kusoma Kiarabu ili wafundishe Kiswahili kwa kina. Na ushahidi nimeweka. pitia post namba 33 ufaidike.

Nina vingi vya kunisababisha nifaidike, lakini siyo ambacho unataka kuniaminisha.
 
Nikuchote akili kwani wewe ni msukule.

Unabwabwaja na kuhororja lakini bado hujaja na cha maana na inaonesha hata mada hukuielewa.

Ngoja nikuanzie taratiiiiib, maana unakuja na utumbo mreeefu lakini mada unaipiga chenga:

Hii ni sentensi ya kwanza kwenye mwanzo wa hii mada, nieleze unachokipinga hapa ni nini?

Kiswahili ni lugha ambayo imetokana na Kiarabu na Kibantu na maneno mengine machache yaliongezeka kidogo kidogo kutoka lugha zingine za Afrika, Uropa na Asia.

Ninachopinga ni hilo neno imetokana, ukisema Kiswahili kimetokana na Lugha za Kiarabu na Kibantu maana yake ni kwamba Kiswahili ni sehemu ya lugha Kiarabu na hapo ndipo ninapopinga kwani siyo kweli bali Kiswahili kimetokana na Lugha za kibantu na kuazima baadhi ya maneno yake kutoka lugha nyingine zisizo za kibantu kikiwemo Kiarabu, Kijerumani, kiingereza, Kireno n.k! Kwa kifupi Kiswahili siyo sehemu ya lugha ya Kiarabu bali ni sehemu ya Lugha za Kibantu kwa 100%
 
Ninachopinga ni hilo neno imetokana, ukisema Kiswahili kimetokana na Lugha za Kiarabu na Kibantu maana yake ni kwamba Kiswahili ni sehemu ya lugha Kiarabu na hapo ndipo ninapopinga kwani siyo kweli bali Kiswahili kimetokana na Lugha za kibantu na kuazima baadhi ya maneno yake kutoka lugha nyingine zisizo za kibantu kikiwemo Kiarabu, Kijerumani, kiingereza, Kireno n.k! Kwa kifupi Kiswahili siyo sehemu ya lugha ya Kiarabu bali ni sehemu ya Lugha za Kibantu kwa 100%

Bishana na hawa Wasomi: KISWAHILI LANGUAGE AND ITS UNDENIABLE ARABIC ORIGIN | Israel Ntaganzwa - Academia.edu

Sasa niambie neno Kiswahili linatokana na lugha ipi?
 
Bishana na hawa Wasomi: KISWAHILI LANGUAGE AND ITS UNDENIABLE ARABIC ORIGIN | Israel Ntaganzwa - Academia.edu

Sasa niambie neno Kiswahili linatokana na lugha ipi?


Kwanza kabisa neno Kiswahili limetokana na neno la kiarabu suahel (sina uhakika na uandikwaji wake) na maana yake ni watu wa Pwani (Peoples of the coast) na jina la lugha halisemi kitu chochote kuhusu asili ya lugha yenyewe! Waarabu walivyokuja walikikuta kiswahili kinaongewa lkn hakikujulikana kwa jina la Kiswahili bali kiliitwa vingine na wakaamua kukipa jina la suehel wakimaanisha watu waishio Pwani, yaani watu wabantu waliowakuta pale huyo Scholar wako sijui chanzo cha Habari yake lakini hata common sense tu ya kawaida inakwambia kwamba Kiswahili ni lugha ya Kibantu na hii imeshathibitishwa Dunia nzima na Linguistcs na ethnologists na Kiarabu ni sehemu ya Afro semitic language sasa huo ukweli unafaa kuzika hoja yoyote ile inayosema ya kwamba Kiswahili ni Kiarabu common sense tu ya kawaida! Naambatnaisha hapa mmandiko kuhusu asili ya Kiswahili!

Origin




Although originally written with the Arabic script, Swahili is now written in a Latin alphabet that was introduced by Christian missionaries and colonial administrators. The text shown here is the Catholic version of the Lord's Prayer.[SUP][11][/SUP]


Swahili is traditionally regarded as being the language of coastal areas of Tanzania and Kenya, formalised after independence by presidents of the African Great Lakes region. It was first spoken by natives of the coastal mainland and spread as a fisherman's language to the various islands surrounding the Swahili Coast. Traders from these islands had extensive contact with the coastal peoples from at least the 2nd century A.D. and Swahili began to spread along the Swahili Coast from at least the 6th century. There is also cultural evidence of early Zaramo people settlement on Zanzibar from Dar-es-salaam in present-day Tanzania. The African population of the island holds the tradition that it is descended from these early settlers.[SUP][citation needed][/SUP]

Clove farmers from Oman[SUP][12][/SUP] and the Persian Gulf farmed the Zanzibar Archipelago, slowly spreading Islam and adding a few words to Swahili language and building forts and castles in major trading and cultural centers as far as Sofala (Mozambique) and Kilwa (Tanzania) to the south, Mombasa and Lamu in Kenya, the Comoros Islands and northern Madagascar in the Indian Ocean, and Barawa to the north in southern Somalia. Demand for cloves soon established permanent trade routes, and Swahili-speaking merchants settled in stops along the new trade routes. For the most part, this process started the development of the modern Swahili language. However, the spread was hampered during the European colonial era and did not occur west of Lake Malawi, in what was then called the Belgian Congo, and is now Katanga Province of the Democratic Republic of the Congo, thus making it a secondary rather than a primary language in that region.[SUP][citation needed][/SUP]

The earliest known documents written in Swahili are letters written in Kilwa in 1711 A.D. in the Arabic script. They were sent to the Portuguese of Mozambique and their local allies. The original letters are now preserved in the Historical Archives of Goa, India.[SUP][13][/SUP] Another ancient written document is an epic poem in the Arabic script titled Utendi wa Tambuka (The History of Tambuka); it is dated 1728. However, the Latin script later became standard under the influence of European colonial powers.
 
Bishana na hawa Wasomi: KISWAHILI LANGUAGE AND ITS UNDENIABLE ARABIC ORIGIN | Israel Ntaganzwa - Academia.edu

Sasa niambie neno Kiswahili linatokana na lugha ipi?


Ndugu kwanza kabisa neno Kiswahili limetokana na neno la kiarabu suahel (sina uhakika na uandikwaji wake) na maana yake ni watu wa Pwani (Peoples of the coast) na jina la lugha halisemi kitu chochote kuhusu asili ya lugha yenyewe!
Waarabu walivyokuja walikikuta kiswahili kinaongewa lkn hakikujulikana kwa jina la Kiswahili bali kiliitwa vingine na wakaamua kukipa jina la suehel wakimaanisha watu waishio Pwani, yaani watu wabantu waliowakuta pale huyo Scholar wako sijui chanzo cha Habari yake lakini hata common sense tu ya kawaida inakwambia kwamba Kiswahili ni lugha ya Kibantu na hii imeshathibitishwa Dunia nzima na Linguistics na ethnologists na Kiarabu ni sehemu ya Afro semitic language sasa huo ukweli unafaa kuzika hoja yoyote ile inayosema ya kwamba Kiswahili ni Kiarabu common sense tu ya kawaida! Naambatanisha hapa maandiko kuhusu asili ya Kiswahili!

Origin




Although originally written with the Arabic script, Swahili is now written in a Latin alphabet that was introduced by Christian missionaries and colonial administrators. The text shown here is the Catholic version of the Lord's Prayer.[SUP][11][/SUP]


Swahili is traditionally regarded as being the language of coastal areas of Tanzania and Kenya, formalised after independence by presidents of the African Great Lakes region. It was first spoken by natives of the coastal mainland and spread as a fisherman's language to the various islands surrounding the Swahili Coast. Traders from these islands had extensive contact with the coastal peoples from at least the 2nd century A.D. and Swahili began to spread along the Swahili Coast from at least the 6th century. There is also cultural evidence of early Zaramo people settlement on Zanzibar from Dar-es-salaam in present-day Tanzania. The African population of the island holds the tradition that it is descended from these early settlers.[SUP][citation needed][/SUP]

Clove farmers from Oman[SUP][12][/SUP] and the Persian Gulf farmed the Zanzibar Archipelago, slowly spreading Islam and adding a few words to Swahili language and building forts and castles in major trading and cultural centers as far as Sofala (Mozambique) and Kilwa (Tanzania) to the south, Mombasa and Lamu in Kenya, the Comoros Islands and northern Madagascar in the Indian Ocean, and Barawa to the north in southern Somalia. Demand for cloves soon established permanent trade routes, and Swahili-speaking merchants settled in stops along the new trade routes. For the most part, this process started the development of the modern Swahili language. However, the spread was hampered during the European colonial era and did not occur west of Lake Malawi, in what was then called the Belgian Congo, and is now Katanga Province of the Democratic Republic of the Congo, thus making it a secondary rather than a primary language in that region.[SUP][citation needed][/SUP]

The earliest known documents written in Swahili are letters written in Kilwa in 1711 A.D. in the Arabic script. They were sent to the Portuguese of Mozambique and their local allies. The original letters are now preserved in the Historical Archives of Goa, India.[SUP][13][/SUP] Another ancient written document is an epic poem in the Arabic script titled Utendi wa Tambuka (The History of Tambuka); it is dated 1728. However, the Latin script later became standard under the influence of European colonial powers.
 
Mkuu umeshusha hadhi ya maprofesa yaani huyu kizee FaizaFoxy awe profesa?
Profesa hana kazi ya kufanya ni anashida kwenye mitandao ya kijamii na kuandika ----- tu?
_Basi kila mtu ni profesa!

Una matatizo kweli kweli ya uelewa, au ni viroba?

Kamsome tena unioneshe ni wapi kaniita "professor"?

Wacha kiherehere.
 
Ndugu kwanza kabisa neno Kiswahili limetokana na neno la kiarabu suahel (sina uhakika na uandikwaji wake) na maana yake ni watu wa Pwani (Peoples of the coast) na jina la lugha halisemi kitu chochote kuhusu asili ya lugha yenyewe!

Jisome hapo kwanza ulivyoandika "Ndugu kwanza kabisa neno Kiswahili limetokana na neno la kiarabu", halafu nisome mimi:

Kiswahili ni lugha ambayo imetokana na Kiarabu na Kibantu na maneno mengine machache yaliongezeka kidogo kidogo kutoka lugha zingine za Afrika, Uropa na Asia.

Juu huko umesema unapinga hilo halfu wewe mwenyewe unaji "contradict" na kusema hilohilo! Unashangaza!

Halafu hiyo "suahel" unavyoandika si hivyo ni "s'wahil" ndiyo maana nikasema ungekuwa unajuwa herufi za Kiarabu isingepata shida kabisa na usingijistukia kusema kuwa "(sina uhakika na uandikwaji wake)".

Hiyo ndiyo the whole point. Na umeyakinisha nilichokiandika. kasome tena post namba moja para ya tatu, au nikuwekee hapa usipate tabu:

"Nnadiriki kusema leo hii, ili uongee na kuandika Kiswahili fasaha inabidi ujuwe Kiarabu. Bila hivyo utaboronga tu."

Umejiona ulivyojistukia kuwa "umeboronga" mpaka ukaweka indhari kwenye mabano?

Bado hapo una ubishi zaidi?
 

Waarabu walivyokuja walikikuta kiswahili kinaongewa lkn hakikujulikana kwa jina la Kiswahili

Jisome tena halafu uone unavyozidi kuboronga. Unasikitisha sana tena sana.
 
FaizaFoxy;

Nina wasiwasi na uelewa wako wa Lugha na nafikiri una mapungufu katika hilo!
Kama hiyo ndiyo hoja yako na Je ili uongee Kiingereza fasaha ni lazima ujue Kifaransa? Kwa maana Kiingereza kimeazima zaidi ya asilimia 50 ya maneno yake kutoka Lugha ya Kifaransa sasa Waingereza wote ni lazima wajifunze Kifaransa ili waweze kuongea Lugha yao ya kiingereza?

Kwa taarifa yako tu kama ulikuwa labda haufahamu Lugha ya Kiarabu imetoa maneno mengi sana kwenye lugha nyingi sana Duniani Kihindi chenyewe zaidi ya asilimia 60% ya maneno yake kimeazima ktk kiarabu, Kimalay (Malaysia) zaidi ya asilimia 60%, Kiindonesia kina maneno mengi zaidi ya Kiarabu zaidi ya Kiswahili, Kiirani na hata Lugha kama Kihispaniola, Kireno, Kiitaliano, Kiingereza n.k maneno kama Algebra, cotton, alcohol, alkali n.k hasa kwenye sayansi yamezimwa ktk kwenye Kiarabu sasa kwa nini usiseme pia kuwa hizo lugha zote kwa kuwa zina maneno ya Kiarabu basi zimetokana na Kiarabu? Kwa nini usemee Kiswahili tu?
Kuna tofauti gani kati ya Uazimwaji wa maneno wa Kihispania au Kituruki ktk kiarabu na uazimwaji wa maneno wa Kiswahili ktk Kiarabu?
 
Last edited by a moderator:
Jisome tena halafu uone unavyozidi kuboronga. Unasikitisha sana tena sana.


Wewe ndiyo una matatizo ya kuelewa (labda ni tatizo langu nashindwa kujieleza na kueleweka kwako, hicho pia ni kipaji!) nimekwambia Waarabu kabla hawajakuja Lugha ya Kiswahili iilikuwepo lakni ilikuwa haiitwi Kiswahili walichokifanya Waarabu ni kuwaita Watu wa hao wa Pwani Wazaramo &Co. Suahel yaani watu wa pwani ni kama vile walivyowaita watu wa Sudani maana yake nchi ya Watu weusi sasa sielewi shida yako nini hapo!

Ngoja nikusaidie kama shida yako ni jina, mfano Wazungu wanaoishi Afrika Kusini Lugha yao inaitwa Kiafrika (afrikaans) sasa hilo jina limetoka wapi? Kiafrika hiki ni Kiholanzi hawa wazungu walipofika AK wakaamua kubadilisha jina la Lugha yao badala ya kiholanzi wakaamua kuiita Kiafrika sasa leo hii unaweza kusema kwamba Kiafrikaans ni Kiafrika kwa sababu kinaitwa Afrikaans?
 
@faizafox hapa leo umechemka sana kiswahili uhusiano wake na kiarabu ni mdogo sana tena upo katika kukopeshana maneno machache tu,

waarabu weneyewe hawakijui kiswahili inakuwaje ili ujue kiswahili lazima ujue kiarabu?

Kiaraabu kinaandikwa kutoka kulia kwenda kushoto kiswahili ni kinyume chake uhusiano wake uko wapi hapa?
Pili waarabu wakati wanaingia afrika mashariki tayari kulikuwa na watu wanaishi katika maeneo haya na lugha zao hivyo iliwalazimu waarabu kujifunza lugha za wakazi wa maeneo husika ndipo kiswahili kilipoibuka kweli uhusiano huu unaweza kutufanya tuamini kuwa mama wa kiswahili ni kiarabu?

No you are completely wrong.
 
Wewe ndiyo una matatizo ya kuelewa (labda ni tatizo langu nashindwa kujieleza na kueleweka kwako, hicho pia ni kipaji!) nimekwambia Waarabu kabla hawajakuja Lugha ya Kiswahili iilikuwepo lakni ilikuwa haiitwi Kiswahili walichokifanya Waarabu ni kuwaita Watu wa hao wa Pwani Wazaramo &Co. Suahel yaani watu wa pwani ni kama vile walivyowaita watu wa Sudani maana yake nchi ya Watu weusi sasa sielewi shida yako nini hapo!

Ngoja nikusaidie kama shida yako ni jina, mfano Wazungu wanaoishi Afrika Kusini Lugha yao inaitwa Kiafrika (afrikaans) sasa hilo jina limetoka wapi? Kiafrika hiki ni Kiholanzi hawa wazungu walipofika AK wakaamua kubadilisha jina la Lugha yao badala ya kiholanzi wakaamua kuiita Kiafrika sasa leo hii unaweza kusema kwamba Kiafrikaans ni Kiafrika kwa sababu kinaitwa Afrikaans?


Wewe unajuwa tatizo lako, ni kuwa huijuwi historia, "Waarabu kabla ya kuja"? kuja kutoka wapi? lini? na Pwani ya Afrika Mashariki walimkuta nani anaeongea Kiswahili?
 
Wewe unajuwa tatizo lako, ni kuwa huijuwi historia, "Waarabu kabla ya kuja"? kuja kutoka wapi? lini? na Pwani ya Afrika Mashariki walimkuta nani anaeongea Kiswahili?

Sasa hiyo ni mada nyingine kabisa unayotaka kuieleta na inastahili labda ufungue ukurasa Mpya! Ila kwenye swala la Lugha ni kwamba Kiswahili ni Lugha ya Kibantu na Kiarabu ni Semitic languages linguistically na ethnologically hizo ni lugha mbili tofauti na hazina uhusiano wowote ule na hilo limeshathibitishwa Duniani kote hayo mengine ni mambo ya emotions tu na hayana nafasi kwenye ukweli!
Hapo chini ni Ramani inayoonyesha semitic languages zilipo kikiwemo pia Kiarabu!


640px-Semitic_languages.svg.png

 

Attachments

  • 300px-Semitic_languages.svg.png
    300px-Semitic_languages.svg.png
    16.1 KB · Views: 87
Sasa hiyo ni mada nyingine kabisa unayotaka kuieleta na inastahili labda ufungue ukurasa Mpya! Ila kwenye swala la Lugha ni kwamba Kiswahili ni Lugha ya Kibantu na Kiarabu ni Semitic languages linguistically na ethnologically hizo ni lugha mbili tofauti na hazina uhusiano wowote ule na hilo limeshathibitishwa Duniani kote hayo mengine ni mambo ya emotions tu na hayana nafasi kwenye ukweli!
Hapo chini ni Ramani inayoonyesha semitic languages zilipo kikiwemo pia Kiarabu!



Umekwepa maswali ya msingi kwani ni wewe uliyeanzisha somo la nani kaja na kakuta nani na si mimi, sasa nnakuuliza kuhusu hayo hayo uliyoyaleta unasema hiyo mada nyingine! Hivi unaelewa ulichokiandika awali, hebu rudi kajisome.

Au umeona hapo hapajibiki ni suicide?

Sasa nnakupa challenge ndogo sana, katika hizo post zako ulizoandika Kiswahili, yatowe maneno yanayotokana na Kiarabu halafu tuone kama tutakuelewa ulichokiandika.
 
Hii thread imenipa elimu kubwa sana. Ngoja niendelee kuwasoma wataalam wa kiswahili.
 
Back
Top Bottom